ndugu wanalugha, baada ya kuhamasishwa na mjadala mkali kuhusu uzawa, uasili, uzalendo na uraia nimeamua kubadili jina langu lisilo la kiafrika ili niwe na jina la kikwetu. Sasa shida niliyo nayo ni kupata jina muafaka. Nachotaka ni jina la kiafrika/kitanzania. Laweza kuwa la kibantu au la ili mradi liwe la kiafrika. Tena liwe na maana inayojulikana na inayoweza kuhamasisha uzalendo. Kwa sasa nimepata majina hayo hapo chini, naomba mniongezee mengine ili nipanue wigo wa uchaguzi.
1. Bimwenyi
2. Ngabuto
3. Zakenda
4. Mwakisaka
5. Vavi
kalagesye