666 ilikua kwenye utawala wa Rumi (Warumi) mtawala wa kipindi hicho alikua anaitwa NERO, huyu Bwana Nero alikua ni katiri wa dunia nzima Hitler akasome, alikua anawaua wale wote wanaosema wanamfuata Yesu kwa mateso makali na vifo vya aibu, ndipo wakristu wakaona isiwe tabu wakaunda namba kuonyesha ukatiri wa Nero kwa namba 666, baada ya hapo ndipo namba 666 ikaanza kutumika kuonyesha ukatiri wa mtawala Nero, maana alikua akiua wakristu wote wakati wa utawala wa Rumi Ila baadae kilichokuja kutokea ndio ulipoibuka Ukatoriki, sitaki kuingia huko
Maana ya 666 kwa kipindi hicho ilikua ikimaanisha MPINGA KRISTU au kwa lugha nyingine ilimaanisha wewe upo upande wa mtawala Nero na utawala wake wa Rumi na unampinga Kristu kwa hio ukionyesha hio nembo hivyo ndio pona yako awakuui kinyume na hapo unauawa unakufa sababu wewe unamfuata Kristu, Ila baadae alipokuja mtawala mwingine baada ya kifo Cha mtawala Nero ambae alikua nu muuaji/katiri ndipo ikawa imeondolewa hio taratibu ya kuua wakristu kwa ambao hawana nembo ya 666 na utawala wa Rumi ukakubari ukristu uingie ndani ya Rumi na hapo ndipo ukawa mwanzo wa kuibuka kwa Roman Catholic, neno Roman Catholic lina maana yake
Kwa kipindi hicho Roman Catholic ilichanganyikana na Jamii ya watu waitwao Wajenzi Huru (Freemasons) ambao walikua na taratibu zao na mienendo yao ambayo wale wasimamizi na waendeshaji wa Imani ya kikristu ndani ya RC hawakuzipenda (ingawa hili RC hua hawapendelei kabisa kabisa kulizingumzia kwa undani) hivyo wakawaondoa Jamii hio ya Wajenzi Huru ambao wanaitumia nembo ya 666 km moja wapo ya nembo zao mpaka leo,
Ila pia hapo kuna mkanganyiko kidogo, maana ukifuatilia kwa makini unaambiwa wakristu waliokua wakiuawa kipindi Cha utawala wa Nero na utawala wa Rumi waliundiwa nembo ya 666 kuonyesha ishara ya kua wapo upande wa Mpinga Kristu (Nero) Ila Freemasons wameichukua hio nembo na ni nembo wanaitumia kuonyesha ishara ya utajiri na njia ya mafanikio, ingawa huko RC huwachukulia Freemasons km wapinga Kristu sababu wanaitumia hio nembo ya kuonyesha na kumaanisha Mpinga Kristu 666