ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,673
- 21,792
Mengine nakuachia mwenyewe ila nitajibu yale ambayo yanaingia akiliniHahah sawa bhana..
Mwanzo 1:26.
26. Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
Mungu hakuumba ulimwengu ili yeye atawale.. aliuumba ulimwengu akatuumba binadamu ili tuutawale ulimwengu..
Hatukuweza kuutawala mpaka mwisho tulimpa mamlka yetu shetani ya kuutawala ulimwengu kupitia Adam.. imeenda kizazi mpaka kizazi..
Manabii walikuwepo kila mmoja akitabiri atakuja masihi.. Huyu masihi ni nani na anakuja kwa kazi gani ambao hawa manabii wengi hawakuweza kufanya.. maana kama maelekezo si walikuwa wanapokea kutoka kwa Mungu sasa kwanini aje masihi?
Toka juu nimesema Mungu alituumba tuwe wake lakini tutawale eneo letu ambalo ndio hii dunia..
Na Mungu ni roho ili utawale dunia yetu unahitaji nini vile? Mwili ili usurvive ili ufanye kitu kuwa kitu inabidi uwe na mwili achana na mapepo na majini..
Kwahiyo toka adam aliposea mpaka vizazi vyetu tumebeba asili ya adamu.. Inamaana sote si tumetoka kwa adam.. kwahiyo mtindo ni ule ule kama alivyokesea adam na sisi hivyo hivyo tunakosea kwasababu tu wa asili yake..
Ndio maana tunasema na ndivyo ilivyo.. Mungu aliuvaa ubinadamu ili kutuokoa na dhambii
Mungu alivaa asili ya mwili ili kuondoa tatizo la dhambi.. Angeweza kuamua kama unavyosema tu lakini angekuwa ametengua neno lake mwenyewe la sisi kutawala ulimwengu..
Tutazame basi kuzaliwa kwake huyo masihi.. kwanini kuwe tofauti na manabii wengine..
Kwanini azaliwe bila baba? Inamaana kuna kitu anakuja kufanya.. maana kusema kuzaliwa bila baba inamaana asili ile ya adam haifanyi kazi wala haipo ndani yake.. basi sasa huyu anakuwa na asili ya nani?
Moja wapo ambalo linaingia akilini ni hili la Yesu kuzaliwa bila baba,na huu ni muujiza mahsusi kwa waja wa Allah ili waone uumbaji wake
Kwahiyo ni neno ambalo alipuuliziwa bikira maria na akabeba mimba yake hatimaye kuzaliwa kwa Yesu
Kabla sijaendelea mbele,porojo nyingine inakuja tena,kwanini Mungu au roho yake isijiingize moja moja kwa bi mariam na kuwa mimba,hapo unaona kwamba Malaika wanafanya kazi ya kuingiza roho ya mungu kwa bikira maria,je hii imekaaje? Ndio mwendelezo wa porojo zile zile
Any way,tuendelee,je huu ndio muujiza pekee ambao unawashangaza watu juu ya ukuu wa mungu?
Yesu kazaliwa na mwanamke si ndio? Vipi kuhusu Adam aliyeumbwa bila mama wala baba?
Boss tupo pamoja?