Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 18,081
- 12,238
Ndugu zangu Watanzania,
CHADEMA ni chama cha ajabu sana,ni chama kinachotia aibu sana,ni chama kinacholeta fedheha kubwa sana,ni chama kinachoendeshwa na kwenda utafikiri mtu aliyepofuka macho,ni chama kisicho heshimu hata uwepo wa viongozi wake wa ngazi za juu,ni chama ambacho kinawakatisha na kuwavunja moyo wafuasi wake kila uchwao,ni chama kilichojaa ubabaishaji na janja janja sana.
Nimeshangaa kutazama video ikionyesha wafuasi na wanachama wa CHADEMA wakijaribu kupigana ngumi huku wakishikwa na kuzuiwa na wenzao katika uchaguzi ambao umeishia kuvunjika kwa mara ya pili tena baada ya kutokea kwa vurugu huko mkoani Njombe.
Kikao ambacho alikuwepo pia Naibu katibu mkuu wake Bara Benson Kigaila. Mambo ambayo kamwe na katu huwezi kuyaona yakitokea wala kufanyika ndani ya CCM. huwezi ukakuta mambo ya aibu kiasi kile cha kuzua vurugu mbele ya kiongozi wa kitaifa yakitokea. Sasa leo CHADEMA inashindwa kusimamia hata suala dogo tu la uchanguzi wa ndani na kuishia kuvunjika.
Kigaila mwenyewe ni kama haeleweki na haelewi afanye nini kusimamia uchaguzi ufanyike na kumalizika kwa amani. Maana nilipomsikiliza akizungumza nikagundua hata yeye anaweza kuwa sehemu ya chanzo cha vurugu.kwa sababu ilitakiwa awasomee wajumbe kanuni zinazoongoza uchaguzi huo kwa mujibu wa katiba ya chama .ilitakiwa aeleze waziwazi kabisa ni nani ni wajumbe halali na wanapatikanaje. Badala ya kutumia maneno ya ubabe na vitisho jambo ambalo wajumbe wamegoma kukubaliana nalo.
Hivi CHADEMA ni lini chama hiki kitakomaa? Ni lini chama hiki kitaacha ubabaishaji na vululu vululu? CHADEMA ni chama cha ajabu na kilichokosa muelekeo na Dira. Nimewasikia wajumbe pia wakilalamika pia kuwa kuna kiongozi mkubwa wa juu ndio anavuruga uchaguzi huo kwa maslahi yake .
CHADEMA ina mengi sana ya kujifunza kutoka kwa CCM chama kiongozi barani Afrika na mfano wa kuigwa DUNIANI kwote. Ndio maana wanachadema wengi sana wanaendelea kumiminika kwa wingi sana kuchukua kadi za CCM kuwa wanachama wake ,baada ya kuwa wamechoka na ubabaishaji unaofanyika na kuendelea ndani ya CHADEMA.
Nachukua nafasi hii kuwakaribisheni ndani ya CCM wana CHADEMA wote waliochoshwa na ubabaishaji wa huko.njooni tujenge nchi yetu,njooni tuungane na Mama yetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan mama mwenye upendo na uzalendo wa dhati kwa Taifa letu. Nendeni kwenye matawi ya CCM mchukue kadi na kuungana na mamillioni ya wazalendo waliopo ndani ya CCM.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
CHADEMA ni chama cha ajabu sana,ni chama kinachotia aibu sana,ni chama kinacholeta fedheha kubwa sana,ni chama kinachoendeshwa na kwenda utafikiri mtu aliyepofuka macho,ni chama kisicho heshimu hata uwepo wa viongozi wake wa ngazi za juu,ni chama ambacho kinawakatisha na kuwavunja moyo wafuasi wake kila uchwao,ni chama kilichojaa ubabaishaji na janja janja sana.
Nimeshangaa kutazama video ikionyesha wafuasi na wanachama wa CHADEMA wakijaribu kupigana ngumi huku wakishikwa na kuzuiwa na wenzao katika uchaguzi ambao umeishia kuvunjika kwa mara ya pili tena baada ya kutokea kwa vurugu huko mkoani Njombe.
Kikao ambacho alikuwepo pia Naibu katibu mkuu wake Bara Benson Kigaila. Mambo ambayo kamwe na katu huwezi kuyaona yakitokea wala kufanyika ndani ya CCM. huwezi ukakuta mambo ya aibu kiasi kile cha kuzua vurugu mbele ya kiongozi wa kitaifa yakitokea. Sasa leo CHADEMA inashindwa kusimamia hata suala dogo tu la uchanguzi wa ndani na kuishia kuvunjika.
Kigaila mwenyewe ni kama haeleweki na haelewi afanye nini kusimamia uchaguzi ufanyike na kumalizika kwa amani. Maana nilipomsikiliza akizungumza nikagundua hata yeye anaweza kuwa sehemu ya chanzo cha vurugu.kwa sababu ilitakiwa awasomee wajumbe kanuni zinazoongoza uchaguzi huo kwa mujibu wa katiba ya chama .ilitakiwa aeleze waziwazi kabisa ni nani ni wajumbe halali na wanapatikanaje. Badala ya kutumia maneno ya ubabe na vitisho jambo ambalo wajumbe wamegoma kukubaliana nalo.
Hivi CHADEMA ni lini chama hiki kitakomaa? Ni lini chama hiki kitaacha ubabaishaji na vululu vululu? CHADEMA ni chama cha ajabu na kilichokosa muelekeo na Dira. Nimewasikia wajumbe pia wakilalamika pia kuwa kuna kiongozi mkubwa wa juu ndio anavuruga uchaguzi huo kwa maslahi yake .
CHADEMA ina mengi sana ya kujifunza kutoka kwa CCM chama kiongozi barani Afrika na mfano wa kuigwa DUNIANI kwote. Ndio maana wanachadema wengi sana wanaendelea kumiminika kwa wingi sana kuchukua kadi za CCM kuwa wanachama wake ,baada ya kuwa wamechoka na ubabaishaji unaofanyika na kuendelea ndani ya CHADEMA.
Nachukua nafasi hii kuwakaribisheni ndani ya CCM wana CHADEMA wote waliochoshwa na ubabaishaji wa huko.njooni tujenge nchi yetu,njooni tuungane na Mama yetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan mama mwenye upendo na uzalendo wa dhati kwa Taifa letu. Nendeni kwenye matawi ya CCM mchukue kadi na kuungana na mamillioni ya wazalendo waliopo ndani ya CCM.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.