Ndesamburo anunua helkopta za kampeni Chadema

Nimeipenda hii line of thought, na ingekuwa bora kuiangalia vizuri. Swali la Ufadhili wa vyama vya siasi ni muhimu sana katika nchi inayofuata mfumo wa demokrasia. Ishu inakuja hasa kwenye swali la wafadhili na remuneration. Mara nyingi wafadhili watapenda kupata something in return na ndio kilicholeta hili swali la kwanza...

Jibu la Balantanda ni zuri lakini limeacha mengi wazi...


Kwa mfano: Je ni haki ya mfadhili kuwa remunirated? Na kama ni haki/sawa, ni remuniration gani inayokubalika?
Umejibu swali kwa kusema jirani(CCM) anafanya, hivyo ni haki kwa Chadema nao kufanya hivyo. Okay...Lakini katika jibu umeingiza neno UFISADI. This takes the conversation katika direction nyingine.
Kwanza, kwangu mimi neno UFISADI = the use of public funds for private benefit. Hivyo katika jibu lako, ume-imply kuwa ni haki kuwarudishia Wafadhili chao hata kama itafikia kiwango cha kuwapa Mali ya Umma. Nadhani hapo tunakuwa tumevuka mpaka. Kuendesha vyama vya siasi ina cost kubwa, na ndio maana kila chama kina power base yake, ambayo kwa mara nyingi ndio wafadhili wao. Kwa mfano katika nchi zilizoendelea kisiasi, unakuta chama chenye policies za kibepari huwa na wafadhili wengi kutoka watu wa business class - yani watakao faidi matunda ya policies za chama. Hivyo hii relationship kati ya Chama na Wafadhili inakuwa ipo katika level ya 'strach my back and i will scratch yours'. Lakini relationship hii inafikia kikwamo pale Chama kitakapotumia Mali ya Umma katika kuwa-remunerate Wafadhili. Nadhani jibu la MWJJ limeongelea hichi:

vyama vyote vya siasa duniani vina wafadhili wake, na ndio wafadhali wakubwa wana sauti zaidi kwenye vyama hivyo na huzawadiwa nafasi mbalimbali tena kwa uwazi. Lakini kwenye nchi za kidemokrasia mfadhili ni lazima awe yule ambaye hana tuhuma za ufisadi au uvunjaji wa sheria au kuhusishwa na mambo yaliyo kinyume. Ndio maana kwenye nchi kama Marekani mfadhili akigundulika kuwa si "msafi" mgombea au kiongozi hulazimika kurudisha ufadhili wake![/quote]

Solution ya hili tatizo:
1. Kuweka expenditure limits katika kampeni
2. Ku-fund Vyama vya Siasi kwa pesa ya Umma pekee.
3. Kuweka hesabu za vyama wazi kwa lengo la kujua wafadhili wao, na kuweka heavy penalties kwa vyama vitakavyoficha hesabu kwa mfano kushindwa kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao, nk.

Kuchukulia hili swala ki-lele mama ni kuonyesha kutokukomaa kisiasi. Ni wazi kuwa Wafadhili ni watu muhimu sana, hasa ukizingatia gharama za kuendesha vyama, na cost za kampeni. Lakini, kesho kutwa mtoto wa Ndesa akipewa Contract ya ku-supply umeme, nk nchi nzima, msishangae. Kwa maoni yangu, hii ndio mbegu ya Ufisadi. Na tukikaa kimya ni kuipalilia. Kama kutakuwa na uwazi na uwezo wa ku-trace hizi relationship, itakuwa step kubwa sana ya kupambana na Ufisadi.
comment of the week
stunning
safi sana
 
tunachotaka ni utumiaji wa fedha kwa usahi najua hata ulaya watu wanafanya fund raising kupata pesa za kampani na wengine wanakopa, lakini wanazingatia sana idadi ya pesa watakayo tumia....for me kuna mengi chadema wanatakiwa kufanya kuliko kununua helkopta...me metoa mfano wa shule za abino na ndo naung'ang'ania huo kwani ndo jambo linalo ikumba taifa kwa sasa.......

wajenge shule za albino wakati CCM inafanya nini.We lala bana unaudhi watu tu hapa.tuache na CHADEMA yetu na wewe kaa na li CCM lako
 
sio kila kitu what ccm does ndo wapinzani waige usikurupuke mkuu
hongera kwa kuwa chadema me i'vnt decided yet
namaana helkopta si muhimkama matatizo yaliyopo sasa
 
Nimeipenda hii line of thought, na ingekuwa bora kuiangalia vizuri. Swali la Ufadhili wa vyama vya siasi ni muhimu sana katika nchi inayofuata mfumo wa demokrasia. Ishu inakuja hasa kwenye swali la wafadhili na remuneration. Mara nyingi wafadhili watapenda kupata something in return na ndio kilicholeta hili swali la kwanza...

Jibu la Balantanda ni zuri lakini limeacha mengi wazi...


Kwa mfano: Je ni haki ya mfadhili kuwa remunirated? Na kama ni haki/sawa, ni remuniration gani inayokubalika?
Umejibu swali kwa kusema jirani(CCM) anafanya, hivyo ni haki kwa Chadema nao kufanya hivyo. Okay...Lakini katika jibu umeingiza neno UFISADI. This takes the conversation katika direction nyingine.
Kwanza, kwangu mimi neno UFISADI = the use of public funds for private benefit. Hivyo katika jibu lako, ume-imply kuwa ni haki kuwarudishia Wafadhili chao hata kama itafikia kiwango cha kuwapa Mali ya Umma. Nadhani hapo tunakuwa tumevuka mpaka. Kuendesha vyama vya siasi ina cost kubwa, na ndio maana kila chama kina power base yake, ambayo kwa mara nyingi ndio wafadhili wao. Kwa mfano katika nchi zilizoendelea kisiasi, unakuta chama chenye policies za kibepari huwa na wafadhili wengi kutoka watu wa business class - yani watakao faidi matunda ya policies za chama. Hivyo hii relationship kati ya Chama na Wafadhili inakuwa ipo katika level ya 'strach my back and i will scratch yours'. Lakini relationship hii inafikia kikwamo pale Chama kitakapotumia Mali ya Umma katika kuwa-remunerate Wafadhili. Nadhani jibu la MWJJ limeongelea hichi:


comment of the week
stunning
safi sana

Bonyeza kile kitufe cha thanks basi...hahahaha
 
Hivi nchini kwetu hawajaona umuhimu wa kuwepo regulatory body especially kwenye hii misaada kwa chama au mgombea. Maana mtu anapofikia kutoa milioni mia nne kwa chama unategemea utamnyamazisha pale atakapodai kitu fulani ndani ya chama au kwa muhusika?
Hii ni hatari sana kwa demokrasia.
 
Ni mwanzo mzuri...... kama chama lazima wawe na vitendea kazi ili kurahisisha kazi zao kwa sababu CCM wananjenga barabara bagamoyo tu.
 
sijasema kuwa CCM wapo sawa, mpaka sasa CCM 0 upinzani 0, ila tukipata chama bora ambacho kitamwakilisha kila mtanzania itakua CCM 0 upinzani 1...lakini kwa sasa chama tawala tulicho nacho hakina dira ya maendeleo, na upinzani bado hawapo kikamilifu..chakufanya ni kuunda chama kipya tu..au alternatively kujikita saana kwemye ubunge
pia vyama hivi vituonyeshe mfano ambao uwe tofauti na CCM na si kurudia madudu ya CCM

Hicho chama hakiwezi kushuka toka Mbinguni Mkuu, ni lazima kijengwe na Binadamu kama wewe, na kumbuka kuwa binadamu hao hawakusanyi kodi, so wanategemea zaidi Michango ya watu kama Nyinyi akina Semenya ili waweze kufika sehemu Mbalimbali za Nchi na wakiweza kuwafikia wananchi tukapata uwakilishi mzuri hapo ndipo hizo result ( matokeo) yako yataonekana.

Huwezi kulalamika eti wajenge Shule kwani wao ndio wanakusanya Kodi? Hivi unajua maana ya Serikali kukusanya Kodi wewe?
 
Ni mwanzo mzuri...... kama chama lazima wawe na vitendea kazi ili kurahisisha kazi zao kwa sababu CCM wananjenga barabara bagamoyo tu.


Mkuu magezi nimeipenda hii sana sana mkuu . Ni kweli CCM sasa kila kitu Bwagamoyo .
 
sio kila kitu what ccm does ndo wapinzani waige usikurupuke mkuu
hongera kwa kuwa chadema me i'vnt decided yet
namaana helkopta si muhimkama matatizo yaliyopo sasa

Semenya,kuwafikia wananchi na kuwaeleza kuwa matatizo yaliyopo sasa yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na upigaji kura wao si muhimu?
 
Haya ni matokeo ya nadharia za sasa ya CHADEMA kuhusu watanzania

  • Halaiki ya mashabiki na wafuasi katika siasa za kitanzania inavutwa na kitu ambacho wengi wangependa kukiona kwa karibu, mf.Helkopta
  • Halaiki ya wafuasi na wanachama katika siasa za kitanzania inapenda kujitambulisha na chama kinachomiliki mali inayoashiria ukwasi wa chama husika,mf.Helkopta
 
Ndesa anatengeneza justification ya kutafuna pesa za kampeni za Chadema kwa kisingizio cha mafuta na matengenezo ya Chopa. Wajinga ndio waliwao, chambo cha maini hicho mzee Ndesa atakamua ki ulaini ( off course akishirikiana na Mbowe )
 
kumbe ccm ina wafadhili!!!
mimi nilikuwa sijui
mtu anakuibia bilioni 4 halafu baadae anakuja anakupa mil 400 ili usimshitaki, ukishapokea hiyo hela badala ya kumshitaki unamuita mfadhili, du!

ndesamburo anaweza ku qualify kuwa mfadhili kama ajakiibia chadema, watu mlio ndani ya chadema mnaweza kuthibitisha hili
 
sijasema kuwa CCM wapo sawa, mpaka sasa CCM 0 upinzani 0, ila tukipata chama bora ambacho kitamwakilisha kila mtanzania itakua CCM 0 upinzani 1...lakini kwa sasa chama tawala tulicho nacho hakina dira ya maendeleo, na upinzani bado hawapo kikamilifu..chakufanya ni kuunda chama kipya tu..au alternatively kujikita saana kwemye ubunge
pia vyama hivi vituonyeshe mfano ambao uwe tofauti na CCM na si kurudia madudu ya CCM

Sasa kwa nini usianzishe hicho chama mkuu?

Unataka nani akuanzishie chama kisha wewe ujiunge? wewe ni mtanzania na kama kweli unayosema ni ya ukweli na sio unafiki tu ili ukubali status quo ya jini likujualo (ccm) basi anzisha chama.

Anzisha chama safi mkuu semenya na utapata wafuasi safi.
 
Ndesa anatengeneza justification ya kutafuna pesa za kampeni za Chadema kwa kisingizio cha mafuta na matengenezo ya Chopa. Wajinga ndio waliwao, chambo cha maini hicho mzee Ndesa atakamua ki ulaini ( off course akishirikiana na Mbowe )

Naona mkuu umeanza utabiri. Yangu macho tu ila mzee Ndesa mambo yake anayofanya jimboni kwake ni makubwa - sijui kama hizo pesa nazo anatumia ili kuwaibia wana jimbo wake.
 
Ndesa anatengeneza justification ya kutafuna pesa za kampeni za Chadema kwa kisingizio cha mafuta na matengenezo ya Chopa. Wajinga ndio waliwao, chambo cha maini hicho mzee Ndesa atakamua ki ulaini ( off course akishirikiana na Mbowe )


Masatu,

Iwapo Chadema katika chaguzi zake huwa wanakodisha Chopa kwa 500USD kwa siku; na sasa Mzee Ndesa amekubali kuwakodishia wa 250USD kwa siku kwa nini unasema wajinga ndio waliwao wakati ambapo pesa za wanachadema zinatumika kwa ufanisi zaidi??
 
Masatu Ndesa hana shida ya pesa. Gharama ya helicopta mbili huwezi kuirudisha kwa bei ya mafuta!! hiyo investment inachekesha!. Masatu ni lazima tufikirie kidogo kabla ya kutoa mawazo. Ukweli ni kwamba huyu ni mzee tajiri, kafanya biashara kihalali na anajali watanzania.Siyo kila mtu anayesaidia au kuwana uchungu wa nchi ana agenda ya siri kuna watu wengi wenye uchungu na nchi na wanataka kutumia pesa zao kusaidia maisha ya watanzania. Huyu mzee ameamua kusaidia kwa kuwa mwanaharakati.
 
Masatu Ndesa hana shida ya pesa. Gharama ya helicopta mbili huwezi kuirudisha kwa bei ya mafuta!! hiyo investment inachekesha!. Masatu ni lazima tufikirie kidogo kabla ya kutoa mawazo. Ukweli ni kwamba huyu ni mzee tajiri, kafanya biashara kihalali na anajali watanzania.Siyo kila mtu anayesaidia au kuwana uchungu wa nchi ana agenda ya siri kuna watu wengi wenye uchungu na nchi na wanataka kutumia pesa zao kusaidia maisha ya watanzania. Huyu mzee ameamua kusaidia kwa kuwa mwanaharakati.

Kamundu
Ni kweli. Huyu mzee angekuwa mwizi CCM wangeshamtenda vibaya siku nyingi. Huyu ni kati ya wazee wachache sana wanaozekeeka vizuri sana. Kukomaa na jimbo la Moshi Mjini na bado jamaa hata CCM wanampa salute, si mchezo ina maana anafanya kazi
 
*Zitaanza uchaguzi wa serikali za mitaa

Boniface Meena, Moshi

i.

Alisema kuwa helkopta hizo zitaanza kufanya kazi katika kampeni za serikali za mitaa katika majimbo yote ya Mkoa wa Kilimanjaro na baadaye katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana ni kuwa Chadema imesimamisha wagombea zaidi ya robo tatu katika kila jimbo mkoani Kilimanjaro.

Katika Jimbo la Moshi Mjini, chama hicho kimesimamisha wagombea 60Â na Jimbo la Rombo kimesimamisha wagombea 52.


Kulikoni Helkopta na Mkoa wa Kilimanjaro?????? Tukisema CHADEMA ni ya wachaga tutakosea au jamaa anajaribu kujenga mazingira aendelea na ubunge bila kupingwa kama Mheshimiwa Mwenyekiti wao?

Ushauri wa bure kwa CHADEMA acheni kutoa kipaumbele uchagani mjenge chama chenu maana neema zote zahamia huko au mnafikiri wanachama wenu hawalitambui hilo.....Pelekeni kwa zitto kigoma au mikoa ya kusini ambako CCM inajitanua kwa kukosa chama cha kuwafumbua macho wamakonde wale.
 
Kulikoni Helkopta na Mkoa wa Kilimanjaro?????? Tukisema CHADEMA ni ya wachaga tutakosea au jamaa anajaribu kujenga mazingira aendelea na ubunge bila kupingwa kama Mheshimiwa Mwenyekiti wao?

Ushauri wa bure kwa CHADEMA acheni kutoa kipaumbele uchagani mjenge chama chenu maana neema zote zahamia huko au mnafikiri wanachama wenu hawalitambui hilo.....Pelekeni kwa zitto kigoma au mikoa ya kusini ambako CCM inajitanua kwa kukosa chama cha kuwafumbua macho wamakonde wale.

Mkuu hizo ni Helicopter za Ndesa na Siyo za CHADEMA. Kwa nini wewe usinunue upeleke huko Kusini?
 
Mkuu hizo ni Helicopter za Ndesa na Siyo za CHADEMA. Kwa nini wewe usinunue upeleke huko Kusini?

Hapa tunamzungumzia Ndesamburo kanunua helkopta kwa ajili ya CHADEMA soma hiyo headline vizuri ili uache kujibu PUMBA.

Na suala la Helikopta kuwa mali yake asingeuambia umma kuwa amewanunulia CHADEMA....tena zitaanza kutumika uchagani. Huoni kama ni coincidence....hiki cha kilichokuwa kikijulikana kama "Chaga Development Man" au hukumbi ile kashfa ya ukabila kujaa kwenye hiki chama.
 
Back
Top Bottom