mama D
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 19,760
- 35,205
Rais John Pombe Magufuli ametoa msimamo wa taifa kuhusiana na maambukizi ya Corona pamoja na chanjo inayopigiwa kampeni na dunia kwamba kila nchi lazima ipatiwe chanjo hiyo.
Watanzania wengi wamemuelewa Rais na wanachukua tahadhari na pia wameelewa msimamo wa Rais kuhusu chanjo ya Corona. Ila penye wa kuelewa na wakupinga hawakosekani, na kuna watanzania wengi haswa wenye itikadi tofauti za kisiasa wanampinga Rais tena wakitumia nguvu kubwa sana kuhamasisha watu wakachanjwe.
Mimi binafsi nina maswali machache kuhusu hiyo chanjo:
1. Imetumika wapi kama majaribio na matokeo yake ni yapi hadi tuje kuchomwa huku kwetu? Tusisahau mwaka Jana walisema kabisa chanjo ingepatikana ilitakiwa ianzie kutumika Africa wakatoa sababu eti kuna uhaba wa health facilities kwa hiyo kukinga ni bora kuliko kutibu, sasa wameona ngoma imegoma na waafrika hawajaathirika kwa kiasi kikubwa walivyotaka bado wanalazimisha, kulikoni?
2. Wakati UK wanareport wastani wa vifo 1000 kwa siku, USA wao wana wastani wa vifo 4000 kwa siku. Kwanini wasitoe hiyo chanjo kwenye hizi nchi zilizoathirika zaidi ili kuonyesha effectiveness ya chanjo na kutokomeza vifo kabla ya kuja Africa?
3. Wataalamu wa mfumo wa upumuaji wanasema hakuna chanjo inayoweza kupambana na virus vya mfumo wa upumuaji kwa 100%, wanasema kama kuna chanjo inaweza kuwa effective 50% 60% ila kikubwa wanachoshauri ni wanadamu kubadili mfumo wa maisha ikiwa ni pamoja na Kula, kunywa na kubadili tabia zinazoweza kuchochea maambukizi. Je, kwanini WHO hawatumii nguvu kubwa kutoa hii hamasa kwa dunia kama wanavyohamasisha chanjo?
4. Tumsikilize Mtanzania mwenzetu hapa chini na tutafakari huu upendo mkubwa hivi kwa mataifa yaliyoendelea wa kutaka kutulinda ili tusife wakati wao wanakufa kila siku tena kwa maelfu unasababishwa na nini?
I STAND WITH MY PRESIDENT JOHN POMBE MAGUFULI
Pongezi kwa serikali ya Zambia kwa kuvunja ukimya
MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU IBARIKI AFRIKA🙏
Watanzania wengi wamemuelewa Rais na wanachukua tahadhari na pia wameelewa msimamo wa Rais kuhusu chanjo ya Corona. Ila penye wa kuelewa na wakupinga hawakosekani, na kuna watanzania wengi haswa wenye itikadi tofauti za kisiasa wanampinga Rais tena wakitumia nguvu kubwa sana kuhamasisha watu wakachanjwe.
Mimi binafsi nina maswali machache kuhusu hiyo chanjo:
1. Imetumika wapi kama majaribio na matokeo yake ni yapi hadi tuje kuchomwa huku kwetu? Tusisahau mwaka Jana walisema kabisa chanjo ingepatikana ilitakiwa ianzie kutumika Africa wakatoa sababu eti kuna uhaba wa health facilities kwa hiyo kukinga ni bora kuliko kutibu, sasa wameona ngoma imegoma na waafrika hawajaathirika kwa kiasi kikubwa walivyotaka bado wanalazimisha, kulikoni?
2. Wakati UK wanareport wastani wa vifo 1000 kwa siku, USA wao wana wastani wa vifo 4000 kwa siku. Kwanini wasitoe hiyo chanjo kwenye hizi nchi zilizoathirika zaidi ili kuonyesha effectiveness ya chanjo na kutokomeza vifo kabla ya kuja Africa?
3. Wataalamu wa mfumo wa upumuaji wanasema hakuna chanjo inayoweza kupambana na virus vya mfumo wa upumuaji kwa 100%, wanasema kama kuna chanjo inaweza kuwa effective 50% 60% ila kikubwa wanachoshauri ni wanadamu kubadili mfumo wa maisha ikiwa ni pamoja na Kula, kunywa na kubadili tabia zinazoweza kuchochea maambukizi. Je, kwanini WHO hawatumii nguvu kubwa kutoa hii hamasa kwa dunia kama wanavyohamasisha chanjo?
4. Tumsikilize Mtanzania mwenzetu hapa chini na tutafakari huu upendo mkubwa hivi kwa mataifa yaliyoendelea wa kutaka kutulinda ili tusife wakati wao wanakufa kila siku tena kwa maelfu unasababishwa na nini?
I STAND WITH MY PRESIDENT JOHN POMBE MAGUFULI
Pongezi kwa serikali ya Zambia kwa kuvunja ukimya
MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU IBARIKI AFRIKA🙏