- Thread starter
- #3,401
Mimi sina uwezo wa kukuunganisha nao zaidi ya hiki tunachokifanya hapa JF kwa sasa.Naomba unikutanishe na Arsis au Bakora niongee nao maana nina changamoto kubwa sana naimani watanipa ushauri na matibabu.
Simba.
Mimi sina uwezo wa kukuunganisha nao zaidi ya hiki tunachokifanya hapa JF kwa sasa.Naomba unikutanishe na Arsis au Bakora niongee nao maana nina changamoto kubwa sana naimani watanipa ushauri na matibabu.
Elimu ndio tumeshaianza hapa, Uwe unanisoma kwa makini tu. kama hukuelewa kitu katika maandiko yangu uliza.Sijawahi,mwaga elimu tujifunze
Nakusoma sana,tupo pamojaElimu ndio tumeshaianza hapa, Uwe unanisoma kwa makini tu. kama hukuelewa kitu katika maandiko yangu uliza.
Hujawahi nini?
Simba.
Ahsante sana kwa ushauri wako, tutalifanyia kazi.Mbali na mafundisho unayotupa mimi ni nafatilia kwa karibu sana stori na visa unavyoturushia humu.
Nina ombi moja kwako, kama inawezekana uandike kitabu cha simulizi zote ulizopitia lakini ndani yake uweke mafundisho ambayo yatatusaidia zaidi katika maisha yetu ya kila siku. Naimani kitabu kitauza sana na kitawafikia watu wengi sana ambao wapo nje ya mtandao.
TTfadhali nipe [post namba. Nikaweke sawa.story nzuri ila uandishi bado sana ulivyoishia pale mpe ocean road aris basi umenichanganya tena sijaelewa kabsa mtiririko uliofuta nmeshindwa hata kusoma ... I hope utakaa chini na kuandika vizuri kwa mtiririko mzuri then utaanza upya kupost big up
Kilemba chako kinanikumbusha kilemba cha mtu mwenye majini niliekutana nae Dar. Sijaleta kisa chake. Huyo jamaa alikua ana majini kwa maelfu.Ni kweli wewe hauna uwezo,ila una connection moja kwa moja na viumbe ambao wanaujuzi zaidi wa shida zinazotukabili nje ya mfumo wa kawaida.
Mfano ulimpiga beat huyo mkuu wa vibuki aachane na dokta kabisa.
Mbona babu yako yeye alikua hawaambii wenye matatizo kwamba wasali sana.
Ndo maana akakuunganisha na kina Arsis ili ikitokea changamoto unasaidia kama ulivosaidia mengineyo ya misukule n.k
Mkuu wala sijamaanisha mipasho wala sina kusudi hilo, pole ni kuwa nahurumia nafsi yangu na kukupa pole kwa kutaka kukupa mzigo ni hilo tu, samahani kama nimekukwazaUnampa pole mtu unaempa hafahamu kwanini? Hapo wa kupewa pole ni wewe.
Nakushauri piga goti usome, sana tu. Mipasho ya kijinga haitakusaidia kitu. Unatakiwa upite kwenye njia ilionyooka.
Sifahamu kwa wewe, lakini nfahamu Kiislam tunaomba kwa uchache kutwa mara 17, tuongozwe na muumba wetu katika njia ilionyooka.
Au hujamsoma mose kasema nini kuhusu moyo?
Simba.
Tukaenda na swahiba alipotuagiza Meneja tukamkuta manager peke yake kasimama jirani na hapo, tukasalimiana pale.
Meneja: <Mgeni alietualika ni mumewe Bi Sh alikuja kutaka ushauri wangu kuhusu hoteli ya Bi Sh na amekodisha room atakua hapa mpaka kesho, watakuja baada ya muda si mrefu, wite mabiie wa Dar wapo na T chumbani kwao wanajitayarisha, si unajua wanawake hawana dogo.
Na mumewe Bi Sh anategemea wageni wawili kawaalika chakula poia, mke na mume, wataingia muda eoeote kuanzia sasa. Karibuni agizeni vinywaji.
Mimi; Tutasubiri, mimi naoimba mniwie radhi kidgo kuna miss calls nataka niende pambeni nikapige nyinyi endeleeni na vinywaji, sichelewi nitarudi. Nikaenda mbali kabisa na pale ili nisiwakere na maongezi yangu, nikaona kibanda kimoja cha makuti kipo peke yake na hakuna watu saa hzi beach isipokua wazungu mmoja mmoja.
Nikapiga simu hya kwanza namba nisioijua akapoke Bi S. Mkubwa wa vibuki, Tukasalimiana pale.
Bi S; Simba bado upo Unguja au umeshaondoka?
Mimi -; Bado nipo.
Bi S; Ulinambia upo hoteli?
Mimi; Ndio, nipo hoteli.
Bi S; nimekupigia sana nikasema hupokei namba usizozijua?
Mimi; hapana, nilikua nimekaa na watu na si vizuri kupokea simu mbele za watu nitawakera.
Bi S; Watu wengine hawana hilo kabisa, hata akiwa mgeni kwako, basi ataaanza kuonge na simu kama yupo kwake, hata mimi siwezi, mamboi hayo. Watu na mna hiyoi ni selfish.
Nikapata jina jipya la watu wasioheshimu utu wa watu wenhgine kwa kujibu na kuongea na simu zao hovyo, mbele za watu hata wasiowajua. Binafsi nashindwa.
Bi S; Nimekupigia nilikua naongea na BiH 1 wa Dar, akataja kua kuna kuna kijan yupo hoteli waliofikia, anahisi ni ndugu yake Meneja wa hapo, alivyotaja jina Simba, mimi sikumuulliza zaidi na sikumwambia kama nakufahamu. Ni kweli?
Mimi; Kweli nipo naoi hoteli moja, yeye na mwenzake na kweli Meneja ni kama ndugu yangu wa kushibana sio wa ukoo.
Bi S; Huyo meneja wa hio hoteli moto wetu wa Kingazija huyo, sema miaka mingi alikua anaishi nje hata jamaaa zake hatujui, Marehemu mamake alikua karibu sana na sisi. Niliposikia nikaona nikupigie kucheki ndio wewe au mwengine.
Mimi: Ahsante kwa kunijulisha.
Bi S; Kwanini unakaa hoteli, si uje kukaa kwangu hapa, nyumba kubwa hii, halafu Bi S kanifahamisha mamako, namfahamu, sio sana lakini tushaonana mara mbili tatu Dar kwenye shughuli za huyo Bi S. Njoo hamia nyumbanni utakaaje hoteli na sisi tupo?
Mimi: Ahsabte Bi S, In shaa siku zingine nikija nitakuja rasmi, kwa sasa ni mgenoi wa Meneja hapa.
Bi S; Una nafasi ya kuongea? Kuna vitu muhimu sana nataka kuongea na wewe Simba.
Mimi; Ongea gtu Bi S, nipo peke yangu.
Bi S; Simba nataka kujua, wewe ulikuja kutokea kwa Dar kwa ajili ya Dokta?
Mimi; Ndio.
Bi S; Tafadhali nifungikie, mimi kicheo cha vibuki nipo chini yako lalkini sasa hivi sikuulizi kama kibuki, nakuuliza kama mimi S. Ilikuaje hata ukaja?
Mimi; Nilikutana na Dokta kwa mganga wa Kipemba, nadhani hilo unalifahamu.
Bi S; Ndio, kwa mzee Ali wa buguruni.
Mimi; Meew ali ndio akanifahamisha mtTIO Ykw na utatuzi ni lazima aje yaitwe maruhani ya kibuki wafanye muafaka kwa sababu ni wa ukoo. Nikashauriwa nije kujionea. Ndio nikaja.
Bi S; Mbona ulivyokuja siku ya kwana hukuniambia hayo?
Mimi; Sikua na sababu ya kukueleza hayo, kama mkiubwa wa vibuki ungejua tu.
Bi S; Nilipata habari kua huyo aliekuja ni mkubw sana lakini sikujua vibuli wanamaanisha nini mpaka nilipokukuta ndani tukaongea. Sasa nilikua nataka kujua, wewe Simba unatibu watu?
Mimi; hpana mimi sitibu watu wala sijui tiba wala sio mganga.
Bi S; Ilikuaje sasa ukajuana na Mzee Ali?
Mimi; Mzee Ali ni maarufi sana Dar nilipelekwa na babangu nikajionee shughuli zake. Ndio nikagfahamiana nae na nikamuta Dokta hukohuko.
Bi S; Ikawaje ukaja hapa?
Mimi; Nilishauriwa nije, tafadhali usitake kujua na nani.
Bi S; Nimefahamu.
Mimi; Kwanini ulitaka kujua kama na tibu?
Bi S; kwa sababu una nguvu sana sio za kawaida, na sisituna watu wengi sana wene matatizo wanaonifata, nilitaka kujua unaweza kutusaidia vipi?
Mimi; Bi S, mimi sina nilijualao, kama umeshajua walionishauri nije, wao ndio wanatibu, mpaka waamue wao, mimi sina nilijualo, mimi fundi magari.
Bi S; Ni hsayo tu, niliku nstsks kukufhamisha, Eakuu wa viuki walinigiza Dokta audishiwe pesa zake na vibuki wake wasaimsogelee kabisa mpaka atake yeye mwenyewe tena mpaka wao wakuu waidhinishe, kwa hio kwa sasa wale vibuki wa Ndama, hawatomkaribia tena, alionao sasa ni wale wa kwa uoande wa mamake, sisis hatiruusiwi hata kuwataja wanaitwaje. Na ana vijini vingine vya Mzee Ali. Nilikua nakuomba simba, mkikutana na Daktari, nagahamu yeye kaondoka leo, aliniaga. Tafadhali usimueleze chochote kuhusu niliokwambia, mwache aishi kwa salama na amani, na sisi tutamkaribisha kwetu kama mtu wa kawaida lakini hattoshirikishwa kwa chochoite na vibuki wala hatokua kwenye chama chetu, tumepigwa marufuku kabisa. lakini yeye hafahamu hilo.
Mimi; kwanini unanambia yote hayo?
Bi S; Mimi nagahamu unayajua yote lakini nilitaka mimi kama mimi mbali ya vibuki niliweke sawa kwako usinifikirie vibaya, kama kuna nililkosea tusameheane kama binadamu. Mabio ya mila na jdai tuyaache kimila na jadi.
Mimi; Bi S, nirudie nilichokwambia kwako?
Bi S; hapana baba, nayagahamu yote.
Mimi; Nakukumbusha moja tu; toiba mama toba.
Bi S; Nimekuelewa baba. Niombee dua.
Mimi; Amiin. Kusongea tu hilo ni dua.
Bi S; Nakukaribisha sana nyumbani, nikia leo mna dinnet huko mmealikwa na mumewe Sh, Wamenambia wapo huko, walinambia nije, lakini wamenambia wakati mbaya ningewachelewesha sana, sikuweza kuja. Tungeonana huko sijui ningekutazama vipi?
Mimi; Usiwe hivyo, uliyoyangia na nia ya kyfabya toiba ni kubwa sana, mimi nichukukie kama mwanao tu, Wla usijisikie vibaya kabisa kuniona. Ongea na mimi kwa simu wakati wowote, hii namba yako naisave.
Bi S; Sawa, basi ahasante nisikucheleweshe mamboi yako, nikiwa na lolote tutaongea.
Mimi sawa, ahasnate kwa kua muwazi na mkweli. Kwa heri.
Tukaagana pale natazama upande wa meza ya chkula nika ona kama kuna wayti wameongeeka wapo zaoidi ya wawili, nikaenda nikawakuta Meneja, Swahiba, mwanamme na mwanamke siwajui. Tukaslimian Meneja akatulisha wote.
Meneja; Huyiu ndugu yangu anaishi Dar kaja kututembelea, lakini ahatki kukaa sana kesho anaondoka
Mgeni 1) Kwnini Simba, Unguja ni njema.
Mimi: Nimekaa sana bila kazi nimeshazowea pirika pirika za Dar.
Mgeni 1; Dar kuna pirika hasa mimi siziwezi nimeizowea Unguja yetu ingawa na yenyewe siku hizi inaanza kuwa na pirika pirika nyingi.
Meneja; Ndio maendeleo.
Mgeni; Sikujau kama nitakutana na swahiba hapa, tunajuana miaka mingi sana, tupo uradi mmoja huyu kila alkhamis, ndio masheikh zetu, mtoto wa Sheikh na yeye anafata nyayo.
swahiba,, Ahh unanipaisha sana bwana, mimi maamuma tu lakini In shaa Allah kauli yako iwe dua ya kheri.
Mimi: Amiin.
Kidogo kina dada wakaingia, kikundi wameingia kama midege inayosaka mizoga, katikati yao yupo mwanamme, anainesha ni mtu mzima kidogo lakini smart kabisa na yupo fit, anaonesha wazi umri unaenda lakini ni mgtu wa mazoezi alikua nimpana kiasi lakini hana manyama uzembe. Tukasalimiana pale.
H1; Ngija niwatambuloishe mimi> Huyu Mumewe BSh ndio alimkimbiza kwenye picnic yetu kwa Meneja, maana ni nyumbni pale lakini ilikua ni picnic, bahari ipo mbele yetu. nimtqmbulishe na vyeo vyake? Huyu ni Mjeshi, mwenyewe anasema mstaafu, lakini nijuavyo hakuna mwanajeshi mstaafu, kahamia kazi nyingine tu, Ssa hivi ni Waziri wa wa Serikali ya Mapinduzi. Na huyu mshajuana? hwataki kusema hawa Waunguja, huyu ni katibu Mkuu wizatra ya nini vile? Mliasili na Utalii si ndio. Na huyiu ni mkewe wa pekee, lakini anaonesha ana utotori wa nyumba ndogo, Unguja hii? Ji hansome kama hili? hata mimi akinikalia swa simwachi.
Mimi nikajua huyu Bibi kiwhazivuta huko chumnbani.
H1; Na huyu jamani mtoto wa haoa hapa kwenu Unguja swahiba yuake Simba huyu bila simba tungepaya wapi mhumba mpya? Huyu ndio mchumba wa T kuanzi leo.
T alikua akwa anachek chek kumtazam nikaona yeye huyu kishazitia kabla hawatoka huko ndani. ;akini katokezea huyo, T ni mzuri sana kupita maelezo, kavaa dress fulani hivi nyepesi kajitupia na mtandio mabegani kuficha juu ipo wai wazi. Imemtoa sana.
H1: hawa wengine mnajuana, enhee na huyu bibi Mke wa katibu Mkuu nisimsahau, huyu jamani mfanya bishara na mama wa nyumbani lakini yupo nae group moja, asiwstue, tutasema mambo yake sasa hivi mbele ya mumewe hapa.
Waziri; Semaaaaa.
Mumewe; Semaaaa
Menje; Usisemeeee
Hw: Semaaaaa maana anajifanya ka sio yeye huyu, eeh mwanamke ana vituko huyu, sijapata kuona.
Mke wa KM; jamani hii dinner leo ya kusakamwa mimi, ngojeni nile basi halafu muanze. Mnianzia mapema namna hii, nipisheni huko?
Sh; Si huyu akishakunywa mipombe yake kusema hivyo kama mwehu.
H1; Wewe saa hizi una kauli eeh, mwepesi, Mjeshi kishatoka kukufanyisha mazoezi, usio na haya wewe. Na mjeshi ulishikwa sana, si una mke mkubwa wewe? Ile kufika tu na chumba mkajifungia ndani, mnatichelewesha kula. Tunekaa kila mkao tunawangoja. Meneja kabla hawajaagiza hawa tafadhal sana ile supu, ilee ya kitai. hakuna kulala leo, hawa wanawake tutabadilishana vyumba tu.
Sh; Nyoo usiekua na haya wewe ubadilishane chumba na nani?
H1 basi wote twendeni tukanyanduane chumba kimoja, au unasemaje Meneja?
Meneja akawa abacheka cheka, tu anaona haya.
Mjeshi; Sh, Mimi nipo tayari huyu rafiki yako T leo ahamie chumbani kwetu, kitanda kikubwa kile.
Sh; tena nakuona siku nyingi uanvymtolea macho mtoto wa watu,ute unakutoka ukimuona. Utamuona hivyo hivyo kwa mbali.
Meneja; Tuanze kuleta chakula, ni vile vile kama tiulivyopanga Mheshimiwa?
Mjeshi; Vilevile hakuna mabadiliko.
Meneja; Haya jamani nyinyi kaeni ndani ha muda mchavhe watakuja wahudumu, igtawekwa meza ya chakula hapa wagtakua wanahudumia.
Akanyanyuka akaendandani, haijapita hata dakika ikawekwa meza kubwa kama mita gtano hivi na tulipokaa, yakaanza kuletwa mashani na mabakuli yale makubwa ya silva ya kuwekea vyakla zikaleytwa na sahani juu ya meza yake, ndogo tayari wapakuaji wamejipanga hapo.
H1: meneja ile supou ipo?
Meneja; ndio ipo hio tu, hakuna supu nyingine.
H1; haya asie na mwana aeleke jiwe. Supu ya Kitailendi hio, nyie wenye waume zenu, sijui huyu meneja anaitia unga wa viagra hio supu, mtakoma ubishi, lakini msijali, tupo sisi kuwapa huduma ya kwanzza mkizidiwa.
Meneja: Mheshimiwa karibu utufungulie kuanza kuchukua chakula wew ndio mwenyeji wetu leo.
Mjeshi; haya karibu nyite jamani, msimuone haya H1.
Akaanza waziri pale, tukafata nyuma yeje wenginewote, tukapakulia tukala, tukacheka, tukafurahi mapaka tunaliza vitanu tamu (desert) na kahawa mwisho, yamepita kama masaa mawili.
Katibu Mkuu akamshukuru waziri kwa kumualika, akaaga huku anasema jamani natamani tungekaa zaidi lakini majukumu. Wakaondoka na T baada ya kuagana ku hug na nini tena.
H 1: umemrushia mwamba hapa ndege wake. Mwamba hata namba basi hujachukua?
Swahiba: Mimi huyo sina haja ya namba mimi nakwenda kwao.
Sh; Waarabu wale unfate binto yao nyumbani utamuona hata alipo?
T; Huyo anaingia kwetu kama kwao. Muulzieni atawaambia, tunagoja alete posa tu.
Wakaondoka tuukawasinf)dikiza mpaka parking, Tuliporusi tukakuta pamesha safishwa, Meneja akatushukuru akasema na yeye anakwenda kupumzika mapema, ana kazi asubihi sana. n swahiba yangu akaaga.
H1; Unaenda wewe Muunguja, tumebaki wawili kwa wawili, Supu haijafanay kazi kwako? Joo mpenzi, twende mimi nikakutulize mzuka wa supu, huyu mwachie Simba hapa.
Simba; na mimi nakwnda zangu, kesho nasafiri mapema.
H2; Boti ya kwanza?
Mimi; haoana naondoka na ndege, saa nne niwe airport. Inabidi niamke mapema kujitayarisha. Nataka kupita mjini ninunue halawa ya zawadi.
H1: na mimi umenikumbusha, tena wewe oengine tunaondoka ndege moja, H2 umechukua boarding pass?
H2: bado tutachukua wakati wa kuondoka time nitatazama kwenye simu.
H1; kam ndege ni hiyo ya saa nne baso na sisi tuwahi mapema asubuhi tujkanunue Halwa ya zawadi, simba umetukumbusha jambo.
Nikawaaga, nikanyuka kumsinidikiza swahiba.
H1; Nyie mbona sio ma gentleman, mtaondokaje mtuwache wanawake pekeetu?
Mimi: Namsindikiza tu narudi.
HJ2: Ngojeni, H1 twende acha uvivu tuwasundikize yupite na resepshen tu print kabisa biarding pass zetu.
Wakanyanyuka tukatoka nao wote mpaka parking wakahug swhiba, wakahakikisha wanachukua namba za simu H1 akamsisitizia, nipo serious kuhusu biashra ya laptos na ikiwezekana hata hilo duka la simu hata huku Unguja nipo tayari kufungua duka, mabo ya mtaji usiwe na shaka, yupo H2 hapa titamkopa, huyu msimuone anakaa kimya tu. Mumewe na amiviwanda mijubwa mij)kubwa anannukia pesa hapa alipo.
Tukaagana wao wakaenda resepshen mimi nikaenda moja kwa moja chumbani kwangu. Nikajimwagia maji ya shower, sikua na haja ya kupiga simu wala nini, nikapiga rakaa zangu nikalala.
...
Khodam ni neno linalotumiwa katika fumbo la Kiislamu na hurejelea aina ya chombo cha kiroho au msaidizi anayeaminika kuwa na uwezo wa kuwasaidia watu binafsi kwenye njia yao ya kiroho. Katika Usufi, ambao ni aina ya mafumbo ya Kiislamu, khodam wakati mwingine hufafanuliwa kama viumbe vya kimalaika au viongozi wa kiroho ambao wanaweza kutoa mwongozo, ulinzi, na usaidizi kwa wale wanaotafutaTupe Kiswahili chake basi kwa faida ya wengi.
Simba.
Mbona umesaini kua ni Simba?Khodam ni neno linalotumiwa katika fumbo la Kiislamu na hurejelea aina ya chombo cha kiroho au msaidizi anayeaminika kuwa na uwezo wa kuwasaidia watu binafsi kwenye njia yao ya kiroho. Katika Usufi, ambao ni aina ya mafumbo ya Kiislamu, khodam wakati mwingine hufafanuliwa kama viumbe vya kimalaika au viongozi wa kiroho ambao wanaweza kutoa mwongozo, ulinzi, na usaidizi kwa wale wanaotafuta
Simba...
Na mimi ni simba vilevile.... Utani ndugu yangu nimeku tag weweMbona umesaini kua ni Simba?
Simba.
Soma tena post #3413 tuliiongezea maini.Simba.. Leo umetuacha sana bila episode hata mbili tatu sheikh...
Mkuu Samahan I! Nina changamoto kubwa kulingana na namna ulivyoeleza na majibu ya arsis nimekua interested sana huenda nkapata nusra kupitia kwenu na sheikh bakoraSoma tena post #3413 tuliiongezea maini.
Simba.
Hii umenikumbusha sana elimu ya masufi.Mwalimu wako uliemfata haelewi.
Mimi nakuuliza maswali, uliwahi kufanya mazoezi ya kuona mbali na kusikiliza vya mbali, au minong'ono au hata kujua mawasiliano ya mnyama yeyote yule?
Simba.
Simba kakumbana na simba.Na mimi ni simba vilevile.... Utani ndugu yangu nimeku tag wewe
Tuendeleee na mjadala tuliokuwa tunaendelea nao.
Asante
Nimemuelewa kuwa hajawahi kujifunza yote uliyomuuliza.Elimu ndio tumeshaianza hapa, Uwe unanisoma kwa makini tu. kama hukuelewa kitu katika maandiko yangu uliza.
Hujawahi nini?
Simba.
Kama sijakosea wewe hapo ulikuwa stage ya pili bro.... baada ya REM unaingia kwenye paralysis (hapa ndo ulikuwa wewe) ukitoka hapo utaingia kwenye vibration na baada ya hapo ndo unapita last stage then boom (maajabu yanaanza😂Duu kwel ulikomaa,ebu niambie ile ganzi ulikomaa nayo ikafika mwili mzima au inashia stage fulani
Ingia tu YouTube kaka.... Mimi nimejifunzia mtandaoni (nilianza na yoga then meditation then lucid dreaming mwisho nikajikuta nimedondokea kwenye astro projection 🤝Acha woga. Hiyo process tuelekezane nifanye nije niwape mrejesho. Ila pasiwepo na ishu za majini