Natafuta Kazi Usalama Wa taifa

Natafuta Kazi Usalama Wa taifa

Status
Not open for further replies.
usalama wa taifa wanakutafuta wenyewe si wewe ndio unawatafuta ka wakikuona unafaa wanakuomba u join nawo
 
Sijui kama utapata kazi kule. Nimeona siku za karibuni wamefanya recruiting sana.
Lakini kama unataka kuwa Usalama wa Taifa,usimwambie mtu yoyote kwamba unataka kuwa Usalama wa Taifa. Halafu watafute hao watu.

Kumbuka ile ni kazi ya kikachero,kwa hiyo usimwambie mtu yoyote.
 
Tathmini yangu ni kwamba mjadala wa namna ya kupata kazi Usalama wa Taifa umekuwa na sura nyingi zenye kupingana. Baadhi ya masuala yanaonekana ni ya kufikirika zaidi. Kama alivyo P53 nami ningependa kupata kazi Usalama wa Taifa kwa sababu hizo hizo za uzalendo kwani naamini chombo hiki kina nafasi muhimu ya kujenga taifa. Miongoni mwa mikanganyiko niliyoipata ni kama ifauatavyo:-

SHY anasema Mtanzania ataajiriwa Usalama wa Taifa baada ya kutoa taarifa fulani fulani kuhusu mambo fulani au kuomba magazetini kisha atajikuta yuko Usalama wa Taifa.

SHAYCAS anatuambia kama unataka kazi huko kamwone au wasiliana na mtu anayefanya kazi au aliyewahi kufanya kazi huko.

CHUMA anatuaelekeza kuwa kuingia Usalama wa Taifa hakuhitaji ‘connections’ kwa sababu utaratibu mpya wa sasa waombaji kazi Usalama wa Taifa huanza kwa kuajiriwa kama wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani.

DISSOFFICERREC anasema kazi za Usalama wa Taifa hazitoki magazetini.


PHILLEMON MIKAEL anatueleza kuwa Waziri Mkuu MIZENGO PINDA alipokuwa mwaka wa kwanza Mlimani ( chuo Kikuu cha Dar es salaam) alianza kwa ‘ assignment’ kupeleka taarifa msasani na baada ya kumaliza chuo akapelekwa Ikulu. Hivi hizo ‘assigments’ hazikuwa za siri kama utaratibu wa kazi za namna hiyo?

Kuna wanaotuambia ili kupata kazi Usalama wa Taifa tuwasiliane na kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ulinzi na Usalama au Makamanda wa Polisi.

Yupo anayesema Usalama ni ya watu wa Ikulu pekee hapo hapo anatusihi tuombe kazi huko.

Lakini pia katika ya mjadala tunaambiwa kuwa kama shuleni ulikuwa mbumbumbu huwezi kuajiriwa na chombo cha intelijensia.

Vilevile katika mjadala huu imejitokeza kuwa Usalama wa Taifa wana ‘target’ zao na kama wewe siyo lengo kamwe huwezi kuchukuliwa.

Katika maelezo mengine ni mchanganyiko wa hapa na pale!!! Hivi katika mjadala huu ni nani mkweli ili anisaidie na mimi kuingia huko?


KUKIRI KWAMBA JAMBO SILIFAHAMU SI UPUMBAVU BALI NI UKOMAVU WA AKILI.

Mkuu upo kitengo gani? Nimekuogopa tayari.
 
WanajamiiF kazi hizi za usalama wa taifa zipo ila ni kwa nini wewe uone kazi ni usalama wa taifa tu......baba yangu ni mkulima wa mpunga na mahindi na yeye pia ni usalama wa taifa...''he is a national security officer to secure the nation from being affected by famine okey you can judge yourself under any aspect like my father as well as me myself I am a carpenter''....msing'ang'anie kazi huenda Mungu anataka kukuepusha na uuaji...because si wote wanashika peni wengine wanashika bastola kuwaua wema.
 
WanajamiiF kazi hizi za usalama wa taifa zipo ila ni kwa nini wewe uone kazi ni usalama wa taifa tu......baba yangu ni mkulima wa mpunga na mahindi na yeye pia ni usalama wa taifa...''he is a national security officer to secure the nation from being affected by famine okey you can judge yourself under any aspect like my father as well as me myself I am a carpenter''....msing'ang'anie kazi huenda Mungu anataka kukuepusha na uuaji...because si wote wanashika peni wengine wanashika bastola kuwaua wema.

Bora umeniunga mkono maana mm niliamua kuji recruit mwenyewe kuilinda nchi kwa maombi na sala na sihaba Mungu ananifungua macho naona visivyoonekana na kupata habari kabla hazijawa habari....Kwa wanaotamani self employment kwenye field hii nipo tayari kutoa coaching...
 
Hivi kweli Tanzania nako kuna 'Usalama wa Taifa' kwa maana ya intelligence agency au kitu kama hicho? Watu wanaozidiwa maarifa hadi na waandishi wa udaku? Kule siku hizi kuna wasengenyaji tu! 'Usalama wa Taifa' ilikuwepo enzi ya Mwalimu Nyerere na ilizikwa pamoja naye.
 
kazi kweli*2, nashangaa sana ndg zangu, wewe unataka uwe usalama kisha iweje? Unashindwa kufiri ni jinsi gani waweza kupata trekta uka54me, tafakari
 
CIA (TISS) Vision, Mission & Values

Vision

One Agency. One Community. An Agency unmatched in its core capabilities, functioning as one team, fully integrated into the Intelligence Community.

Mission


We are the nation's first line of defense. We accomplish what others cannot accomplish and go where others cannot go. We carry out our mission by:
  • Collecting information that reveals the plans, intentions and capabilities of our adversaries and provides the basis for decision and action.
  • Producing timely analysis that provides insight, warning and opportunity to the President and decisionmakers charged with protecting and advancing America's interests. (Tanzanian Interest)
  • Conducting covert action at the direction of the President to preempt threats or achieve US (TZ) policy objectives.
Core Values

  • Service. We put Country first and Agency before self. Quiet patriotism is our hallmark. We are dedicated to the mission, and we pride ourselves on our extraordinary responsiveness to the needs of our customers (Umma).
  • Integrity. We uphold the highest standards of conduct. We seek and speak the truth-to our colleagues and to our customers. We honor those Agency officers who have come before us and we honor the colleagues with whom we work today.
  • Excellence. We hold ourselves-and each other-to the highest standards. We embrace personal accountability. We reflect on our performance and learn from that reflection.






Posted: Apr 04, 2007 03:54 PM

Last Updated: Jun 02, 2008 09:36 AM

Last Reviewed: Apr 12, 2007 07:39 AM


Hapa inabidi tuangalie, huyu mtu anatakiwa awe kichwa kweli, aimudu profession na awe mzalendo kweli. Hawezi kutumika kuchakachua matokeo yoyote yale.

Huyu sio mtoto wa mjomba.:msela:

Kwa nini natoa mfano wa USA:
Hawa wamekaa kimaslahi ya umma wao zaidi, hebu angalia walivyo sambaa:

United States
Sasa uwanja wake ni mpana sana, inategemea na upeo wa Nchi wa kuona mambo. Sijui utafiti wapi tukuchukue.
 
Mjomba mwenye thread unayeomba kazi usalama wa Taifa,kama kweli una Masters degree,basi bado una nafasi ya kupata kibarua kizuri tu hapa bongo.Sijui lengo lako hasa ni nini huko usalama wa Taifa,lakini binafsi ningekushauri utafute kazi nyingine tu kama kweli una elimu uliyoisema.
 
Kazi nyingine mnazo taka hamzijui na unaingia kichwakichwa kushtukia umenaswa huwezi kusema hutaki kufanya kazi hiyo ukiona huipendi.
Ukiwa Askari wa kawaida kama jeshi la wananchi, polisi uko huru kufanya kazi kwa mkataba ulioweka na serikali na kisha makataba unaweza amua kuendelea au la. Kazi hizi za kishushushu ama usalama wa taifa zinafanyika katika mazingira ya kutunza siri nzito za watu na serikali na kwa maana hiyo unabaki shushushu hadi siku umekata pumzi tukuteremshe kwenda ahera.
Uhuru nao ni muhimu kwani kufanya kazi kwa kufuata maelekezo ya bosi wako utake usitake lazima ifanye ilivyokusudiwa na bosi wako hata kama dhamira yako haikubali.
Ndiyo maana hiyo ni idara pekee aya serikali mbayo haina utaratibu wa uwazi wa kuajiri isipokuwa huajiri kwa usiri mkubwa na kwa taratibu wanazojua wenyewe.
kwa kukusaidia jaribu kujenga urafiki na mmoja unayemfikiria ni shushushu huyo ndiyo atakayekunyooshea njia na kukuunganishia.
 
Nakubali.

Lakini sister brother p53, hata kama ungekuwa na jina la Baba wa matawi ya juu, au mtoto wa masikini, hutakiwi kukubali kupitia kwa watu maarufu, the Apson's and the Kitine's of the world, ili upate kazi sehemu kama Usalama wa Taifa. Ndio ufisadi wenyewe huo. Kwamba, my point is, p53, mambo ya connection connection na kujuana juana haya nishai. Mimi hapa nilipo sitaki kujuana na Kitine au Apson hata kama ningekuwa na access nao, hata kama wao ndio the go-to guys wa kukutafutia kazi Usalama. Sitaki, sitaki kuwajua. Wakae na ukuu wao na utajiri na umaarufu wao, waanze mbele!

Kwa nini tusijenge nchi ambayo sio lazima uka kiss ass kwa Kitine ili akuunganishie kazi Usalama wa Taifa? Yani mimi siwezi, siwezi, sijui ni kiburi cha kutotaka kuuza utu wangu, lakini sitaki.

Huyu Shycass anaweza kuwa na Kitine au jamaa yake fulani ambae anaweza kumuunganishia mahala akapeta, lakini ambacho hakijui ni kwamba mtoto wake Shycass akija baadae anaweza kuwa hamjui mtu, kwa hiyo yeye, kizazi cha baadae, atapata shida, kwa hiyo tusipojenga mazingira ambayo hayajitaji kujuana kwa kweli si poa kwa nchi yetu.

So, to hell with kujuana na the Hassi Kitine's of the world. Screw that!

Ebwana Kuhani umepotelea wapi mazee??Rudi tukate inshu mazee!!
 
Hata wewe unaweza kuwa usalama wa taifa unaweza kutumika sehemu fulani fulani kutoa taarifa fulani kuhusu mambo fulani mwanzo huwa ni hapo wakati mwingine ni hizi kazi za magazetini wewe apply tu utajiona siku dili na usalama wa taifa hilo limekuangukia

Yes kama wewe ulivyo au sio...
 
Mie mwenyewe nataman kufanya kaz usalama wa Taifa.sifa ninazo.nimewachunguza wapenz wangu wote mpaka kuwafumania wale wasiokuwa waaminifu.nimetunza siri za mahusiano yangu hakuna mpnz aliyegundua km nilizoea kumsaliti.ujuzi wa kujilinda ninao,sijawahi kuvamiwa na mwizi tangu nianze kuishi peke yangu.nahitaji kweli hii kazi ili kuokoa Taifa langu
 
Mie mwenyewe nataman kufanya kaz usalama wa Taifa.sifa ninazo.nimewachunguza wapenz wangu wote mpaka kuwafumania wale wasiokuwa waaminifu.nimetunza siri za mahusiano yangu hakuna mpnz aliyegundua km nilizoea kumsaliti.ujuzi wa kujilinda ninao,sijawahi kuvamiwa na mwizi tangu nianze kuishi peke yangu.nahitaji kweli hii kazi ili kuokoa Taifa langu

Wakikutuma kwenda kumwagia madawa yanayonuka na kuwasha mtu fulani utakuwa tayari kwenda kufanya kazi hiyo? Jua lazima Mungu umweke kando kwanza ila amri ya cheif wako ndiyo Mungu wako
 
how and why?

Umepoteza sifa kwa kuwa kule wanachukua form 4 na 6 mbaya au mtu aliyepata gentleman Chuo Kikuu. KWa kifupi wanachukua wapuuzi ili waweze kuwatawala kiakili. Sasa kama wewe unafanya masters, labda kama unafanya by course work ujipatie gentleman ndio utafaa. Kama una akili, hama kabisa ikiwezekana hata Tanzania maana wanaofanikiwa Tanzania ni mazuzu tu
 
Baada ya kusoma maelezo yako na kuyahusianisha na swali (kichwa) la mada yako,
"Nani mwenye sifa za kufanya kazi usalama wa taifa?"
Jibu 1:
Ni yule anayetakiwa kuwa na uwezo wa kuchunguza kwa makini, mfano hili swali lako na kisha kufanya uamuzi yenye ufanisi kwa wakati muafaka wa kulikarabati lisomeke:
" Ni sifa gani zitakiwazo kumfanya mtu aweze kufanya kazi Usalama wa Taifa?"

Jibu 2: Sifa zitakiwazo zinapatikana katika viapo viwili vya Watumishi wa UWT:-

1. i. Uwezo wa kutekeleza Kiapo cha Kazi (Ofisi)
(Kuajibika kwa uaminifu na pasipo upendeleo kwa uwezo wote kutekeleza majukumu utakayopewa ndani ya UWT)

2. ii. Uwezo wa kutekeleza Kiapo cha Ulinzi na Usalama
(Kutotoa taarifa ulizozipata katika majukumu ya UWT pasi kibali cha Mamlaka husika)
 
Wengi wamekuwa huku wakisikia watu wakijiita Usalama wa taifa. Lakini wengi hao ukiwauliza hao wanaojiita usalama wa Taifa wanapatikanaje jibu litakuwa sijui. Maana nafasi hizo huwa hazitangazwi.

Kwa wale wanaofaham aina ya selection yaani kuchagua mfanyaki hiyo huwa inaitwa internal selection. Yaani mtu anaingia pale kutokana na kuwa anafahamiana na mtu, au rafiki na hata ndugu. Kwa maana nyingine imekuwa kama ni kazi ya uganga au wale wafanyabiashara maarufu-yaani kazi ya kurithi.

Hili ni taifa letu sote. Kila mtu ana haki ya kulitumikia Taifa lake. Na katiba ya nchi inakataza kabisa kubagua na ndio nguzo mama ya maswala yetu yote yahusuyo nchi yetu. Inawezekana waanzilishi wa mfumo huu kwa mtazamo wa wakati huo walikuwa sahihi lakini kwa wakati wa sasa si mtazamo sahihi.

Tunaweza kujiuliza kuna nini kinachofichwa mpaka mfumo huo uendelee kuwa wa siri mpaka leo? Je hawaoni kuwa kuendelea kufanya hivyo ni kuwanyima watu wenye uwezo zaidi wa kufanya kazi kuisaidia taasisi ile nyeti? Kwani wakitangaza nafasi, hawawezi kufanya vetting kujua kama kuna tatizo na muhusika? Kwani kutegemea family ties au urafiki hakuwezi kusababisha mtu asiyetakiwa naye akaingia?

Imefika wakati mfumo ule ubadilike na kila Mtanzania apewe nafasi kama ilivyo taasisi nyingine. Mbona MI5 wao na wengine wengi tu hutangaza nafasi zile? Labda kama kuna utaratibu mwingine wa uwazi, tujuzane hapa jamvini.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom