Binaadam ananguvu kubwa kuliko jinn, ndivyo Allah alivyotaka iwe hvyo!!
Swali n je,,,, mbona sisi ni dhahifu sana tofauti na majinn?
Binaadam alipata upendeleo wa kuwa na nguvu kubwa kuliko viumbe wengine ambayo nguvu hyo humfanya kuwa mtawala Dunian (khalifa)
Na upendeleo huo ukaja na masharti mawili
A. Binaadam hatoishi umri mrefu katika ardhi
B. Nguvu hiyo binaadam hatoweza kuitumia mpaka ifunguliwe kwa taratibu maalum
Hapo tumeona kumbe binaadam nguvu anayo ndani lakini imelala✍️
Ndio utaona watu wa meditation, kundalin awakening n.k huwa wanaamini Kuna nguvu ambayo ipo ndani ya mtu anatakiwa kuiamsha
(Utaenda kusoma article zao utapata kitu)
Sasa Kuna nguvu ya asili kimaumbile katika kila kitu, hiyo nguvu inamajina tofauti tofauti kutokana na eneo au jamii husika ....... hiyo power ndio source ya kila kitu (hapa ndo tunapata nadharia ya Mungu.)
Sasa binaadam ili aweze kuwa na nguvu kuliko viumbe wengine tumesema n lazima aweze kufungua nguvu ya asili iliyopo ndani yake,,,, ambayo nguvu hiyo imefungwa na Nguvu kuu (Mungu mwenyew) pia hufunguliwa na hiyo hiyo Nguvu Kuu.
Twende taratibu..... Nguvu kuu ikampa mwanaadam sharti au mapatano au Nini afanye ili afungue nguvu yake ya ndani.... ambapo taratibu hizo binaadam tukaziita DINI
Dini ni promis za kuifikia Ile nguvu kuu...
Ndo maana dini ni nyingi lakini lengo n moja tu, kuifikia Ile Nguvu kuu
Dini ikawa n mkataba wa gain and loss baina ya binaadam na Ile Nguvu kuu... kwamba ili binaadam awe mfalme kwa viumbe wengine sharti awe mtumwa kwa Ile Nguvu kuu✍️
Kwahyo dini zote lengo n kumfika Mungu na ukimfika Mungu ndio unafungua nguvu ya asili ya binaadam...... hakuna shortcut!!
Hapa naizungumzia nguvu ya asili ya binaadam ili uwe Bora kuliko majinn kama ulivyotaka.
Note: Kutokana na uwezo wa mwanaadam kuwa n mkubwa sana ikiwa utafunguliwa..... ikabidi upite mchujo mkali ili kubakiza wachache wataokidhi vigezo haswaa
Ndio utaona Sheria karibu zoote za dini ni ngumu na zinataka ukandamize nafsi ili uvuke.... utaona unakatazwa kufanya vitu unavyopenda halafu unalazimishwa kufanya vitu usivyopenda
(Uswali mara 5 per day tena bila kusahau asubuh na baridi lake ukashike udhu😂)
Hapa n kwamba mashart lazima yawe mengi ili kuchuja vizuri sababu malipo yake n makubwa kupita kawaida
Kwahyo mwanaadam nguvu anayo ndani yake ila ili ifunguke akubali kupita kwenye katiba ya Nguvu kuu!!!
Majinn pia wanamapito Yao huko ambayo hayafanani na yetu... wao pia wananamna Yao kuifikia nguvu kuu (ambayo n hii hii moja)
Swali lako n gumu sana, ila nimejitahidi hvyohvyo kadiri nnavyoelewa
Lidafo
Vizuri
Arsis ...... angechambua hilo swali maana Lina Siri nyingi tusizozijua