Niliroga sana

Niliroga sana

Umenifanya namimi nianze kuwaza mengine sasa! Shetani shindwa!🙌🏿🏃🏿😂
#DarkFantasy #HornedGoddess #AfroMythic #FantasyAe.jpeg
 
Muda mwingine ni harakati za kimaisha ndio zinapelekea mtu kuroga, fungua biashara uswahilini afu ndio utajua umuhimu wa waganga.
Phone book yako taratibu itaanza kujaa namba waganga, ili wasijulikane utawaita majina kama ostadh.
 
Muda mwingine ni harakati za kimaisha ndio zinapelekea mtu kuroga, fungua biashara uswahilini afu ndio utajua umuhimu wa waganga.
Phone book yako taratibu itaanza kujaa namba waganga, ili wasijulikane utawaita majina kama ostadh.
ili wasijulikane utawaita majina kama ostadh. 😀
 
Niliroga mchana nikaroga usiku, niliroga kushoto nikaroga kulia, niliroga mashariki nikaroga magharibi, niliroga kaskazini nikaroga kusini. Niliroga chini nikaroga juu, niliroga mbele nikaroga nyuma, niliroga jua nikaroga mwezi, niliroga nyota nikaroga mawingu.

Niliroga milima nikaroga mabonde, niliroga bahari nikaroga nchi kavu, niliroga mito nikaroga chemchemi, niliroga upepo nikaroga dhoruba. Niliroga moto nikaroga majivu, niliroga masika nikaroga kiangazi, niliroga kila pembe nikaroga dunia nzima, lakini bado siri haikufunuka wala moyo wangu haukutulia.

Lakini mwisho nilitubu na kumrudia mola wangu, nikaacha giza na kufuata mwanga, nikavunja vibuyu na kutupa matunguli. Nilisafisha mikono yangu kwa maji ya toba, nikapiga magoti kwa unyenyekevu mkuu, nikapokea amani ambayo dunia isingeweza kunipa. Yale yote niliyoyatafuta kwa waganga na ramli, nikayapata bure kwa neema na rehema zake, kwani hakuna mkuu zaidi ya Muumba wa mbingu na ardhi.

Sasa mimi ni mpya na wa nuruni, giza limepita na mambo yote yamekuwa mapya, ninasimama imara katika mstari wa haki. Tabia za kale zimezikwa katika kaburi la historia, mavazi ya huzuni yamevuliwa na nimevikwa vazi la sifa na utukufu. Hatua zangu sasa zinaongozwa na mwanga wa kimungu, kila neno langu linajenga badala ya kubomoa, na moyo wangu umejaa amani tele, furaha isiyo na kifani, na tumaini la milele.
Hongera kwa kuwa mkweli sana, Katika maisha yangu moja ya vitu ambavyo sikuwahi kuamini toka nikiwa mtoto ni uchawi! Nilikuwa naamini na ndivyo ninavyoamini hata sasa siwezi kurogwa! Wakati fulani kazini kwangu kulikuwa na jopo la watu wabadhirifu, niliwasimamisha kazi, lilikuwa kundi la watu wanaogopeka liliongozwa na Mzee mmoja wa kindengereko al maarufu kwa jina la Matimbwa, wakachanga mapesa kwenda kwa mganga hakuna kitu niliona, japo kuna kijana alikuwa rafiki yangu babu yake ni mganga hatari visiwani na wakuu huruka kumfuata, akaniambia niende kwa babu yake anigange, nilimkatalia. Sijawahi kuogopa uchawi .
 
Unajua dini nao ni uchawi?
Hapana, dini si uchawi

Kidini, kihistoria na kisosholojia, mambo haya mawili yana misingi, malengo na taratibu tofauti kabisa.

Angalia tofauti kubwa kati ya dini na uchawi:
1. Chanzo cha Nguvu na Mamlaka
Dini:
Huamini uwepo wa Mungu mmoja au miungu, ambaye ndiye muumba wa vyote na mwenye mamlaka ya mwisho. Waumini humwomba Mungu na kukubali mapenzi yake.

Uchawi:
Hutegemea mbinu za siri, nguvu za kishirikina, au majini/mizimu ili kulazimisha matokeo fulani kutokea. Mchawi anajaribu kudhibiti asili au watu kwa kutumia maarifa yake ya siri.
 
Hongera kwa kuwa mkweli sana, Katika maisha yangu moja ya vitu ambavyo sikuwahi kuamini toka nikiwa mtoto ni uchawi! Nilikuwa naamini na ndivyo ninavyoamini hata sasa siwezi kurogwa! Wakati fulani kazini kwangu kulikuwa na jopo la watu wabadhirifu, niliwasimamisha kazi, lilikuwa kundi la watu wanaogopeka liliongozwa na Mzee mmoja wa kindengereko al maarufu kwa jina la Matimbwa, wakachanga mapesa kwenda kwa mganga hakuna kitu niliona, japo kuna kijana alikuwa rafiki yangu babu yake ni mganga hatari visiwani na wakuu huruka kumfuata, akaniambia niende kwa babu yake anigange, nilimkatalia. Sijawahi kuogopa uchawi .
Uchawi upo na unafanya kazi lakini si kila anayerogwa anarogeka na sababu nyingi mojawapo ikiwa ni ulinzi wa kiroho, usafi wa kiroho.. Imani juu ya Mungu nknk
 
Mtu anayekataa au kusema vibaya Ulozi na ushirikina, ni hayajamkutaa.

Mie na Mambo ya ushirikina ni ulalo ulalooo tuu.
😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom