Nchi hii haitafanikiwa kwenye jambo lolote la maana mpaka mwisho wa Dunia

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,709
36,166
Ukiuliza sera ya serikali kwa sasa ni nini hata viongozi wenyewe hawajui. Wataanza kukutajia SGR, Bwawa la kufua umeme la Mwalimu Nyerere, watakutajia Bandari na kadhalika.

Kwa ufupi hata viongozi hawajui Tanzania na Watanzania wanahitaji nini.

Watanzania wenyewe pia hawajui wanahitaji nini kwasasa, miaka na miaka kazi kulalama kuwa maisha magumu.

Ukimuuliza Mtanzania kwanini maisha magumu utamsikia anasema serikali ndio sababu.

• Kwa wingi huu wa rasilimali sikutarajia mpaka sasa kuona wamama wajawazito Dar es salaam wakienda kujifungua na mapegi mgongoni yaliyojaa vifaa vya kujifungulia.

• Kwa wingi huu wa rasilimali sikutarajia kuona a baadhi ya shule za msingi Dar es salaam darasa Moja kurundikana wanafunzi zaidi ya mia moja.

• Ardhi yenye rutuba ipo , viwanda vya sukari vipo lakini sasa mwaka wa 8 bei ya sukari si himilivu.

Kwa ufupi Watanzania watapata taabu mpaka mwisho wa Dunia.

Anayebisha abishe lakini akumbuke matumaini waliyopewa Watanzania 2012/2013 jinsi gesi ya Mtwara itakavyoondoa umaskini. Leo hii ni miaka 10 tangu mradi uanze.

Kiko wapi?
 
Tukiweza kupata Viongozi sahihi kwenye nafasi ya juu yote yanawezekana. Saivi watu wanapata nafasi kwa kuwa chawa sio kutokana na how smart they are.

Watu smart hawawekwi kwenye nafasi nyeti na muhimu kupanga na kutengeneza mustakabali muhimu kwa taifa letu kwa miaka mingi ijayo badala yake wanawekwa watu wasiostahili angalau just kwa sababu ni machawa au wana nidhamu ya uoga. Sasa tutegemee nini hapo?
 
Tukiweza kupata Viongozi sahihi kwenye nafasi ya juu yote yanawezekana. Saivi watu wanapata nafasi kwa kuwa chawa sio kutokana na how smart they are.

Watu smart hawawekwi kwenye nafasi nyeti na muhimu kupanga na kutengeneza mustakabali muhimu kwa taifa letu kwa miaka mingi ijayo badala yake wanawekwa watu wasiostahili angalau just kwa sababu ni machawa au wana nidhamu ya uoga. Sasa tutegemee nini hapo?
Hao viongozi makini wakiingia tu kwenye uongozi Ibilisi anaharibu ufahamu wao wanaanza kuwaza pesa na vyeo.
 
Hawajui wanachotaka, hawajui wanakwenda wapi, wanatoka wapi ndio maana kila siku kuna kauli na mipango mipya .
Mipango mfu
Aisee, kwa maneno yako naona unaijali sana nchi yako.
Hivi ni suluhisho gani linatakiwa kuiokoa Tanzania?

Wapewe Serikali vyama vingine vya Siasa?

Au, tuwachague kwa kuwapigia Kura? Manake yawezekana wao wana Sera, au ndio kusema hata wao hawajui wanachotaka na hawajui wanapoenda?
 
Ukiuliza sera ya serikali kwa sasa ni nini hata viongozi wenyewe hawajui. Wataanza kukutajia SGR, Bwawa la kufua umeme la Mwalimu Nyerere, watakutajia Bandari na kadhalika.

Kwa ufupi hata viongozi hawajui Tanzania na Watanzania wanahitaji nini.

Watanzania wenyewe pia hawajui wanahitaji nini kwasasa, miaka na miaka kazi kulalama kuwa maisha magumu.

Ukimuuliza Mtanzania kwanini maisha magumu utamsikia anasema serikali ndio sababu.

• Kwa wingi huu wa rasilimali sikutarajia mpaka sasa kuona wamama wajawazito Dar es salaam wakienda kujifungua na mapegi mgongoni yaliyojaa vifaa vya kujifungulia.

• Kwa wingi huu wa rasilimali sikutarajia kuona a baadhi ya shule za msingi Dar es salaam darasa Moja kurundikana wanafunzi zaidi ya mia moja.

• Ardhi yenye rutuba ipo , viwanda vya sukari vipo lakini sasa mwaka wa 8 bei ya sukari si himilivu.

Kwa ufupi Watanzania watapata taabu mpaka mwisho wa Dunia.

Anayebisha abishe lakini akumbuke matumaini waliyopewa Watanzania 2012/2013 jinsi gesi ya Mtwara itakavyoondoa umaskini. Leo hii ni miaka 10 tangu mradi uanze.

Kiko wapi?
Kwasababu ccm wameshindwa kuiletea nchi maendeleo hadi watu kukata tamaa kiasi hiki,nashauri tuwape Chadema nao tuwaangalie wasipofanikisha maendeleo Kwa nchi ndipo uachie hiyo laana.
 
Aisee, kwa maneno yako naona unaijali sana nchi yako.
Hivi ni suluhisho gani linatakiwa kuiokoa Tanzania?

Wapewe Serikali vyama vingine vya Siasa?

Au, tuwachague kwa kuwapigia Kura? Manake yawezekana wao wana Sera, au ndio kusema hata wao hawajui wanachotaka na hawajui wanapoenda?
Wapewe vyama vingine vya siasa hususan Chadema,nchi itainuka upya chief.
 
Enyi waafrika mlio wajinga na mazuzu pamoja na wapumbavu,mlipo ambiwa hamuwezi kujitawala hamkumuelewa Botha sawasawa.

"Tuliamua kuwaengua waafrika katika mipango ya maendeleo ya Afrika kusini,sababu wangeharibu"Botha

Upumbavu ni kipaji kama ilivyo kwa urefu na ufupi huwezi muelimisha mpumbavu akaacha upumbavu wake"Mwl.Nyerere

Hakuna mahali popote duniani ambapo vilaza walipewa uongozi na kuleta mageuzi,hakuna.
 
Tanzania hakuna over population.
Karibu zaidi ya 80% ya ardhi ya Tanzania haikaliwi na watu.
China wenye overpopulation wangekuwa mafukara zaidi yetu kwa minajiri hiyo
wewe rasilimali unayoangalia ni ardhi tu. China hawana middle class either ni matajiri au ni workmen. ardhi ya kutosha lakini bado wanaishi kwenye vimiji concentrated. kwasababu uchumi sio ardhi. hatuko karne ya 15.

hatuna rasilimali wala uchumi wa ku-support watu milioni 60 waishi maisha at least yenye utu.na hata tujitahidi vipi hatuwezi . hii nchi maximum ni 40M.. Marekani wenye nchi ya dunia ya kwanza ina watu milioni 330 lakini zaidi ya milioni 30 hawana makazi ya kudumu, bado hujakutana na homeless wanaoishi nje kabsa + kuna mizozo imeanza ya kuzuia immigrants kuingia.

dunia imebadilika na hivi karibuni kuna recession inakuja.
 
Back
Top Bottom