Natafuta Kazi Usalama Wa taifa

Natafuta Kazi Usalama Wa taifa

Status
Not open for further replies.
Kwani kazi ya usalama wa Taifa mpaka ujue Karate? au ndio kigezo cha nchi yenu?

mi navyojua usalama wa taifa ni uwigo mpana sana kuna kitengo cha mawasiliano, uchumi, ulinzi, ujasusi nk,
na saa nyingine akili, uelewa, upelelezi, umakini, uchambuzi mzuri wa mambo ni kitu cha kwanza kuliko hayo mapigano

good luck wamekusikia na watakuchukua

Hizo mishemishe zilizo red ndizo nizitakazo mimi! Ningepewa nafasi; kazi yangu ya kwanza ingekuwa ni kuifitinisha Kenya na Sudan Kusini ili taifa hilo changa liangukie mikononi mwetu na tufanye nao butter trade vizuri!
 
ukifanya hii,utakuwa umewaconvince kama unaweza kuwa kwenye hili kundi.VUA NGUO KASHINDE POSTA MPYA SIKU ZIMA
 
Hachana na hizo post zinawenyewe hizo, kwani usiwe mwandishi wa habari upate kipato chako halali? shauriako my .. was there? hapafahi kabisa kama hauna network yakueleweka, fikiri hata ualimu m2 wangu riziki ni kokote au haulifahamu ili kama vipi kuwa hata karetia si umesema upo vizuri?
 
Jaribu kupiga hodi ofisi yao ya Kijitonyama. Kama unajua karate,hiyo ni plus,kwa sababu Usalama wa Taifa kazi yao ni karate tu na pistol shooting.
Pia lazima uwe mzalendo,kama ulivyosema wewe ni mzalendo.
Namaneno aliyosema Lt. Gen Mayunga tulipouwa Kurasini TMA tunasubiri kuanza Basic Training. Alisema,''Vijana,kama mmechagua kuwa wanajeshi,mmechagua kazi nzuri''
Kwa hiyo kama wewe unataka kazi ya Usalama wa Taifa,hiyo pia ni kazi nzuri.
 
wakuu kumbe bado mnakimbizana na hii thread.tayari nilishaghairi kufanya kazi huko.nimepata ofa ya kuuza kuuza tende mtaa wa kongo-dsm.lol

Kwa nini ulighairi kufanya kazi huko?Au ndio umeshaipata umeianza kwa mtindo wa kuuza tende?
 
Mwana huko kugumu,kwanza mchongo wake ni tight na deal za huko ni issue...we uza hata mapera mwana utatoka tu.
 
Usikate tamaa tembelea balozi zetu au ofisi zao Nyumbani. Ni watu wa kawa sana. Hakuna jipya sana. Kama ni ambition yako nenda wizara ya mambo ya ndani na omba kuonana na afisa mwajiri na utapata utaratibu wote. Asante.
 
wakuu shida yangu ni kupata ajira idara ya usalama wa taifa.sifaham ofisi zao zilipo wala mfumo wao wa kupokea maombi.
nina degree ya mass comm.nina moyo wa kizalendo,nacheza karate.mkakamavu nina sifa za ziada kem kem.nisaideni.
[/QUOTE=pole kaka chuo gani umesoma]
 
...unaona sasa, ushapoteza sifa ya pili hiyo kwa hilo swali lako...🙁

P53-are you the "interviewer" or just an ignorant! So you mean if you want a certain job you are not supposed to know some basic info about it!
 
Umepoteza sifa kwa kuwa kule wanachukua form 4 na 6 mbaya au mtu aliyepata gentleman Chuo Kikuu. KWa kifupi wanachukua wapuuzi ili waweze kuwatawala kiakili. Sasa kama wewe unafanya masters, labda kama unafanya by course work ujipatie gentleman ndio utafaa. Kama una akili, hama kabisa ikiwezekana hata Tanzania maana wanaofanikiwa Tanzania ni mazuzu tu

Kwa kuandika tu eti wanaofanikiwa Tanzania ni mazuzu, WEWE NI ZUZU NA TAHIRA NAMBA MOJA!unaishi wapi na kimaisha uko wapi! Tuna wangapi waliofanikiwa Tanzania!Kwa hiyo wote ili tufanikiwe tuhame nchi au sababu kila Mtanzania anataka kufanikiwa? Ebu acha story za kuvunjana moyo!
 
Ivi ni usalama wa taifa au wa "sisiemu"...
 
jaman ni weng tunaopenda kufanya kaz usalama wa taifa lakin hatujui tuanzie wap tusaidien wengine toka utoto wetu tunapenda tuwe watu wa usalama wa taifa
 
Zamani walikuwa wakipita shuleni hasa sekondari...nimesoma Tabora School form1-6...kila mwaka walikuwa wakija na kupick vijana wa form6 kabla ya kumaliza,wakimalza unaunganisha...vijana weng(Sio wote) walomaliza Tabora School(Boys and Girls) wapo UWT....wana shule wanazopendlea,hawajiendeiendei tu!
 
kwani usalama wa taifa ni wati wa cadre gani je polisi,wanajeshi,magereza,uhamiaji etc sio usalama wa taifa?
 
kwani usalama wa taifa ni wati wa cadre gani je polisi,wanajeshi,magereza,uhamiaji etc sio usalama wa taifa?
Ninaamini 'wamo' baadhi ya wafanyakazi katika taasisi ulizozitaja ni UWT. Lakini si wote. Na kumbuka hata walimu, madaktari ...n.k wamo pia UWT. Kwa kifupi katika almost every sector wapo hawa jamaa. Hii ni ninavyoamini!
 
Usalama wa taifa ni kitu nyeti sana. Tabia ya mtu mfano kutokuwa mropokaji ovyo unayeweza kutunza siri na uwe na afya njema na uwezo mzuri wa kiakiri vinaweza vikakupatia nafasi hiyo. Lakini tu endapo utaonekana na watu wanaofanya recruitment.. Kwa ninavyokuona wewe huna sifa hiyo kwani ile tu kuulizia kazi hizo inaashiria unaajenda fulani hidden.Watu wanaopata hizo nafasi na wao ilitokea kama zali tu, hawakuwa na malengo ya kufanya kazi hizo.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom