Nimeibiwa simu yenye thamani ya Tshs laki 6

Nimeibiwa simu yenye thamani ya Tshs laki 6

Nicheki nikuunganishe na jamaa yangu yeye ni pongo, atakutrakia kwa malipo kiduchu yamkini ukaipata..yuko smart sana kwenye hizo mambo
Huyo ni Polisi?.Kuna Mtu hapo juu amehoji kama tracking inaweza kufanywa pia na Mtu binafsi?.
 
Mkuu walinambia simu yako imesoma ipo kariakoo nitume pesa ya mafuta ili waende kumkamata mhusika hapo mimi nikiwa niko kazini nikatuma toka siku hiyo mpaka leo bado hawajamkamata mhusika ni mwaka na ushee🤨😬😬
TCRA wanasema huduma hiyo ni bure lakini polisi hiyo huduma siyo bure unalipia lakini ni nadra simu kupatikani
 
Mimi nimelipia 90000 ya ku track simu walipo nambia imepatikana ipo kariakoo nikawapa sh40000 ya mafuta.
Nenda ukaonane nao ana kwa ana wakurudishie hiyo pesa ila kumbuka kiendacho kwa mganga hakirudi lakini kumbuka pia maboss wa hao mapolisi wapo kwanini usiende kuwaona hapa tuna badilishana uzoefu tu
 
Nenda ukaonane nao ana kwa ana wakurudishie hiyo pesa ila kumbuka kiendacho kwa mganga hakirudi lakini kumbuka pia maboss wa hao mapolisi wapo kwanini usiende kuwaona hapa Tina badilishana uzoefu tu
Mimi police aliyenitapeli ni yule mpelelezi aliyekabidhiwa kesi yangu na mwenzie,yaani nikastaki kwa Askali kwamba wameniibia wasije wakanipoteza bure chozi langu haliendi bure.
 
Nimeibiwa sim na nisharipot police

Sasa niitrack au police watakula ela zangu

Nawaza niachane nayo tu lakini moyo unasema labda nijaribu upande mwingine naona nitapoteza mida na fedha
Maana nimejaribu kupitia nyuzi hapa hamna mtu anakiri alishawahi pata simu kwa kupitia police

Kama ni iphone unaweza jaribu.Ila kama ni aina nyingine basi fanya tu upate line yako tu basi.
 
Uko sahihi
Siyo mbaya kujifunza.waende hata kwa kagame hapo wajifunze.Kuna jamaa yangu aliibiwa laptop yake kwenye gari. alipokwend kureport police walimwambia aache details/contacts zake .next day akapigiwa simu aemde aka collect laptop yake
 
Siyo mbaya kujifunza.waende hata kwa kagame hapo wajifunze.Kuna jamaa yangu aliibiwa laptop yake kwenye gari. alipokwend kureport police walimwambia aache details/contacts zake .next day akapigiwa simu aemde aka collect laptop yake
Hawawezi kwenda
 
Sasa hio ndio vise-verse. Watu Wengi wanajua iPhone ndio zinatrakiwa hivyo wakizipata moja kwa moja kwa fundi simu ili kuuza spares.
Ila kwa androids sasa ndio wanaamini haiwez kutrakiwa. Mie yangu Samsung A53 na niliipata
Nenda Msimbazi na Oysterbay kuna kesi nyingi sana mamia za wizi wa simu, kila siku kesi mpya. Tazama kesi nyingi ni za simu gani, na hapo Apple ni kampuni mojawapo kati ya makampuni kadhaa common hapa bongo kwenye smartphones.

Simu zinazoibwa zaidi ni iPhone na mwizi hawazi habari ya wewe kukamatwa. Anachofanya anakuibia simu anaipeleka kwa IT inakuwa bypassed then anaiuza sokoni kwa wale wakurupukaji wa bei ya chini. Kama mwizi hana hiyo hela ya kubypass anamuuzia huyo mtaalamu, wapo wachache sana Kariakoo wengine waliuwawa, wengine walitoroka mji na wengine walipotezwa haijulikani wako wapi.

Samsung nyingi midrange na low end hazina ugumu, mamia ya Samsung A series za mkopo zimebadilishwa IMEI na hazisomeki kwenye systems za wakopeshaji mpaka mtu aki-reset ndio anakuta kumbe ilifungiwa muda mrefu.

Leo hii hamna mtu anaiba iPhone anaenda kutoa spare parts, hiyo ni zamani au mtu kaiokota ila mwizi anayejipanga anajua cha kufanya.
 
Nimeibiwa sim na nisharipot police

Sasa niitrack au police watakula ela zangu

Nawaza niachane nayo tu lakini moyo unasema labda nijaribu upande mwingine naona nitapoteza mida na fedha
Maana nimejaribu kupitia nyuzi hapa hamna mtu anakiri alishawahi pata simu kwa kupitia police
Polisi mafisi lazima yakutake Kwanza.
 
Back
Top Bottom