Ndugulile: WhatsApp call zimeathiri simu za nje

Ndugulile: WhatsApp call zimeathiri simu za nje

Ongezeni ubunifu katika kutafuta maendeleo sio kutafuta mtu anayetukana mitandaoni....!!!
acheni kujikita kwenye mambo ambayo hayana economic value
 
Binafsi namuona huyu Waziri kama mshamba, kiherehere na Mwenye kujipendekeza tu. Hana msaada wowote wa kitaalam ktk Wizara.
Yy ni kudhibiti tu. Haongelei Kasi ya Internet, connection ya Mkonga wa Taifa wa mawasiliano ktk familia (kama Kenya), nk...
Umemaliza mkuu umeandika vizuri sana.
 
ama kweli bora kuzaliwa mbwa ulaya kuliko binadamu africa, tunarud enzi za ujima ndugu zangu,tutaambiwa tuanze kulipia na text za whatsapp sasa
 
Teknolojia hiyoooo imekua
Zamani kupiga international call ilikuwa
Ghali sana mpaka kufanya watu kuunganisha
Na kuwapigisha sim kutumia line za uwizi
Wateja
Teknolojia kukua imeondoa automatically hali hiyo

Ova
hawafikirii ni biashara ngapi zimefanikiwa kwa kurahisishwa mawasiliano kupitia whatsap!!

Ila hawa wenzetu wanawaza kwa kutumia nini?
why are they this negative?!!!
 
Huyo alitakiwa abaki kwenye afya, huko kwingine atapuyanga sana
Hii wizara ilitakiwa akae kijana wa kisasa msomi mwenye exposure .....
mwenye kujua fursa zinazopatikana kupitia maendeleo ya technologia
ili kupunguza tatizo la ajira nchini
 
Je ulifuatilia Action za Google na Fb baadae? Serikali yao ikawa inalialia tu tena!
 
Ile shit hole country imepatikana
 
Mh hajiulizi kwanini gharama za kupiga simu Tz kutokan nje ni kubwa kuliko EAC na SADC kwa ujumla

Kwanini Watanzania wanendekeza roho za korosho kama hizi, yaani anaona kulipia bundle haitoshi lazima yawepo mapato mengine kwa maana gharama zaidi kwa watumiaji.

Mambo kama haya yanafanya kila taasisi, shirika au kampuni inayokuja EAC kuweka kambi Nairobi.

Tunakuwa vituko tuu duniani kila siku na kila nyanja

JokaKuu

Ndio maana wafanyabiashara wengi wanahamishia biashara zao nje ya nchi, huku sheria zinawabana na kuwaumiza. si TRA wala TCRA wote majanga.
Kuna watu hata kufikiri inakuwa shida mradi waropoke kinachotoka kinywani
Dunia inasonga mbele kwa kurahisisha mambo sisi wanataka tuendelee na jembe la mkono tu

Huyo ndugulile akumbuke wakina nani wamemchagua, aise sifa haimwachi mtu salama....siku wakimtema sijui atapeleka wapi uso wake kwa fedheha. Ajitathmini upya
 
Je ulifuatilia Action za Google na Fb baadae? Serikali yao ikawa inalialia tu tena!
Google walikubali na wako kwenye mazungumzo (possibly wamemshakubaliana) na kampuni za habari Australia wawalipe. FB walitingisha kiberiti waka backoff.

Nadhani waliona local innovation na innovators wengine wanachukua soko wakaona heri wakubali shari iishe.
 
Kwenye interview na Dr. Nduguile hapa karibu wamedai kuwa mapato ya international calls yameshuka sana hapa karibuni baada ya ujio wa WhatsApp calls. Watu wanatumia WhatsApp calls na hawalipii tena international calls. Pia wanadai kuwa hawawezi ku monitor utapeli kupitia WhatsApp calls. Hvyo wanataka kuweka makato kwa WhatsApp calls (tofauti na bundle) na kuwa na uwezo wa ku monitor hzi WhatsApp calls.

Habari kamili hapa: Tanzania mulls over charging whatsApp calls due to falling revenue from International calls

Je, mnaona hii ni sawa kweli?

Je, WhatsApp (Facebook) watakubali kuwapa access ya WhatsApp call ukizingatia kwamba hapa karibuni WhatsApp wameweka end to end encryption ya calls?

Kwanini serikali inataka kuingilia service za watu kwa sababu wanaona hawana control na hawanufaiki directly.

Mimi binafsi sioni kma hii ni sawa. Hii ni njia tu ya kutaka kunyonya watu hela zaidi na kumonitor private conversations za watu. Ukizingatia kwamba hakuna sheria zozote za privacy zinazomlinda mwananchi dhidi ya serikali.

Naona mwaka huu wamejipanga kutunyonya hela mpaka tukome. Kma watu hawaridhiki na hzo bei za international calls na service inayotolewa wako huru kutafta njia nyingine ya mawasiliano bila kuwekewa vikwazo.

Kwa namna hii hatutakuja endelea kwenye technology hapa Tanzania. Baadala ya ku embrace new technologies tunataka kuzikandamiza ili mabeberu waendelee kufaidika huku wakiumiza walalahoi.
 
Huyu waziri nilikuwa namuheshimu lakini sasa hivi nimemuweka kundi moja na akina Del Kisandu
 
Technology inabadilika haraka sana mnataka zile enzi za kuomba simu za nje control room ya TTCL zirudi?
 
Dunia inakimbia mbele kwa kasi sisi tunatafuta namna ya kurudi nyuma kwa kasi.

Basi mfumo wa mawasiliano ya barua kwa posta na call box nayo yarudi tuziondoe kabisa mobile phones.
 
Back
Top Bottom