Natafuta Kazi Usalama Wa taifa

Status
Not open for further replies.
Huyo anayetafuta kazi usalama wa taifa hana nia ya kufanya kazi uko.....
 
Natafuta kazi Usalama wa Taifa,hata leo naomba mnipe tena naomba mnipe mapema
Nahitaji kazi ambayo nitaifanya kwa malipo madogo ila kwa ajili ya wanajamii
Nataka kuwasaidia kuwajua kwa undani wale waliochukua Pesa za EPA ili wajulikane
Nataka niajiliwe ili nionane na Rais na nimwambie yaliyo moyoni mwa watanzania


Nataka kazi usalama ili na mie nichukue pesa za EPA na niwagawie watanzania Masikini
Nataka tu sababu najua nikiwaomba pesa kwa njia ya kawaida hawatanipa.
Nafuta kazi ili niwape watanzania habari wanazotaka kujua
Niko tayari kufanya nao kazi kwa masharti ya uwazi na ukweli

Nataka Rais Ajue kwamba watu wanafanya ufisadi wa khali ya juu kwasababu ni rafikize
Nataka nimwambie Rais jinsi wachache wanavyowadharau walio wengi
Nataka nimwambie Rais ni watu wangapi mpaka sasa ni mafisadi wakubwa
Nataka kazi usalama ili nimjue vizuri rais wetu na tabia yake ya maamuzi

Nataka kazi usalama ili nifanye uchunguzi kuhusu BOT,
Nataka nimjue mmiliki wa Kagoda alipewa shilingi ngapi ?
Nataka niwajue waliorudisha Pesa za EPA mpaka sasa
Nataka kazi Usalama ili niwaambie watanzania ukweli ni wapi alipo Balali

Nataka kazi Usalama wa taifa ili nitoe majibu kuhusu Chenge
Natafuta kazi usalama ili niwaambie jinsi Dili ya RDC ilivyosukwa
Natafuta kazi ili nijue je Rais anawachukuliaje walihsuika na Richmond
Nataka kujua ni kwanini serikali hawatoi majibu ya Ripoti ya Richmons na EPA


Natafuta kazi siyo kwa ajili ya kumlinda Kada wa CCM wala kiongozi
Natafuta kazi ili kulisnda heshima ya nchi yetu
Natafuta kazi ili nchi hii iwathamini wafanyakazi na wakulima
Niko tayari kwa mshahara mdogo ila niwe huru kuwaambia wananchi

Ndiyo nataka Kazi Usalama wa Taifa na nataka Nafasi ya Ukurugenzi ndiyo ninayo itaka

Haka kawimbo safi sana.:D Beti zote!

Rudia kiitikio..."Natafuta Kazi Usalama Wa taifa"
 
Hata wewe unaweza kuwa usalama wa taifa unaweza kutumika sehemu fulani fulani kutoa taarifa fulani kuhusu mambo fulani mwanzo huwa ni hapo wakati mwingine ni hizi kazi za magazetini wewe apply tu utajiona siku dili na usalama wa taifa hilo limekuangukia
 
shy,nimwone nani ili anitume kutoa hizo taarifa?hizo kazi za magazetini ni kazi gani na kwenye magazeti gani?
 
Unaweza kumwona MH.HASSI KITINE,ATAKUAMBIA MENGI ILA INAONEKANA WEWE NI MWOGA WA MAFUNZO YA KIJESHI AU UNA MTIZAMO HASI NA JESHI.
Basic training for (TISS) is nine months which comprises of "military"training,how to secure info and to protect it against un authorized personnel + much more to keep you fit for the job.
 
sawa mkuu.siliogopi jeshi lolote ila sina mpango wa kujiunga huko.hiyo basic training ya 9months im ready to do it sema kitine ndiyo hao high profile figures wa bongo kwahiyo ku mingle na watu kama hao kama huna jina ni shughuli
waweza kunipa contacts zake ili nijaribu?
 
wakuu heshima mbele sana
kwa mnaojua,nisaidieni kunipatia vigezo ambavyo vinaweza kumfanya mtanzania kufanya kazi usalama wa taifa.mtaani nimesikia wakisema hizi kazi huwa unachaguliwa tangia ukiwa shule ya msingi au sekondari huwezi kujipeleka mwenyewe kuomba hizi kazi.je ni kweli?je ni kweli ni lazima upitie mafunzo ya kijeshi kabla ya kujiunga usalama wa taifa?
mimi napenda sana kufanya kazi na usalama wa taifa je siwezi kujiunga uko baada ya miaka 2 nikimaliza masomo yangu(nina miaka 28,nafanya masters sasa).
mods naomba muiache kidogo halafu mnaweza kuiamisha panapostahili.

Habari za mtaani ulizosikia zaweza kuwa na ukweli fulani. Nafahamu jamaa mmoja anafanya kazi usalama wa taifa. Process yake alifuatiliwa long time tokea anasoma Tabora boys na watu hawa waliokuwa wanamfuatilia walikuwa makini; maana hata alipotoka nje ya Dar walimfuatilia pia. Ila jamaa alikuwa Scout na alifanya vyema alivyokuwa Scout. Suala la Jeshini sikujui.

Ila kwa siku kila kitu hela, system ilishaoza; kama una hela mbona kila sehemu unapenya bwerere tu. Ndio maana kwa sasa Bongo wafanyakazi asilimia kubwa hawana sifa ya kufanya hizo kazi; sababu wamezipata kwa hongo na ndio maana uvurundo kila siku. But keep trying; u never know what happens and u gotta nothing to loose though!
 
Mkuu jipe moyo tu kila kitu kinawezekana ni wewe tu kujitahidi na kuwa na nia na kitu unachotaka kufanya ni hivyo tu!!
 
Unaweza kumwona MH.HASSI KITINE,ATAKUAMBIA MENGI ILA INAONEKANA WEWE NI MWOGA WA MAFUNZO YA KIJESHI AU UNA MTIZAMO HASI NA JESHI.
Basic training for (TISS) is nine months which comprises of "military"training,how to secure info and to protect it against un authorized personnel + much more to keep you fit for the job.

Shaycas,

Unamaanisha watu wanaotaka kazi Usalama wa Taifa Tanzania wakapange mstari nyumbani kwa mstaafu Mkurugenzi wa Usalama, Hassi Kitine, kwa mazungumzo ya faragha, ndio wewe ulivyopata kazi hivyo huko Usalama? Na kama mtu hamjui Kitine akamwone nani, Apson? Hakuna utaratibu rasmi, sio?

Mjomba, usifikiri kila mwananchi ana access na the Apson's and the Kitine's of the world. Hivi mbona watu wengine wako so out of touch?

Eti unafundishwa "how to secure info and to protect it against un authorized personnel"!

Ndio ukachero huo uliofundishwa huko?
 
Habari za mtaani ulizosikia zaweza kuwa na ukweli fulani. Nafahamu jamaa mmoja anafanya kazi usalama wa taifa. Process yake alifuatiliwa long time tokea anasoma Tabora boys na watu hawa waliokuwa wanamfuatilia walikuwa makini; maana hata alipotoka nje ya Dar walimfuatilia pia. Ila jamaa alikuwa Scout na alifanya vyema alivyokuwa Scout. Suala la Jeshini sikujui.

Ila kwa siku kila kitu hela, system ilishaoza; kama una hela mbona kila sehemu unapenya bwerere tu. Ndio maana kwa sasa Bongo wafanyakazi asilimia kubwa hawana sifa ya kufanya hizo kazi; sababu wamezipata kwa hongo na ndio maana uvurundo kila siku. But keep trying; u never know what happens and u gotta nothing to loose though!


kwahiyo kihalali kazi za usalama wa taifa ni wakulu wenyewe kukupendekeza wakiona unafaa na kukufuatilia na huwezi kwenda mwenyewe kuomba kazi vinginevyo ufanye mazabe na wakulu ili wakuingize.nashukuru kwa mchango wako mkuu.
 
Mkuu jipe moyo tu kila kitu kinawezekana ni wewe tu kujitahidi na kuwa na nia na kitu unachotaka kufanya ni hivyo tu!!

nashukuru kwa courage mkuu.wanasema penye nia pana njia.sasa mimi nia ninayo naitafuta hiyo njia sasa!
 
Shaycas,

Unamaanisha watu wanaotaka kazi Usalama wa Taifa Tanzania wakapange mstari nyumbani kwa mstaafu Mkurugenzi wa Usalama, Hassi Kitine, kwa mazungumzo ya faragha, ndio wewe ulivyopata kazi hivyo huko Usalama? Na kama mtu hamjui Kitine akamwone nani, Apson? Hakuna utaratibu rasmi, sio?

Mjomba, usifikiri kila mwananchi ana access na the Apson's and the Kitine's of the world.
Hivi mbona watu wengine wako so out of touch?

Eti unafundishwa "how to secure info and to protect it against un authorized personnel"!

Ndio ukachero huo uliofundishwa huko?

huo ndiyo ukweli wenyewe.kama wazee wako hawana jina basi kuwaona hao wakulu ni ndoto.
nilitaka kujua jinsi ya kujiunga huko kama utaratibu ni mpaka wakuone wenyewe unafaa au unaweza mwenyewe kuomba kazi kama ukitaka.sasa mkulu ananiambia nimuone kitine tena bila hata kunipa details za kumuona huyo kitine!
 
huo ndiyo ukweli wenyewe.kama wazee wako hawana jina basi kuwaona hao wakulu ni ndoto.

Nakubali.

Lakini sister brother p53, hata kama ungekuwa na jina la Baba wa matawi ya juu, au mtoto wa masikini, hutakiwi kukubali kupitia kwa watu maarufu, the Apson's and the Kitine's of the world, ili upate kazi sehemu kama Usalama wa Taifa. Ndio ufisadi wenyewe huo. Kwamba, my point is, p53, mambo ya connection connection na kujuana juana haya nishai. Mimi hapa nilipo sitaki kujuana na Kitine au Apson hata kama ningekuwa na access nao, hata kama wao ndio the go-to guys wa kukutafutia kazi Usalama. Sitaki, sitaki kuwajua. Wakae na ukuu wao na utajiri na umaarufu wao, waanze mbele!

Kwa nini tusijenge nchi ambayo sio lazima uka kiss ass kwa Kitine ili akuunganishie kazi Usalama wa Taifa? Yani mimi siwezi, siwezi, sijui ni kiburi cha kutotaka kuuza utu wangu, lakini sitaki.

Huyu Shycass anaweza kuwa na Kitine au jamaa yake fulani ambae anaweza kumuunganishia mahala akapeta, lakini ambacho hakijui ni kwamba mtoto wake Shycass akija baadae anaweza kuwa hamjui mtu, kwa hiyo yeye, kizazi cha baadae, atapata shida, kwa hiyo tusipojenga mazingira ambayo hayajitaji kujuana kwa kweli si poa kwa nchi yetu.

So, to hell with kujuana na the Hassi Kitine's of the world. Screw that!
 
Nakubali.

Lakini sister brother p53, hata kama ungekuwa na jina la Baba wa matawi ya juu, au mtoto wa masikini, hutakiwi kukubali kupitia kwa watu maarufu, the Apson's and the Kitine's of the world, ili upate kazi sehemu kama Usalama wa Taifa. Ndio ufisadi wenyewe huo. Kwamba, my point is, p53, mambo ya connection connection na kujuana juana haya nishai. Mimi hapa nilipo sitaki kujuana na Kitine au Apson hata kama ningekuwa na access nao, hata kama wao ndio the go-to guys wa kukutafutia kazi Usalama. Sitaki, sitaki kuwajua. Wakae na ukuu wao na utajiri na umaarufu wao, waanze mbele!

Kwa nini tusijenge nchi ambayo sio lazima uka kiss ass kwa Kitine ili akuunganishie kazi Usalama wa Taifa? Yani mimi siwezi, siwezi, sijui ni kiburi cha kutotaka kuuza utu wangu, lakini sitaki.

Huyu Shycass anaweza kuwa na Kitine au jamaa yake fulani ambae anaweza kumuunganishia mahala akapeta, lakini ambacho hakijui ni kwamba mtoto wake Shycass akija baadae anaweza kuwa hamjui mtu, kwa hiyo yeye, kizazi cha baadae, atapata shida, kwa hiyo tusipojenga mazingira ambayo hayajitaji kujuana kwa kweli si poa kwa nchi yetu.

So, to hell with kujuana na the Hassi Kitine's of the world. Screw that!


mkuu nakubaliana na maelezo yako.lazima tujenge mazoea ya kujiamini tunapotaka kufanya kitu fulani kama tuna uwezo na sifa zinazotakiwa kufanya kitu hicho bila kupitia migongo ya watu.
nimesema kuwaona wa kina kitine ni mbinde kwakuwa nilidhani huo ndiyo utaratibu wenyewe kama unataka kazi usalama wa taifa lazima umuone kitine manake swali langu la msingi ni kujua utaratibu mzima wa kujiunga huko,swali ambalo mpaka sasa sijajibiwa zaidi ya kuambiwa nimtafute kitine.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom