Dume la Mende
JF-Expert Member
- Mar 23, 2011
- 423
- 66
Acha kulialia wewe,, gangamala
umenistua nilifikiria wametoa tangazo la kazi nitume maombi.
Tatizo langu ni hapo ambao si lazima wote wajue kwanini? Kwanini hatutaki kujifunza? Wale wanaotangaza kwenye website zao je inakuwaje? Infiltration ya foreign agents haiwezi kutokea kwa namna hiyo?Ndugu Anfaal,
Nakubali kuwa suala la kujuana linaweza kuwepo (karibu kila idara TZ iko hivyo), ila nafikiri utaratibu wa haki pia upo. Lakini utaratibu wenyewe nafikiri ni sehemu pia ya "usalama wa Taifa" kwa hiyo si lazima wote tuufahamu ili kuepusha "infiltration of foreign agents". Nafikiri kuna information huwa zinakuwa released based on "need to know".
Hii umeitoa wapi? Ninawafahamu wengi saaana ambao waliajiriwa kwa sababu tu baba zao au jamaa na rafiki wako kule. Hii ni mentality mbaya saana. Halafu kwanini wemegwe tofauti? Kazi hizi ni tofauti saana zilivyo na ndio maana hata wizara ni tofauti na namna ya utendaji ni tofauti. Mtu anaweza asiwe na interests na polisi lakini akawa na interests usalama na kinyume chake.Usalama una aply polisi afu wao ndo wanamega baadhi kwenda mafunzo ya usalama wa taifa. Huwa sehemu tofaut na wanaofanya upolisi
Sikiliza bwana mdogo, hakuna mtu mwenye shida ya kazi bali tatizo tunalohangaika ni usawa hapa.Acha kulialia wewe,, gangamala
Ndugu Anfaal,
Inawezekana kabisa kuwa umejaribu kutafuta kazi ukakosa au umeona kuwa kazi unazopata hazilipi. Ukiangalia neno 'Usalama wa Taifa' utadhani ni very sensitive job ila kazi hizi huunganisha kuanzia polisi, JWTZ, askari kanzu, wapelelezi n.k, Ukija kwenye kazi kama JWTZ, Polisi hawa kazi zao hutangazwa.
Ila linapokuja suala la upelelezi [Hapa nina maana siyo kupeleleza kesi na matukio ya jinai bali ni kupeleleza wananchi (informer/shushu, nusanusa, mnoko, umbeya n.k) ili kujua kama kuna njama zozote zile zinazoweza kuitia nchi katika msukosuko wa kiuongozi kama uasi, mapinduz i(japo siku hizi yamekosa msukumo baada ya jumuiya za kimaifa kuwatenga wapinduaji)] hapo kidogo inakuwa ni sensitive, maana ukishamjua mbeya huwezi ku-disclose issue yoyote nyeti kwa kuhofia kuwa atawapelekea watawala.
Hawa ni lazima wawe watu walio under cover. Na wengi wao huwa na kazi nyingine kabisa zaidi ya upashaji wa habari za kimbeya. Ila katika group hili wapo wa aina mbili kuna wale ambao ni permanently employed na wanajulikana kama analysts, wao kazi yao ni kukusanya habari toka kwa wapashaji na kuzianalyse na kuchukua genuine na kuzipeleka kwa baraza la usalama for action na mara nyingi hukabidhiwa rais. Hawa ma analyst hata ukiwajua haitasaidia kitu kwani wao si frontliners, watu ambao wapo kwenye risk zaidi ni frontliners ambao kama wakujulikana huweza hata kupoteza maisha na ndiyo maana wanalindwa kwa kuwa under cover.
Lakini ukiangalia historia ya usalama wa taifa utaona imeanzia Egypt kwa Filauni (Pharao) ambaye alipata habari ya kuja kwa nabii Mussa ambaye ataushinda utawala wake toka kwa mtabiri wake aliyemwamini sana. Filauni alipoona hivyo akaweka watu kuchunguza kila mtoto atakayezaliwa popote ajulikane na kama ni wa kiume auwawe kabla ya kuja kuwa adui wa utawala wake na kumuangusha, hapo ndipo chanzo cha usalama wa Taifa ulipoanzia.
Kwa nini wewe unataka kazi hii??
Husninyo, hata ingekuwa Tangazo unajua barua zinatumwa wapi? Hiyo title ilibidi iwe hivyo ili tu........umenistua nilifikiria wametoa tangazo la kazi nitume maombi.
nijifanye mara ngapi?Jifanye mwanaharakati utafuatwa na kuajiriwa.
dah! Labda makao makuu sijui wapi wapi kuleeee!Husninyo, hata ingekuwa Tangazo unajua barua zinatumwa wapi? Hiyo title ilibidi iwe hivyo ili tu........
Tatizo langu ni hapo ambao si lazima wote wajue kwanini? Kwanini hatutaki kujifunza? wale wanaotangaza kwenye website zao je inakuwaje? Infiltration ya foreign agents haiwezi kutokea kwa namna hiyo?
wanijuze na mimi niapply. Lol.wenyewe wapo hapa,watakujuza kwa PM!
Asante kwa maelezo yako.
Sijatamka kuwa ninaitaka kazi hii sehemu yoyote hapo. Na si kwamba kazi yangu ni mbaya. Hapana, ni bora saana na ninaipenda na sijutii kuwa kwenye hii proffesional maana imenifikisha nilipo. Lakini ninachozungumzia ni uwazi wa recruitment naomba tuelewanae. Si selection wala namna wanavyofanya kazi. Kuna watu wangependa kuwa huko lakini kwa bahati mbaya mfumo mbovu wa utoaji kazi hizi haueleweki.
Hii kazi ni kama kazi yoyote vile. Leo unasikia fulani ni polisi bila kujua polisi wanapatikana vipi. Popote pale kwenye kificho ndio chanzo cha rushwa. nakumbuka miaka hiyo tumemaliza form 6 kuna mtu alikuwa anapita anawaambia watu wampe pesa atawaingiza usalama. Why?
Nimesema mwazoni kwanini iunganishwe na polisi au JWTZ. Historia ipo, yes, lakini iwe chanzo cha kutupeleka mbele sio kung'ang'ania utaratibu uliopo.
Hivi ni visingizio ambavyo vinakwamisha saana maendeleo yetu. Hivi unafaham kwamba wale wanaopelekwa na ndugu zao wanafanyiwa vetting tena wakati fulani huchukua hata miaka miwili. Sasa kama wanaweza kuwafanyia vetting hao kwanini wasifanye kwa wote.Nchi yetu huwezi kulinganisha na UK au USA au na nchi zingine nyingi tu zilizotuacha kimaendeleo.
Nchi za wenzetu, institutions zao nyingi ndani ya serikali, zipo kamili. Mtu una-apply hata kutoka kwenye website zao, lakini wanaweza wakakufahamu hata kabla hawajakuita. Sisi tupo nyuma sana, kiasi kwamba hata vitambulisho vya uraia hatuna, vitambulisho vya kazini na kupigia kura, hata asiye raia anaweza kuwa navyo, kwa namna hii, nafikiri utaratibu wetu inabidi uwe crude. Isitoshe, si ajabu wengi kwenye UWT hata level zao za IT zikawa chini, wakitumia websites labda hata vijana wa hapa jukwaani wanaweza ku-hack. Unaweza kukuta Mkurugenzi mwenyewe anatetemeka kushika mouse ya computer.
Nafikiri tuwape benefit of doubt, kwamba hata kama hatujui wanavyopeana kazi, basi wanapeana kwa kufuata misingi fulani ya haki, huku wakitunza siri za usalama wa nchi yetu.
Kwa bahati mbaya siongei nisilolifaham kama unavyotaka kuniaminisha. Hata wale top uwaonao wamefika pale mostly through promotion.Frontliners wa UWT hata siku moja hawawezi kutangazwa kama vile wanavyotangaziwa "state attorneys et al" Sababu kubwa ni kwamba wanatakiwa kufanya kazi under cover full stop, anaweza kuwa lecturer wako chuoni, manager wako kazini, katibu mkuu wako wizarani, katibu muhtasi wako kazini.
Recruitment ya watu hawa ni sensitive na unaweza fuatwa na mtu usimfahamu aka kushawishi, then utajikuta unatembelewa na strangers kukuchimba, bila kujua ndiyo usaili wenyewe huo, sasa wewe baada ya hapo unapelekwa kwenye mafunzo. Nchi nyingi duniani hutumia mfumo huu, lengo likiwa ni kuhakikisha informer abakia kuw under cover ili kumlinda yeye uwezo wake wa kupata habari. Mara nyingi akiisha julikana tu basi huwa ni mwisho wa kazi hiyo, au anahamishiwa sehemu isiyohitaji cover.
Jaribu hata kuwa unafuatilia hata sinema za kipelelezi basi mambo mengine ni common sense tu si lazima uwe huko.
Hili linategemea nchi na nchi.
Ziko nchi nyingine wanatangaza kabisa (soma hapa Vacancies in Intelligence Bureau Recruitment (Central Intelligence Officer) 2009 …….; https://www.cia.gov/careers/opportun...obs/index.html).
Hata hapa kwetu wanatangaza ila huwezi kujua kama hizo ndizo kazi zenyewe. Kwa mfano ukishakubali kuajiriwa PCCB ujue ni UWT. Hata hivyo ishu ya usalama wa taifa ni "complex" maana kila sehemu wapo. Kwa mfano katika vyuo vikuu hawa wapo na ili kurahisisha wanakuwa ni wafanyakazi wa taasisi hiyo. Muda mwingine tax driver ambaye hajaenda hata shule wanafanya hiyo kazi wapo tunawajua. Hata mkeo anaweza kuwa shushushu wako na usijue.
Zamani enzi tukiwa shule ya msingi mwalimu mkuu alikuwa anapewa jukumu la kutafuta vijana safi kimaadili ambao baadaye walikuja kuwa UWT.