Ndugu unaempa mtaji ajitegemee anaanza upya kukuomba pesa hana mshipa wa aibu?

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,033
Ni ndugu yangu mwenye miaka 26, kamaliza chuo mwaka juzi.

Hapo zamani mara kwa mara alikuwa akiniomba pesa za kutatua shida zake, hizi elfu 20 nimemtumia sana.

Nikaona isiwe taabu, kitu anachoomba ni kama samaki naowavua basi nayeye nimpe ndoano awe anajivulia, Tulikaa chini pamoja nikamuuliza kama yupo tayari kufanya biashara, hili ndio lilikuwa swali la msingi zaidi maana asije kuwa na mambo yake yatayomtinga, akasema yupo tayari. Swali la pili nikamwambia aende kujitafakari vizuri anataka kufanya biashara ipi ya mtaji wa milioni 4 za kununulia mzigo jibu anipe baada ya wiki, biashara aliyochagua ni nzuri tu sikuwa na shaka nayo.

Katika maandalizi ya kumfungulia duka niligharamika takribani milioni 1 na nusu ya ziada kulipia kodi ya miezi 6 ya fremu, mafundi wa mbao, makufuli imara, kabati la bidhaa, kusajili biashara, leseni ya biashara, kupata tin ya eneo la biashara, tax clearance, n.k.

Biashara akaanza rasmi nami nilipata furaha mno kuona ndugu yangu nae kaanza safari ya kujitegemea kama mwanaume kamili.

Ajabu ni kwamba baada ya miezi kadhaa akaanza upya kuniomba hizi 10 mara 20, n.k.

Baada ya uchunguzi nimekuja kujua kwamba alianza kutumia pesa kuzidi faida anayoingiza, strarehe !

Undugu wetu upo pale pale, wala hatujavunja undugu, wala simdai hata shilingi 50, naumia kuona tu kwamba ndugu yangu pamoja na usomi wake nilitegemea atachangamkia hii fursa ili na yeye aanze kufaidi maokoto yake ila imekuwa ndivyo sivyo, Malengo yangu yalikuwa kwamba huyu akianza kujitegemea nisaidie wengine na pengine nae awe msaada kwa wengine ila ndio hivyo tena !! Ile milioni 5.5 inaweza kuwa ndogo kama unajijali peke yako lakini kiasi hiki kinaweza kusaidia watu wenye shida nayo, mfano nina baadhi ya ndugu kijijini wanachota maji mbali, ingetumika kuchimba kisima ingekuwa msaada mkubwa, muda wa kwenda kuchota maji watu wangetumia kupata kufanya shughuli zingine, hatari za kwenda kuchota maji umbali mrefu zingekwepeka, n.k.

Hana mshipa wa aibu??
 
Undugu kazi sana, Million 4 inafanya unatangazwa hadi Jamii Forum. Damu nzito kuliko hata hio hela.
Wewe kuwa ndugu yangu siyo kwamba mimi ndiyo nna jukumu la kukulea wewe ikitokea nimekusaidia ni bahati tu
Umebahatika kuwa na ndugu kama mimi na ambaye nimekusaidia lakini siyo haki yako sana kwamba uanze kulazimisha kusaidiwa
Damu ni nzito kuliko maji pande zote

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Ni ndugu yangu ana mwenye miaka 26, kamaliza chuo mwaka juzi.

Hapo zamani mara wa mara alikuwa akiniomba pesa za kutatua shida zake, hizi elfu 20 nimemtumia sana.

Nikaona isiwe taabu nikampa mtaji wa milioni 4 pesa taslimu ili nae afanye biashara aweze kujitegemea, nilimuasa sana kwamba pesa hizo ndio maisha yake asije akazichezea.. Wazee wenye hekima waliwahi kusema ni heri mtu ajifunze kujivulia samaki kuliko kupewa dagaa.

Nje ya mtaji nilimsaidia kulipia fremu miezi 6, mafundi wa mbao, makufuli mazuri, kabati, kusajili biashara, kupata leseni ya biashra, kupata tin ya Tra mpaka tax clearance ya kulipia kodi.

Ajabu ni kwamba kaanza upya kuniomba hizi 10 mara 20, n.k.

Kilichonisukuma ili nimsaidie si kwamba mimi ni tajiri, NO!! hio pesa na muda niliompa kumsaidia ilibidi nisitishe mambo yangu kadhaa, Lengo kuu lilikuwa kumfanya ajitegemee maana wahenga walisema mtegemea cha ndugu anaweza kufa masikini, ila sasa nasikitika sana anarudi kule kule,

Hana mshipa wa aibu ??
Mbona hata serikali yetu inapewa trilions of coins lakini haiishi kupitisha bakuli, huenda huyo ulliyemsaidia hajafikia malengo, kaa naye msikilize
 
Ni ndugu yangu ana mwenye miaka 26, kamaliza chuo mwaka juzi.

Hapo zamani mara wa mara alikuwa akiniomba pesa za kutatua shida zake, hizi elfu 20 nimemtumia sana.

Nikaona isiwe taabu nikampa mtaji wa milioni 4 pesa taslimu ili nae afanye biashara aweze kujitegemea, nilimuasa sana kwamba pesa hizo ndio maisha yake asije akazichezea.. Wazee wenye hekima waliwahi kusema ni heri mtu ajifunze kujivulia samaki kuliko kupewa dagaa.

Ile milioni 4 kwakuwa ilikuwa ya mtaji sikutaka ipungue, nikafharamia takribani milioni 1.5 nililipia kodi ya miezi 6 ya fremu aliyoitafuta, mafundi wa mbao, makufuli imara, kabati la bidhaa, kusajili biashara, leseni ya biashara, kupata tin ya eneo la biashara, tax clearance, kiti, n.k.

Ajabu ni kwamba kaanza upya kuniomba hizi 10 mara 20, n.k.

Kilichonisukuma ili nimsaidie si kwamba mimi ni tajiri, NO!! hio pesa na muda niliompa kumsaidia ilibidi nisitishe mambo yangu kadhaa, Lengo kuu lilikuwa kumfanya ajitegemee maana wahenga walisema mtegemea cha ndugu anaweza kufa masikini, ila sasa nasikitika sana anarudi kule kule,

Hana mshipa wa aibu ??
Mvizie halafu gonga nyundo ya kupasulia mawe kwenye kidole kikubwa cha mguu mpaka kiwe kama chapati lile jini la kukopela litamtoka.Nyau sana huyo.
 
Back
Top Bottom