Me ilikuwa hivii, nilichaguliwa pcb o level nilipiga B physics, B chemistry na A biology, nimefika tu advance shule ya serikali, hamna waalimu,hamna viti na meza, hamna vitanda watu wanalala kwa shift, waalimu hawafundishi halaf unakuja kupewa paper tu, nilikuwa na score marks za umri wa Serengeti boys (below 18)... Kuna mda nilikuwa narudi nyumbani tu bila sababu niliwaambia wanihamishe au niende chuo, lakini mungu alinitia nguvu ya kutokata tamaa, na hapo ninapata 16 physics sio kwamba sisomi, nlikuwa nakula msuli nahisi mkoa mzima mm ndio nilikuwa nakua wa mwisho kulala....Ila mda huo nimepata 16, kuna mdau nalala nae bweni moja alikuwa anapiga 80+, nikawa nafanya nae discussion za kutosha, na kuadopt mfumo anaotumia kusoma mtihani uliofata nilipiga 72, hivohivo mpk mwisho wa siku necta nimepiga div1.7, nimeshaapply vyuo vinne, nasubiri matokeo ya first round yanatoka mwezi huu trh25...