Donnie Charlie
JF-Expert Member
- Sep 16, 2009
- 15,159
- 16,243
kuanzia sasa mpe nauli tu ya kuendea kwenye interview zake
Mi pia leo kuna rafiki kaniambia anaomba hata ya kufagia...Inauma ila no way , asubuhi ya leo rafiki yangu anaomba hata nikisikia kazi za ulinzi wa nyumba ya mtu alafu ni mdqda dah nilijisikia vibaya sana
Alafu kuna kakiumbe kamoja kanakataa kazi , world is not fair anymore
Ana ndugu wengi huyuu atoe mchongoMkuu weka hapa hiyo fursa ya Kazi humu pia sote ni ndugu zako.
Sio vichaa ila ni wasaka notiMuache achapike na maisha miaka kama 7 mbele hivi bila ajira ndio atakapojua kumbe waokota makopo sio vichaa
Mwache.kamaliza chuo mwaka juzi ila hadi sasa hana shughuli, alikuja hapa mjini pasaka mwaka jana ila nikamwambia abaki baki ajiskie huru hasa ukizingatia nyumbani kwangu kuna vyumba vya nje kwa hio haikuwa taabu kumuhifadhi. sina ubaya wala hila, mimi kila wiki huwa nampa 50 kwajili ya matumizi, kuna kipindi nikiwa chuoni mwaka wa mwisho nilikosa kabisa ada kama laki 6 hivi, mama yake aliniokoa, hivyo mama yake ana mchango mkubwa.
alikuwa ananiambia ana apply kazi serikalini lakini kwa hali ilivyo nilimwambia ajira ziekuwa ngumu hivyo nimtaftie, ni kama mara 2 hivi nilitaka kumsaidia mchongo ila alikuwa anakazia kwamba kuna interview anakaribia kuitwa.
Basi mimi nikaamua nimtaftie kazi sehemu ya mtu tunaejuana (connection) ila pia tuna undugu pia kwa mbali, sehemu ile kazi huwa ni jumatatu hadi ijumaa saa 1 na nusu hadi saa 12 jioni.. na jumamosi huwa ni saa tatu hadi saa nane hivi.
Mshahara ni laki 3 na kitu ila haujazidi 350k.
Sasa nilipompa hii habari ni kama hajaichukulia vizuri, alipoanza kuniambia nisubiri subiri kuna interview anaisikilizia nikamwambia wala asiwe na hofu, akiitwa kwenye interiew ataenda ila hii kazi inabidi aianze,, kiukweli kwa jinsi alivyochukulia hisi suala ni wazi kabisa ni kama vile haitaki.
Jana ndio nimefowadiwa mesej screenshot analalamika kwamba namfanyia manyanyaso kwamba kazi ina mda kidogo wa kupumzika, malipo kidogo, n.k.
Sawasawa na kuja kumringishia mlevi chupa ya bia , akiwa mjanja atawapiga hata pesa ya mboga ya udalali mPM ya mkuu itakuwa imefurika...
Ajira zilivyo ngumu...
Connection tuu ndo uchawi...
Ndy hivyo tena no way , ila sisi vijana kuna haja ya kusaidiwa labda kuambiwa maisha sasa sio ya kujilegeza tena .Mi pia leo kuna rafiki kaniambia anaomba hata ya kufagia...
Imeniuma...
KweliMkuu weka hapa hiyo fursa ya Kazi humu pia sote ni ndugu zako.
Hatari sanalazima...ugali wa bure