Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Simba ndio Corazon au Arsis? Sasa kama ni Corazon kwani unafanya kazi gani kwa elimu uliyopata?
Swali zuri sana.

Mimi Simba, Corazon Espinadp lilikataliwa na Arsis, amesema kama yeye anakuja kujibu maswali iwe simba, nikamuuliza kwanini isiwe Arsis? Akasema sawa weka Arsis lakini usiweke Corazon Espinado.

Nikamuuliza kwanini? Akanambia wewe unasikiliza wanaimba lakini hujui maana ya hao mashetani wanaoimba. Akanipa bonge la story la ushetani wa mwanamziki Carlos Santana. Halafu ndio akanambia maana ya corazon ni. mapenzi ndani ya roho na espinado ni miiba mikali. Roho nzuri ilioingiwa na miiba ndio maana yake kwa ufupi.
Mkitaka kisa chake nitawapa, hii kanijulisha juzi, kuelewa tu, mwenyewe nikabadili ID.

Ukiona signature chini ya Simba, ujue sio Arsis.
Simba.
 
MIE NAISHIA HAPA MAANA BWANA SIMBA KATUKIMBIA NA SIMULIZI YAKE.

ILA NIWAPE TU USIA ALONIPA BABA YANGU KABLA HAJAFARIKI,ALINIAMBIA MWANANGU ISHI MAISHA YA KUMPENDEZA MWENYEEZI MUNGU,MTEGEMEE MWENYEEZI MUNGU POPOTE ATAKUVUSHA SALAMA.BABA YAKO SIO TAJIRI SIJAKUACHIA MALI ILA QURAN NA SUNNA ZA MTUME WETU MUHAMMAD S. A. W USISAHAU KUMSWALIA.

AMKA USIKU SEMA ONGEA NA MWENYEEZI MUNGU KWA KUMAANISHA MOYONI NA MDOMONI.
USISAHAU KUWA NA HURUMA KWA WENGINE NA KUTOA SADAKA HASWA WAJANE NA MAYATIMA.

HIVYO USIA WANGU KAMA MPENDA WAGANGA UACHE KUNA WAGANGA NI WABAYA MNO BADALA YA KUKUSAIDIA ANAKUANGAMIZA ZAIDI WANA TABIA YA KUIBA NYOTA WAKATUMIA WAO HIVYO KUWA MWANGALIFU SANA USISIKIE KUNA MGANGA FLANI BASI UNAENDA KESHO UNASIKIA KUNA MWINGINE HASWA WASIO KUWA WACHA MUNGU NI HATARI NI HAYO TU OVER AND OUT.
 
Kiukweli katika hii audio kaka yako ameniangusha sana,yaan nimesikiliza mpaka dakika ya sita nikaona niache

Kwanza anazungumzia mambo ya kurithishana dhambi wakati katika imani ya kiislamu hakuna mambo hayo kabisa

Qur'an inasema mara baada ya Adam kufanya dhambi na mkewe hawa,wao pamoja na ibilisi walifukuzwa peponi,lkn Allah akawaambia kama ukiwafikia muongozo kutoka kwangu na mkaufuata basi mtaokoka


Adam akapokea maneno kutoka kwa mola wake ya kuomba toba ,nayo ni "hakika mimi nimedhulumu nafsi yangu lau kama hutanisamehe nitakuwa miongoni mwa walioghafilika au waliopata hasara kitu kama hicho"

Hapo akasamehewa kasoro ibilisi ambaye alikataa kuomba toba kwa kiburi

Kwahiyo hakukuwa tena na dhambi za kurithi wala za asili,istoshe mola wetu anasema yeye ni mwenye haki hawezi kutuhukumu kwa makosa ya watu wengine

Lakini jambo moja ambalo liko wazi ni kwamba,majanga mengi tunayokutana nayo leo ni kutokana na yale tuliyatanguliza kwa mikono yetu wenyewe,kwa maana madhambi yetu ndiyo sababu ya adhabu tunazo pata kutoka kwa Allah

Kwahiyo kusema watu wanarithi dhambi hapana kwa waislamu hakuna hiyo
Hii mada ya Adam Arsis aliwahi kunipa kivyake yeye, alisema adam sio jina, adam ni cheo, wapo adam wengi sana miaka mingi sana na hata kaumu ya firauni ina mika zaidi ya million moja nayo wanaita adama.

Arsis elimu yake ina utata sana kwetu Waislam na wasio Waislam, anasema watu hawaisomi Qur'an wanawasoma watafsiri wa Qur'an ambao wanawapoteza sana watu.
Simba.
 
Sijapata kumuona akinywa pombe kwenye maisha yake sijui kwenye ngoma zao maana sijawahi kushiriki.
Sio lazima kiti awe kama jini alivyo ,

Maana majini yanayofautiana mpaka tabia pia ndani ya mwili wa kiti huyo huyo mmoja , hivyo kiti ata behave kulingana na jini atakayepanda muda huo.
 
Hii mada ya Adam Arsis aliwahi kunipa kivyake yeye, alisema adam sio jina, adam ni cheo, wapo adam wengi sana miaka mingi sana na hata kaumu ya firauni ina mika zaidi ya million moja nayo wanaita adama.

Arsis elimu yake ina utata sana kwetu Waislam na wasio Waislam, anasema watu hawaisomi Qur'an wanawasoma watafsiri wa Qur'an ambao wanawapoteza sana watu.
Simba.
Arsis ni hatar sana habar zake,ngoja tupate maarifa mapya
 
Nilimuuliza kaka kuhusu familia au ukoo unaweza kukufunga usifanikiwe? Majibu yake kwenye audio
Jana nimesikiliza audo na Arsis kasikiliza na leo nimesikiliza hii, kwa kua sio swali kwa Arsis ikabidi asijibu lakini Arsis amesema ongea wewe Simba.

Mimi nasema hivi; Huyu kaka yako anajua majini kupitia vitabu vya kichawi na masheikh wasio na elimu. Huyu ana kichwa kizuri cha kusoma lakini amesoma elimu sio sahihi. Arsis, Waongo sana alicheka akasema anasoma vitabu vya mashetani wa kipakistani, waongo sana.

Anaelezea majini ndivyo sivyo na tujuavyo sisi, lakini usiwache kuleta audio na elimu yake inatufanya tujipime na yetu. kama anavyoleta mzee wa chai na elimu yake ya muridi.Tunapata kusoma hapa.

Leta vitu.
Simba.
 
Hii nimemuelewa sana, nilishawahi kuandika mada hii JF. Jakuna challenges.

Hapa namuunga mkono Arsis asilimia 100. Niliisikia hii mada kwa Sheikh mkubwa sana na maarufu duniani, ngoja niitafute video clip yake.
Itakua vizuri maana hii mada mimi nimemuelewa lakini mpaka sasa haijaingia akilini. GTuletee clip tuione.
Ndio maana Arsis anakukubali na anakusifia sana wewe na Sheikh Che mittoga mittoga. Wote watata kama arsis, au nyie majini?
Simba.
 
Nimefuatilia story yako toka mwanzo kuna elimu kubwa hapa hasa kuhusu viumbe wengine ambao binadamu tunawachukulia poa lakini maisha yetu mengi yanaathiriwa na viumbe hivyo either in positive way or negative way.
Kwa ufupi nikuwa:-
1. Majini wapo wazuri na wabaya kama walivyo binadamu ila ulimwengu wao hauonekani kwa macho ya kawaida.
2. Majini wema wanaweza kutoa misaada kwa mtu hasa aliyekumbwa na majini wachafu hii kwa wasomaji wa ruqya wanalijua sana
3. Qur an ina nguvu kubwa sana isiyomithilika ila wengi katika waislamu wanaichukulia poa.
Mwisho nina maswali ndugu la kwanza embu muulize Arsis anayajua majina ya BARHATIYAH na je ni katika shirki ?
Swali la pili, Muulize Je ni kweli mafuta ya miski yanawaumiza majini wabaya?
Kwakuwa stori imegusa dini yako (quran) basi umejitia upofu huoni kama ni ya kutunga na bado unajazia nyama! Kila kilichoandikwa humu ni chakufikirika, hakuna ukweli hata 10%. Mtu mzima unaambiwa mtu alifungua chupa akiwa kazungukwa na joka la vichwa vitatu, dragoni anayetoa moto mdomoni sijui na wanyama gani na wewe unaamini kisa kaigusa quran!? Huo ni zaidi ya wendawazimu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom