Nilichofanya leo Mlimani City

Nilichofanya leo Mlimani City

Hivi mnavidharau vyombo vyetu vya usalama?

Au mkiona ndevu tu mnajichatolia?

Hii inanikumbusha kisa cha Singh (singa singa) aliyeuliwa kwa ndevu zake tu baada ya Sept 11. Cha kushangaza katika picha zote zilizotolewa na intelijensia ya USA wale waliodhaniwa kuwa ndiyo wamezipiga zile nyumba za New York hakuna hata mmoja mwenye ndevu na kanzu fupi wala ndefu.

Wasiwasi wako ndiyo maradhi yako.

Hukufanya vibaya kwa kuwa na mawazo ya kizalendo na kujikinga, siku nyingine usitazame wenye ndevu tu na kanzu, wabaya hawana alama.


punguza jazba
 
Ukiachilia mbali kutokuvaa kanzu pia inaonyesha ni watu wenye mbinu sana na mipango yenye ustadi wa hali ya juu ndo ndio sababu unakuta wanafanikiwa kwenye mipango yao.Kama angekuwa mtu mbaya asingetumia mbinu za kitoto kama hizo huyo alikuwa raia mwema tu sema huenda mavazi na ndevu vikachangia kufanya hatiliwe mashaka

Pengine alihitaji mkewe aje kufanya shopping ikabidi ampigie picha ili akifika asihangaike!
 
Hata Wastegate waliona viashiria kama hivi lakini wakadharau.. nasikia hata presidaa aliambiwa ila hawakutilia maanani ikaja kuwacost heavily. Ni muhimu kuwa makini katika kila kitu kusaidia taifa na wengine
 
Mleta mada na wengine, baada ya kuisoma hii report: Undeleted Evidence...: Kenya's Westgate Mall False Flag

Na baada ya kuisoma mada yako, kuna uwezekano huyo jamaa alikuwa anafanya makusudi, kwanza jinsi alivyovaa, kuna kila uwezekano alikuwa anafanya makusudi yatokee yaliyotokea. A "rise attention", aonekane, apigwe picha awe "suspected" na hata akamatwe.

Chakujiuliza, kwanini?

Jamaa anaonesha yuko fit physically na anaonesha ni mtu wa mazoezi kwa posture zake tu.

Nnakupongeza kuliona hilo na atafutwe na afanyiwe uchunguzi wa kina.
 
Bila shaka kama angekuwa mzungu asingeangaika nae kilichompa utata ni ndevu na kanzu tunawaambia hatutaacha kuziachia ndevu na....
 
Ndugu Pongezi sana, Ulichofanya mimi nadhani ungekifikisha Mbele zaidi. Hayo majibu aliyotoa na kupelekea kufuta picha ni suspicious tosha kwa huyo jamaa kuwafanyiwa Interrogation zaidi kwa ajili ya kupata taarifa za kiintelejensia Kama issue nzima itawafikisha kwenye Ukweli huo. Big up man. Bong Security yetu bado sana, kwanza iko lagged behind na Technology.
 
Hawa walinzi wetu wa makampuni ya ulinzi wengi wao ni heri hata ya MGAMBO WA CITY kiufanisi:-(
 
Bila shaka kama angekuwa mzungu asingeangaika nae kilichompa utata ni ndevu na kanzu tunawaambia hatutaacha kuziachia ndevu na....

Acha nasi tuku harass tu..hamna namna nyingine,,
Maana ata kama mtu mkristo,,akivaa kama kadinali maeneo ya public service lazma ata raise attention...nasi tutachukua jukumu lakumhoji pembeni
 
hongera sana watu wengi hawajali usalama usalama wa nchi yetu hao askari ni wazembe hongera kwa hilo
 
mmh isije ikawa alshababu huyo anafanya uchunguzi kwa mda then anakinukisha? mmh nshaogopa tayari sigusi tena pale dadeki!
 
tena mkuu kama angekushtukia unampiga ungemwambia its A PRANK!!!
 
jamaa mwenyewe sura yake tu inamshitaki-ungemuitia polisi kabisa ili wadili naye na aongee vizuri hizo picha napeleka wapi,
 
Safi sana, Naona Magufuli anarudisha Uzalendo kwa vijana!
 
Tukio la westgate nikikumbuka shopping nitaendelea tu kununua vitu tandale
 
Back
Top Bottom