Nataka niache advance PCB nahisi imenishinda

Nataka niache advance PCB nahisi imenishinda

Kweli wewe ni mkata tamaa.. mapemaa umeshaonaa utazungusha zeroo huko mbeleni ila sio mbaya kwa kujiwazia kushindwa..vipi na huko kwenye course zingine masomo yakiwa hayapandi tena utafanyaje....jibu unalijua mwenyewe
Pambana kijana na hali yako usiwe mtu wa kushindwa kizembe ukiwa hivyo mengi yatakushinda
 
Acha uoga kijana endelea kupambana na PCB hakuna kinachoshindikana ukimuweka mungu mbele na kupiga msuli kwa bidii hope matunda utayaona mbeleni kuliko kukata tamaa sasa. Kwani hata huko chuo unapotaka hamna urahisi kihivyo bila ya kukaza napo utaona mauzauza tu.
 
We DG ndoilivyo masomo ya sayanc na wrote tumepitia ukouko yan m from 5 nlikua napata below ad bios nilipata 21 pepa LA kwanza tuu but nlikomaa ckuwah pata below tena nilibundaa cji kusaau afu fom 6 mwanzon nkaugua maskio nkawa sisikii KBS lkn nilikomaa na necta nimefaulu vzr Niko chuo SSA NAKUSHAURI FANYA SHULE kuwa mvumilivu kazana kusoma sanaaa mi shahid ang Tr.angu WA bios yumo umu aje aseme [HASHTAG]#nswima[/HASHTAG] John Edward#

Uko unakokuita chuo ndo kugumu zaid coz nako kuna mitihani vlevle uczan hawafeli wanafeli sanaaaa tena sanaaa MWIKO KUKATA TAMAA...
 
Ushauri wa kuendelea na pcb hapa hautasaidia...mentality yako imeshajitune kushindwa!kama una ndoto za kua kweye field ya afya,hujachelewa kujiunga na vyuo vya CO's!
Kwa pcb advance izo ndio alama zake..mimi o'level pcb nlikua na DBC,ila advance nikapata BAD!!!sitakuja kusahau msuli YATIMA niliopiga those days!!
Sasa ni Medical Doctor,since 2013
Hakika yan amenisikitisha sanaaaa kajiwazia kufeli anatembea kikukushdwa shindwa tuu na ATASHINDWA KWELI nliwah feli lkn niliipnga iyo hali ad kwa machozi...DG akili kaiharbu taar ushaur hauez msaidia JAPO MDA ANAO MZURI SN KUJIPANGA
 
Since nimeingia advance sijawahi kupata zaidi ya 50marks kwenye chem&phys zaid napataga kwa bios isitoshe mtihani wangu wa annul form five nimepata zero ffs respectively kwa pcb sasa nimekata tamaa kabisa nakuona hakuna ninachofanya zaidi ys kwenda kuzungusha form six 2018..hivyo rasmi nahitaji kuongea ba wazazi nitafute alternative ways ya kwenda collage nikachuke course nyingine

N.B sio kwamba sisomi nasoma tena sana ila sielewi kwanini inakuwa hivi
-pia o level nilifaulu vizuri tu kwa CCA in PCB
Pole sana mdogo wangu. Brother wako hapa kilinikuta kitu hicho hicho! Nimetoka o'level vizur sana (division two point 18) nikiwa nmetandaza B kwenye kombi ya PCB, hivyo kama kawaida nikaona advance nikasome PCB.
Nilipofika kule (nilisoma Mtwara tech) mambo hayakuwa kama nilivyotarajia..! Mambo yalikuwa magumu sana! Kwa mwanzo somo nililokuwa nalielewa vizur lilikuwa ni Biology pekee! Chemistry na Physics mambo hayakuwa mazuri kabisa! Yaani mambo yalikuwa yana-vapour kwa haraka mpaka nikaanza kuhisi nmerogwa (ingawa imani hizo siziamini!)
Ilifika kipindi form five ilikuwa nikisoma chemistry or physics ndani ya saa moja nmeshasahau kila kila kitu! Yaani mpaka definition haikai kichwani..! Nilichanganyikiwa kwakweli!

Bahati nzuri nilikuwa napenda kujichanganya na mabrother wa form six and so nikashare nao tatizo langu! Jamaa walinicheka sana (cause nao walipitia issue kama hizo) but walinisaidia kufanya utatuzi wa tatzo langu ingawa bado haikuwa the best solution..!

Namkumbuka bro wangu anaitwa boaz alisema "Ubavu, angalia dogo, chuo wanataka principal mbili tu.! (kwa kipindi kile principal ilikuwa E) so chakalika upate E ya biology na chemistry then off you go to the university"
Kwa kipindi kile niliona hiyo ndo ilikuwa solution and so nikalikacha rasmi somo la physics..! Nikaamia kwa chemistry! Na kweli, muulize mtu yeyote aliyesoma PCMB (phy, chem, bios, or math) advance atakwambia.. Kuwa chemistry ndio somo la kukutoa cause huwa halikatai mtu!

Fortunately, necta ya form six nilipita kwenye tundu ya sindano kwa kutumia formula ya brother boaz kwani nilipata div three (ndipo pcb wengi wanapoangukia hapa) ya point 15 meaning nilikuwa nna D mbili za bios and chem! Hivi sasa nmemaliza chuo na nmepata kajikazi kakujishikiza!
Turudi kwako, mara nyingi sipendi kumpa mtu ushaur mmoja! Huwa napenda kumchambulia mtu pros and Con's za kila option ili mwenyewe ajue wapi ni kuzuri zaidi!
Moja, unaweza kutumia njia yangu ambayo baadae ilinikosti kwa vile physics nilikuja kupata F ila nikaenda chuo! Na sikuweza kufikia malengo ya wanaPCB wengi ya kusoma MD!, hapa unatakiwa pia uchague topics za kusoma pia..! Kwenye chemistry pitia sana physical chemisry, Inorganic chemistry pamoja na General chemisry... Hizi ndio mkombozi wako... Maana kama ukizikazia huwa hazichomoi! Hapa tafuta kitabu cha last papers kutoka mwaka 1987 mpaka 2006! Hiki ndio awe rafiki yako..!maswali yote ya topics hizo nilizokwambia inabidi uwe unayajua ndani nje..! Kuanzia data mpaka solutions! Organic chemistry! Asee huyu mdudu anavitu vingi sana.! Halafu maswali yake huwa hayatabiriki..! Zile conversion inatakuwa kuanzia temperature, catalyst mpaka pressure inayotakiwa ili reaction itake place! Kwa mm niliacha nayo! Ila kama unajiamini unaiweza.. Ukiweza kuimaster hii A ya chemistry inanukia cause organic chemisry hubeba 60%ya maksi zote kwa paper one na two..!
Biology yote inatakiwa iwe at the fingertip of your hand! Meaning swali lolote la topic yoyote inatakiwa usilifikilie zaidi ya dk moja..! Yaani ukishamaliza kulisom swali hakuna muda wa kurudia.. Inatakiwa uwe umeshajua muulizaji anataka nn kwenye swali hilo..! Pia ni muhimu kufupisha jibu lako kuwa fupi ila lenye ujazo wa haja.. Msahihishaji huwa analess than one minute kusahihisha swali moja so hawezi kuhangaika kutafuta jibu katikati ya essay lako! Majibu yawe in bulletin way hata kama swali ni la assay form! Kama ni swali la kudescribe ni lazima uchore mchoro! Kama ni explain ni lazima isizid mistari mitano ya jibu lako! (hapa kuna mengi ambayo siwezi kuyaandika yote so unaweza kuja pm nikupe namba tuongee..). Or

Mbili, unaweza kukaza zaidi! Tafuta likizo hata ya week moja, tulia fikilia ni kwann mambo yamekufika hapo ulipo?! Je ni strategy or materials yanayokufanya ushindwe kuperfom..? Mara nyingi huwa ni strategy..! Kwa maana shule za govt kwa advance ni msuli yatima (meaning unakomaa na materials wewe mwenyewe mpaka kinaeleweka!) so huwa inakuwa how you study and for how long ndicho kinacho-determine ufaulu wako..! Kuna jamaa yangu tulikuwa room moja, alikuwa anastrategy za ajabu sana..! Yeye alikuwa anasema, "Ubavu advance mambo ni mengi sana and so unatakiwa urudie rudie kusoma hizi mambo mara nyingi iwezekanavyo..!" akandelea kusema "inatakiwa uwe umeimaliza syllabus yote ya advance tena ya masomo yote ndani ya week moja..!" wakati huohuo fahamu idadi na uzito wa vitabu vyiiliyopo advance! Mimi ilinishinda njia hii kwakweli"
Hapa nataka niseme neno kidogo!. Hii ndio njia ninayoona at least itakusaidia.. Baada ya kumaliza form six nilikuja kuelewa ni kwann hii ndio njia nzuri! Unajua mtu anavyotoka o'level huwa anaexpectation kusema kuwa "kama nmetoka kwenye masomo tisa na nikafaulu kwann nisifaulu nikiwa na masomo matatu tu!" thats totally wrong! Yaani advance sio ya kuifikilia kihivyo kabisa..! Mimi nilikuwa ni mmoja ya watu wanaoisema serikali kuwa wamekosea kwa kuruhusu watu walioferi form six kuruhusiwa kufundisha o"level kama amesoma deploma ya ualimu..! Ila kwa sasa nmeona ndio option nzuri, kwann nasema hivyo..! Advance mara nyingi mtu huwa afeli kwasababu ya kuto kusoma..! Bali huwa anafeli kwasababu ya kutokujua jinsi ya kulijibu swali la mtihani effectively..! Jamaa aliyepata div four ya advance ukimwambia akufundishe topic moja wapo... Utashangaa jinsi anavyoijua ndani nje... Tena mpaka na mifano..! But ndo hivyo unakuta necta anatoka na four...! Mtu huyu vitu anavijua sema jinsi ya kuviweka kwenye pepa ndo shida...! Unakuta anabeat around the bush mpaka muda unaisha..!
Sasa basi! Jaribu kufanya maswali mengi iwezekanavyo.. Tena sio ya vitabuni peke yake... Fanya mitihani mingi iwezekanavyo! Hapo utajihakikishia kufaulu!

Tatu, kama umeona kuwa hutoweza kutoka kwa njia hii ya advance, unaweza pia kuomba vyuo vya diploma vya afya na ukaacha hiyo advance kiroho safi tu! Tena ndo zinakaribia kufunguliwa sasa..! Njia hii ni nzuri kwa kuwa unakuwa na uhakika wa kutoka... Chuo kufeli ni kutaka mwenyewe tu.. Labda ukushike ugonjwa wa ajabu.. Wakati wa mtihani!

All in all! Advance sio sehemu ya kwenda kujaribu..! Inataka constant discipline ya muda..! Kuanzia unaingia siku ya kwanza mpaka unatioka siku ya mwisho! Elius kiyombo TO wa mwaka 2006 anamisemo yake..! Huwa anasema.. "Ukiwa advanve hakuna rangi utaacha ona" pia husema "siku ya kwanza kuingia form five wote huwa mnakuwa na div one ya point tatu, but huwa inapungua kulingana na aina ya maisha utakayoyaendesha mpaka necta inakufikia.. So inawezekana mwezi mmoja kabla ya necta ukawa umebaki na div one ile ile or umebaki na zero..!
Pia wakati unasoma jaribu kujifananisha na watu wa misuli mirefu..! Jaribu kukaa nao karibu cause watakupa changamoto ya kuongeza msuli wako...! Pamoja na usongo..! Kama unasoma boarding! (tena hapa ndio muhimu) na ngoja niandike kwa herufi kubwa ACHANA NA RATIBA YA SHULE, USIIFATISHE KABISA HII...! NI MBAYA NA HATARI KWA AFYA YAKO YA KUSOMA! Mi ratiba yangu ili kuwa ni kama ifuatavyo..! Naamka saa moja na nusu..! Mbili kamili nipo room kwenye meza yangu naanza misuli ya bios..! Mpaka saa nne muda wa uji nakuwa nmeshapitia topic mbili za bios pekee..! Kuanzia saa tano mpaka saa nane kamiri nakuwa nmeshapitia topic tatu za phy chemistry! Baada ya msosi nalala kuanzia saa kumi mpka saa kumi na mbili..! Then nakula msosi wa jioni..! Napiga story mpaka saa moja na nusu...! Mbili kamili nipo mezani kwenye room yangu misuli inaanza tena (kwa advance hasa watu wa pcbm usiku ndio unatakiwa uwe muda wa kusoma sana..! Unless otherwise usingizi uwe unakushinda nguvu) hapo ntasoma mpaka saa tano na dk 45 (huu ndo muda wa usingizi kuanza kusumbua..) nalala kwa saa moja mpaka saa sita na dk 45 nikiamka nnanguvu mpya..! Kuanzia saa saba kamili mpaka saa kumi na nusu alfajir ni mwendo wa kusoma tu..! Then nalala naamka saa moja tena kazi inaanza tena... Hii ni toka mwezi wa sita wa form five mpaka mwezi wa pili (kipindi chetu ndo papers zilikuwa zinafanywa muda huu) wakati wa necta
Na mwisho kabisa.. Jipatie muda mwingi wa kupumzika.. Ikiwezekana chagua jumamosi (kama wasabato) or jumapili kama waroma nk) or hata ijumaa (kwa waislamu) kuwa ni siku ya mapumziko ukikusanya nguvu..!
Mimi binafsi nilichagua ijumaa kwasababu huwa ni siku fupi sana..! And so ilikuwa ndo siku ya kulala..!
Kama we niwa day..! Uliza wengine...

Ubavu!
 
Mkuu Ubavu umegusa sehemu yake nilipokuwa napataka na mm nina mdogo wangu kachaguliwa comb ya PCB mwaka huu hapo hapo Mtwara Tech kutoka O level ana division 2 ya point 19 shule ya kata ana BCB kwa masomo ya PCB. So naomba unishauri kuhusu hii shule maana nilikuwa nataka nimchukulie uhamisho asome Dar. Je shule kimazingira na taaluma ipo vp kabla ya kufanya uamuzi.
 
Mwanafunzi wa pcb halafu tayari unaijua jf na.mitandao mingine ya kijamii. Sidhani kama utaweza soma chochote kinachohusu sayansi. Nenda veta mkuu.
 
Mwanafunzi wa pcb halafu tayari unaijua jf na.mitandao mingine ya kijamii. Sidhani kama utaweza soma chochote kinachohusu sayansi. Nenda veta mkuu.
Acha ushamba ndugu Kajirutaluka mi nmeingia jf nikiwa form five..! Na ndo ilikuwa moja ya sehemu za kurefresh my mind hasa nnapokuwa na stress.. Mawazo ya necta yakinizidia ilikuwa naenda aidha makonde beach or naenda soko la samaki kuangalia jinsi maisha yananvyoenda kwa local people wa msanga mkuu... Na kama siku hiyo mambo hayaendi kabisa.. Nilikuwa naenda internet cafe... Mitaa ya ocean nnabrowse fb pamoja na jf huku nikiangalia matokeo ya necta ya maryan pamoja na special schools mbalimbali.. Natoka pale nikiwa na nguvu mpya ya misuli..!

Sasa wewe unadhani kwamba mwanafunzi hafai kwenda na technolojia..?!
 
Daah u speak with heart umentouch aisee...kama nauona mwanzo mkuu ila naogopa sana aisee
Wewe sasa umeshakua. Ni lazima uondoe uoga na uongee na wazazi kiutuuzima. Andaa plan b na waeleze utafika tu chuo kikuu na utakuwa pengine ushapata ajira na utajisomesha mwenyewe. Kusoma PCB enzi za mwalimu kulikuwa na heshima mjini lkn msuli wake ni kifo. I dont want to remember those days. It was crazy!
 
Acha ushamba ndugu Kajirutaluka mi nmeingia jf nikiwa form five..! Na ndo ilikuwa moja ya sehemu za kurefresh my mind hasa nnapokuwa na stress.. Mawazo ya necta yakinizidia ilikuwa naenda aidha makonde beach or naenda soko la samaki kuangalia jinsi maisha yananvyoenda kwa local people wa msanga mkuu... Na kama siku hiyo mambo hayaendi kabisa.. Nilikuwa naenda internet cafe... Mitaa ya ocean nnabrowse fb pamoja na jf huku nikiangalia matokeo ya necta ya maryan pamoja na special schools mbalimbali.. Natoka pale nikiwa na nguvu mpya ya misuli..!

Sasa wewe unadhani kwamba mwanafunzi hafai kwenda na technolojia..?!
Kurelax kwa kutembea beach au bustanini si sawa na mitandao ya kijamii. Tunakuelezeni haya kwa kuwa tunapenda wadogo zetu mfanikiwe na wala sio ushamba. Huwezi kupitisha meli nchi kavu hivyo maji lazima yafuate mkondo.
 
Inawezekana....
Ni muuza sura sana shule yan husomi.
Au unasoma bila maswali we na notes notes na ww
Au huwez kwel.....
Jitafakari dogo
 
Maisha n safar ndefu kijana lkn ktk yote,kukata tamaa n jambo baya zaid kulko yote,mm nmeaoma PCB kama ww 2014-2016 ,mwanzon masomo yalikuwa magumu mpk nikawa nahis labfa nmelogwa ..yaan unasoma sana lkn unachokikumbuka baada ya kusoma hakuna..lkn sikukata tamaa kirahis HVO kwa sababu nljua maisha n kupambana ....nljitahd kusoma sana licha ya kwamba wenzangu miliokuwa nasoma nao walikuwa wamecover topic nyng na mm sikuwa na kitu lkn hyo haikunifanya mm nikate tamaa hata kdg.. Nlsoma sana na sana na sitasahau ugumu wa hyo comb maishani mwangu...lkn mchumia juani hulia kivulin!!nilivoendelea kusoma kwa bidii huki nikimuomba Mungu ,naye hakuniacha kamwe na alinisimamia zaid .Huwez kuamin mm ambaye sikuwa nmesoma tuition na ninayetokea familia maskin kulko yako nlmalza form six nikiwa na dvsion one ya point 4 na nikabahatka kuipeperusha shule yangu kwa kuingia top ten best students in science subjects..saiv Niko nasoma doctor of medicine, Muhimbili university... Haya yote n kwa sababu sikukata tamaa kabisa...licha ya kuferi miyuhan mbalmbal hasa mwanzon lkn nljua tu IPO siku Mungu angenipigania kwa juhud zangu hazkuwa za mchezo.Ninakuomba sana mdogo wangu usikate tamaa kwa magumu unayoyaona kwa sasa.Panga ratiba zako vzur..epuka matumiz ya simu uwapo shulen na epuka kujiingiza ktk mapenz kwa umri huo ..kwako ww iwe kusoma na kusali tu ..mm naamin utafanikiwa sana ....a short cut is always a wrong cut my junior...be blessed and welcome to Muhas
 
Mkuu Ubavu umegusa sehemu yake nilipokuwa napataka na mm nina mdogo wangu kachaguliwa comb ya PCB mwaka huu hapo hapo Mtwara Tech kutoka O level ana division 2 ya point 19 shule ya kata ana BCB kwa masomo ya PCB. So naomba unishauri kuhusu hii shule maana nilikuwa nataka nimchukulie uhamisho asome Dar. Je shule kimazingira na taaluma ipo vp kabla ya kufanya uamuzi.
Mkuu! Mtwara tech ni shule nzuri tu...! KWANZA ASIWAHI SHULE..! KAMA ANASOMA TUITION MWAMBIE AMALIZIE TU..! AVUTE MAXIMUM YA WEEK TATU! Kama akiwahi chamoto atakiona!
Kipindi kile mi nasoma mwalimu mkuu alikuwa ni mr. Khaji jamaa msukuma mmoja hivi pande la baba..! Nadhani bado atakuwa ni huyo huyo..! Kwanza inabd ajue ya kwamba anatakiwa kusahau matokeo yake yote ya o'level..! Maana huwa kunakuwaga na majigambo ya chini kwa chini ya nani kaja na one kali! So atapoteza muda kujishughulisha na mambo hayo..! Pia akifika tu achunguze ajue ni form six gani anayejitahidi ku-perfom vizur kwenye mitihani ya CB (bios and chem) pale Shule! Then akae nae karibu kwaajili ya ushauri..!
Shule ile ili ufaulu kwa ufaulu wa kwenda chuo.. Inabidi ujitoe ufahamu..! Ratiba ya shule achana nayo kabisa..! Kuna kengele nyingi sana pale.. Yaani huwezi kukaa masaa matano bila ya kusikia kengele at least mara mbili..! So kinachotakiwa ni kuignore kengele hizo na kupiga misuli yako..!
Pia wanapenda sana kutoa mfano kwa watukutu kwa kupiga suspension ya week tatu..! (sijui kuhusu sasa)

Kama akipangiwa dorms za jamhuri atafaidi sana.. Maana advance huwa wanakaa kule ila kipindi tupo form six..madogo wa form five wakaanza kukakaa dorms za maghalani (waliosoma mtwara tech watakuwa wanaelewa) ambayo haya support maisha ya kinungunungu ambayo ndo maisha ya kukufanya ufaulu..!
Mwambie dogo aende na tubes 5 za kuulia candida (fungi wa sehem za siri) maana kuna kitu kinaitwa pumbuerosion (kama dogo ni wa kiume, kama wa kike sijui)

Muhimu: mwambie akiingia shule kwa form five yote asijihusishe na discussion! Hapo atajikuta anachanganyikiwa sana maana watu wanakujaga wameshamaliza topics zote and so kama anamoyo mdogo anaweza akajikuta analose konfidensi..! Kama naye ni kipanga anaweza kujihisisha na hizo discussion! Mwambi asiwe na wasiwasi maana form six huwa mnaanza moja wote...! (mara nyingi ukiingia form six vitu vya form five vinasahaulika)
Akifika shule mwambie asiwacheke form six kama anaona hawasomi..! Ndo maisha ya shule yalivyo..! Advance kusoma sana ni form five na form six ni miezi mitano ya mwanzo baada ya hapo ni kulala tu (sijui usingizi ule huwa unatokeaga wapi ). MAKUNDI YA KIJINGA AACHANE NAYO! MAANA KUNA WATU HUPENDA KWENDA KWENYE BAR YA BOARD YA KOROSHO KUJIRUSHA WAKATI WA USIKU AND SO KAMA AKIJIFANYA KUJICHANGANYA ANAWEZA AKAJIKUTA ANAPOTEA..!
Pia mwambie aachane na mapenzi..! Advance sio sehem ya kutafuta mademu..! Mwambie pia akifika pale aende akaishi jamhuri c vyumba vya juu ambako ndiko pazuri na pia pana mazingira conducive ya kujisomea.. Room atakayoakaa alale kitanda cha juu upande wa nyuma ya mlango..! Pia asiende na nguo nyingi..! Apate jezi moja nyeusi pamoja na kipensi cha jinzi kwaajili ya kuautika kwenda beach kuogelea siku atakayowasili inabd avae shamba dress ambayo ni T-shirt ya kijani (mtafutie form six 2 zile zinadumu) na sketi or suruali ya brown..! Nguo za kuautika inabdi aziache nje ili walimu wasizione.. Maana wanamchezo wa kukagua baada ya ukaguzi anaweza kuzifata! Kama hataki kukaguliwa mwambie aingie usiku..! Simu ni muhimu sana kwa maisha ya advance.. Mtafutieni kasimu (ingawa shule hairuhusu na kama akikamatwa na simu adhabu ni kuivunja mbele ya assembly na suspension ya week mbili) kabatani ambako atakuwa anawasiliana na nyumbani pia hata wanafunzi wenzie.. Maana information ni muhimu sana wakati wa advance..
Mwambie asijichanganganye akapata demu wa masandube teachers college..!
Kama ni demu mwambie aangalie sana mwalimu wa physics na math (ambaye ni huyo huyo) huwa anamchezo wa kupitia wanafunzi (rumours)

Mwambie pia likizo ya mwezi wa tisa (aaah sorry kumbe hawa likizo zao zimekuwa synchronized na za o'level) basi mwezi wa kumi na mbili arudi dar aje kupiga tuition ya form six... Mwambie akaze sana practical za physics..! .. Maana zinabeba 50% ya tokeo lote la physics..! Rejea post yangu iliyopita niliyokuwa namshauri dogo mwenye huu uzi!

Mwambie kuna maandazi yanapikwaga usiku (kuanzia saa tano usiku) pale duka linaloangalia kituo cha polisi.. Mwambie ni muhimu kuwa anatoka usiku kununua ili yamsaidie kuongeza nguvu ya misuli..!

Kama mna ndugu ambaye anakaa mtwara..! muelekezeni maana msosi wa shule unachosha sana...! So awe anatenga siku moja katika kila week awe anakwenda kula msosi wa home.. Or kama hamna ndugu! Basi akifika form six miezi mitatu ya mwisho muongezeeni pocket money usiku awe anakula pale cafe ya stellar Marris university! Au aende kule mitaa ya ocean kwa wahindi akamuone mama sele (ubwabwa wa nazi )
Zamani khaji alikuwa na pikpiki akaja kununua noah siku hizi sijui anatumia usafr gani so akiwa ameautika awe makini kuangalia asije akakutana na khaji!

Mwisho kabisa shule ile huwa inawa-favour zaidi wavulana kuliko wasichana... Mademu wanaenda kufungiwa saa nne na nusu usiku mpaka saa kumi alfajir! So hiyo inabd iwe considered! Pia ajiweke karibu na mwalimu wa biology na wachemistry (kama bado ni wale wale) ni watu peace sana ingawa hawana mchango academically as teachers but wanaweza mpa kitengo cha laboratory ambapo hutoa mwanya wa kupata chamber ya kupigia misuli isiyo na bugudha..!

Mwambie asiweke kinyongo kwa maticha wa o'level maana baadhi yao wana inferiority complex ambapo wanaweza kukuzingua kama njia zenu zikiwa crossed..! Pia walimu wa field nao ni wazinguaji sana..!

Muhimu: SHULE ZA GOVT ILI UTOKE INABIDI APIGE MSULI YATIMA..! NA HAPO NDIPO ATAKAVYOTOKA..! SO KABLA HAJAENDA SHULE INABDI APIGE AT LEAST 85% YA BIOLOGY TOPICS ZA FORM 5! NA KWA CHEMISTRY APIGE AT LEAST 65 YA FORM 5 YOTE. KWA PHYSICS SIJUI..! MAANA NA F "TAKATIFU" !
 
Since nimeingia advance sijawahi kupata zaidi ya 50marks kwenye chem&phys zaid napataga kwa bios isitoshe mtihani wangu wa annul form five nimepata zero ffs respectively kwa pcb sasa nimekata tamaa kabisa nakuona hakuna ninachofanya zaidi ys kwenda kuzungusha form six 2018..hivyo rasmi nahitaji kuongea ba wazazi nitafute alternative ways ya kwenda collage nikachuke course nyingine

N.B sio kwamba sisomi nasoma tena sana ila sielewi kwanini inakuwa hivi
-pia o level nilifaulu vizuri tu kwa CCA in PCB
Watu tumeanza na 20% za biology, 34% za chemistry, 90% za physics hatukugive up, kaza
 
watu pre necta form six hyo phy na chem tulipata matokeo mabaya kinyama
Lkn tukakaza buti necta tukatusua vzr...........sasa we dogo unakata tamaa mapema sana!!! Komaa mda bado upo ....
 
Kinachonipa uoga nasoma sana na nina elewa na maswali nasolve mpaka nafurahia but since nikifika point ya mtihani duuuh...naishiwa nguvu hapa may nimepifa mock form five nimetoka na div 4 ya mwisho sasa naogopa kupotea form six
muoga wa jf, kabla hatujaendelea na huu mjadala niambie kwanza ni KWANINI unajiita MUOGA wa JF!!!
 
Yaah najua kukariri sana ila nashangaa chem imekuwa complicate sana kwangu physics ndo balaa markd kubwa nilipataga 38
Mkuu hapa ndio nimekuelewa tatizo lako ni kuwa unaweza zaidi kukariri wakati Physics & Chemistry(hasa inorganic) kwa advance na kuendelea huko chuo kikuu unatakiwa uwe na uwezo mkubwa sana wa kuelewa kuliko kukariri. Yaani hayo masomo yanabadilika sana toka o-level na kwenda a-level. Calculation nyingi sana hata ktk chemistry. Huwezi kariri calculation zote hizo, na ukifanikiwa kukariri basi wakigeuza kidogo tu maswali yale yale wanakupiga chenga ya maudhi, ile chenga ya mwili.
 
Yaan C ya Physics na Chemistry ndio ilikupa kiburi cha kwenda PCB? Ulibugi
Acheni kujifanya nyie ndo wakali sana! Mtu alikuwa na Chemistry C na Biology A sasa unataka kusema alistahili combination ipi?! Ulitaka PCM wakati alichofaulu ni biology? Ulitaka aende CBG wakati msingi wa CBG na PCB ni ule ule?! Au ulitarajia angeenda arts au biashara?!
 
Back
Top Bottom