TAJIRI MKUU WA MATAJIRI
JF-Expert Member
- Dec 1, 2010
- 5,721
- 10,220
Nimeota tumepewa paund 200 na bibi yangu, kila mmoja, mama yangu, mimi na mdogo wangu.
Niko kwenye eneo kùbwa la wazi, ni kama karakana, supervisor mzungu akanifuata akaniambia niondoke hapo mara moja. Hali ni mbaya sana nitafute eneo salama.
Nikaingia ndani ya nyumba, na mara ghafla mvua kubwa sana ikaanza kunyesha.
Nyumba ilikuwa ikivuja sana nikaamua kwenda nje nitafute sehemu nitakayoweza kujisitiri.
Baada ya kutoka nje hatua chache nikaona maji yametengeneza mto mkubwa sana sehemu ambayo haijawahi kuwa mto. Nikaogopa.
Nikaamua kurudi nilikotoka. Maji yakawa yameongezeka sana, na mara ghafla nyumba ikaanza kuungua.
Nikawa napiga kelele za moto, moto, moto hamna anayeitikia na kuja kunisaidia.
Nikaamua niende kupanda ukuta wa fence, nao ukaanza kuwaka moto.
Sasa moto ukawa unawaka kwenye kila nyumba. Moto unatoka angani, umesambaa kila mahali, hamna pa kujificha.
Moto unashuka mithili ya mvua, nikasema kufa ndio huku.
Nikaanza kumwambia Mungu, kwa hiyo ndio umeamua tufe? Mungu akasema hata wakati wa gharika wapo waliopona.
Hata nilipoteketeza Sodoma na Gomora wapo waliopona.
Nikashtuka na kujikuta nimelowa sana jasho.
Niko kwenye eneo kùbwa la wazi, ni kama karakana, supervisor mzungu akanifuata akaniambia niondoke hapo mara moja. Hali ni mbaya sana nitafute eneo salama.
Nikaingia ndani ya nyumba, na mara ghafla mvua kubwa sana ikaanza kunyesha.
Nyumba ilikuwa ikivuja sana nikaamua kwenda nje nitafute sehemu nitakayoweza kujisitiri.
Baada ya kutoka nje hatua chache nikaona maji yametengeneza mto mkubwa sana sehemu ambayo haijawahi kuwa mto. Nikaogopa.
Nikaamua kurudi nilikotoka. Maji yakawa yameongezeka sana, na mara ghafla nyumba ikaanza kuungua.
Nikawa napiga kelele za moto, moto, moto hamna anayeitikia na kuja kunisaidia.
Nikaamua niende kupanda ukuta wa fence, nao ukaanza kuwaka moto.
Sasa moto ukawa unawaka kwenye kila nyumba. Moto unatoka angani, umesambaa kila mahali, hamna pa kujificha.
Moto unashuka mithili ya mvua, nikasema kufa ndio huku.
Nikaanza kumwambia Mungu, kwa hiyo ndio umeamua tufe? Mungu akasema hata wakati wa gharika wapo waliopona.
Hata nilipoteketeza Sodoma na Gomora wapo waliopona.
Nikashtuka na kujikuta nimelowa sana jasho.