HAKUNA 'DINI' WALA UHITAJI WA 'DINI MPYA'....
Dini ni katalisti/Kichochezi/Kiuhuishisaji cha 'Mfumo/Mifumo'... Kwa mfano, ilikuwepo na 'fanusi jamii--functional society', ni lazima mazingira yawepo kwa ajili ya 'Kuijumuisha Jamii--integrative factor/basis'--mambo kama vile sheria, miongozo, maono n.k
Dini ni 'Shughuli' ya kuijumuisha Jamii ili 'ijiweze ama/na kujimudu' mapito ya matamanio yake ya Kiutu...
SASA, jamii inaweza kujumuishwa kwa 'ladha mbalimbali' za Utu na Kujichagulia--'sura' ama/na 'utukufu' mbalimbali; lakini 'Ukweli' wa 'Uzima/Sifa/Hali/Mwenendo' wa jamii huwa na 'Mbegu yake Mahsusi'--mbegu mahsusi ya 'Utabia wa Kishirika--organizational behaviour' wa wanajamii wowote.
Dini ni 'Shughuli' ya kuratibu 'Utabia wa Kishirika' wa 'Fanusi Jamii' yoyote; kuhakikishia wanajamii mazingira rafiki ya kukuwa na kustawi kiutamaduni kama jamii moja.
Ni kwa mintarafu ya haya, Dini, daima huwa ni 'Udhamirifu wa Kujumuisha na kutangamanisha' yote ya watu/wanajamii--mambo ya 'MRABA' wa 'Wakati-Jamii-Machaguo ya Kitaasisi-Matukio'.
Hili ndilo linaweza kushangaza humu kwa nini 'kinara' wa Uzi huu 'hana nongwa' kuhusishwa na 'Dini Yoyote'--iwe tuseme Uhindu, Uislam, Ukristo n.k.
Hivi ni kwa kuwa,
Siri ya Dini ipo kwenye 'Ufahamu'--mambo ya maandiko na mapelekeo ya tafsiri; ndiyo 'tatizo la kiufundi' la wanadamu na vipawa vya akili/kiakili.
Sasa, siyo kila mtu mwenye 'daraja' ni bingwa ama fundi wa 'maneno'... Hili linaweza kuwashangaza wengi kusikia hivi... Kwa hivyo kudhani 'kinara' wa huu uzi 'atamudu' maswali na udadisi kwa 'maajabu' ni 'shauri mushkeli'....
'Tatizo la Kiufundi' la wanadamu na vipawa vya akili/kiakili linatatuliwa kwa udhamirifu wa 'Maarifa' na 'Maarifu' kupitiliza 'mashauri ya kawaida' ya 'habari na kuhabarika'...
Kwa hivyo,
ukisikia mtu anazungumza kuhusu 'code' ama 'password', kiufundi huyu anakumbushia 'umma kujiongeza': 'kujua-maarifa-maarifu' huja kwa 'alama za kiutambuzi' na 'wepesi wa kuifungua milango ya fahamu'; si kumendea 'stori stori za mambo ya maajabu'...
Hichi ndicho hata humu, kwenye huu uzi, bado kidogo ni 'mtihani', ila In Shaa Allah, Elimu na Ilimu tayari imeshajengewa msingi kwa hili jukwaa. Siku za mbele kidogo, mwishoni mwa mwaka huu ama kufika mwakani, humu watakuwepo wadau wengi ambao si 'wanadamu wa Duniani' ila watashiriki 'maarifa na funguo za mafahamu'--wapo kwenye 'maandalizi ya kidiplomasia'; jambo linalotaka sana humu kusisitiza 'mkao sahihi' wa kunufaika na mambo/shughuli kama hizi za makutano ya 'viumbe-wanadamu na viumbe-watu wengine wenye nasibu ya mawanda yenye kutofautiana mapana ya fahamu/ufahamu'.
Jambo linaweza kujenga mnufaiko na mambo/shughuli kama hizi za makutano ya 'viumbe-wanadamu na viumbe-watu wengine wenye nasibu ya mawanda yenye kutofautiana mapana ya fahamu/ufahamu' ni UONO NA UFIKIRIFU MIFUMO...
SASA, asili ya
'code' ama 'password' ni mambo ambayo humu wengi hawajajiandaa kumaizi kwa kuwa hapa Duniani kuna matatizo ya 'Kielimu' yanayofanya watu wawe na tabia 'kudaka hili na kutupa lile' eti kwa kuwa habari zake si za eneo la utaalam/usomi wa mtu--hili jambo ni kasumba, na ubovu wa kimaarifa; tena linaathiri moja kwa moja mawezekano ya 'Mageuzi ya Kijamii' na Uwezo wake kukumbatia 'Nuru ya Ufahamu'--ilivyo ni njia ya Wongofu...
Kwa hivyo, jambo moja la muhimu na tena la msingi kuwakumbusha watu wote, wale wanaodhani wanayoyakunufaika na 'wageni' ama 'wenyeji' wenye mapana zaidi ya fahamu na ufahamu, ni kufuta na kuondoa kasumba juu ya visomo-maarifa-ujuaji walivyonavyo.
Haifadii mtu kusema yeye 'si msomi'--hajasoma shule; ama 'hana elimu ya kutosha'; basi huyu akiona mwanajamii mwenzake anadadavua jambo kwa fasaha na mapana yeye kujiambia 'Hii michosho/Kuchoshana/Ndefu--nitasoma baadaye'... Kwa kuwa inawezekana hayo yanawekwa hivyo ili iwepo 'Subira'--siku akiwa tayari kuijaribu 'Elimu' basi akitulia na kudhamiria atanufaika moja kwa moja...
Haifadii mtu kusema yeye 'ni msomi'--amesoma na madigrii kama yote katika sheria, sanaa ama/na uhandisi; basi huyu akiona mwanajamii mwenzake anadadavua jambo kwa fasaha na mapana nje ya ugani wake wa kitaaluma basi ajiambia: ah huyu anaandika 'mambo yake sana'; ama hata mimi nimesoma sana--najua mengi; tusichoshane! Kwa kuwa 'usomi' na 'kujisikia' vinaweza kuwa kiburi na ujivuni. Kwa hivyo si ajabu kuona watu wengi wakishakuwa na 'elimu za vyeti' akili zao zikalala na vyeti vyao masandukuni ama zimetundikwa ukutani na vyeti--hawana maajabu! Si kwa maneno ama busara ya mapana ya mambo...
Uono na Ufikirifu Mifumo ni Elimu 2.0; hii inahusika kwa wote wenye 'kudhamiria kujua ilivyobora' na basi inawezekana kwa 'Msomi' na hata vile vile mtu 'Asiye Msomi' kwa dhana ya 'Madarasa'... Elimu 2.0 ni mwanzo wa 'Hekima'; na Hekima ni Uhuru...
Mambo ya
'Code' na 'Password' ni mambo ya Elimu 2.0 kujinasibu na Elimu 3.0; Ambavyo Elimu 3.0 ni ILIMU--ILIMU ilivyo ni metafizikia ya Elimu. Basi yawa, NENO ILIMU limeshatohorewa rasmi kuwa msamiati wa lugha ya Kiswahili kumaanisha 'UGANI WA MAARIFA NA MAARIFU' ya 'MIFUMO'--Mifumo ya UTU-MAISHA-UISHO.
Kwenye maarifa ya Elimu ya Jamii, 'sosholojia' ELIMU 3.0 ndiyo mambo yanayohusiana na 'Ualama Oanifu' wa 'Kawaida za Jamii'. Kwa mintarafu ya hivi, mifumo yote huja kutokana na 'Mwangaza wa Jamii', 'Kujichagulia' na 'Matendo'--Mambo yanafanya kwa mfano Elimu, Siasa na Mipango kuwa pembetatu ya Utaifa/Jamii/Dola...
Kwa nchi ya Tanzania kwa mfano, 'Code' na 'Password' ya Elimu na 2.0 na Elimu 3.0 huja kwa '
Mazingatio ya Kikatiba': Udhamirifu wa Taifa la watu wenye kusudi la kuijenga na kuilinda nchi-dola kwa misingi ya UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI. Ni adha ya jamii 'kujisahau' tu ama 'Kutojitambua' kusudi la utaifa na maisha yao... Haya manne ni 'Code' na 'Password' ya Nchi ya Watanzania...
Kwa hivyo kwa mtu wa Elimu 2.0 na Elimu 3.0 anaweza kuzibaini hizi 'codes' na 'Password' kirahisi kabisa; kwa mfano hivi vinne hukadirisha MRABA wa NISHANI ya UTU BORA. Kwenye Elimu na ILIMU ya mapokeo ya Ukristo UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI ni kode za
Uzabibu 13--Ufahamu Kristu. Kwenye Elimu na ILIMU ya mapokeo ya Uislam UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI ni ufunguo wa Imani kwa 'Allah'--
Katika majina 99 ya ALLAH, kuna haya ambayo huleta 'kumcha Mola' kwa baraka ya nusuru ya nchi-dola:, (1) AN NUR (Mwenyekuwa MWANGAZA), (2) AL JAAMI(Mwenye Kuwakusanya Waja Wema), (3) AL-'ADL (Mwenyekuwa na Uadilifu katika HAKI), na (4) AS SALAAM (Mwenyekuwa na Salama).
Sasa, ipo namna ya kutanuka haya yote kwa Elimu 2.0 na Elimu 3.0; In Shaa Allah, tuombe kheri haya tupate kuyafahamu kwa jicho jema na yatuingie moyoni na akilini...
Hmmm