Natafuta Kazi Usalama Wa taifa

Natafuta Kazi Usalama Wa taifa

Status
Not open for further replies.
nimesoma kila post ili kujaribu kujua kama atatokea angalau mmoja nim-PM ili tulambe ajira wajamen......! Na nikipata kazi huko la kwanza ni kupambana na RUSHWA popote ilipo
 
nimesoma kila post ili kujaribu kujua kama atatokea angalau mmoja nim-PM ili tulambe ajira wajamen......! Na nikipata kazi huko la kwanza ni kupambana na RUSHWA popote ilipo

1) TAKUKURU wana ajiri, nenda makao makuu, Upanga Dar.

2) Kupambana na rushwa unaweza kuwa "vigilante" na si lazima uajiriwe, nakumbuka maneno ya Mkapa, Mei Mosi 2001:

"Lakini napata taabu nikiambiwa wafanyakazi wanalalamikia rushwa. Maana, hakuna mtu anayeitwa Serikali anayepokea rushwa. Mpokea rushwa si Serikali; ni mfanyakazi mwenzetu, tunamjua, lakini tunaoneana haya. Huo ndio ukweli, na unafanya kazi yetu iwe ngumu sana."
 
Mbona mimi ni mlinda Usalama wa Taifa na sijaajiriwa na mtu? nimejitolea kulinda Taifa langu.

Kweli wewe wote tunakujua ni mwajiriwa wa Nepi. Role yako ni kutetea serikali chovu ya CCM na mafisadi wake wote.
 
Hata hapa kwetu wanatangaza ila huwezi kujua kama hizo ndizo kazi zenyewe. Kwa mfano ukishakubali kuajiriwa PCCB ujue ni UWT. Hata hivyo ishu ya usalama wa taifa ni "complex" maana kila sehemu wapo. Kwa mfano katika vyuo vikuu hawa wapo na ili kulahizisha wanakuwa ni wafanyakazi wa taasisi hiyo.
Hilo ndo tusilolitaka, unatangaza kazi halafu eti ila huwezi kujua ndio zenyewe. Sasa mtu ataombaje? Hapa inahitajika transparency. Tunataka watu competent kwenye idara zetu wakatu huohuo wapatikane kwa fairness.

Kumpa mtu kazi kwa sababu ya connections ni rushwa pia. Tena kazi yenyewe ni kwenye ofisi ya umma. Huu ni mfumo mbaya na ndio maana watendaji wake wengine ni wale ambao hawakuwa na option ya cha kufanya wakalazimika kuwa kule. Mfumo wowote wa ajira za serikali unatakiwa uwe wazi. Umeonyesha hapo juu CIA na mashirika mengine ya kijasusi kama MI5 wanavyofanya kazi, kwanini hatujifunzi? Hawa jamaa siajabu hata websites hawana. Inaweza kuwa chaka pia la ufisadi kisa ni usalama. Ndio maana utasikia MEREMETA et al. zinasingiziwa maslahi ya nchi.

Halafu kwamba ukiajiriwa na PCCB ndio UWT sio kweli. Ni vitengo tofauti na kila mtu anakazi yake maalamu. Tunahitaji kuifumua hii mifumo ya kizamani isiyokuwa na Tija. Tukawa na watu wachache wenye kuleta ufanisi na kupunguza gharama. Maendeleo ya nchi kamwe hayawezi kupatikana kama kuna weak institutions impounded in poor governance structure.
 
Kwabahati mbaya siongei nisilolifaham kama unavyotaka kuniaminisha.

Hata wale top uwaonao wamefika pale mostly through promotion. najua kuna walimu et al. wanafanya kazi hiyo. Lakini swali ni kwamba, inakuwaje mtu atumike kumuidentify mtu kwa ajili ya kazi yenye maslahi kwa taifa? Anajuaje kwamba hawapo wenye qualification kubwa zaidi na wana interest na kazi hiyo?

Siku hizi dunia imebadilika saana. Sio mfumo wa kila sehem. Pitia baadhi ya websites za vitengo hivyo, unaweza kujifunza kitu. Naendelea kusema tena; informer atakuwa tu undercover lakini recruitment process iwe wazi alafu selection ndio iwe siri. Tatizo nini hapo? Unajua nchi yetu tunadhana ya ajabu saana ya usalama ndio maana hata matapeli hujitangaza ni usalama.

Sasa wewe kama unajua kinachokufanya uulize nonsenses ni nini? Masilahi ya Taifa ni yapi unayoyajua wewe ni yapi? Na wewe kama unajua hilo kwa nini unajifanya kipofu wa kusoma na brainless wa kuelewa na kuendelea kuuliza tu?, au unataka kujaza pages kwenye thread uliyoianzisha?

Na kwa nini ulalamikie kazi za usalama wa Taifa tu usilalamikie uwaziri, ukatibu mkuu, ukuu wa mikoa, ukuu wa wilaya etc, ambazo pia zina masilahi kwa taifa ila hazitangazwi watu wanateuliwa na mtu mmoja, Kwa nini?

Ukinipa majibu ya haya maswali basi niulize swali ila kama huna jibu usiniulize kwani huu ndiyo mchango wangu wa mwisho kwenye hii thread. I am neither here for the league nor for knowledge dispensing as I am doing this from the perspective of common sense and little know how from living in the world.
 
Unajua kuna aina nyingi za recrutment za wafanyakazi, nadhani inayotumika kwa usalama wa taifa ni hiyo ya kuchuja wale watu wanye tabia wanazotaka, kupendekezwa na watuwengine na kuwafuata na kuwapa kazi kama wengine wanavyosema hapo awali.

Nadhani mapungufu yake ni hiyo ya baba kupatia mwanae kazi, lakini lazima kuna watu wengine wanaofaa wengi watakuwa wanaingia humo. Hii njia ni official dunia hii, inatumiwa sana kwa zile sensitive positions.

Hiyo kazi ya usalama wa taifa nadhani ni sensitive kuwa kisirisiri ni haki yake na kuambiana watu unaowajua, nadhani hautapenda mtu mwenye asili labda ya kisomali kwa mbali kuwa huko kwa vile amepita selection criteria given.
 
wakuu shida yangu ni kupata ajira idara ya usalama wa taifa.sifaham ofisi zao zilipo wala mfumo wao wa kupokea maombi.
nina degree ya mass comm.nina moyo wa kizalendo,nacheza karate.mkakamavu nina sifa za ziada kem kem.nisaideni.
 
Ongea na watu wanao fanya kazi Ofisi ya raisi
 
hizo kazi ni mara chache sana kutangazwa kama kazi nyingine... ila jaribu kuwa karibu tu na wafanyakazi wa uko na uwaulizie inakuwa vp kujiunga.
 
Mdogo wangu.....kweli nia unayo tatizo hawa watu huwa ukitaka hawakupi kama ukipata basi itachukua muda since uaply even 10 can pass ndo wakuite...Fika makao makuu pale oysterbay TISS(Tanzania Inteligence Security Services)
 
umepitia shaolin?.....una kifua cha kutunza siri?........unaweza kujifanya kichaa na kula jalalani? unajua kutumia bastola?.....una.....ume...aahhh....maswali ni mengi....ila kila la heri
 
hivi braza nguli upo hapa daslama?...nakumisi sana mwana uwt mwenzangu
 
Una akili timamu?kama ndiyo basi huna kazi,kama hapana hufai kabisa...u need to have extra IQ! Be aware!
 
Mkuu hawa huwa wanatafuta wenyewe, wanaenda kwa watu wanaofahamika na kuwaambia "tunaomba utupe mwanao akafanye kazi usala wa taifa" mfano walishakuja kwa babaangu mkubwa ambeye ni mkuu wa........ Wakamwambia tunaomba kijana wako uliyemzaa wewe akafanye kazi usalama wa taifa. Ba mkubwa akatafuta mtoto wa rafiki yake wakaondoka nae.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom