Mkuu Monaco,
Ulichokifanya umetimiza wajibu wako wa kusaidia kutoa taarifa za kuwepo kwa mtu unaemshuku na bahati nzuri askari au walinzi nao walikwishamgundua nyendo zake.
Hio ni kazi nzuri na uendelee na moyo huo.
Hao askari au walinzi nao wametekeleza wajibu wao wa kumsimamisha na kumhoji huyo jamaa na hatiame kumwamuru afute picha zote alizopiga akiwa ndani ya Mlimani City na kwa kweli hawawezi kwenda mbali zaidi kwakuwa mtu huyo hajatenda kosa.
Nafikiri wamiliki wa Mlimani City wataona bandiko lako na watachukua hatua zaidi za kuweka tahadhari kwa watalii wa sehemu hiyo na watumiaji wengine.
1. Alama za kutahadharisha na kuonya kuhusu kuchukua picha, kwamba hairuhusiwi.
2. Kuonya kwamba yeyote anaeingia humo Mlimani City tayari anakuwa ameridhia kuchukuliwa picha na kufuatiliwa kwenye CCTV.
3. Onyo kwenye nembo kwamba CCTV ipo kwa ajili ya kutambua, kubaini na kulinda dhidi ya vitendo vya uhalifu na kwamba picha na video za CCTV zitatumika mahakamani.
Ila unafaaa sana kwa kazi za ulinzi nakupa 5