Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,189
- 4,103
Habari Wakuu,
Leo 31/ 01/ 2022 shahidi wa 12 Denis Urio anaendelea kutoa ushahidi wake kwenye kesi inayomkabili Mbowe na wenzake 3.
Kujua Kesi ilipoishia fungua kiungo hiki:Yaliyojiri Mahakama Kuu Kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake. Shahidi wa 12 Luteni Urio kuendelea kutoa ushahidi Januari 31, 2022
Fuatana nami kupata yatakayojiri
UPDATES:
Jaji ameingia Mahakamani, Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Jamuhuri Dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani Muda huu
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Ikupendeze naitwa Robert Kidando nipo pamoja na
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa na tutaendelea na Shahidi, Tupo tayari Kuendelea
Shahidi anaingia kutoka Nje
Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Nasisi pia tupo tayari Kuendelea
Jaji: nakukumbusha Kwamba Tarehe 28 ulikuwa upo chini ya kiapo na leo utaendelea kutoa ushahidi wako chini ya kiapo
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba sababu ya kelele za Jenereta tufunge madirisha tafadhali.
Kibatala: Mr Urio how are you?
Shahidi: Am fine
Kibatala: Did you have a nice Weekend?
Shahidi: like speak again
Kibatala: Did you have a nice Weekend?
Shahidi: like That!
Kibatala: Shahidi Umesha wahi Kukutana na Mazingira ya Kuambi Maneno Mazito Unayosema ya Ugaidi
Shahidi: Sijawahi Kukutana nayo
Kibatala: Umesema hauna tatizo la Kumbukumbu
Shahidi: Sina tatizo la Kumbukumbu
Kibatala: Iweje usikumbuke Tarehe 2 Muhimu Wewe Kukutana na Mbowe na Kwenda Ofisini Kwa DCI Ukizingatia wewe ni Mwanajeshi, na Luteni wa Jeshi
Shahidi: Mhe Jaji Mheshimiwa Mbowe alikuwa ni Ndugu yangu, Nilikuwa sijui kuwa ni kweli au si Kweli, Mpaka nikaona kuwa Kumbe ni Serious
Kibatala: Wewe Luteni unaona Umejibu swali Langu la inawezekana Vipi usikumbuke Tarehe
Shahidi: Sijawahi Kusikia Maneno Mazito, Ndiyo Maana Nikaenda kutoa Riport Polisi Wafanye Uchunguzi
Kibatala: Swali langu inawezekana Vipi Ushindwe Kukumbuka Tarehe ya Matukio Kama hayo
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Mimi naona Kama Nimejibiwa
Jaji: Swali lilikuwa linawezekanaje Kuwa asahau Tarehe za Mambo Muhimu
Shahidi: Ilikuwa ni Mara ya Kwanza, Kusikia Kutoka Kwa Mheshimiwa Mbowe, Sikuwa nategemea
Kibatala: Vipi Kuhusu Tarehe ya kwenda Kwa DCI na yenyewe Ulikuwa shocked
Shahidi: Siyo Duty yangu Mimi Kukumbuka, Kazi yangu Ilikuwa Kutoa Riport tu
Kibatala: Kwakuwa Unaomekana Kujivua Duty ya Record Ya Tarehe, Unaweza za Ku tuisaidia Kwanini na Yeye DCI hakumbuki Tarehe Uliyo Kwemda Ofisini Kwake
Shahidi: Sifahamu, Siwezi Kumjibia
Kibatala: Siku Unakwenda Kwa DCI Kingai alikuwa Summoned akaja, Unaweza Kutuisaidia Kwanini huyu Kingai Mtu wa Tatu na Yeye hakumbuki ni Tarehe ipo Mlimkutana
Shahidi: Siwezi Kujua ni Kwa nini
Kibatala: Ni kwanini hata Inspector Swila ambaye ndiyo Afisa wa Upelelezi Aliyefungua Faili Tarehe 18 July 2020, Hakumbuki Tarehe hiyo
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je Kwa wewe Kama Luten Wa Jeshi unaona ni sahihi Kwa Nyinyi Watu wote hakumbuki Tarehe
Shahidi: Siwezi Kujibia
Kibatala: Umewahi Kusikia Msemo "The Lights are on but nobody at home"
Shahidi: Hapana Sijawahi Kusikia
Kibatala: Kwanini Tarehe 11 August 2020 ndiyo Maelezo Yako yaandikwe Mtoa Taarifa Ambaye ndiyo Ulisababisha Faili Kufunguliwa Tarehe 18 July 2020?
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: Wewe ni Luteni wa TPDF uoni Kwamba Inategemewa Maelezo Ya Mtoa Taarifa Kuandikwa Mapema Kadriri inavyowezekana
Shahidi: Siwezi Kujibia Polisi, Sababu Wao Wana Utaratibu Wao wa Kazi na Mimi Nina Utaratibu Wangu Wa kazi
Kibatala: DCI alikifafanulia Kwamba Kwanini Maelezo Yako hayawezi Kuchukuliwa Siku ambayo wewe Umeenda ku report
Shahidi: Hawakufafamua chochote
Kibatala: Tarehe 11 August 2020 kwa Ushahidi Wako Ndiyo Ulikwenda Kutoa Maelezo Ushahidi Wako Kwa Inspector Swila.. Inspector Swila alikufafanulia Kwanini alisubiri Mpaka Mwezi Mmoja Baadae?
Shahidi: Hakufafanulia
Kibatala: Tukisema Kuwa Mlitunga Kesi Mapema Kisha Baadae Ndiyo Makaanza Kutafuta Watuhumiwa, Nitakuwa Nakosea Kwa Fact hizo
Shahidi: Utakuwa unakosea
Kibatala: Unafahamu Dhana ya Infiltration,.?
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Maana yake
Shahidi: Kutoka sehemu Moja Kwenda sehemu Nyingine Kwa siri
Kibatala: Ni sahihi pia Maana yake Pana ni Kutuma Mtu Kwenda Kwenye Kambi ya Upinzani, Ili Kupata Taarifa Kamili
Shahidi: Hapana, Tactics inasema Kwamba ni Kitendo Cha Kutuma Mtu Kwa Siri
Kibatala: Nikumbushe tena Elimu yako
Shahidi: Form Four
Kibatala: Unafahamu Decoy
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Luteni wa Jeshi hufahamu Decoy
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Mlijadili Kwa Pamoja Kumpeleka Mtu kwa Mbowe akiwa na Vifaa aweze Kupeleleza na Kurekodi Ushahidi
Shahidi: Hatujawahi Kujadili
Kibatala: Ni Kweli Katika Ushahidi Wako Kwamba Mheshimiwa Mbowe alikwambia atachukua Dola Kwa namna yoyote, Je Uchaguzi ulitajwa
Shahidi: Nafahamu Uchaguzi Ulitajwa
Kibatala: Bado Jeshi lilikuwa halina Role to Play Kwamba wewe ni Mwanajeshi uliye kazini na Mbowe anataka Ex Commandos, Bado Jeshi lilikuwa halina sababu ya Kupewa Taarifa?
Shahidi: Ni Taarifa ambazo hazina Ushahidi, Bado Jeshi litapeleka Kule Kule Kwa Polisi
Kibatala: Unamfahamu Aliyekuwa Chief of Staff Luteni Generali A. Shimbo
Shahidi: Namfahamu
Kibatala: akiwa katika Majukumu Yake ulikuwa Jeshini
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Namnukuu Tarehe 13 10 2010 "Katika Uchunguzi huu, Jeshi limejipanga Kuhakikisha Uchaguzi Unakuwa wa Amani na utulivu".. Uliwahi Kusikia?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Bado Unasisitiza Kwamba Mambo Ya Kiuchaguzi Jeshi halihusiki
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: huoni Kwamba Kwa Kutoa Kwako Taarifa Jeshi lingefanikisha Kuweka Decoy, (Mamluki) wa Kwenda Kukusanya taarifa ambazo ni sahihi?
Shahidi: The issue ni kwamba Mtu anaitwa Freeman Mbowe hapokei Simu za Kawaida, anasema Nitumie picha na Profile yake ili ajiridhishe Kwamba bado Wapo Katika Service, Kwa hiyo Endapo tungetuma Mtu ambaye bado yupo katika Service angegundua
Kibatala: Kwa hiyo Tactical appreciation Yako ilikwambia Kwamba Mheshimiwa Mbowe ana uwezo wa Kujua profile zao?
Shahidi: Ndiyo, Unafikiri Kwanini alitaka Picture na Profile zao?
Kibatala: Katika Ushahidi Wako Wote Kuna Mahala Popote Ulisema Kwamba Mbowe alikwambia Kwamba ana Access ya Mtu Mwingine Jeshini
Shahidi: Hapana
Kibatala: Tujadili Kuhusu Tactical Appreciation, Ni sahihi Kwamba Kamanda anakutana na Mazingira Fulani ambayo Kamanda anapanga Vikosi Vyake Kukabiliana na Mazingira hayo kwa Muda kwa Kupanga Mkakati
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Sasa Wewe Palikuwa na Several Unknown, Nimekuuliza Kama Mbowe alikuwa na Access Jeshini Ukasema hujui, Sasa huoni Kwamba Tactical appreciation Yako Ilikuwa si sahihi
Shahidi: Huyu Bwana ningemwambia kuwa Sitaki angemtumia nani, Ndiyo Maana nilifanya Tactical Appreciation na Kwenda Kuripoti Kwa DCI
Kibatala: Unakubaliana na Mimi kwamba Katika hali hiyo Kuna mambo Kadhaa wa Kadhaa ulikuwa huyafahamu, Ndiyo Maana Ukasema Kwamba Ulikuwa hujui Kama alikuwa ameshaongea na Watu Wengine
Shahidi: Ndiyo nilikuwa sina Uhakika Kama Mbowe ana Option A, B na C
Kibatala: Sasa Jambo hilo Linaendana na Tactical Appreciation
Shahidi: Ndiyo linaendana
Kibatala: Kazi yangu ni Kuuliza Maswali
Kibatala: Umesema Ulikuwa huna Uhakika Mbowe alikuwa na Option A, B na C, Je ulijihakikishia Kwa Kumuhoji
Shahidi: Sikumuhoji
Kibatala: Unathibitisha alikuwa na Trust Yako yote
Shahidi: Sijui Kwa Yeye Sasa
Kibatala: Nakuuliza Wewe
Shahidi: Je ni Mimi peke yangu anaye niamini
Kibatala: Hakuna Mahala Uliposema Kwamba Mbowe alikutishia Wewe au Familia yako
Shahidi: Sijasema
Kibatala: Kwamba Mbowe alikuahidi Cheo Kama Incentive yako
Shahidi: Mbowe Hawezi Kunipa Cheo Jeshini
Kibatala: Kwa hiyo Mbowe alikuwa hawezi Kukuhaidi Cheo Sababu alikuwa Mbunge
Shahidi: Sahihi hawezi
Kibatala: Nashukuru Kwa jibu lako Zuri
Kibatala: Wakati Mbowe anakupa Maombi , Ulimkubalia au Moyoni Ulimkatalia
Shahidi: Ilikuwa Tactical Appreciation, Ile Kwamba nitachoma Vituo Vya Mafuta, Kuchoma Masoko,
Kibatala: Na Kumdhuru Sabaya pia Ulikuwa Unachakata
Shahidi: Sijawahi Kumtaja Sabaya Mimi, Nilitaja Viongozi
Kibatala: Akili ya Kawaida ya Luteni haikuwa na zaidi ya Kumchimba Kwamba anataka Kulipua Vituo gani, Kukata Miti sehemu gani?
Shahidi: Hata Ingekuwa ni Mimi, Ukishaanza Kunidodosa nakosa trust na wewe.
Kibatala: Wakati Mnakutana Kupanga Matendo ya Ugaidi, Mahakama Itakapopima, Maneno yako Dhidi ya Maneno ya Mbowe sababu Hakuna Sauti Nyingine wala Decoy?
Shahidi: Ndiyo Maana nikatuma Vijana
Kibatala: Kwani Vijana hawa si Washtakiwa? Au Wapelelezi Wako?
Shahidi: Washtakiwa
Kibatala: Unakubaliana na Mimi sasa Mahakama itabidi ipime neno lako dhidi ya Mbowe kwa sababu Hapakuwa na Mtu Mwingine pale
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unakumbuka Wakati wa Utejelezaji Wa Majukumu Yako, namna ulipompata Ling'wenya
Shahidi: Nakumbuka
Kibatala: Unakumbuka Uliongea na Baba Yake Ling'wenya
Shahidi: Nakumbuka
Kibatala: Unakumbuka Kwamba uliongea naye Tarehe ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Unakumbuka uliongea naye Majira gani
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Unafahamu a kwamba Mzee Ling'wenya alikukatalia Kumtoa Mwanaye sababu ya Mambo yaliyomtokea Mwanaye Jeshini
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu kwamba Yeye alishamtafutia Mwanaye Kazi ya kokoto
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba huyu Mzee (Baba yake Ling'wenya) ni Mwenyekiti wa Kijiji fulani huko Kusini
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Baba Yake alipokutafuta baada ya Kusikia Mwanae kakamatwa Unakumbuka Ulimjibu nini
Shahidi: Sikumbuki, Ila Niliwambia kuwa amuulize Boss wao
Kibatala: Kwani Boss wao ndiye aliye Mpigia Kumuombea Ruhusa Kwamba Kuna kazi
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: Ulimwambia Mzee Ling'wenya Kwamba Kuna kazi Kwa Mbowe lakini nataka akafanye Mipango ya Ugaidi
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Unafahamu Maana ya Intrapment
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Maana ya Kumtoa Mtu kafara
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Unakumbuka Kwamba Nilikuuliza Unasali Wapi kwa sababu gani
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: umeapa kwa Biblia Je Unafahamu Kuhusu Daniel
Shahidi: Nafahamu Kuwa walitupwa Kwenye Tundu la Simba
Kibatala: Wewe Kuna tofauti na Walichomfanyia Daniel na Ling'wenya Mkristo Mwenzangu.?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwamba Ling'wenya alikuwa na kazi yake ya Kubonda Kokoto wewe Kwa Kikao Chenu na DCI ukamtafuta Kumwimgiza kwenye Matatizo
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Wakati Baba Yake Ling'wenya anakutafuta Kukuuliza Kwamba Mwanaye yupo wapi Ukajibu Ongea na Boss wake, Ni kweli
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unafahamu kwamba Mzee Ling'wenya alistaafu Bila Doa Lolote Serikalini
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Kama Mzazi, anaumia Ka Ilivyokatwa kwa Mama Maria Kumuona Mwanaye anateseka Msalabani wakati hajafanya Kitu chochote
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Je inawezekana kwa Mafunzo yako wewe yanaruhusu Kiongozi wa Askari Wa Chini, awaache Askari Wake Wa Chini wakati wa hatari.?
Shahidi: Inategemea kwa Mazingira
Kibatala: Je ni Mazingira Gani kwa Mafunzo yako wewe yanaruhusu Kiongozi wa Askari Wa Chini, awaache Askari Wake Wa Chini wakati wa hatari?
Shahidi: Kiongozi anaweza asiwe Sehemu Moja
Kibatala: Unafahamu Kwamba Kwanini Kwenye Platoon Kiongozi anakuwa Mbele, Hata katika Biblia
Shahidi: Sifahamu, Sijawahi Kuona
Kibatala: Unafahamu Kwamba Adam Kasekwa alipatwa na Battle Traumatic Fatigue
Shahidi: Mimi sifahamu Sijawahi Kusikia ana historia hiyo
Shahidi: Je Shahidi alitoa cheti cha Daktari
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Ulisema Kwamba ulienda Kwenye Ofisi ya Admin officer ukasoma Mafaili yao
Shahidi: Siyo Mafaili ya Taarifa individual, Bali Taarifa za Matukio tangu Siku Natoka
Kibatala: Je ni sahihi Kwamba Ujui sababu ipi ambayo ilipelekea Adam Kasekwa Kufukuzwa Jeshini
Shahidi: Sijui zaidi ya Utovu wa Nidhamu
Kibatala: Unafahamu ni Maeneo gani Mahususi ambayo Walitembelea kwa ajili ya Kumdhuru Sabaya
Kibatala: Wewe Ukiwa katika kazi Maalum, Hukuona sababu kuuliza Kwa Bwire ni wapi Walipanga Kufanya Uhalifu
Shahidi: Mimi siyo Kazi Maalum
Kibatala: Kwani aliyetafuta Vijana ni Polisi au wewe?
Shahidi: Mimi
Kibatala: Mbowe aliomba Polisi wamtafutie Vijana?
Shahidi: Hapana
Shahidi: Bwire Hakuniambia
Kibatala: Katika Ushahidi Wako hujui wala hujazungumzia Kuhusu Milestone, Kokoriko na Triple B
Shahidi: Sijazungumzia
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Walikamatwa kwa tuhuma za Kupanga Kufanya Uhalifu wa Kumdhuru Sabaya
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Ni kweli Uliwatafuta Vijana Kwa ajili ya Kufanya Ukamataji kabla ya Uhalifu haujatokea
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Bado Hukuona Sababu ya Kumuuliza Bwire
Shahidi: Polisi Walitakiwa Wafanye Uchunguzi Wao
Kibatala: Kwani nani aliyemtafuta Adamoo
Shahidi: Ni mimi
Kibatala: Kwani nani alikuwa anaaminiwa na Adamoo kati yako na Polisi
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: akuna Taarifa a kwamba siku za Adamoo na Ling'wenya Wanakamatwa walikuwa wanapokea Taarifa Kutoka kwa Msiri wao, Je huyo Msiri ni wewe
Shahidi: Siyo Mimi
Kibatala: Je Kwa Ufahamu Wako palikuwa na amtu Mwingine aliyekuwa anatoa Taarifa kwa DCI na Kingai
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Kwa Ufahamu Wako wewe Kuna mtu Mwingine ambaye alikuwa anawajua Adamoo na Ling'wenya
Shahidi: Hapana
Kibatala: Unafahamu Kwamba Adamoo na Ling'wenya Siku Wanakamatwa pale Rau Madukani walikuwa wanafanya nini.
Shahidi: Wala sijui Kama Walikamatwa Rau Madukani
Kibatala: Unafahamu a kwamba pale Rau Madukani Mohammed Ling'wenya alikuwa na Dada yake anaitwa Athima
Shahidi: Sifahamu, Hakuwahi kuniambia
Kibatala: Wewe Hukumu uliza Bwire
Shahidi: Sikumuuliza
Kibatala: Ulikuwa unafahamu Kwamba Moses Lijenje ana Dada yake anaishi Arusha
Shahidi: Hapana Sijui
Kibatala: Na wala Msiri wao unasema Siyo wewe
Shahidi; Siyo Mimi
Kibatala: Kuna sehemu katika maelezo yako Uliandika "Nilimpatia ACP kingai Namba za Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya aweze Kuwa fuatilia" ni sahihi
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Swala la Kwamba ACP kingai alikuwa namba za watu Watatu Mpaka Siku wanakamatwa, Je uliliongelea.?
Shahidi: Sikuongelea
Kibatala: Ni Suala la Kuwapa namba za Simu ni Swala la Muhimu au siyo la Muhimu
Shahidi: Ni suala la Muhimu
Kibatala: Unafahamu kwanini Kingai Wala Mtu Mwingine yoyote Hakuna anaye zungumzia Swala la Wewe Kuwapa namba za Simu kabla
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Swala la Kingai Kuwa na namba za Simu za Watu hawa Zina Implication gani Katika Uchunguzi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Mashahidi ambao Wamekutangulia, Walikuwa Wanamtafuta Lijenje Manually wakati Wana namba zao za simu
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba hata baada ya Watu hawa kukamatwa Kingai hakufanya chochote Katika Kuwafahamisha Wapendwa Wao
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: Wakati Wa Tarehe 12 August 2020 Ulisema Ulimkabidhi Inspector Swila na kuandikishwa ID02
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Mwanzo Ukasema Kwamba Wakati Unamkabidhi Simu yako Ulitoa Line ya Vodacom ambayo ilikuwa na Mawasiliano yako na Watu Wengine
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Kwahiyo wewe Ulimkabidhi Inspector Swila Simu bila Sim card
Shahidi: Nilitoa ya vodacom ni kabakisha Moja
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Sim Card ya Vodacom,ulirudisha lini.?
Kibatala: Katika Nyaraka ipi Tukiangalia Tutaona Mlikabidhiana Sim Card ya Vodacom na Inspector Swila
Shahidi: Ipo
Kibatala: Ipo hapa Mahakamani
Shahidi: Hapana, Hapa Mahakamani Haipo
Kibatala: Ipo wapi
Shahidi: Sikujua Kama Inahitajika Mahakamani
Kibatala: Ile Simu ya Tecno Uliyowasha hapa, Ina SimCard ndani
Shahidi: Sikukagua kama ina Sim Card ndani
Kibatala: aliye sema Kwamba Ile simu ina Sim Card ndani ni nani
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: nikuombee utuonyeshe sim Card
Shahidi: Vyovyote Vile itakayokuwa
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo P34
Kibatala: haya Fungua utuonyeshe humo ndani Kuna Sim Card ya Mtandao gani
Shahidi anafungua
Shahidi: HAKUNA LINE HATA MOJA (SimCard)
Kibatala: Unafahamu thamani ya Kiapo chako
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba unawajibu wa Kulinda hadhi ya Jeshi la Wananchi Tanzania
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Ukweli na Uongo wako Unapimwa Katika Vitu Vidogo Vidogo Kama hivyo
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Nakuuliza tena, Wakati Unakabidhi Inspector Swila Simu Ilikuwa na Sim Card au Haina Sim Card
Shahidi: Ilikuwa na Sim Card
Kibatala: Unafahamu kwamba SimCard imepelekwa Wapi
Shahidi: Ilikuwa na Line ya Airtel Iliyobakia, Sifahamu Ipo wapi
Kibatala: Ile Sim Card Ya Vodacom na Zile simu zingine 3, katika Maelezo Yako ya Tarehe 12 August 2020 Ulizungumzia Katika Maelezo yako?
Shahidi: Sikuandika katika Maelezo Yangu
Kibatala: sisi tuna thibitisha Wapi Kwamba Ulikabidhi hizo Simu 3 wakati hazipo katika Maelezo yako wala Hakuna Hati ya Makabidhiano
Shahidi: lakini zipo Hapa Mahakamani
Kibatala: Ungekuwa Polisi Nimgekuuliza Unafahamu Chain of Custody wewe, ila wewe Afisa wa Jeshi Nitakuonea
Kibatala: Unafahamu Kwamba Hizo Simu 3 Zina Mahusiano na Kesi Hapa Mahakamani
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Je Ulimwambia Jaji Kwamba Zile simu zingine Mbili Kule Morogoro ulimwachi nani na Zilikuwa Chini ya Uangalizi wa nani
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Wala Hukumwambia Jaji Kama huko Ulipoziacha Zina password au hazina
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Je unafahamu Kwa nini yule aliyekwambia ulete Simu 3 Kesho yake, hajazungumzia chochote Kuhusu hizo Simu 3
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu au hufahamu Kwamba Freeman Mbowe alikuwa na Kaka wa Damu, Generali ambaye katika Kifo cha huyo Generali Rais Magufuli alienda kwa Mbowe Kumpa pole
Shahidi: Nilisikia
Kibatala: Na unataka tukubali sisi watu wazima Kuwa aliacha Ndugu yake wa damu aliyenyonya naye ziwe Moja akutafute wewe?
Shahidi: Yule si alishastaafu
Kibatala: alistaafu lini
Shahidi: Sijui
Kibatala: Kati ya Wewe Luteni uliye kazini na Generali ambaye amestaafu nani anawafahamu Watu wengi Jeshini Waliopo na Waliotangulia?
Shahidi: Jenerali
Kibatala: Unasema Siku ya Kwanza Mbowe alikutafuta Siku ya Kwanza, Ukashangaa
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Kitendo Cha Mtu wa Kukupigia Simu bila Ridhaa Yako unaweza kutolea Taarifa
Shahidi: Rudia Swali
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Kitendo Cha Mtu wa Kukupigia Simu Mtu Muhimu Kama wewe bila Ridhaa Yako unaweza kutolea Taarifa
Shahidi: Kwanza Mimi siyo Mtu Muhimu
Kibatala: Wacha Jaji aandike Kuwa wewe siyo Mtu Muhimu
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Kitendo Cha Mtu wa Kukupigia Simu bila Ridhaa Yako unaweza kutolea Taarifa
Shahidi: Siyo Utamaduni Wetu
Kibatala: Je ulitoa Taarifa Jeshini Kwamba Kiongozi Wa Chama Cha Upinzani Chadema Kakutafuta
Shahidi: Sikutoa
Kibatala: Kwenye Maelezo Yako Ulisema Kuwa Mliendelea Kuwasiliana naye kwa sababu wewe na Yeye Wote ni Kabila Moja
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Kwa hiyo hili la Ukabila ndiyo Kilikufanya uendelee Kuwasiliana na Mbowe
Shahidi: Hapana ni Mawasiliano
Kibatala: si Ndiyo Mawasiliano na Mwenyekiti wa Chadema wakati wewe Umesema hamfungamani na Chama Chochote
Shahidi: Mbowe ni Mbowe na Chadema ni Chadema
Kibatala: Kwanini sasa Katika Maelezo yako unasema "Freeman Mbowe Mwenyekiti Wa Chadema"
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: hapo ulimtenganisha Mbowe na Chadema?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Shahidi Ushahidi Wako Unasema Kwamba TSh 500,000 ulitoa TSh 300,000 Ikabakia TSh 200,000, Ukawapa Adamoo Ling'wenya TSh 199,000
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: katika Maelezo yako Uliandika Kwamba Mhe Mbowe alikumbushia Kuhusu Vijana, ukamwambia Kuwa wamepatikana 2
Kibatala: kwa hiyo wewe Kwa Maelezo Yako Ulisema Tarehe 20 July 2020 alinitumia Laki TSh 500,000 nikatoa TSh 300,000 Laki 2 Ikabakia Kwenye simu
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Katika Maelezo Hakuna Mahala Ulisema Uki Alisha TSh 200,000 Kwenye simu
Shahidi: Hakuna nilipoandika
Kibatala: Alikwambia Inspector Swila Maana ya haya Maelezo
Shahidi: Hakuniambia
Kibatala: Baada ya Siku Chache wapatikama Vijana Wawili nikawapatia TSh 195,000
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Maelezo yako na unachosema Kwenye Kizimba Vinafanana au Vinatofautiana?
Shahidi: Vinatofautiana
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba P 1 na P 13
Kibatala: Nimeshika hapa Maelezo ya Onyo ya Adam Kasekwa ambayo Wenzetu Wanasema alikiri
Kibatala: Katika Ushahidi Wako, Unasema Uliwapa Tsh 195,000 katika TSh 199,000 Uliyotumiwa, Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba TSh 4,000 Ilienda wapi
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Kwa hiyo TSh 4,000 ya Ugaidi hujasema Ipo wapi
Shahidi: SIYO YA UGAIDI, BALI YA KUWASAFIRISHA
Kibatala: kwa hiyo Wenzetu Wanasema Yote TSh 199,000 ilitumika Kwenye Ugaidi, Kumbe siyo Ugaidi
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Kibatala: Maelezo haya yanasema kuwa alipokea TSh 87,000 kila Mmoja, Je Ni kweli au si Kweli
Shahidi: Sikumpatia Mtu Mmoja Mmoja, Niliwapa Kwa Pamoja
Kibatala: Kama Adam Kasekwa kasema Walipewa TSh 87,000, Atakuwa Kasema Uongo
Shahidi: atakuwa kasema Uongo
Kibatala: Unakubaliana Kuwa 87,000 Mara Mbili ni TSh 174,000? Unakubali unakataa
Shahidi: amount hiyo Mimi sijui
Kibatala: Nakuuliza kimahesabu 87,000 Mara Mbili ni TSh 174,000
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Adam Kasekwa anasema Jumla Uliwapa Tsh 174,000, Wewe Unasema TSh 195,000, Je Inatofautiana
Shahidi: Inatofautiana
Kibatala: Na Adam Kasekwa anasema Kwamba Fedha hiyo Uliyotumiwa na Mbowe ilikuwa ni Kuwarejeshea (Refund) ni sahihi au Siyo Sahihi
Shahidi: Ni sahihi
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba na sisi tuwe tunaangalia Kama Maelezo yapo Sahihi
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Pia awe anasoma Kile ambacho Kimeandikwa Kwa Mfano Hakuna Sehemu imeandikwa TSh 174,000 lakini Kuna TSh 87,000
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Sasa Kwa Majibu Kuhusu Majibu ya Kielelezo P 1 yaondoke
Kibatala: Ni sawa tufute Mstari Mmoja halafu tuanze Upya
Kibatala: Sasa Nilikuwa nakuuliza awali shahidi Kuhusu Maelezo yako inasema hivi, Baada ya Siku Mbili Waliopatikana Vijana Wawili Adamoo na Ling'wenya Ambao Niliwapatia TSh 195,000, tulipo kutana Eneo la Msavu
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Kwa hiyo Ni sahihi Kwamba hiyo Tsh 195,000, Kwamba Uliwapatia Kama Gharama ya Nauli zao Kutoka Walipo toka Kuja Morogoro
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Walipo kuja Morogoro Kutoka Walipo toka Uliwapa Tsh 195,000 kwa Ujumla au Lah.
Shahidi: Niliwapa Kwa Ujumla
Kibatala: Adam Kasekwa anasema Walikuja na Ling'wenya, "kwa kutumia Simu ya Mke wangu, Alinipigia Kuna kazi ya VIP PROTECTION, Maelezo sahihi anayo Luteni Urio"
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: anasema "alitupatia Kila Mmoja TSh 87,000 Kwa Maelezo ya Ling'wenya"
Shahidi: sahihi
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Fedha zote hizo ilikuwa kwa ajili ya Refund
Shahidi: Ilikuwa kwa ajili ya Kuwafidia
Kibatala: Safi sana
Kibatala: Unakumbuka Ulisema Kwamba Uliwapa Nauli ya kwenda Wapi Adamoo na Ling'wenya Kutoka Morogoro
Shahidi: Niliwapa Cash Tsh 195,000, ila Sikumbuki niliwapatena TSh ngapi
Kibatala: Ni sahihi Kwamba ile 199,000 Iliyotuma Baadae ndiyo Uliwapa Nauli ili waende Kwa Mbowe
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unafahamu Katika Maelezo Yake Adam Kasekwa, Katika Ukurasa wa Nne Mstari ya Mwisho, ni kila Mtu Kufika Moshi.. Wewe Unasema Walikwenda Dar es Salaam Kukutana na Mbowe, Je Statement hii Inafanana au inatofautiana?
Shahidi: Inatofautiana
Kibatala: nimeshila Maelezo ya Mohammed Ling'wenya Kielelezo namba P13, anasema kuwa "Baada ya mazungumzo Luteni Urio Aliniuliza Kuwa Mshahara wa Mtwara TSh ngapi, Nika jibu ni posho ya Elfu 15 kwa Siku, Basi Luteni Urio akanishauri Mshahara uwe Kuanzia TSh 800,000"
Je, ni sahihi Kwamba Ulimshauri Kuhusu Mshahara
Shahidi: Hapana
Kibatala: anaendelea Kusema Kuwa "alitupatia TSh 190,000 nauli ya kwenda Moshi"... Je ni sawa au zinatofautiana na Maelezo yako
Shahidi: tofauti, Pia tofauti hata na Ile ya Adamoo
Kibatala: You're Very Smart
Kibatala: Ling'wenya anazungumzia TSh 190,000, wewe unazungumzia TSh 199,000, Kuna tofauti ya TSh 9000
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unakubaliana na Mimi Kuwa Wapokeajo wa hizi pesa wanasema Kuwa Matumizi Yake yalikuwa siyo Ugaidi bali nauli
Shahidi: Sikubaliani na wewe
Kibatala: Kwani wewe Umesikia Wao wanasema Kwamba ile Fedha ilikuwa kwa ajili ya Nini, Adama Kasekwa Si kwa ajili ya Refund na Mohamed Ling'wenya ilikuwa kwa ajili ya Kwenda Moshi?
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Hapa Walikuwa wamekutana na Mbowe?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Walikuwa bado hawajafanya Ugaidi
Shahidi: Walikuwa ndiyo hawajafanya Ugaidi
Kibatala: Unafahamu kwamba wenzio Wanasema Hizo TSh 199,000 Mbowe zilifadhili ugaidi?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: ooh! Kumbe hata wenzako wamekuficha?
Kibatala: Ling'wenya nasema pia alipewa pesa akanunue Mavazi, Ni kweli
Shahidi: Si Kweli
Kibatala: Kwamba wewe unasema Ling'wenya alipewa pesa ya Kwenda Dar es Salaam, Yeye anasema Kwenda Moshi, Mmetofautiana..?
Shahidi: Ni sahihi tumetofautiana
Kibatala: eneo lingine Mlilotofautiana Ling'wenya anasema alipewa pesa ya Kurejeshwe Nauli wewe Unasema Nauli ya kwenda Dar es Salaam
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Nipewe Kielelezo Namba P 26
Kibatala: Ni kweli Kwamba Mbowe alikwambia umtafutie Ex commandos bila Kikomo
Shahidi: Hakuniambia Idadi yeye alisema Wao Waje tu
Kibatala: Kwenye Kielelezo P26, Ni sahihi Kwamba Kwa Mujibu wa Tarehe 20 July 2020 Saa 1 na Dakika 39 yeye Mbowe anasemaje
Shahidi: "Kaka Wale Mtu tatu au Nne ni Muhimu sana"
Shahidi: Lakini kabla ya hiyo Meseji Kuna Mawasiliano ya Simu
Kibatala: Yapo wapi
Shahidi: Hayapo hapo
Kibatala: Soma Kama Ilivyo, Kwa Mujibu Wa Meseji hiyo Mbowe anauliza Watu wangapi
Shahidi: Kaka Wale Mtu tatu au Nne ni Muhimu
Kibatala: kwa hiyo Namba hapo ni 3 au 4
Shahidi: Ndiyo Waliopatikana
Kibatala: Nenda Kwenye Meseji ya Tarehe 20 July 2020 Saa 2 na Dakika 3 na sekumde 30, Nani katuma hiyo Meseji
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: Unafahamu hiyo namba hapo
Shahidi: naona Meseji Kwemda Kwa Mbowe tu
Kibatala: kwa ni Meseji hiyo Uliyotuma hiyo Meseji Kwenda Kwa Mbowe, Je ni Namba ipi ya simu
Shahidi: Nilitumia Mtandao Wa Telegram
Kibatala: Mtandao Wa Telegram Unapotumia unahitaji Mtandao
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Namba Uliyotumia Mtandao huo wa Telegram ni namba ipi
Shahidi anaangua kichekoo ghafla hapa.....
Kibatala: Shahidi Usiche, Ndiyo Maana nilikwambia The Truth Shall set you Free.. Mwambie Mheshimiwa Jaji namba yako ipo au haipo
Shahidi: Haipo
Kibatala: Soma Katika Extraction Report hapo Wanasema Namba gani hiyo
Shahidi: 1130138344 DENIS OWNER
Kibatala: Namba hiyo Unaifahamu au huifahamu
Shahidi Sifahamu
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Shahidi apewe nafasi ya Kutoa Ufafanuzi
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Wakili anataka Kufanya Submission Muda huu, asubirie Kwenye Re: examination, Swali langu Je Shahidi anaifahamu namba au haifahamu?
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Kama anataka Kuuliza namba, Ni Vizuri Shahidi afafanue tu
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji mimi naona Kuna tatizo na Line
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Wametoa OBJECTION Nime re-battle, Wao Wafanye rejoinder siyo Mr. Kidando atoe Hoja mpya..
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Kwenye Rekodi za Mahakama Aliyetoa Kielelezo hicho ni Inspector Ndowo, Hatuoni Haki Kwa shahidi Kuulizwa Kielelezo hicho, Si Sawa kuzuiwa Kutoa Maelezo
Jaji: Kama nimesikia Vizuri Mr. Kibatala alikuwa anauliza Kuwa Shahidi anaifahamu au haifahamu hiyo namba, Mimi sijasikia akijibu hilo swali, alipotaka Kufanya Kufafanua Ndiyo Mr Kibatala akakataa, sasa hayo atamueleza Wakili Wake
Jaji: Ni Sahihi Kwa Shahidi Kujibu Maswali anayo Ulizwa na Wakili tu..
Kibatala: Shahidi Hiyo namba Unaifahamu au haifahamu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Wakati Wa Ushahidi Wako Kuna Wakili yoyote alikwambia Fafanua
Shahidi: Hapana
Kibatala: Unafahamu Juu ya Application inaitwa Free Sms
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Ni application ambayo unatuma Meseji halafu pia unaweka namba kwa namba yako na Kuweka ya mtu unaye mtumia
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kuna wakili yoyote aliyekuuliza Kuhusu Free Sms
Shahidi: Hakuna
Kibatala: na Hakuna Wakili yoyote amekuomgoza Kuitambua hiyo Free Sms ilikuondoa hiyo dhana
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Soma, Hapo, Kuna Maelezo Unasema su siyo Salama Sana, Niwezeshe ili tuweze Kukutana
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Kuna Sehemu Yoyote Katika Kielelezo namba P 34 ambayo Freeman Mbowe amekueleza wewe Kwamba Mtumie Njia ya Mawasiliano Mbadala Kwa Sababu Simu Siyo Salama
Shahidi: Meseji ya Mwisho
Kibatala: haya tusomee
Shahidi: "Hellow Bro Nilishindwa Kupokea Simu yako Sababu Deshi Deshi"
Kibatala: kwa hiyo kwa Tafsiri yako Ndiyo Kasema kuwa Simu Siyo Salama
Shahidi: Ndiyo Nilivyo Tafsiri
Kibatala: Katika hiyo Meseji ya Mwisho Kuna Neno simu siyo Salama
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Taja namba ya Mbowe Katika hiyo Meseji ya Mwisho
Shahidi: 0713933386
Kibatala: Soma Sasa Katika Kielelezo Kama hizo Meseji zinafanana au Tofauti
Shahidi: Zinafanana
Kibatala: Sasa soma namba ambayo ipo katika Kielelezo namba P 26 Meseji hiyo hiyo
Shahidi: Inatoka namba 729414989
Kibatala: ambayo ni Namba ya nani
Shahidi: FREE
Kibatala: Je namba ULIYOSOMA Mwanzo na Sasa hivi zinafanana.?
Shahidi: Hapana hazifanani
Kibatala: Kuna tofauti eeeeh!?
Shahidi: Ndiyo Kuna tofauti
Kibatala: Kubwa au Ndogo
Shahidi: Kubwa
Kibatala: Uliongozwa Kufafanua hiyo Tofauti
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Tafuta Meseji ya Tarehe 20 July 2020, Saa 2 na Dakika 15 na Sekunde 54
Shahidi: "Naomba nitumie nauli ya Ku' mobilise nikutane nao Moro"
Kibatala: Nani alikuwa anaomba nauli
Shahidi: Mimi ndiye niliye kuwa naomba nauli
Kibatala: Kwa hiyo DENIS URIO ndiye aliye Omba nauli kwa ajili ya Kuwa Mobilise
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Baada ya wewe kuomba nauli ndiyo Mbowe sasa akatuma TSh 500,000
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Nitafutie Meseji yoyote ambayo Mbowe anatoa wazo yeye la kutuma yeye TSh 500,000
Shahidi ametumia dakika 1 kutafuta hapa..
Shahidi: HAKUNA
Kibatala: Ni nani kwa mujibu wa Kielelezo namba P 34 (Simu) aliye propose kuwa pesa ya Ku'. obilise iwe TSh 500,000?
Shahidi: Mimi Denis Urio
Kibatala: Kwa Mujibu Wa Meseji ya Tarehe Ngapi na Mwezi wa Ngapi ambayo wewe ndiyo Mtoa wazo
Shahidi: Meseji ya Tarehe 20 July 2020 Saa 2 na Dakika 19 na Sekunde 53
Kibatala: ambayo Meseji hiyo wewe Ulituma Kutoka Kwenye namba gani ya Kwako
Shahidi: Haionekani namba
Kibatala: ONGEZA SAUTI
Shahidi: Haionekani namba
Kibatala: Tafuta Meseji ya Tarehe 20 July 2020 Saa 2 na Dakika 24 na Sekunde 02
Shahidi: "Usiwe unatumia namba yako Kutuma Pesa, Tumia Wasaidizi Wako au Wakala Kutuma"
Kibatala: Ni nani aliyetuma Meseji hii
Shahidi: Mimi Denis Urio
Kibatala: Nikumbushe Kule Kwa DCI na Kingai Uliambiwa Jambo gani Vile
Shahidi: Kuwapeleka Watu
Kibatala: Ni sahihi Katika Maelezo Yako uliyo andika, Uliambiwa Uendelee na kazi ya kumtufutia Vijana na Kuku Sanya Ushahidi
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Hao Wasaidizi Wa Mbowe Washa wahi Kukutumia pesa
Shahidi: Hapana
Kibatala: Katika Mawasiliano yako na Mbowe Uliwahi kutajiwa au Kupatiwa Fedha Kufanya Muamala na Mtu anaitwa Willy Kijana wa Mbowe? Na Wily alikutumia TSh ngapi
Shahidi: 199,000
Kibatala: Ndiyo Fedha ambazo Uliwapa Adamoo na Ling'wenya
Shahidi: Ndiyo hiyo
Kibatala: Swali la Mwisho kabla ya Lunch
Kibatala: Hiyo namba ya Willy ambayo ilituma hiyo Fedha ya TSh 199,000, Uliwapa akina DCI na Kingai
Shahidi: Haikuja namba, Alinitumia namba baadae
Kibatala: Hiyo namba hata Ka Ulipewa baadae, Ulimpa DCI au Kingai
Shahidi: Sikumpa
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba Kama Wenzangu wataridhia tupate Health Break baadae tuendelee na Cross Examination, Naomba pia nirudishe Vielelezo
Jaji: nahairisha Kwa Dakika 45 Mpaka Saa 7 na Dakika 45 ambapo Shahidi ataendelea Kutoa Ushahidi
Jaji: anatoka Mahakamani
*******************************
Mahakama imerejea. Muda ni saa 8:07
Jaji amerejea mahakamani.
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Ikupendeze Mheshimiwa Jaji Quorum ya Upande Wa Jamhuri ipo Ka Ilipokuwa Mwanzoni
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji na sisi Kwa Upande Wetu Quorum yetu ipo Kama Ilivyo kuwa awali, Tupo tayari Kuendelea
Jaji: Shahidi nakukumbusha tena Kuhusu Kiapo chako, Utaendelea Kutoa Ushahidi Chini ya Kiapo
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba kwa Hisani tukumbushwe Jibu la Mwisho
Jaji: kama alimpa DCI na Kingai Namba ya Willy
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kumpa Shahidi Kielelezo namba P34
Shahidi: anapewa Kielelezo ambacho ni simu
Kibatala: Shahidi Ni sahihi Kwamba meseji ya Tarehe 22 July 2020 Saa 3 na Dakika 19 Sekunde 30
Shahidi: "Namba ya Dereva Wangu anaitwa Willy, Wamtafute yeye"
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Kielelezo namba P 26 Saa 9 na Dakika 30 Sekunde 45 ulipokea hiyo namba
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: na Wewe Saa 9 na Dakika 36 na Sekunde 39 ukasema " Nimepata namba, Nitawapa"
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Hao unaosema utawapa ndiyo akina Khalfani..?
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Niomyeshe Meseji ambayo Inaonyesha Kwamba Mbowe alituma namba Pele yake Kama Meseji
Shahidi: alituma lakini hapa Haipo
Kibatala: Ipo wapi
Shahidi: alituma Kwa Meseji ya Kawaida, au Sikumbuki Kama alituma wapi
Kibatala: Ipo wapi
Shahidi: Sikumbuki ipo wapi
Kibatala: Kama Nakumbuka Vizuri wewe hujawahi Kukutana na Willy
Shahidi: Sijawahi Kukutana naye
Kibatala: Tu assume Kama Mambo yalivyotokea, Je Freeman Mbowe aliluomba umtafutie Walinzi au Magaidi
Shahidi: Kwa hao nilikuwa namtafuta Watu Wa Kwenda Kufanya kazi ya Ulinzi
Kibatala: Yeye Mbowe alitaja Walinzi au hakutaja
Shahidi: Alitaja Walinzi
Kibatala: Ndiyo Maana wewe Uliwatafuta watu wa kwenda Kufanya Ulinzi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mbowe alikwambia ukionana nao Uwaambie hivi na Vile?
Shahidi: Hapana
Kibatala: aliye, waambia Kuwa Mnaenda Kufanya Kazi ya Ulinzi ni wewe
Shahidi: Ndiyo ni Mimi
Kibatala: Wakina Inspector Swila Walikwambia Kuwa actually Unatakiwa uwe Mshtakiwa namba Moja au namba Mbili
Shahidi: Hawajawahi Kuniambia
Kibatala: DCI au Kingai Walikwambia Kuwa Watakupatia Kinga Dhidi Ya Mashtaka?
Shahidi: Hawajawahi Kuniambia
Kibatala: Tarehe 22 July 2020 Saa 6 Na Dakika 27 na Sekunde 23 Soma
Shahidi: "Kama Ikikupendeza uwe unanitumia Pesa ya Kutosha kwa ajili ya Kuwa Mobilise kwa ajili ya Kuwafanyia Vetting"
Kibatala: Nani Katuma hiyo Meseji
Shahidi: Ni Mimi Denis Urio
Kibatala: Wakati Unatuma Meseji hii, Khalfani Bwire na Moses Lijenje Walikuwa wameshakwenda Kwa Mbowe?
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Katika Kukamilisha zoezi la Kutafuta Vijana hao ambao Hakutaja Kikomo, Freeman Mbowe alinitumia TSh 500,000, Ambapo nilizitoa, Je Kwa Maelezo Haya si ni Kwamba Ulitoa Laki 5 kwa Mkupuo Wa Pamoja
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Maelezo Yako Ya Ushahidi Wako na Maelezo Yako ya statement Vinapishana au Kuna vinaendana
Shahidi: vinaendana ila tofauti Kwenye Tafsiri tuh, (anaonyesha Kwa Mikono)
Kibatala: Sasa nakurudisha Kwenye Meseji
Kibatala: Ni sahihi Kwa Meseji hii Ulikuwa Unaomba Pesa za Ziada Kwa Freeman Mbowe?
Shahidi: Ni sahihi Ili Kufanya Mambo kwa Urahisi
Kibatala: Ulikuwa Unaomba Pesa za Ziada Kwa Mtu ambaye bila Shaka Unafahamu Kwamba ana Mipango ya Ugaidi
Shahidi: Ndiyo nafahamu, Kwa Kuwawezesha Watu aliokuwa anawahitaji,
Kibatala: Si Ndiyo Watu ambao alikuwa anataka Kuwatoa Kwa Ugaidi?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unafahamu Kuhusu Neno SOLICIT
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa Clarity wakati Unatuma Meseji Kwamba awe anatuma pesa za Kutosha ulikuwa Umeshapokea TSh 500,000
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwa hiyo awe anatuma pesa zaidi ya 500,000 sasa
Shahidi: Ni sahihi Kwa Kadiri Itakavyo Mpendeza
Kibatala: Ulisema Kwamba Kila ulikuwa unamfahamisha Kingai
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Katika Simu hiyo Kuna Meseji za Kumtaarifu Kingai Kuhusu Kutumia TSh 500,000
Shahidi: Hakuna, Ni kuwa naongea naye kwa simu
Kibatala: Je Kuna Meseji ya Mhamala Wa TSh 500,000 Ulitumia Kingai Kwenye Njia ya Meseji Kuonyesha Kingai kama Ushahidi
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Tarehe hiyo Hapo Ulimsalimia Mtuhumiwa Wa Ugaidi Shikamoo Mkuu, Ani sahihi
Shahidi: Sikuwa na Ugomvi naye
Kibatala: Mtu akiwa Adui wa Nchi yako si ni Adui Yako
Shahidi: Sikuwa na Ugomvi naye
Kibatala: Unasema Tarehe 04 August 2020 Khalfani Bwire alikupigia kuwa Adamoo na Ling'wenya Wapo Moshi Kumdhuru Sabaya
Shahidi: Tuweke Vizuri, Mimi ndiye niliye Mpigia kisha akanipigia
Kibatala: Kwa Maelezo yako Khalfani Bwire alikuwa Dar es Salaam au Moshi
Shahidi: alisema Kwamba Wale Madogo Wapo Moshi, sikujua yeye Yupo wapi
Kibatala: Kwa Maelezo Yako wewe Ka. Luten Wa Jeshi, Maelezo Yako Ya Wale Madogo Wapo Moshi, Ulitafsiri kuwa Bwire hayupo Moshi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Katika Maelezo Yako Kuna Maelezo Wale madogo wapo Moshi
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Maelezo Mnamo tarehe 04 August 2020 Khalfani Bwire alinijulisha Wapo Moshi Kumdhuru Sabaya, Kwani Tarehe 12 August 2020 Wanatakiwa Kurudi Dar es Salaam, Je Bwire bado yupo Dar es Salaam
Shahidi: Kwa Mtazamo wangu Mimi
Kibatala: Katika Statement hii Kuna Mahala Popote umeandika Kwamba Bwire yupo Dar es Salaam
Shahidi: sikuandika
Kibatala: Kwanini Huku andika Kwamba Bwire alikuwa Yupo Dar es Salaam
Shahidi: hakunitajia Location
Kibatala: Katika Maelezo Yako Mstari Wa Kwanza, Unasema "Nakumbuka Mwaka 2008 Nilikutana na Freeman Mbowe, Kwakuwa wote ni Kabila Moja, Mimi na Freeman Mbowe tumekutana tena CASA Motel kwa Maongezi". Je Neno Kukutana naye tena, Ni Mara ya Kwanza.?
Shahidi: Miye ndiyo Nilikutana naye Kwa Mara ya Kwanza
Kibatala: Lakini haya ni Maelezo yako Uliyosoma Na Kuyathibitisha..
Kibatala: Ni sahihi Kwamba kabla ya Kukutana naye ana kwa ana alikuwa anakutakia Heri za Sikukuu na Event Mbalimbali
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Ni sahihi Moja ya Njia ambayo Freeman Mbowe mnawasiliana alikutumia Pongezi za Maonyesho Ya Sherehe ya Muungano
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Mtu ambaye anatuma Ujumbe wa Pongezi Kwa niaba ya JWTZ, Kutokana na Maonyesho ya Muungano.. Ni Mzalendo au Jahiri
Shahidi: Kwa Kipindi Kile niliona Mzalendo
Kibatala: Katika Ushahidi Wako ulitoa Katika Kizimba Ulisema Kwamba Freeman Mbowe ndiye alikuta futa Mara Mliyopelekea Kukutana katika Mambo ya Ugaidi
Shahidi: yeye ndiye alinitafuta
Kibatala: alikutafuta Kwa Njia ipi
Shahidi: Kupitia Kwa namba za Watu wengine
Kibatala: Namba ambazo alikuwa anazitumia Uliwapa DCI na Kingai
Shahidi: Si Kuwapa
Kibatala: Ulizitolea Vipi Maelezo na Namba ambazo huzijui
Shahidi: Sikutoa sababu Nilikuwa sizijui
Kibatala: Mpaka unaenda Kuona Mbowe akakwambia Ishu za Ugaidi, Nani alimtafuta Mwenzie
Shahidi: Mimi Ndiye nilimtafuta, Akakuta Missed Call akanirudia Jioni
Kibatala: Kwa hiyo ambaye Ali prompt Kuonana, Siyo wewe ni simu ya Mbowe
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Kibatala: Nani aliye andika Kwamba Mwezi July Tarehe za katikati nilimtafuta ili tuweze Kuonana, Nani Kasa haya Maelezo
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: Narudia tena Kusoma
Kibatala: Kuna Eneo lolote ambalo Palikuwa na Missed Call na Baadae auka Return Call.?
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Je Kuna tofauti kati ya Maelezo na Unachosema Kizimbani
Shahidi: Ndiyo Tofauti Zipo
Kibatala: Katika Maelezo Yako, Kuna Maelezo yoyote Kwamba Ulipo Mpigia Simu DCI , Kuna Maelezo Kwamba Ulijitambulisha Kwake in fully
Shahidi: Nilitijambulisha
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kama Wenzangu hawatokuwa na Pingamizi naomba Wanipe nimuonyeshe Shahidi Maelezo yake, Kama ni Foundation nimefanya hivyo Kwa Zaidi ya Masaa Mawili
Kibatala: Shika hayo Maelezo Kwa Dakika 2 au 3 Kwamba Ulipo Mpigia Simu DCI Ulimpigia na Kujitambulisha Kuwa wewe ni Afisa wa Jeshi na Maelezo Yako yote
Jaji: Kanuni zinasemaje Kabla hajatafuta
Kibatala: Sawa Mheshimiwa Jaji Asante,
Shahidi Si Unaifahamu hiyo Statement
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Sasa Shika hayo Maelezo Kwa Dakika 2 au 3 Kwamba Ulipo Mpigia Simu DCI Ulimpigia na Kujitambulisha Kuwa wewe ni Afisa wa Jeshi na Maelezo Yako yote
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Ushahidi Wako na Hayo Maelezo hilo Eneo Kuna tofautiana au hapatofautiani
Shahidi: Kwenye hilo Eneo ni tofauti
Kibatala: Kwenye Maelezo Yako Ukisoma hapo, Kuhusu Pongezi ya JWTZ
Shahidi: Ni Meseji ya Pongezi
Kibatala: Maelezo hayo Yanatofautiana au hayatofautiani
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Kanuni inasema Kwamba isomwe Kwanza
Kibatala: Baada ya Maelekezo ya Mahakama tafadhali Soma hiyo Statement Yote Kwa Sauti
Shahidi ........ ANASOMA
Shahidi: Nimemaliza
Kibatala: Unakumbuka Nilikuuliza Kwamba unaishi Wapi Ukasema Ngerengere
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa Ngerengere na Kihonda Kuna Umbali Kiasi gani
Shahidi: Ni Mbali sana
Kibatala: Rejea Katika Maelezo Yako hapo Juu, Adress yako unaishi Wapi
Shahidi: Kihonda
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuhusi tofauti hiyo
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Nani alikuwa ana Propose Kuwa Msitumie Simu kwa Sababu Simu Siyo Salama
Shahidi: Mimi
Kibatala: Katika Statement Yako Unasema Mbowe alikwambia Kuwa Telegram Ndiyo Salama
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwenye Meseji Kuna sehemu tumeona Mbowe Kasema hivyo
Shahidi: Kimyaaa
Kibatala: Shahidi haya si Maelezo yako
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Una tatizo tukimpa haya Maelezo Jaji ayatumie katika Kutenda Haki
Shahidi: Hakuna tatizo
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Shahidi Kama alivyo Omba, Tunaomba iingie Kama Kielelezo
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi
Jaji: ni Kielelezo namba Ngapi
Kibatala: Kama Kielelezo namba D4
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji tunaomba tujikumbushe ni Kielelezo namba ngapi
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji ni sahihi Kuwa ni D4
Jaji: Nayapokea Maelezo Haya Kama Kielelezo namba D4 Mawakili wa pande zote mbili wanakubaliana na Uamuzi Jaji kwa Kusimama na Kumuinamia Kidogo
Kibatala: Shahidi Nilikuuliza Kuhusu ile Meseji ya Saa 12 na Dakika 27 na Sekunde 23 Mchana kwa ajili ya Kuwa Mobilise na Kuwafanyia Vetting na Kuwaleta Dar es Salaam
Shahidi: Nimeona
Kibatala: Focus yangu Ilikuwa katika Kuwa Fanyia Vetting, Ni Vetting ya Nini hasa
Shahidi: Kuwa Brief Kwamba Mnaenda Katika Kazi ya Ulinzi na Mkikuta Vitu Kinyume Mnitaarifu
Kibatala: Ndiyo Maana ya Vetting?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Hiyo Meseji Kaandika nani hapo
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: Kwani Mbowe alikuwa anajua kuwa Vetting Yako Ilikuwa inafanyika Vipi
Shahidi: Vetting kama Kufanyia Orientation
Kibatala: Vetting Siyo Kumuangalia Back ground na Kumuangalia Sifa zake Kama Kweli au za Uongo
Shahidi: Sikuwa na Tafsiri hiyo Mimi
Kibatala: Kwa hiyo Kuna Kitu gani ulitaka Kufanya Mpaka Ukataka pesa zaidi?
Shahidi: Ni hiyo Kuwa Orient tu
Kibatala: Bwire na Lijenje Uliwa' Orient au Hukuwa' Orient?
Shahidi: Niliwa' Orient
Kibatala: Sasa Bwire na Lijenje Kuna Mahala walisema Kwamba Pesa haiwatoshi, Mpaka Upate pesa za Ziada.?
Shahidi: pesa ya awali ilishakuwa Consumed tayari
Kibatala: pesa ya Awali Iliyokuwa Consumed ni TSh ngapi
Shahidi: Ni TSh 500,000
Kibatala: Shahidi nataka Kujua bado Kwanini kwenye Meseji Kuna Nyongeza ya Vetting
Shahidi: Ilikuwa Kuwafanyia Orientation
Kibatala: kwa hiyo ni pesa ya Mbowe ndiyo imefadhili Ugaidi halafu Pia Ukatoa Mafunzo Kuwa Wasifanye Ugaidi?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Tarehe 22 July 2020 Saa 8 na Dakika 3 na Sekunde 53 Soma hiyo Meseji
Shahidi: Lakini wewe Usitume kwa namba yako
Kibatala: Nani alituma hiyo meseji
Shahidi: Mimi Denis Urio
Kibatala: Kwanini Ulimtumia Mbowe Taarifa hiyo
Shahidi: Ilikuwa Kuongeza Trust
Kibatala: Lakini Wewe una Maagizo ya DCI ya Kukusanya Ushkabidibkwa Kadri ya Uwezo Wako
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Tarehe 22 July 2020 Saa Saba na Dakika 51 na Sekunde 04
Shahidi: Nimeona
Kibatala: Soma
Shahidi: Pamoja na pesa ya Kula Tuma TSh 200,000
Kibatala: Ilikuwa pesa ya nini
Shahidi: Nauli pamoja na Kula
Kibatala: Tafuta Meseji ya Tarehe 22 July 2020 Saa 5 na Dakika 59, na Sekunde 31
Shahidi: Nimeona
Kibatala: S O M A
Shahidi: Kuna pamoja na Mambo Mengine Kuna Swala la Mishahara
Kibatala: Mishahara Uliyokuwa unazungumzia ilikuwa ya kazi gani
Shahidi: Kufanya Uhalifu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Kutolipa Mishahara ni Kosa la Jinai
Shahidi: Sifahamu Sheria
Kibatala: Pale Kuna sehemu unasema Kuna Masuala ya Utawala Wanauliza na Mishahara, Je Utawala Una manisha nini?
Shahidi: Utawala ni Masuala ya chakula
Kibatala: Utawala ni Chakula tu?
Shahidi: Pamoja na malazi
Kibatala: Watu wanaokwenda Katika Uhalifu Wanatakiwa Kuwa na Administration Obligation?
Shahidi: Ndiyo Kwani hawali, hawalali, hawavai?
Kibatala: Sawa Shahidi, Twende taratibu tu, tutaelewana
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba P20
Kibatala: Kuna Mahala ulikuwa unasa Kwamba Ulikuwa Unawasiliana na Khalfani Bwire kupitia namba 0782 237913 Sasa Nakuonyesha Kielelezo namba P 20 Ni kweli au Siyo Kweli Kwamba Ulituma Kiasi cha TSh 190,000 kutoka 0787 555200 kwenda Kwenye namba 0782 237913
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Ulituma TSh ngapi
Shahidi: TSh 200,000
Kibatala: Sasa Ulisema Kwamba Khalfani Bwire Ulimpa TSh 300,000, Je ulitolea Maelezo Kwa Jaji
Shahidi: Transactions hiyo ya Bwire Sikumbuki na Sijatolea Maelezo
Kibatala: Kuna Mahala fulani ambapo inasemekana Mbowe, Kama sehemu ya Kutekeleza Mpango huo Alitakiwa Kupata Mabomu kutoka Ngerengere!?
Wakili wa Serikali, Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Samahani, Sina Hakika Kama Kuna Mahala Popote ambapo imesemwa hilo..
Kibatala: Wacha wanisaidie Kutafuta, Nitarudi baadae
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji hilo Swala Halipo hata Akitafuta
Kibatala: Nitaliacha hilo, Nitarudi baadae
Kibatala: Kwani shahidi unaweza kulipua bila ya Kuwa na material ya kulipua (vilipuzi?)
Shahidi: huwezi
Kibatala: Ni kweli Kwamba Mbowe alishawahi kukushirikisha kutafuta material ya Kulipua
Shahidi: hajawahi kunishirikisha
Kibatala: Je Katika Ushahidi Wako Uliwahi Kusema Kwamba Khalfani Bwire, Mohammed Ling'wenya na Adam Kasekwa walikuwa na access ya Kupata Milipuko kutoka 92 KJ?
Shahidi: Sijawahi Kusema
Kibatala: Je umewahi Kuzungumzia Kuhusu Bunduki aina ya Bastola aina ya Luger A5340 kuwa ni Standard Bunduki za Makomandoo
Shahidi: Sijawahi Kusema
Kibatala: Ulisema Kwamba Mohammed Ling'wenya baada ya Kufika Kwa Mbowe Tarehe 24 hujawahi Kuzungumza naye
Shahidi: Hapana, Nilimtafuta bila Mafanikio
Kibatala: Je unasema Kwamba Mbowe aliacha Kuwasiliana na wewe Tarehe ngapi
Shahidi: Tarehe 24 July 2020
Kibatala: Kwa hiyo Kwenye Kielelezo namba P 34 Kuna Meseji ambazo Ulimtumia Mbowe Hakujibu?
Shahidi: Zipo
Kibatala: Meseji hizo Ulimuonyesha Mheshimiwa Jaji ambazo hazikujibiwa na Mbowe Kwa Kuongozwa na Mawakili wa Serikali
Shahidi: Sikuonyesha
Kibatala: Vipi Kuhusu Calls, Ulimuonyesha Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Hapana
Kibatala: Kwenye hii Meseji Mbowe anasema sikuona Simu yako Kwa Sababu Deshi Deshi, l hope Umenielewa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: alisema Simu yako au Simu zako
Shahidi: Simu yako
Kibatala: Kwa kuwa wewe Ulikwepo Kwa DCI na Kingai, Nasikia kuwa Kingai aliteuliwa Kama Mpelelezi
Shahidi: Haja wahi Kuniambia kuwa ni Mpelelezi, alisema Taarifa Utampa Kingai
Kibatala: Katika Maelezo Yako Uliwahi Kufahamu Kwamba Inspector Swila Ndiyo Mpelelezi Wa Kesi yako
Shahidi: Hiyo sifahamu
Kibatala: Wala Ufahamu Kwamba Baada ya Inspector Swila Kufungua Faili, DCI alimteua kuwa Mpelelezi wa Kesi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unaweza Kukumbuka Kwamba Mohammed Ling'wenya alikuwa Sudani katika Peace Keeping
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Wakati Unatoa Ushahidi Kambi ya Makomando ipo Ngerengere au Kizuka
Shahidi: Ipo Kizuka
Kibatala: Wakati Wa Maelezo Yako Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kambi ya Komandoo ipo Kizuka
Shahidi: Sikutoa Maelezo
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Wakati upo Sudani Kwenye Peace Keeping Kambi yenu ilikuwa inaitwa KAUBECHE
Shahidi: Inaitwa COLABECHE
Kibatala: Mlipokuwa Sudani, Kiongozi wenu alikuwa Kanali Mbwilo
Shahidi: Hapana ni General Mbwilo
Kibatala: Body Guard Wa huyu Generali Mbwilo yupo hapa Mahakamani
Shahidi: hayupo
Kibatala: Unamfahamu Luteni Omary ambaye alikuwa Sudani
Shahidi: Namfahamu
Kibatala: Je Luteni Msandawe
Shahidi: By Then Namfahamu
Kibatala: Ijumaa Nilikuuliza Maswali Kuhusu namba za Kingai MLIZO badilishana Kwa DCI
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ukasemaje
Shahidi: Niliacha Hotelini
Kibatala: Kwahiyo baada ya Kesi Kuhairishwa Utakuwa Umekuja nayo Leo Diary Yako
Shahidi: Sikuja nayo, Sikuelekezwa na Mahakama
Kibatala: Majibu Kuhusu Pass pale Jeshini Ilikuwaje
Shahidi: Pass ya zaidi ya Wiki Moja napewa Karatasi, Kwenda Katika Ofisi yoyote ninapokwepo.. Pass Chini ya Wiki naandika katika Daftari pale Kambini
Kibatala: Uliulizwa Ukasema Movement Order Ipo wapi
Shahidi: Ipo Hotelini
Kibatala: Wakati Unaitwa Mahakamani Ulipewa Summons au Maboss Zako Walikwambia Unatakiwa kutoa Ushahidi
Shahidi: Nilitoka Kwenye Operesheni Maalum Boss wangu akaniambia kariport kwa DCI
Kibatala: Boss wako anaitwa Nani
Shahidi: Light Kenoth
Kibatala: Ulipo surrender Simu zako zote toka Tarehe 12 August 2020, Ulifafanua Kwa Jaji Kuwa Ulikuwa unatumia Simu gani
Shahidi: Hapana Siku fafanua
Kibatala: Unaweza Kutuambia Kwanini Wewe Kama Mtoa Taarifa Baada ya Kuchukua Simu zako, Hawajawahi Kukupa Simu zako Mpaka
Kibatala: Unakutana nazo tena Hapa Mahakamani
Shahidi: Waliniambia Kuwa Wanafanyia Uchunguzi
Shahidi: Ndiyo Mara ya Mwisho Kama Mwaka Mmoja Umepita nilienda Kuulizia
Shahidi: Kwa Documents walizonipa
Kibatala: ambayo ni Moja
Shahidi: Hapa ninayo Moja lakini Zingine ninazo Nyumbani
Kibatala: Ukiangalia suala hili limeanza Tangu June 2020 Mpaka August 2020
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: kwa hiyo Tukiangalia katika Telegram hatutoona Mawasiliano yako wewe na Mbowe kabla ya Tarehe 25 June
Shahidi: Tulikuwa tunawasiliana Kupitia Whatsup
Kibatala: Mlikuwa Mnawasiliana kabla ya Kipindi cha Hili Tukio au ni Wakati wa Jambo hili tuh
Shahidi: Kimyaaaaaaaaa
Kibatala: Tarehe 07 August 2020 ulikuwa wapi
Shahidi: Nilikuwa Nipo kazini Sanga Sanga
Kibatala: Ni nini ambacho tunaweza Kuku Omba ukatuletea kuwa Ulikuwa kazini
Shahidi: Nilkuwa Commander wa QRF (QUICK RESPONSE FORCE)
Kibatala: zaidi ya Kuandikishana Kielelezo namba P 36 ni Ushahidi I alp Kwamba Inspector Swila Aliingizwa Simu katika Kitabu Kisha Wote Wewe na Yeye Mkasaini Kitabu
Shahidi: Mimi Siku Saini Kitabu
Kibatala: Na Yeye Hukumuona akiandika chochote Katika Kitabu
Kibatala: Zaidi ya Hand over Document, Je Uliwahi Kupewa Risiti yoyote ya Simu zako
Shahidi: Sijawahi Kupewa Risiti
Kibatala: Je Wakati Unamkabidhi Simu Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Inspector Swila alikuwa anabandika Makaratasi Katika Simu (Exhibit)
Shahidi: Sijawahi Kuona
Kibatala: Katika Maelezo ya Ushahidi Ulisema Kwamba haukujisumbua tena Kuhusiana na BWIRE kwa Sababu Lengo lilikuwa Limeshatimia
Shahidi: Nakumbuka nilisema
Kibatala: Lilikuwa Lengo lipi
Shahidi: Baada ya Wahalifu Kukamatwa
Kibatala: Kwa hiyo Lengo lako wewe lilikuwa Kuhakikisha Wahalifu Wanakamatwa
Shahidi: Nazuia uhalifu
Kibatala: Je ilikuwa kazi yako ya Kazi ya Polisi
Shahidi: Ilikuwa kazi ya Polisi
Kibatala: Malya alikuuliza Kwamba Uliwanunulia akina Adamoo Chakula
Shahidi: Nililipa Mimi lakini pesa Nilipewa na Mbowe
Kibatala: Je Ulizungumzia Katika Ushahidi Wako Mkuu Kuwa katika Pesa niliyowapa Adamoo na Ling'wenya Sehemu ya pesa ile Walitumia palepale Kulipa Chakula
Kibatala: Kwa kuwa wewe ulikuwa na Mawasiliano Moja kwa Moja na DCI na Kingai, Uliwahi Kufahamu Kwamba Hakuna Simu ya Mbowe hata Moja iliyokamatwa
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa Maana hiyo Ufahamu Pia Kwamba Polisi Wameshindwa Kuthibitisha Mawasiliano yako wewe na Mbowe
Kibatala: Mhe Jaji Nauliza Swali la Mwisho halafu nitatoa hoja
Kibatala: Ulisema Bwire Alikwambia Wapo katika Utekelezaji Wa Mpango
Shahidi: Siyo Mpango, alisema Samahani Bro tumeshakengeuka, Tumeshawishiwa na Freeman Mbowe, Na Vijana Wapo Kilimanjaro Katika Utejelezaji
Kibatala: Wewe Ulikuwa na Mamlaka Yoyote Ya Kiupelelezi zaidi Ya Kutoa Taarifa
Shahidi: Kila Mtanzania ni Mpelelezi, Sina Mamlaka Nyingine Ya Kiupelelezi
Kibatala: Hoja yangu Ulipata wapi Power Ya Kuagiza Waendelee na Uhalifu
Shahidi: nilishatoa Taarifa
Kibatala Mheshimiwa Jaji Bado Nina Maswali Kadhaa, Naomba tuhairishe Cross Examination, Mpaka Kesho February, Ilituweze Kuendelea.. Ni hayo tu.
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi, lakini tunaomba Kesho Tukiendelea Mwenzetu ajieleleze Katika Maeneo ambayo bado hajayahoji
Jaji: Unasemaje
Wakili Peter Kibatala: Hakuna Neno Mheshimiwa Jaji
Jaji: Shauri hili limehairishwa mpaka kesho Tarehe 01.02.2022, Shahidi namba 12 ataendelea Kuwa Mahakamani Kuendelea Kutoa Ushahidi Wake. Washtakiwa wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Kesho Asubuhi Saa 3 Asubuhi.
Jaji anatoka Saa 10: 38
Leo 31/ 01/ 2022 shahidi wa 12 Denis Urio anaendelea kutoa ushahidi wake kwenye kesi inayomkabili Mbowe na wenzake 3.
Kujua Kesi ilipoishia fungua kiungo hiki:Yaliyojiri Mahakama Kuu Kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake. Shahidi wa 12 Luteni Urio kuendelea kutoa ushahidi Januari 31, 2022
Fuatana nami kupata yatakayojiri
UPDATES:
Jaji ameingia Mahakamani, Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Jamuhuri Dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani Muda huu
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Ikupendeze naitwa Robert Kidando nipo pamoja na
- Wakili Pius Hilla,
- Abdallah Chavula
- Jenitreza Kitali
- Nassoro Katuga
- Esther Martin
- Ignasi Mwinuka
- Tulimanywa Majige
- Wakili Michael Mwangasa
- Sisty Aloyce
- Gaston Garubindi
- Idd Msawanga
- Maria Mushi
- Nashon Nkungu
- John Mallya
- Dickson Matata
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa na tutaendelea na Shahidi, Tupo tayari Kuendelea
Shahidi anaingia kutoka Nje
Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Nasisi pia tupo tayari Kuendelea
Jaji: nakukumbusha Kwamba Tarehe 28 ulikuwa upo chini ya kiapo na leo utaendelea kutoa ushahidi wako chini ya kiapo
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba sababu ya kelele za Jenereta tufunge madirisha tafadhali.
Kibatala: Mr Urio how are you?
Shahidi: Am fine
Kibatala: Did you have a nice Weekend?
Shahidi: like speak again
Kibatala: Did you have a nice Weekend?
Shahidi: like That!
Kibatala: Shahidi Umesha wahi Kukutana na Mazingira ya Kuambi Maneno Mazito Unayosema ya Ugaidi
Shahidi: Sijawahi Kukutana nayo
Kibatala: Umesema hauna tatizo la Kumbukumbu
Shahidi: Sina tatizo la Kumbukumbu
Kibatala: Iweje usikumbuke Tarehe 2 Muhimu Wewe Kukutana na Mbowe na Kwenda Ofisini Kwa DCI Ukizingatia wewe ni Mwanajeshi, na Luteni wa Jeshi
Shahidi: Mhe Jaji Mheshimiwa Mbowe alikuwa ni Ndugu yangu, Nilikuwa sijui kuwa ni kweli au si Kweli, Mpaka nikaona kuwa Kumbe ni Serious
Kibatala: Wewe Luteni unaona Umejibu swali Langu la inawezekana Vipi usikumbuke Tarehe
Shahidi: Sijawahi Kusikia Maneno Mazito, Ndiyo Maana Nikaenda kutoa Riport Polisi Wafanye Uchunguzi
Kibatala: Swali langu inawezekana Vipi Ushindwe Kukumbuka Tarehe ya Matukio Kama hayo
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Mimi naona Kama Nimejibiwa
Jaji: Swali lilikuwa linawezekanaje Kuwa asahau Tarehe za Mambo Muhimu
Shahidi: Ilikuwa ni Mara ya Kwanza, Kusikia Kutoka Kwa Mheshimiwa Mbowe, Sikuwa nategemea
Kibatala: Vipi Kuhusu Tarehe ya kwenda Kwa DCI na yenyewe Ulikuwa shocked
Shahidi: Siyo Duty yangu Mimi Kukumbuka, Kazi yangu Ilikuwa Kutoa Riport tu
Kibatala: Kwakuwa Unaomekana Kujivua Duty ya Record Ya Tarehe, Unaweza za Ku tuisaidia Kwanini na Yeye DCI hakumbuki Tarehe Uliyo Kwemda Ofisini Kwake
Shahidi: Sifahamu, Siwezi Kumjibia
Kibatala: Siku Unakwenda Kwa DCI Kingai alikuwa Summoned akaja, Unaweza Kutuisaidia Kwanini huyu Kingai Mtu wa Tatu na Yeye hakumbuki ni Tarehe ipo Mlimkutana
Shahidi: Siwezi Kujua ni Kwa nini
Kibatala: Ni kwanini hata Inspector Swila ambaye ndiyo Afisa wa Upelelezi Aliyefungua Faili Tarehe 18 July 2020, Hakumbuki Tarehe hiyo
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je Kwa wewe Kama Luten Wa Jeshi unaona ni sahihi Kwa Nyinyi Watu wote hakumbuki Tarehe
Shahidi: Siwezi Kujibia
Kibatala: Umewahi Kusikia Msemo "The Lights are on but nobody at home"
Shahidi: Hapana Sijawahi Kusikia
Kibatala: Kwanini Tarehe 11 August 2020 ndiyo Maelezo Yako yaandikwe Mtoa Taarifa Ambaye ndiyo Ulisababisha Faili Kufunguliwa Tarehe 18 July 2020?
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: Wewe ni Luteni wa TPDF uoni Kwamba Inategemewa Maelezo Ya Mtoa Taarifa Kuandikwa Mapema Kadriri inavyowezekana
Shahidi: Siwezi Kujibia Polisi, Sababu Wao Wana Utaratibu Wao wa Kazi na Mimi Nina Utaratibu Wangu Wa kazi
Kibatala: DCI alikifafanulia Kwamba Kwanini Maelezo Yako hayawezi Kuchukuliwa Siku ambayo wewe Umeenda ku report
Shahidi: Hawakufafamua chochote
Kibatala: Tarehe 11 August 2020 kwa Ushahidi Wako Ndiyo Ulikwenda Kutoa Maelezo Ushahidi Wako Kwa Inspector Swila.. Inspector Swila alikufafanulia Kwanini alisubiri Mpaka Mwezi Mmoja Baadae?
Shahidi: Hakufafanulia
Kibatala: Tukisema Kuwa Mlitunga Kesi Mapema Kisha Baadae Ndiyo Makaanza Kutafuta Watuhumiwa, Nitakuwa Nakosea Kwa Fact hizo
Shahidi: Utakuwa unakosea
Kibatala: Unafahamu Dhana ya Infiltration,.?
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Maana yake
Shahidi: Kutoka sehemu Moja Kwenda sehemu Nyingine Kwa siri
Kibatala: Ni sahihi pia Maana yake Pana ni Kutuma Mtu Kwenda Kwenye Kambi ya Upinzani, Ili Kupata Taarifa Kamili
Shahidi: Hapana, Tactics inasema Kwamba ni Kitendo Cha Kutuma Mtu Kwa Siri
Kibatala: Nikumbushe tena Elimu yako
Shahidi: Form Four
Kibatala: Unafahamu Decoy
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Luteni wa Jeshi hufahamu Decoy
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Mlijadili Kwa Pamoja Kumpeleka Mtu kwa Mbowe akiwa na Vifaa aweze Kupeleleza na Kurekodi Ushahidi
Shahidi: Hatujawahi Kujadili
Kibatala: Ni Kweli Katika Ushahidi Wako Kwamba Mheshimiwa Mbowe alikwambia atachukua Dola Kwa namna yoyote, Je Uchaguzi ulitajwa
Shahidi: Nafahamu Uchaguzi Ulitajwa
Kibatala: Bado Jeshi lilikuwa halina Role to Play Kwamba wewe ni Mwanajeshi uliye kazini na Mbowe anataka Ex Commandos, Bado Jeshi lilikuwa halina sababu ya Kupewa Taarifa?
Shahidi: Ni Taarifa ambazo hazina Ushahidi, Bado Jeshi litapeleka Kule Kule Kwa Polisi
Kibatala: Unamfahamu Aliyekuwa Chief of Staff Luteni Generali A. Shimbo
Shahidi: Namfahamu
Kibatala: akiwa katika Majukumu Yake ulikuwa Jeshini
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Namnukuu Tarehe 13 10 2010 "Katika Uchunguzi huu, Jeshi limejipanga Kuhakikisha Uchaguzi Unakuwa wa Amani na utulivu".. Uliwahi Kusikia?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Bado Unasisitiza Kwamba Mambo Ya Kiuchaguzi Jeshi halihusiki
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: huoni Kwamba Kwa Kutoa Kwako Taarifa Jeshi lingefanikisha Kuweka Decoy, (Mamluki) wa Kwenda Kukusanya taarifa ambazo ni sahihi?
Shahidi: The issue ni kwamba Mtu anaitwa Freeman Mbowe hapokei Simu za Kawaida, anasema Nitumie picha na Profile yake ili ajiridhishe Kwamba bado Wapo Katika Service, Kwa hiyo Endapo tungetuma Mtu ambaye bado yupo katika Service angegundua
Kibatala: Kwa hiyo Tactical appreciation Yako ilikwambia Kwamba Mheshimiwa Mbowe ana uwezo wa Kujua profile zao?
Shahidi: Ndiyo, Unafikiri Kwanini alitaka Picture na Profile zao?
Kibatala: Katika Ushahidi Wako Wote Kuna Mahala Popote Ulisema Kwamba Mbowe alikwambia Kwamba ana Access ya Mtu Mwingine Jeshini
Shahidi: Hapana
Kibatala: Tujadili Kuhusu Tactical Appreciation, Ni sahihi Kwamba Kamanda anakutana na Mazingira Fulani ambayo Kamanda anapanga Vikosi Vyake Kukabiliana na Mazingira hayo kwa Muda kwa Kupanga Mkakati
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Sasa Wewe Palikuwa na Several Unknown, Nimekuuliza Kama Mbowe alikuwa na Access Jeshini Ukasema hujui, Sasa huoni Kwamba Tactical appreciation Yako Ilikuwa si sahihi
Shahidi: Huyu Bwana ningemwambia kuwa Sitaki angemtumia nani, Ndiyo Maana nilifanya Tactical Appreciation na Kwenda Kuripoti Kwa DCI
Kibatala: Unakubaliana na Mimi kwamba Katika hali hiyo Kuna mambo Kadhaa wa Kadhaa ulikuwa huyafahamu, Ndiyo Maana Ukasema Kwamba Ulikuwa hujui Kama alikuwa ameshaongea na Watu Wengine
Shahidi: Ndiyo nilikuwa sina Uhakika Kama Mbowe ana Option A, B na C
Kibatala: Sasa Jambo hilo Linaendana na Tactical Appreciation
Shahidi: Ndiyo linaendana
Kibatala: Kazi yangu ni Kuuliza Maswali
Kibatala: Umesema Ulikuwa huna Uhakika Mbowe alikuwa na Option A, B na C, Je ulijihakikishia Kwa Kumuhoji
Shahidi: Sikumuhoji
Kibatala: Unathibitisha alikuwa na Trust Yako yote
Shahidi: Sijui Kwa Yeye Sasa
Kibatala: Nakuuliza Wewe
Shahidi: Je ni Mimi peke yangu anaye niamini
Kibatala: Hakuna Mahala Uliposema Kwamba Mbowe alikutishia Wewe au Familia yako
Shahidi: Sijasema
Kibatala: Kwamba Mbowe alikuahidi Cheo Kama Incentive yako
Shahidi: Mbowe Hawezi Kunipa Cheo Jeshini
Kibatala: Kwa hiyo Mbowe alikuwa hawezi Kukuhaidi Cheo Sababu alikuwa Mbunge
Shahidi: Sahihi hawezi
Kibatala: Nashukuru Kwa jibu lako Zuri
Kibatala: Wakati Mbowe anakupa Maombi , Ulimkubalia au Moyoni Ulimkatalia
Shahidi: Ilikuwa Tactical Appreciation, Ile Kwamba nitachoma Vituo Vya Mafuta, Kuchoma Masoko,
Kibatala: Na Kumdhuru Sabaya pia Ulikuwa Unachakata
Shahidi: Sijawahi Kumtaja Sabaya Mimi, Nilitaja Viongozi
Kibatala: Akili ya Kawaida ya Luteni haikuwa na zaidi ya Kumchimba Kwamba anataka Kulipua Vituo gani, Kukata Miti sehemu gani?
Shahidi: Hata Ingekuwa ni Mimi, Ukishaanza Kunidodosa nakosa trust na wewe.
Kibatala: Wakati Mnakutana Kupanga Matendo ya Ugaidi, Mahakama Itakapopima, Maneno yako Dhidi ya Maneno ya Mbowe sababu Hakuna Sauti Nyingine wala Decoy?
Shahidi: Ndiyo Maana nikatuma Vijana
Kibatala: Kwani Vijana hawa si Washtakiwa? Au Wapelelezi Wako?
Shahidi: Washtakiwa
Kibatala: Unakubaliana na Mimi sasa Mahakama itabidi ipime neno lako dhidi ya Mbowe kwa sababu Hapakuwa na Mtu Mwingine pale
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unakumbuka Wakati wa Utejelezaji Wa Majukumu Yako, namna ulipompata Ling'wenya
Shahidi: Nakumbuka
Kibatala: Unakumbuka Uliongea na Baba Yake Ling'wenya
Shahidi: Nakumbuka
Kibatala: Unakumbuka Kwamba uliongea naye Tarehe ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Unakumbuka uliongea naye Majira gani
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Unafahamu a kwamba Mzee Ling'wenya alikukatalia Kumtoa Mwanaye sababu ya Mambo yaliyomtokea Mwanaye Jeshini
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu kwamba Yeye alishamtafutia Mwanaye Kazi ya kokoto
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba huyu Mzee (Baba yake Ling'wenya) ni Mwenyekiti wa Kijiji fulani huko Kusini
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Baba Yake alipokutafuta baada ya Kusikia Mwanae kakamatwa Unakumbuka Ulimjibu nini
Shahidi: Sikumbuki, Ila Niliwambia kuwa amuulize Boss wao
Kibatala: Kwani Boss wao ndiye aliye Mpigia Kumuombea Ruhusa Kwamba Kuna kazi
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: Ulimwambia Mzee Ling'wenya Kwamba Kuna kazi Kwa Mbowe lakini nataka akafanye Mipango ya Ugaidi
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Unafahamu Maana ya Intrapment
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Maana ya Kumtoa Mtu kafara
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Unakumbuka Kwamba Nilikuuliza Unasali Wapi kwa sababu gani
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: umeapa kwa Biblia Je Unafahamu Kuhusu Daniel
Shahidi: Nafahamu Kuwa walitupwa Kwenye Tundu la Simba
Kibatala: Wewe Kuna tofauti na Walichomfanyia Daniel na Ling'wenya Mkristo Mwenzangu.?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwamba Ling'wenya alikuwa na kazi yake ya Kubonda Kokoto wewe Kwa Kikao Chenu na DCI ukamtafuta Kumwimgiza kwenye Matatizo
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Wakati Baba Yake Ling'wenya anakutafuta Kukuuliza Kwamba Mwanaye yupo wapi Ukajibu Ongea na Boss wake, Ni kweli
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unafahamu kwamba Mzee Ling'wenya alistaafu Bila Doa Lolote Serikalini
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Kama Mzazi, anaumia Ka Ilivyokatwa kwa Mama Maria Kumuona Mwanaye anateseka Msalabani wakati hajafanya Kitu chochote
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Je inawezekana kwa Mafunzo yako wewe yanaruhusu Kiongozi wa Askari Wa Chini, awaache Askari Wake Wa Chini wakati wa hatari.?
Shahidi: Inategemea kwa Mazingira
Kibatala: Je ni Mazingira Gani kwa Mafunzo yako wewe yanaruhusu Kiongozi wa Askari Wa Chini, awaache Askari Wake Wa Chini wakati wa hatari?
Shahidi: Kiongozi anaweza asiwe Sehemu Moja
Kibatala: Unafahamu Kwamba Kwanini Kwenye Platoon Kiongozi anakuwa Mbele, Hata katika Biblia
Shahidi: Sifahamu, Sijawahi Kuona
Kibatala: Unafahamu Kwamba Adam Kasekwa alipatwa na Battle Traumatic Fatigue
Shahidi: Mimi sifahamu Sijawahi Kusikia ana historia hiyo
Shahidi: Je Shahidi alitoa cheti cha Daktari
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Ulisema Kwamba ulienda Kwenye Ofisi ya Admin officer ukasoma Mafaili yao
Shahidi: Siyo Mafaili ya Taarifa individual, Bali Taarifa za Matukio tangu Siku Natoka
Kibatala: Je ni sahihi Kwamba Ujui sababu ipi ambayo ilipelekea Adam Kasekwa Kufukuzwa Jeshini
Shahidi: Sijui zaidi ya Utovu wa Nidhamu
Kibatala: Unafahamu ni Maeneo gani Mahususi ambayo Walitembelea kwa ajili ya Kumdhuru Sabaya
Kibatala: Wewe Ukiwa katika kazi Maalum, Hukuona sababu kuuliza Kwa Bwire ni wapi Walipanga Kufanya Uhalifu
Shahidi: Mimi siyo Kazi Maalum
Kibatala: Kwani aliyetafuta Vijana ni Polisi au wewe?
Shahidi: Mimi
Kibatala: Mbowe aliomba Polisi wamtafutie Vijana?
Shahidi: Hapana
Shahidi: Bwire Hakuniambia
Kibatala: Katika Ushahidi Wako hujui wala hujazungumzia Kuhusu Milestone, Kokoriko na Triple B
Shahidi: Sijazungumzia
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Walikamatwa kwa tuhuma za Kupanga Kufanya Uhalifu wa Kumdhuru Sabaya
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Ni kweli Uliwatafuta Vijana Kwa ajili ya Kufanya Ukamataji kabla ya Uhalifu haujatokea
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Bado Hukuona Sababu ya Kumuuliza Bwire
Shahidi: Polisi Walitakiwa Wafanye Uchunguzi Wao
Kibatala: Kwani nani aliyemtafuta Adamoo
Shahidi: Ni mimi
Kibatala: Kwani nani alikuwa anaaminiwa na Adamoo kati yako na Polisi
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: akuna Taarifa a kwamba siku za Adamoo na Ling'wenya Wanakamatwa walikuwa wanapokea Taarifa Kutoka kwa Msiri wao, Je huyo Msiri ni wewe
Shahidi: Siyo Mimi
Kibatala: Je Kwa Ufahamu Wako palikuwa na amtu Mwingine aliyekuwa anatoa Taarifa kwa DCI na Kingai
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Kwa Ufahamu Wako wewe Kuna mtu Mwingine ambaye alikuwa anawajua Adamoo na Ling'wenya
Shahidi: Hapana
Kibatala: Unafahamu Kwamba Adamoo na Ling'wenya Siku Wanakamatwa pale Rau Madukani walikuwa wanafanya nini.
Shahidi: Wala sijui Kama Walikamatwa Rau Madukani
Kibatala: Unafahamu a kwamba pale Rau Madukani Mohammed Ling'wenya alikuwa na Dada yake anaitwa Athima
Shahidi: Sifahamu, Hakuwahi kuniambia
Kibatala: Wewe Hukumu uliza Bwire
Shahidi: Sikumuuliza
Kibatala: Ulikuwa unafahamu Kwamba Moses Lijenje ana Dada yake anaishi Arusha
Shahidi: Hapana Sijui
Kibatala: Na wala Msiri wao unasema Siyo wewe
Shahidi; Siyo Mimi
Kibatala: Kuna sehemu katika maelezo yako Uliandika "Nilimpatia ACP kingai Namba za Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya aweze Kuwa fuatilia" ni sahihi
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Swala la Kwamba ACP kingai alikuwa namba za watu Watatu Mpaka Siku wanakamatwa, Je uliliongelea.?
Shahidi: Sikuongelea
Kibatala: Ni Suala la Kuwapa namba za Simu ni Swala la Muhimu au siyo la Muhimu
Shahidi: Ni suala la Muhimu
Kibatala: Unafahamu kwanini Kingai Wala Mtu Mwingine yoyote Hakuna anaye zungumzia Swala la Wewe Kuwapa namba za Simu kabla
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Swala la Kingai Kuwa na namba za Simu za Watu hawa Zina Implication gani Katika Uchunguzi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Mashahidi ambao Wamekutangulia, Walikuwa Wanamtafuta Lijenje Manually wakati Wana namba zao za simu
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba hata baada ya Watu hawa kukamatwa Kingai hakufanya chochote Katika Kuwafahamisha Wapendwa Wao
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: Wakati Wa Tarehe 12 August 2020 Ulisema Ulimkabidhi Inspector Swila na kuandikishwa ID02
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Mwanzo Ukasema Kwamba Wakati Unamkabidhi Simu yako Ulitoa Line ya Vodacom ambayo ilikuwa na Mawasiliano yako na Watu Wengine
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Kwahiyo wewe Ulimkabidhi Inspector Swila Simu bila Sim card
Shahidi: Nilitoa ya vodacom ni kabakisha Moja
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Sim Card ya Vodacom,ulirudisha lini.?
Kibatala: Katika Nyaraka ipi Tukiangalia Tutaona Mlikabidhiana Sim Card ya Vodacom na Inspector Swila
Shahidi: Ipo
Kibatala: Ipo hapa Mahakamani
Shahidi: Hapana, Hapa Mahakamani Haipo
Kibatala: Ipo wapi
Shahidi: Sikujua Kama Inahitajika Mahakamani
Kibatala: Ile Simu ya Tecno Uliyowasha hapa, Ina SimCard ndani
Shahidi: Sikukagua kama ina Sim Card ndani
Kibatala: aliye sema Kwamba Ile simu ina Sim Card ndani ni nani
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: nikuombee utuonyeshe sim Card
Shahidi: Vyovyote Vile itakayokuwa
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo P34
Kibatala: haya Fungua utuonyeshe humo ndani Kuna Sim Card ya Mtandao gani
Shahidi anafungua
Shahidi: HAKUNA LINE HATA MOJA (SimCard)
Kibatala: Unafahamu thamani ya Kiapo chako
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba unawajibu wa Kulinda hadhi ya Jeshi la Wananchi Tanzania
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Ukweli na Uongo wako Unapimwa Katika Vitu Vidogo Vidogo Kama hivyo
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Nakuuliza tena, Wakati Unakabidhi Inspector Swila Simu Ilikuwa na Sim Card au Haina Sim Card
Shahidi: Ilikuwa na Sim Card
Kibatala: Unafahamu kwamba SimCard imepelekwa Wapi
Shahidi: Ilikuwa na Line ya Airtel Iliyobakia, Sifahamu Ipo wapi
Kibatala: Ile Sim Card Ya Vodacom na Zile simu zingine 3, katika Maelezo Yako ya Tarehe 12 August 2020 Ulizungumzia Katika Maelezo yako?
Shahidi: Sikuandika katika Maelezo Yangu
Kibatala: sisi tuna thibitisha Wapi Kwamba Ulikabidhi hizo Simu 3 wakati hazipo katika Maelezo yako wala Hakuna Hati ya Makabidhiano
Shahidi: lakini zipo Hapa Mahakamani
Kibatala: Ungekuwa Polisi Nimgekuuliza Unafahamu Chain of Custody wewe, ila wewe Afisa wa Jeshi Nitakuonea
Kibatala: Unafahamu Kwamba Hizo Simu 3 Zina Mahusiano na Kesi Hapa Mahakamani
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Je Ulimwambia Jaji Kwamba Zile simu zingine Mbili Kule Morogoro ulimwachi nani na Zilikuwa Chini ya Uangalizi wa nani
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Wala Hukumwambia Jaji Kama huko Ulipoziacha Zina password au hazina
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Je unafahamu Kwa nini yule aliyekwambia ulete Simu 3 Kesho yake, hajazungumzia chochote Kuhusu hizo Simu 3
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu au hufahamu Kwamba Freeman Mbowe alikuwa na Kaka wa Damu, Generali ambaye katika Kifo cha huyo Generali Rais Magufuli alienda kwa Mbowe Kumpa pole
Shahidi: Nilisikia
Kibatala: Na unataka tukubali sisi watu wazima Kuwa aliacha Ndugu yake wa damu aliyenyonya naye ziwe Moja akutafute wewe?
Shahidi: Yule si alishastaafu
Kibatala: alistaafu lini
Shahidi: Sijui
Kibatala: Kati ya Wewe Luteni uliye kazini na Generali ambaye amestaafu nani anawafahamu Watu wengi Jeshini Waliopo na Waliotangulia?
Shahidi: Jenerali
Kibatala: Unasema Siku ya Kwanza Mbowe alikutafuta Siku ya Kwanza, Ukashangaa
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Kitendo Cha Mtu wa Kukupigia Simu bila Ridhaa Yako unaweza kutolea Taarifa
Shahidi: Rudia Swali
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Kitendo Cha Mtu wa Kukupigia Simu Mtu Muhimu Kama wewe bila Ridhaa Yako unaweza kutolea Taarifa
Shahidi: Kwanza Mimi siyo Mtu Muhimu
Kibatala: Wacha Jaji aandike Kuwa wewe siyo Mtu Muhimu
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Kitendo Cha Mtu wa Kukupigia Simu bila Ridhaa Yako unaweza kutolea Taarifa
Shahidi: Siyo Utamaduni Wetu
Kibatala: Je ulitoa Taarifa Jeshini Kwamba Kiongozi Wa Chama Cha Upinzani Chadema Kakutafuta
Shahidi: Sikutoa
Kibatala: Kwenye Maelezo Yako Ulisema Kuwa Mliendelea Kuwasiliana naye kwa sababu wewe na Yeye Wote ni Kabila Moja
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Kwa hiyo hili la Ukabila ndiyo Kilikufanya uendelee Kuwasiliana na Mbowe
Shahidi: Hapana ni Mawasiliano
Kibatala: si Ndiyo Mawasiliano na Mwenyekiti wa Chadema wakati wewe Umesema hamfungamani na Chama Chochote
Shahidi: Mbowe ni Mbowe na Chadema ni Chadema
Kibatala: Kwanini sasa Katika Maelezo yako unasema "Freeman Mbowe Mwenyekiti Wa Chadema"
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: hapo ulimtenganisha Mbowe na Chadema?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Shahidi Ushahidi Wako Unasema Kwamba TSh 500,000 ulitoa TSh 300,000 Ikabakia TSh 200,000, Ukawapa Adamoo Ling'wenya TSh 199,000
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: katika Maelezo yako Uliandika Kwamba Mhe Mbowe alikumbushia Kuhusu Vijana, ukamwambia Kuwa wamepatikana 2
Kibatala: kwa hiyo wewe Kwa Maelezo Yako Ulisema Tarehe 20 July 2020 alinitumia Laki TSh 500,000 nikatoa TSh 300,000 Laki 2 Ikabakia Kwenye simu
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Katika Maelezo Hakuna Mahala Ulisema Uki Alisha TSh 200,000 Kwenye simu
Shahidi: Hakuna nilipoandika
Kibatala: Alikwambia Inspector Swila Maana ya haya Maelezo
Shahidi: Hakuniambia
Kibatala: Baada ya Siku Chache wapatikama Vijana Wawili nikawapatia TSh 195,000
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Maelezo yako na unachosema Kwenye Kizimba Vinafanana au Vinatofautiana?
Shahidi: Vinatofautiana
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba P 1 na P 13
Kibatala: Nimeshika hapa Maelezo ya Onyo ya Adam Kasekwa ambayo Wenzetu Wanasema alikiri
Kibatala: Katika Ushahidi Wako, Unasema Uliwapa Tsh 195,000 katika TSh 199,000 Uliyotumiwa, Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba TSh 4,000 Ilienda wapi
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Kwa hiyo TSh 4,000 ya Ugaidi hujasema Ipo wapi
Shahidi: SIYO YA UGAIDI, BALI YA KUWASAFIRISHA
Kibatala: kwa hiyo Wenzetu Wanasema Yote TSh 199,000 ilitumika Kwenye Ugaidi, Kumbe siyo Ugaidi
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Kibatala: Maelezo haya yanasema kuwa alipokea TSh 87,000 kila Mmoja, Je Ni kweli au si Kweli
Shahidi: Sikumpatia Mtu Mmoja Mmoja, Niliwapa Kwa Pamoja
Kibatala: Kama Adam Kasekwa kasema Walipewa TSh 87,000, Atakuwa Kasema Uongo
Shahidi: atakuwa kasema Uongo
Kibatala: Unakubaliana Kuwa 87,000 Mara Mbili ni TSh 174,000? Unakubali unakataa
Shahidi: amount hiyo Mimi sijui
Kibatala: Nakuuliza kimahesabu 87,000 Mara Mbili ni TSh 174,000
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Adam Kasekwa anasema Jumla Uliwapa Tsh 174,000, Wewe Unasema TSh 195,000, Je Inatofautiana
Shahidi: Inatofautiana
Kibatala: Na Adam Kasekwa anasema Kwamba Fedha hiyo Uliyotumiwa na Mbowe ilikuwa ni Kuwarejeshea (Refund) ni sahihi au Siyo Sahihi
Shahidi: Ni sahihi
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba na sisi tuwe tunaangalia Kama Maelezo yapo Sahihi
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Pia awe anasoma Kile ambacho Kimeandikwa Kwa Mfano Hakuna Sehemu imeandikwa TSh 174,000 lakini Kuna TSh 87,000
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Sasa Kwa Majibu Kuhusu Majibu ya Kielelezo P 1 yaondoke
Kibatala: Ni sawa tufute Mstari Mmoja halafu tuanze Upya
Kibatala: Sasa Nilikuwa nakuuliza awali shahidi Kuhusu Maelezo yako inasema hivi, Baada ya Siku Mbili Waliopatikana Vijana Wawili Adamoo na Ling'wenya Ambao Niliwapatia TSh 195,000, tulipo kutana Eneo la Msavu
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Kwa hiyo Ni sahihi Kwamba hiyo Tsh 195,000, Kwamba Uliwapatia Kama Gharama ya Nauli zao Kutoka Walipo toka Kuja Morogoro
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Walipo kuja Morogoro Kutoka Walipo toka Uliwapa Tsh 195,000 kwa Ujumla au Lah.
Shahidi: Niliwapa Kwa Ujumla
Kibatala: Adam Kasekwa anasema Walikuja na Ling'wenya, "kwa kutumia Simu ya Mke wangu, Alinipigia Kuna kazi ya VIP PROTECTION, Maelezo sahihi anayo Luteni Urio"
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: anasema "alitupatia Kila Mmoja TSh 87,000 Kwa Maelezo ya Ling'wenya"
Shahidi: sahihi
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Fedha zote hizo ilikuwa kwa ajili ya Refund
Shahidi: Ilikuwa kwa ajili ya Kuwafidia
Kibatala: Safi sana
Kibatala: Unakumbuka Ulisema Kwamba Uliwapa Nauli ya kwenda Wapi Adamoo na Ling'wenya Kutoka Morogoro
Shahidi: Niliwapa Cash Tsh 195,000, ila Sikumbuki niliwapatena TSh ngapi
Kibatala: Ni sahihi Kwamba ile 199,000 Iliyotuma Baadae ndiyo Uliwapa Nauli ili waende Kwa Mbowe
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unafahamu Katika Maelezo Yake Adam Kasekwa, Katika Ukurasa wa Nne Mstari ya Mwisho, ni kila Mtu Kufika Moshi.. Wewe Unasema Walikwenda Dar es Salaam Kukutana na Mbowe, Je Statement hii Inafanana au inatofautiana?
Shahidi: Inatofautiana
Kibatala: nimeshila Maelezo ya Mohammed Ling'wenya Kielelezo namba P13, anasema kuwa "Baada ya mazungumzo Luteni Urio Aliniuliza Kuwa Mshahara wa Mtwara TSh ngapi, Nika jibu ni posho ya Elfu 15 kwa Siku, Basi Luteni Urio akanishauri Mshahara uwe Kuanzia TSh 800,000"
Je, ni sahihi Kwamba Ulimshauri Kuhusu Mshahara
Shahidi: Hapana
Kibatala: anaendelea Kusema Kuwa "alitupatia TSh 190,000 nauli ya kwenda Moshi"... Je ni sawa au zinatofautiana na Maelezo yako
Shahidi: tofauti, Pia tofauti hata na Ile ya Adamoo
Kibatala: You're Very Smart
Kibatala: Ling'wenya anazungumzia TSh 190,000, wewe unazungumzia TSh 199,000, Kuna tofauti ya TSh 9000
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unakubaliana na Mimi Kuwa Wapokeajo wa hizi pesa wanasema Kuwa Matumizi Yake yalikuwa siyo Ugaidi bali nauli
Shahidi: Sikubaliani na wewe
Kibatala: Kwani wewe Umesikia Wao wanasema Kwamba ile Fedha ilikuwa kwa ajili ya Nini, Adama Kasekwa Si kwa ajili ya Refund na Mohamed Ling'wenya ilikuwa kwa ajili ya Kwenda Moshi?
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Hapa Walikuwa wamekutana na Mbowe?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Walikuwa bado hawajafanya Ugaidi
Shahidi: Walikuwa ndiyo hawajafanya Ugaidi
Kibatala: Unafahamu kwamba wenzio Wanasema Hizo TSh 199,000 Mbowe zilifadhili ugaidi?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: ooh! Kumbe hata wenzako wamekuficha?
Kibatala: Ling'wenya nasema pia alipewa pesa akanunue Mavazi, Ni kweli
Shahidi: Si Kweli
Kibatala: Kwamba wewe unasema Ling'wenya alipewa pesa ya Kwenda Dar es Salaam, Yeye anasema Kwenda Moshi, Mmetofautiana..?
Shahidi: Ni sahihi tumetofautiana
Kibatala: eneo lingine Mlilotofautiana Ling'wenya anasema alipewa pesa ya Kurejeshwe Nauli wewe Unasema Nauli ya kwenda Dar es Salaam
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Nipewe Kielelezo Namba P 26
Kibatala: Ni kweli Kwamba Mbowe alikwambia umtafutie Ex commandos bila Kikomo
Shahidi: Hakuniambia Idadi yeye alisema Wao Waje tu
Kibatala: Kwenye Kielelezo P26, Ni sahihi Kwamba Kwa Mujibu wa Tarehe 20 July 2020 Saa 1 na Dakika 39 yeye Mbowe anasemaje
Shahidi: "Kaka Wale Mtu tatu au Nne ni Muhimu sana"
Shahidi: Lakini kabla ya hiyo Meseji Kuna Mawasiliano ya Simu
Kibatala: Yapo wapi
Shahidi: Hayapo hapo
Kibatala: Soma Kama Ilivyo, Kwa Mujibu Wa Meseji hiyo Mbowe anauliza Watu wangapi
Shahidi: Kaka Wale Mtu tatu au Nne ni Muhimu
Kibatala: kwa hiyo Namba hapo ni 3 au 4
Shahidi: Ndiyo Waliopatikana
Kibatala: Nenda Kwenye Meseji ya Tarehe 20 July 2020 Saa 2 na Dakika 3 na sekumde 30, Nani katuma hiyo Meseji
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: Unafahamu hiyo namba hapo
Shahidi: naona Meseji Kwemda Kwa Mbowe tu
Kibatala: kwa ni Meseji hiyo Uliyotuma hiyo Meseji Kwenda Kwa Mbowe, Je ni Namba ipi ya simu
Shahidi: Nilitumia Mtandao Wa Telegram
Kibatala: Mtandao Wa Telegram Unapotumia unahitaji Mtandao
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Namba Uliyotumia Mtandao huo wa Telegram ni namba ipi
Shahidi anaangua kichekoo ghafla hapa.....
Kibatala: Shahidi Usiche, Ndiyo Maana nilikwambia The Truth Shall set you Free.. Mwambie Mheshimiwa Jaji namba yako ipo au haipo
Shahidi: Haipo
Kibatala: Soma Katika Extraction Report hapo Wanasema Namba gani hiyo
Shahidi: 1130138344 DENIS OWNER
Kibatala: Namba hiyo Unaifahamu au huifahamu
Shahidi Sifahamu
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Shahidi apewe nafasi ya Kutoa Ufafanuzi
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Wakili anataka Kufanya Submission Muda huu, asubirie Kwenye Re: examination, Swali langu Je Shahidi anaifahamu namba au haifahamu?
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Kama anataka Kuuliza namba, Ni Vizuri Shahidi afafanue tu
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji mimi naona Kuna tatizo na Line
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Wametoa OBJECTION Nime re-battle, Wao Wafanye rejoinder siyo Mr. Kidando atoe Hoja mpya..
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Kwenye Rekodi za Mahakama Aliyetoa Kielelezo hicho ni Inspector Ndowo, Hatuoni Haki Kwa shahidi Kuulizwa Kielelezo hicho, Si Sawa kuzuiwa Kutoa Maelezo
Jaji: Kama nimesikia Vizuri Mr. Kibatala alikuwa anauliza Kuwa Shahidi anaifahamu au haifahamu hiyo namba, Mimi sijasikia akijibu hilo swali, alipotaka Kufanya Kufafanua Ndiyo Mr Kibatala akakataa, sasa hayo atamueleza Wakili Wake
Jaji: Ni Sahihi Kwa Shahidi Kujibu Maswali anayo Ulizwa na Wakili tu..
Kibatala: Shahidi Hiyo namba Unaifahamu au haifahamu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Wakati Wa Ushahidi Wako Kuna Wakili yoyote alikwambia Fafanua
Shahidi: Hapana
Kibatala: Unafahamu Juu ya Application inaitwa Free Sms
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Ni application ambayo unatuma Meseji halafu pia unaweka namba kwa namba yako na Kuweka ya mtu unaye mtumia
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kuna wakili yoyote aliyekuuliza Kuhusu Free Sms
Shahidi: Hakuna
Kibatala: na Hakuna Wakili yoyote amekuomgoza Kuitambua hiyo Free Sms ilikuondoa hiyo dhana
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Soma, Hapo, Kuna Maelezo Unasema su siyo Salama Sana, Niwezeshe ili tuweze Kukutana
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Kuna Sehemu Yoyote Katika Kielelezo namba P 34 ambayo Freeman Mbowe amekueleza wewe Kwamba Mtumie Njia ya Mawasiliano Mbadala Kwa Sababu Simu Siyo Salama
Shahidi: Meseji ya Mwisho
Kibatala: haya tusomee
Shahidi: "Hellow Bro Nilishindwa Kupokea Simu yako Sababu Deshi Deshi"
Kibatala: kwa hiyo kwa Tafsiri yako Ndiyo Kasema kuwa Simu Siyo Salama
Shahidi: Ndiyo Nilivyo Tafsiri
Kibatala: Katika hiyo Meseji ya Mwisho Kuna Neno simu siyo Salama
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Taja namba ya Mbowe Katika hiyo Meseji ya Mwisho
Shahidi: 0713933386
Kibatala: Soma Sasa Katika Kielelezo Kama hizo Meseji zinafanana au Tofauti
Shahidi: Zinafanana
Kibatala: Sasa soma namba ambayo ipo katika Kielelezo namba P 26 Meseji hiyo hiyo
Shahidi: Inatoka namba 729414989
Kibatala: ambayo ni Namba ya nani
Shahidi: FREE
Kibatala: Je namba ULIYOSOMA Mwanzo na Sasa hivi zinafanana.?
Shahidi: Hapana hazifanani
Kibatala: Kuna tofauti eeeeh!?
Shahidi: Ndiyo Kuna tofauti
Kibatala: Kubwa au Ndogo
Shahidi: Kubwa
Kibatala: Uliongozwa Kufafanua hiyo Tofauti
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Tafuta Meseji ya Tarehe 20 July 2020, Saa 2 na Dakika 15 na Sekunde 54
Shahidi: "Naomba nitumie nauli ya Ku' mobilise nikutane nao Moro"
Kibatala: Nani alikuwa anaomba nauli
Shahidi: Mimi ndiye niliye kuwa naomba nauli
Kibatala: Kwa hiyo DENIS URIO ndiye aliye Omba nauli kwa ajili ya Kuwa Mobilise
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Baada ya wewe kuomba nauli ndiyo Mbowe sasa akatuma TSh 500,000
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Nitafutie Meseji yoyote ambayo Mbowe anatoa wazo yeye la kutuma yeye TSh 500,000
Shahidi ametumia dakika 1 kutafuta hapa..
Shahidi: HAKUNA
Kibatala: Ni nani kwa mujibu wa Kielelezo namba P 34 (Simu) aliye propose kuwa pesa ya Ku'. obilise iwe TSh 500,000?
Shahidi: Mimi Denis Urio
Kibatala: Kwa Mujibu Wa Meseji ya Tarehe Ngapi na Mwezi wa Ngapi ambayo wewe ndiyo Mtoa wazo
Shahidi: Meseji ya Tarehe 20 July 2020 Saa 2 na Dakika 19 na Sekunde 53
Kibatala: ambayo Meseji hiyo wewe Ulituma Kutoka Kwenye namba gani ya Kwako
Shahidi: Haionekani namba
Kibatala: ONGEZA SAUTI
Shahidi: Haionekani namba
Kibatala: Tafuta Meseji ya Tarehe 20 July 2020 Saa 2 na Dakika 24 na Sekunde 02
Shahidi: "Usiwe unatumia namba yako Kutuma Pesa, Tumia Wasaidizi Wako au Wakala Kutuma"
Kibatala: Ni nani aliyetuma Meseji hii
Shahidi: Mimi Denis Urio
Kibatala: Nikumbushe Kule Kwa DCI na Kingai Uliambiwa Jambo gani Vile
Shahidi: Kuwapeleka Watu
Kibatala: Ni sahihi Katika Maelezo Yako uliyo andika, Uliambiwa Uendelee na kazi ya kumtufutia Vijana na Kuku Sanya Ushahidi
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Hao Wasaidizi Wa Mbowe Washa wahi Kukutumia pesa
Shahidi: Hapana
Kibatala: Katika Mawasiliano yako na Mbowe Uliwahi kutajiwa au Kupatiwa Fedha Kufanya Muamala na Mtu anaitwa Willy Kijana wa Mbowe? Na Wily alikutumia TSh ngapi
Shahidi: 199,000
Kibatala: Ndiyo Fedha ambazo Uliwapa Adamoo na Ling'wenya
Shahidi: Ndiyo hiyo
Kibatala: Swali la Mwisho kabla ya Lunch
Kibatala: Hiyo namba ya Willy ambayo ilituma hiyo Fedha ya TSh 199,000, Uliwapa akina DCI na Kingai
Shahidi: Haikuja namba, Alinitumia namba baadae
Kibatala: Hiyo namba hata Ka Ulipewa baadae, Ulimpa DCI au Kingai
Shahidi: Sikumpa
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba Kama Wenzangu wataridhia tupate Health Break baadae tuendelee na Cross Examination, Naomba pia nirudishe Vielelezo
Jaji: nahairisha Kwa Dakika 45 Mpaka Saa 7 na Dakika 45 ambapo Shahidi ataendelea Kutoa Ushahidi
Jaji: anatoka Mahakamani
*******************************
Mahakama imerejea. Muda ni saa 8:07
Jaji amerejea mahakamani.
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Ikupendeze Mheshimiwa Jaji Quorum ya Upande Wa Jamhuri ipo Ka Ilipokuwa Mwanzoni
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji na sisi Kwa Upande Wetu Quorum yetu ipo Kama Ilivyo kuwa awali, Tupo tayari Kuendelea
Jaji: Shahidi nakukumbusha tena Kuhusu Kiapo chako, Utaendelea Kutoa Ushahidi Chini ya Kiapo
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba kwa Hisani tukumbushwe Jibu la Mwisho
Jaji: kama alimpa DCI na Kingai Namba ya Willy
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kumpa Shahidi Kielelezo namba P34
Shahidi: anapewa Kielelezo ambacho ni simu
Kibatala: Shahidi Ni sahihi Kwamba meseji ya Tarehe 22 July 2020 Saa 3 na Dakika 19 Sekunde 30
Shahidi: "Namba ya Dereva Wangu anaitwa Willy, Wamtafute yeye"
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Kielelezo namba P 26 Saa 9 na Dakika 30 Sekunde 45 ulipokea hiyo namba
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: na Wewe Saa 9 na Dakika 36 na Sekunde 39 ukasema " Nimepata namba, Nitawapa"
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Hao unaosema utawapa ndiyo akina Khalfani..?
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Niomyeshe Meseji ambayo Inaonyesha Kwamba Mbowe alituma namba Pele yake Kama Meseji
Shahidi: alituma lakini hapa Haipo
Kibatala: Ipo wapi
Shahidi: alituma Kwa Meseji ya Kawaida, au Sikumbuki Kama alituma wapi
Kibatala: Ipo wapi
Shahidi: Sikumbuki ipo wapi
Kibatala: Kama Nakumbuka Vizuri wewe hujawahi Kukutana na Willy
Shahidi: Sijawahi Kukutana naye
Kibatala: Tu assume Kama Mambo yalivyotokea, Je Freeman Mbowe aliluomba umtafutie Walinzi au Magaidi
Shahidi: Kwa hao nilikuwa namtafuta Watu Wa Kwenda Kufanya kazi ya Ulinzi
Kibatala: Yeye Mbowe alitaja Walinzi au hakutaja
Shahidi: Alitaja Walinzi
Kibatala: Ndiyo Maana wewe Uliwatafuta watu wa kwenda Kufanya Ulinzi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mbowe alikwambia ukionana nao Uwaambie hivi na Vile?
Shahidi: Hapana
Kibatala: aliye, waambia Kuwa Mnaenda Kufanya Kazi ya Ulinzi ni wewe
Shahidi: Ndiyo ni Mimi
Kibatala: Wakina Inspector Swila Walikwambia Kuwa actually Unatakiwa uwe Mshtakiwa namba Moja au namba Mbili
Shahidi: Hawajawahi Kuniambia
Kibatala: DCI au Kingai Walikwambia Kuwa Watakupatia Kinga Dhidi Ya Mashtaka?
Shahidi: Hawajawahi Kuniambia
Kibatala: Tarehe 22 July 2020 Saa 6 Na Dakika 27 na Sekunde 23 Soma
Shahidi: "Kama Ikikupendeza uwe unanitumia Pesa ya Kutosha kwa ajili ya Kuwa Mobilise kwa ajili ya Kuwafanyia Vetting"
Kibatala: Nani Katuma hiyo Meseji
Shahidi: Ni Mimi Denis Urio
Kibatala: Wakati Unatuma Meseji hii, Khalfani Bwire na Moses Lijenje Walikuwa wameshakwenda Kwa Mbowe?
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Katika Kukamilisha zoezi la Kutafuta Vijana hao ambao Hakutaja Kikomo, Freeman Mbowe alinitumia TSh 500,000, Ambapo nilizitoa, Je Kwa Maelezo Haya si ni Kwamba Ulitoa Laki 5 kwa Mkupuo Wa Pamoja
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Maelezo Yako Ya Ushahidi Wako na Maelezo Yako ya statement Vinapishana au Kuna vinaendana
Shahidi: vinaendana ila tofauti Kwenye Tafsiri tuh, (anaonyesha Kwa Mikono)
Kibatala: Sasa nakurudisha Kwenye Meseji
Kibatala: Ni sahihi Kwa Meseji hii Ulikuwa Unaomba Pesa za Ziada Kwa Freeman Mbowe?
Shahidi: Ni sahihi Ili Kufanya Mambo kwa Urahisi
Kibatala: Ulikuwa Unaomba Pesa za Ziada Kwa Mtu ambaye bila Shaka Unafahamu Kwamba ana Mipango ya Ugaidi
Shahidi: Ndiyo nafahamu, Kwa Kuwawezesha Watu aliokuwa anawahitaji,
Kibatala: Si Ndiyo Watu ambao alikuwa anataka Kuwatoa Kwa Ugaidi?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unafahamu Kuhusu Neno SOLICIT
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa Clarity wakati Unatuma Meseji Kwamba awe anatuma pesa za Kutosha ulikuwa Umeshapokea TSh 500,000
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwa hiyo awe anatuma pesa zaidi ya 500,000 sasa
Shahidi: Ni sahihi Kwa Kadiri Itakavyo Mpendeza
Kibatala: Ulisema Kwamba Kila ulikuwa unamfahamisha Kingai
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Katika Simu hiyo Kuna Meseji za Kumtaarifu Kingai Kuhusu Kutumia TSh 500,000
Shahidi: Hakuna, Ni kuwa naongea naye kwa simu
Kibatala: Je Kuna Meseji ya Mhamala Wa TSh 500,000 Ulitumia Kingai Kwenye Njia ya Meseji Kuonyesha Kingai kama Ushahidi
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Tarehe hiyo Hapo Ulimsalimia Mtuhumiwa Wa Ugaidi Shikamoo Mkuu, Ani sahihi
Shahidi: Sikuwa na Ugomvi naye
Kibatala: Mtu akiwa Adui wa Nchi yako si ni Adui Yako
Shahidi: Sikuwa na Ugomvi naye
Kibatala: Unasema Tarehe 04 August 2020 Khalfani Bwire alikupigia kuwa Adamoo na Ling'wenya Wapo Moshi Kumdhuru Sabaya
Shahidi: Tuweke Vizuri, Mimi ndiye niliye Mpigia kisha akanipigia
Kibatala: Kwa Maelezo yako Khalfani Bwire alikuwa Dar es Salaam au Moshi
Shahidi: alisema Kwamba Wale Madogo Wapo Moshi, sikujua yeye Yupo wapi
Kibatala: Kwa Maelezo Yako wewe Ka. Luten Wa Jeshi, Maelezo Yako Ya Wale Madogo Wapo Moshi, Ulitafsiri kuwa Bwire hayupo Moshi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Katika Maelezo Yako Kuna Maelezo Wale madogo wapo Moshi
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Maelezo Mnamo tarehe 04 August 2020 Khalfani Bwire alinijulisha Wapo Moshi Kumdhuru Sabaya, Kwani Tarehe 12 August 2020 Wanatakiwa Kurudi Dar es Salaam, Je Bwire bado yupo Dar es Salaam
Shahidi: Kwa Mtazamo wangu Mimi
Kibatala: Katika Statement hii Kuna Mahala Popote umeandika Kwamba Bwire yupo Dar es Salaam
Shahidi: sikuandika
Kibatala: Kwanini Huku andika Kwamba Bwire alikuwa Yupo Dar es Salaam
Shahidi: hakunitajia Location
Kibatala: Katika Maelezo Yako Mstari Wa Kwanza, Unasema "Nakumbuka Mwaka 2008 Nilikutana na Freeman Mbowe, Kwakuwa wote ni Kabila Moja, Mimi na Freeman Mbowe tumekutana tena CASA Motel kwa Maongezi". Je Neno Kukutana naye tena, Ni Mara ya Kwanza.?
Shahidi: Miye ndiyo Nilikutana naye Kwa Mara ya Kwanza
Kibatala: Lakini haya ni Maelezo yako Uliyosoma Na Kuyathibitisha..
Kibatala: Ni sahihi Kwamba kabla ya Kukutana naye ana kwa ana alikuwa anakutakia Heri za Sikukuu na Event Mbalimbali
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Ni sahihi Moja ya Njia ambayo Freeman Mbowe mnawasiliana alikutumia Pongezi za Maonyesho Ya Sherehe ya Muungano
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Mtu ambaye anatuma Ujumbe wa Pongezi Kwa niaba ya JWTZ, Kutokana na Maonyesho ya Muungano.. Ni Mzalendo au Jahiri
Shahidi: Kwa Kipindi Kile niliona Mzalendo
Kibatala: Katika Ushahidi Wako ulitoa Katika Kizimba Ulisema Kwamba Freeman Mbowe ndiye alikuta futa Mara Mliyopelekea Kukutana katika Mambo ya Ugaidi
Shahidi: yeye ndiye alinitafuta
Kibatala: alikutafuta Kwa Njia ipi
Shahidi: Kupitia Kwa namba za Watu wengine
Kibatala: Namba ambazo alikuwa anazitumia Uliwapa DCI na Kingai
Shahidi: Si Kuwapa
Kibatala: Ulizitolea Vipi Maelezo na Namba ambazo huzijui
Shahidi: Sikutoa sababu Nilikuwa sizijui
Kibatala: Mpaka unaenda Kuona Mbowe akakwambia Ishu za Ugaidi, Nani alimtafuta Mwenzie
Shahidi: Mimi Ndiye nilimtafuta, Akakuta Missed Call akanirudia Jioni
Kibatala: Kwa hiyo ambaye Ali prompt Kuonana, Siyo wewe ni simu ya Mbowe
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Kibatala: Nani aliye andika Kwamba Mwezi July Tarehe za katikati nilimtafuta ili tuweze Kuonana, Nani Kasa haya Maelezo
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: Narudia tena Kusoma
Kibatala: Kuna Eneo lolote ambalo Palikuwa na Missed Call na Baadae auka Return Call.?
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Je Kuna tofauti kati ya Maelezo na Unachosema Kizimbani
Shahidi: Ndiyo Tofauti Zipo
Kibatala: Katika Maelezo Yako, Kuna Maelezo yoyote Kwamba Ulipo Mpigia Simu DCI , Kuna Maelezo Kwamba Ulijitambulisha Kwake in fully
Shahidi: Nilitijambulisha
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kama Wenzangu hawatokuwa na Pingamizi naomba Wanipe nimuonyeshe Shahidi Maelezo yake, Kama ni Foundation nimefanya hivyo Kwa Zaidi ya Masaa Mawili
Kibatala: Shika hayo Maelezo Kwa Dakika 2 au 3 Kwamba Ulipo Mpigia Simu DCI Ulimpigia na Kujitambulisha Kuwa wewe ni Afisa wa Jeshi na Maelezo Yako yote
Jaji: Kanuni zinasemaje Kabla hajatafuta
Kibatala: Sawa Mheshimiwa Jaji Asante,
Shahidi Si Unaifahamu hiyo Statement
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Sasa Shika hayo Maelezo Kwa Dakika 2 au 3 Kwamba Ulipo Mpigia Simu DCI Ulimpigia na Kujitambulisha Kuwa wewe ni Afisa wa Jeshi na Maelezo Yako yote
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Ushahidi Wako na Hayo Maelezo hilo Eneo Kuna tofautiana au hapatofautiani
Shahidi: Kwenye hilo Eneo ni tofauti
Kibatala: Kwenye Maelezo Yako Ukisoma hapo, Kuhusu Pongezi ya JWTZ
Shahidi: Ni Meseji ya Pongezi
Kibatala: Maelezo hayo Yanatofautiana au hayatofautiani
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Kanuni inasema Kwamba isomwe Kwanza
Kibatala: Baada ya Maelekezo ya Mahakama tafadhali Soma hiyo Statement Yote Kwa Sauti
Shahidi ........ ANASOMA
Shahidi: Nimemaliza
Kibatala: Unakumbuka Nilikuuliza Kwamba unaishi Wapi Ukasema Ngerengere
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa Ngerengere na Kihonda Kuna Umbali Kiasi gani
Shahidi: Ni Mbali sana
Kibatala: Rejea Katika Maelezo Yako hapo Juu, Adress yako unaishi Wapi
Shahidi: Kihonda
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuhusi tofauti hiyo
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Nani alikuwa ana Propose Kuwa Msitumie Simu kwa Sababu Simu Siyo Salama
Shahidi: Mimi
Kibatala: Katika Statement Yako Unasema Mbowe alikwambia Kuwa Telegram Ndiyo Salama
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwenye Meseji Kuna sehemu tumeona Mbowe Kasema hivyo
Shahidi: Kimyaaa
Kibatala: Shahidi haya si Maelezo yako
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Una tatizo tukimpa haya Maelezo Jaji ayatumie katika Kutenda Haki
Shahidi: Hakuna tatizo
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Shahidi Kama alivyo Omba, Tunaomba iingie Kama Kielelezo
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi
Jaji: ni Kielelezo namba Ngapi
Kibatala: Kama Kielelezo namba D4
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji tunaomba tujikumbushe ni Kielelezo namba ngapi
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji ni sahihi Kuwa ni D4
Jaji: Nayapokea Maelezo Haya Kama Kielelezo namba D4 Mawakili wa pande zote mbili wanakubaliana na Uamuzi Jaji kwa Kusimama na Kumuinamia Kidogo
Kibatala: Shahidi Nilikuuliza Kuhusu ile Meseji ya Saa 12 na Dakika 27 na Sekunde 23 Mchana kwa ajili ya Kuwa Mobilise na Kuwafanyia Vetting na Kuwaleta Dar es Salaam
Shahidi: Nimeona
Kibatala: Focus yangu Ilikuwa katika Kuwa Fanyia Vetting, Ni Vetting ya Nini hasa
Shahidi: Kuwa Brief Kwamba Mnaenda Katika Kazi ya Ulinzi na Mkikuta Vitu Kinyume Mnitaarifu
Kibatala: Ndiyo Maana ya Vetting?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Hiyo Meseji Kaandika nani hapo
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: Kwani Mbowe alikuwa anajua kuwa Vetting Yako Ilikuwa inafanyika Vipi
Shahidi: Vetting kama Kufanyia Orientation
Kibatala: Vetting Siyo Kumuangalia Back ground na Kumuangalia Sifa zake Kama Kweli au za Uongo
Shahidi: Sikuwa na Tafsiri hiyo Mimi
Kibatala: Kwa hiyo Kuna Kitu gani ulitaka Kufanya Mpaka Ukataka pesa zaidi?
Shahidi: Ni hiyo Kuwa Orient tu
Kibatala: Bwire na Lijenje Uliwa' Orient au Hukuwa' Orient?
Shahidi: Niliwa' Orient
Kibatala: Sasa Bwire na Lijenje Kuna Mahala walisema Kwamba Pesa haiwatoshi, Mpaka Upate pesa za Ziada.?
Shahidi: pesa ya awali ilishakuwa Consumed tayari
Kibatala: pesa ya Awali Iliyokuwa Consumed ni TSh ngapi
Shahidi: Ni TSh 500,000
Kibatala: Shahidi nataka Kujua bado Kwanini kwenye Meseji Kuna Nyongeza ya Vetting
Shahidi: Ilikuwa Kuwafanyia Orientation
Kibatala: kwa hiyo ni pesa ya Mbowe ndiyo imefadhili Ugaidi halafu Pia Ukatoa Mafunzo Kuwa Wasifanye Ugaidi?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Tarehe 22 July 2020 Saa 8 na Dakika 3 na Sekunde 53 Soma hiyo Meseji
Shahidi: Lakini wewe Usitume kwa namba yako
Kibatala: Nani alituma hiyo meseji
Shahidi: Mimi Denis Urio
Kibatala: Kwanini Ulimtumia Mbowe Taarifa hiyo
Shahidi: Ilikuwa Kuongeza Trust
Kibatala: Lakini Wewe una Maagizo ya DCI ya Kukusanya Ushkabidibkwa Kadri ya Uwezo Wako
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Tarehe 22 July 2020 Saa Saba na Dakika 51 na Sekunde 04
Shahidi: Nimeona
Kibatala: Soma
Shahidi: Pamoja na pesa ya Kula Tuma TSh 200,000
Kibatala: Ilikuwa pesa ya nini
Shahidi: Nauli pamoja na Kula
Kibatala: Tafuta Meseji ya Tarehe 22 July 2020 Saa 5 na Dakika 59, na Sekunde 31
Shahidi: Nimeona
Kibatala: S O M A
Shahidi: Kuna pamoja na Mambo Mengine Kuna Swala la Mishahara
Kibatala: Mishahara Uliyokuwa unazungumzia ilikuwa ya kazi gani
Shahidi: Kufanya Uhalifu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Kutolipa Mishahara ni Kosa la Jinai
Shahidi: Sifahamu Sheria
Kibatala: Pale Kuna sehemu unasema Kuna Masuala ya Utawala Wanauliza na Mishahara, Je Utawala Una manisha nini?
Shahidi: Utawala ni Masuala ya chakula
Kibatala: Utawala ni Chakula tu?
Shahidi: Pamoja na malazi
Kibatala: Watu wanaokwenda Katika Uhalifu Wanatakiwa Kuwa na Administration Obligation?
Shahidi: Ndiyo Kwani hawali, hawalali, hawavai?
Kibatala: Sawa Shahidi, Twende taratibu tu, tutaelewana
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba P20
Kibatala: Kuna Mahala ulikuwa unasa Kwamba Ulikuwa Unawasiliana na Khalfani Bwire kupitia namba 0782 237913 Sasa Nakuonyesha Kielelezo namba P 20 Ni kweli au Siyo Kweli Kwamba Ulituma Kiasi cha TSh 190,000 kutoka 0787 555200 kwenda Kwenye namba 0782 237913
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Ulituma TSh ngapi
Shahidi: TSh 200,000
Kibatala: Sasa Ulisema Kwamba Khalfani Bwire Ulimpa TSh 300,000, Je ulitolea Maelezo Kwa Jaji
Shahidi: Transactions hiyo ya Bwire Sikumbuki na Sijatolea Maelezo
Kibatala: Kuna Mahala fulani ambapo inasemekana Mbowe, Kama sehemu ya Kutekeleza Mpango huo Alitakiwa Kupata Mabomu kutoka Ngerengere!?
Wakili wa Serikali, Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Samahani, Sina Hakika Kama Kuna Mahala Popote ambapo imesemwa hilo..
Kibatala: Wacha wanisaidie Kutafuta, Nitarudi baadae
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji hilo Swala Halipo hata Akitafuta
Kibatala: Nitaliacha hilo, Nitarudi baadae
Kibatala: Kwani shahidi unaweza kulipua bila ya Kuwa na material ya kulipua (vilipuzi?)
Shahidi: huwezi
Kibatala: Ni kweli Kwamba Mbowe alishawahi kukushirikisha kutafuta material ya Kulipua
Shahidi: hajawahi kunishirikisha
Kibatala: Je Katika Ushahidi Wako Uliwahi Kusema Kwamba Khalfani Bwire, Mohammed Ling'wenya na Adam Kasekwa walikuwa na access ya Kupata Milipuko kutoka 92 KJ?
Shahidi: Sijawahi Kusema
Kibatala: Je umewahi Kuzungumzia Kuhusu Bunduki aina ya Bastola aina ya Luger A5340 kuwa ni Standard Bunduki za Makomandoo
Shahidi: Sijawahi Kusema
Kibatala: Ulisema Kwamba Mohammed Ling'wenya baada ya Kufika Kwa Mbowe Tarehe 24 hujawahi Kuzungumza naye
Shahidi: Hapana, Nilimtafuta bila Mafanikio
Kibatala: Je unasema Kwamba Mbowe aliacha Kuwasiliana na wewe Tarehe ngapi
Shahidi: Tarehe 24 July 2020
Kibatala: Kwa hiyo Kwenye Kielelezo namba P 34 Kuna Meseji ambazo Ulimtumia Mbowe Hakujibu?
Shahidi: Zipo
Kibatala: Meseji hizo Ulimuonyesha Mheshimiwa Jaji ambazo hazikujibiwa na Mbowe Kwa Kuongozwa na Mawakili wa Serikali
Shahidi: Sikuonyesha
Kibatala: Vipi Kuhusu Calls, Ulimuonyesha Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Hapana
Kibatala: Kwenye hii Meseji Mbowe anasema sikuona Simu yako Kwa Sababu Deshi Deshi, l hope Umenielewa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: alisema Simu yako au Simu zako
Shahidi: Simu yako
Kibatala: Kwa kuwa wewe Ulikwepo Kwa DCI na Kingai, Nasikia kuwa Kingai aliteuliwa Kama Mpelelezi
Shahidi: Haja wahi Kuniambia kuwa ni Mpelelezi, alisema Taarifa Utampa Kingai
Kibatala: Katika Maelezo Yako Uliwahi Kufahamu Kwamba Inspector Swila Ndiyo Mpelelezi Wa Kesi yako
Shahidi: Hiyo sifahamu
Kibatala: Wala Ufahamu Kwamba Baada ya Inspector Swila Kufungua Faili, DCI alimteua kuwa Mpelelezi wa Kesi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unaweza Kukumbuka Kwamba Mohammed Ling'wenya alikuwa Sudani katika Peace Keeping
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Wakati Unatoa Ushahidi Kambi ya Makomando ipo Ngerengere au Kizuka
Shahidi: Ipo Kizuka
Kibatala: Wakati Wa Maelezo Yako Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kambi ya Komandoo ipo Kizuka
Shahidi: Sikutoa Maelezo
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Wakati upo Sudani Kwenye Peace Keeping Kambi yenu ilikuwa inaitwa KAUBECHE
Shahidi: Inaitwa COLABECHE
Kibatala: Mlipokuwa Sudani, Kiongozi wenu alikuwa Kanali Mbwilo
Shahidi: Hapana ni General Mbwilo
Kibatala: Body Guard Wa huyu Generali Mbwilo yupo hapa Mahakamani
Shahidi: hayupo
Kibatala: Unamfahamu Luteni Omary ambaye alikuwa Sudani
Shahidi: Namfahamu
Kibatala: Je Luteni Msandawe
Shahidi: By Then Namfahamu
Kibatala: Ijumaa Nilikuuliza Maswali Kuhusu namba za Kingai MLIZO badilishana Kwa DCI
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ukasemaje
Shahidi: Niliacha Hotelini
Kibatala: Kwahiyo baada ya Kesi Kuhairishwa Utakuwa Umekuja nayo Leo Diary Yako
Shahidi: Sikuja nayo, Sikuelekezwa na Mahakama
Kibatala: Majibu Kuhusu Pass pale Jeshini Ilikuwaje
Shahidi: Pass ya zaidi ya Wiki Moja napewa Karatasi, Kwenda Katika Ofisi yoyote ninapokwepo.. Pass Chini ya Wiki naandika katika Daftari pale Kambini
Kibatala: Uliulizwa Ukasema Movement Order Ipo wapi
Shahidi: Ipo Hotelini
Kibatala: Wakati Unaitwa Mahakamani Ulipewa Summons au Maboss Zako Walikwambia Unatakiwa kutoa Ushahidi
Shahidi: Nilitoka Kwenye Operesheni Maalum Boss wangu akaniambia kariport kwa DCI
Kibatala: Boss wako anaitwa Nani
Shahidi: Light Kenoth
Kibatala: Ulipo surrender Simu zako zote toka Tarehe 12 August 2020, Ulifafanua Kwa Jaji Kuwa Ulikuwa unatumia Simu gani
Shahidi: Hapana Siku fafanua
Kibatala: Unaweza Kutuambia Kwanini Wewe Kama Mtoa Taarifa Baada ya Kuchukua Simu zako, Hawajawahi Kukupa Simu zako Mpaka
Kibatala: Unakutana nazo tena Hapa Mahakamani
Shahidi: Waliniambia Kuwa Wanafanyia Uchunguzi
Shahidi: Ndiyo Mara ya Mwisho Kama Mwaka Mmoja Umepita nilienda Kuulizia
Shahidi: Kwa Documents walizonipa
Kibatala: ambayo ni Moja
Shahidi: Hapa ninayo Moja lakini Zingine ninazo Nyumbani
Kibatala: Ukiangalia suala hili limeanza Tangu June 2020 Mpaka August 2020
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: kwa hiyo Tukiangalia katika Telegram hatutoona Mawasiliano yako wewe na Mbowe kabla ya Tarehe 25 June
Shahidi: Tulikuwa tunawasiliana Kupitia Whatsup
Kibatala: Mlikuwa Mnawasiliana kabla ya Kipindi cha Hili Tukio au ni Wakati wa Jambo hili tuh
Shahidi: Kimyaaaaaaaaa
Kibatala: Tarehe 07 August 2020 ulikuwa wapi
Shahidi: Nilikuwa Nipo kazini Sanga Sanga
Kibatala: Ni nini ambacho tunaweza Kuku Omba ukatuletea kuwa Ulikuwa kazini
Shahidi: Nilkuwa Commander wa QRF (QUICK RESPONSE FORCE)
Kibatala: zaidi ya Kuandikishana Kielelezo namba P 36 ni Ushahidi I alp Kwamba Inspector Swila Aliingizwa Simu katika Kitabu Kisha Wote Wewe na Yeye Mkasaini Kitabu
Shahidi: Mimi Siku Saini Kitabu
Kibatala: Na Yeye Hukumuona akiandika chochote Katika Kitabu
Kibatala: Zaidi ya Hand over Document, Je Uliwahi Kupewa Risiti yoyote ya Simu zako
Shahidi: Sijawahi Kupewa Risiti
Kibatala: Je Wakati Unamkabidhi Simu Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Inspector Swila alikuwa anabandika Makaratasi Katika Simu (Exhibit)
Shahidi: Sijawahi Kuona
Kibatala: Katika Maelezo ya Ushahidi Ulisema Kwamba haukujisumbua tena Kuhusiana na BWIRE kwa Sababu Lengo lilikuwa Limeshatimia
Shahidi: Nakumbuka nilisema
Kibatala: Lilikuwa Lengo lipi
Shahidi: Baada ya Wahalifu Kukamatwa
Kibatala: Kwa hiyo Lengo lako wewe lilikuwa Kuhakikisha Wahalifu Wanakamatwa
Shahidi: Nazuia uhalifu
Kibatala: Je ilikuwa kazi yako ya Kazi ya Polisi
Shahidi: Ilikuwa kazi ya Polisi
Kibatala: Malya alikuuliza Kwamba Uliwanunulia akina Adamoo Chakula
Shahidi: Nililipa Mimi lakini pesa Nilipewa na Mbowe
Kibatala: Je Ulizungumzia Katika Ushahidi Wako Mkuu Kuwa katika Pesa niliyowapa Adamoo na Ling'wenya Sehemu ya pesa ile Walitumia palepale Kulipa Chakula
Kibatala: Kwa kuwa wewe ulikuwa na Mawasiliano Moja kwa Moja na DCI na Kingai, Uliwahi Kufahamu Kwamba Hakuna Simu ya Mbowe hata Moja iliyokamatwa
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa Maana hiyo Ufahamu Pia Kwamba Polisi Wameshindwa Kuthibitisha Mawasiliano yako wewe na Mbowe
Kibatala: Mhe Jaji Nauliza Swali la Mwisho halafu nitatoa hoja
Kibatala: Ulisema Bwire Alikwambia Wapo katika Utekelezaji Wa Mpango
Shahidi: Siyo Mpango, alisema Samahani Bro tumeshakengeuka, Tumeshawishiwa na Freeman Mbowe, Na Vijana Wapo Kilimanjaro Katika Utejelezaji
Kibatala: Wewe Ulikuwa na Mamlaka Yoyote Ya Kiupelelezi zaidi Ya Kutoa Taarifa
Shahidi: Kila Mtanzania ni Mpelelezi, Sina Mamlaka Nyingine Ya Kiupelelezi
Kibatala: Hoja yangu Ulipata wapi Power Ya Kuagiza Waendelee na Uhalifu
Shahidi: nilishatoa Taarifa
Kibatala Mheshimiwa Jaji Bado Nina Maswali Kadhaa, Naomba tuhairishe Cross Examination, Mpaka Kesho February, Ilituweze Kuendelea.. Ni hayo tu.
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi, lakini tunaomba Kesho Tukiendelea Mwenzetu ajieleleze Katika Maeneo ambayo bado hajayahoji
Jaji: Unasemaje
Wakili Peter Kibatala: Hakuna Neno Mheshimiwa Jaji
Jaji: Shauri hili limehairishwa mpaka kesho Tarehe 01.02.2022, Shahidi namba 12 ataendelea Kuwa Mahakamani Kuendelea Kutoa Ushahidi Wake. Washtakiwa wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Kesho Asubuhi Saa 3 Asubuhi.
Jaji anatoka Saa 10: 38