Nenda Msimbazi na Oysterbay kuna kesi nyingi sana mamia za wizi wa simu, kila siku kesi mpya. Tazama kesi nyingi ni za simu gani, na hapo Apple ni kampuni mojawapo kati ya makampuni kadhaa common hapa bongo kwenye smartphones.
Simu zinazoibwa zaidi ni iPhone na mwizi hawazi habari ya wewe kukamatwa. Anachofanya anakuibia simu anaipeleka kwa IT inakuwa bypassed then anaiuza sokoni kwa wale wakurupukaji wa bei ya chini. Kama mwizi hana hiyo hela ya kubypass anamuuzia huyo mtaalamu, wapo wachache sana Kariakoo wengine waliuwawa, wengine walitoroka mji na wengine walipotezwa haijulikani wako wapi.
Samsung nyingi midrange na low end hazina ugumu, mamia ya Samsung A series za mkopo zimebadilishwa IMEI na hazisomeki kwenye systems za wakopeshaji mpaka mtu aki-reset ndio anakuta kumbe ilifungiwa muda mrefu.
Leo hii hamna mtu anaiba iPhone anaenda kutoa spare parts, hiyo ni zamani au mtu kaiokota ila mwizi anayejipanga anajua cha kufanya.