Nimemfuma kaka yangu anaabudu mizimu

Nimemfuma kaka yangu anaabudu mizimu

Mpwayungu Village

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2021
Posts
14,591
Reaction score
31,128
Samahani sikuweza kumpiga picha angeniona.

Kweli mnaweza mkawa Familia moja mkidhani ni watu wa dini lakini kuna mmoja yupo tofauti. Ni kaka etu wa kwanza kwenye Familia nimeshuhudia kwa macho yangu katika kipindi hiki nipo kijijini, nilipotoka kanisani ikabidi nichukue baiskel kwenda shambani lakini nilipofika shambani sikumkuta. Nikafikiri labda yupo ndani ya shamba ngoja nimuangalie.

Nilipoona mzigo nyuma umenilemea niliingia polini na kidumu cha maji kwenda kuushusha, lahaulaah!

Sikuamini macho yangu ni kaka angu kabisa anainama na kuinuka huku akisujudu mti. Nikaona sio kweli ikabidi nijifiche ila nilichokishuhudia nikajua kumbe ndomambo yake sisi Jumapil kila tukienda kanisani yeye huwa anasema naenda shambani kumbe ana ibada zake za kipumbavu.

Sasa najipanga namna ya kuliweka wazi hili swala mbele ya baba na mama ilikusudi tusije Pata laana kizazi na kizazi mbele ya Mwenyezi Mungu
 
Samahani sikuweza kumpiga picha angeniona.

Kweli mnaweza mkawa Familia moja mkidhani ni watu wa dini lakini Kuna mmoja yupo tofauti. Ni kaka etu wa kwanza kwenye Familia nimeshuhudia kwa macho yangu katika kipindi hiki nipo kijijini, nilipotoka kanisani ikabidi nichukue baiskel kwenda
Amini unachoamini wewe na Sio unachoamini wewe uwaaminishe wengine
 
Kabla hujaingia humu Kumuanika Kaka Yako Muwe Mnajiulizaga haya

1.. Ninapoomba Mtakatifu Fulani wa Kanisani kwangu huwa naabudu mzimu au laah

Ukiona huwa unasema Mtakatifu Fulani niombee jua ww na Kaka Yako hamna Tofauti

Yesu mwenywe aliabudu Mizimu
 
Leave him alone to decide what kind of believes to follow other wise don't judge a book by its cover.
 
Kabla hujaingia humu Kumuanika Kaka Yako Muwe Mnajiulizaga haya

1.. Ninapoomba Mtakatifu Fulani wa Kanisani kwangu huwa naabudu mzimu au laah

Ukiona huwa unasema Mtakatifu Fulani niombee jua ww na Kaka Yako hamna Tofauti

Yesu mwenywe aliabudu Mizimu
Ulaniwe wewe mwanadamu
 
Aisee watu waliokulia imani flani ni ngumu kutochangama na mabo hayo. Mimi nimetoka kwenye familia ya kichaga watu bado wana imani za mizimu na huku wanaenda kanisani. Nishaona Tanga watu wanasoma kisomo cha Koran wanaisomea mizimu, kisha wanachinja na kufanya matambiko. Sharti kila kilichopikwa ni marufuku kwenda nacho nyumbani, lazima kiliwe sehemu iliyokuwa inaabudiwa. .

Mdogo wangu akiwa mdogo alipelekwa mwananyamala kwa kuingiza mbegu ya chungwa puani. Madaktari walichoma sindani mishipa yote ili mtoto apige chafya lakini wapi. Alikuwa anapumua kwa shida sana madaktari walipambana sana. Mzee kuona haieleweki akatoka nje ya hospital, akatema mate chini na kuomba mzimu kwa kichaga "vameku na vasheku va kasha, ngivaitereveni.....". Mzee kuingia wodini kumshika mtoto kapiga chafya mbegu kule 🙂
wale madaktari walishangaa sana ila ndo ikawa hivyo.

Ila Mungu anaweza, na vijawa wamtafute kwa kuwa Mungu anafanya miujiza mikubwa zaidi. Roho wa Bwana ametenda makuu mengi zaidi ya haya, nimeona hili kupitia mke wangu. Bwana ni Mwema siku zote, msiache kumsihi. .
 
ya kaisari mwachie kaisari...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom