Nashauri Spika Ndugai ajiuzulu
Rais ni Nembo ya nchi yetu na ni sauti halali ya watanzania wote. Kwa misingi hiyo bila kujali mawazo yangu binafsi dhidi ya Rais Samia, lakini anapokuwa anatekeleza majukumu yake kama Rais wa nchi hapaswi kubezwa na mtu yeyote hadharani. Mtu akifanya hivyo anakuwa ametudhalilisha watanzania wote tuliompa dhamana Rais wetu kutenda na kuongoza kwa niaba yetu.

Kwa hiyo mh Ndugai tumng'ang'ie na tumwajibishe ili liwe fundisho kwa yeyote mwenye mwelekeo wa kudhalilisha taasisi hii muhimu ya urais. NINAMWOMBA RAIS SAMIA ASIWASHIKE MIKONO WOTE WALIOAMUA KUMWAJIBISHA HUYU ALIYELEWA MADARAKA NA KUDHANI MAMLAKA YA URAÌS YANAPUNGUKA KAMA JINSI YA "KE" IKIWA IMEKALIA KITI CHA URAIS!!!

Ndugai lazima ANG'OKE.
Kauli ya Ndugai itawaprove wrong. Kukopa hovyo na kupeleka kujenga matundu ya vyoo, ndio hela itarudi? Matundu ya vyoo yanaongezaje uwezo wa serikali wa kukusanya kodi za kuweza kurejesha mkopo?
 
Hakuna chochote, uzushi uliozoeleka kila siku, ni kama ule uzushi wenu wa Msoga ndiyo inaongoza Ikulu, Nonsense

Ninakazia "minyukano yenu huko havituhusu."

Katiba mpya ndiyo pekee kinacho tufikirisha.
 
Ninakazia "minyukano yenu huko havituhusu."

Katiba mpya ndiyo pekee kinacho tufikirisha.
Na hiyo katiba haiwezi kupatikana bila Samia na Chama chake kuridhia, na maridhiano hayo yanakuja kwa mazungumzo na siyo kususia kama last borns.
 
Endeleeni na huo uanaharakati wenu tuone utawafikisha wapi, hizo harakati zimeshindwa hata kumpatia dhamana Mkiti wenu ndiyo zitatuletea jambo kubwa kama katiba? Evolve guys, hatupo tena kwenye dunia ya akina Che Guavara

Dunia ya akina Guevara inaishi na itaendelea kuishi.

Uzuri ni kuwa hatuwahitaji.

Kila mtu na ajishindie mechi zake.
 
Dunia ya akina Guevara inaishi na itaendelea kuishi.

Uzuri ni kuwa hatuwahitaji.

Kila mtu na ajishindie mechi zake.
Sawa Chief, Ila sidhani kama uzinjanthropus utawatoka siku za karibuni
 
Umevisahau ghafla vilivyo fanywa Chatto na kanda pendwa kwa ujumla, walipaji sisi?

Chato kupo hivi. Je, hii ngozi haivutwi mno?

Cheti? No wonder nina vyeti matata sana kuliko utakavyoweza kuvipata maishani mwako mburula wewe.

Hata hivyo nisiache kukwambia. Msituhusishe na mambo yenu. Habari nzima iko hapa:

1. Minyukano ndani ya CCM haitusaidii kwenye madai yetu ya katiba mpya.
2. Mwendazake hayupo tena, makando kando yake tuhangaike nayo kwenye "haki na maridhiano" baada ya katiba mpya.
3. Agenda yetu ni ya kudumu si marafiki.


Pambaneni na hali zenu huko.
Inaonekana kamavile unastress na dishi limeyumba kidogo.
Kwani wewe ulitaka hiyo barabara ikajengwe mkoa ama wilaya gani ndio ungeridhika.
 
Inaonekana kamavile unastress na dishi limeyumba kidogo.
Kwani wewe ulitaka hiyo barabara ikajengwe mkoa ama wilaya gani ndio ungeridhika.

Mwenye dish lililoyumba ana reference bora kuliko ulizo nazo wewe?

Pambaneni na hali zenu huko.

Sisi hayatuhusu na wala msituhusishe.

Angalizo: Kumbe wewe ni mshika zamu kwenye lindo? Kwa hakika dish kuyumba na stress haziwezi kuwa mbali nawe.

Hiiiiii bagosha!
 
Kukopa ndiyo mojawapo ya nguzo za uchumi, hata uwe tajiri kivipi lazima ukope na kukopesha ili mzunguko wa fedha uwe imara. Kuna mataifa tajiri lakini yana madeni makubwa mno, kwa hiyo tunatakiwa kukopa hata mara 10 ya deni la sasa.
 
Mwenye dish lililoyumba ana reference bora kuliko ulizo nazo wewe?

Pambaneni na hali zenu huko.

Sisi hayatuhusu na wala msituhusishe.

Angalizo: Kumbe wewe ni mshika zamu kwenye lindo? Kwa hakika dish kuyumba na stress haziwezi kuwa mbali nawe.

Hiiiiii bagosha!

Nimekuuliza ulitaka hizo barabara zilizo jengwa huko chato unazosema ni upendeleo ulitaka zijengwe mkoa,ama wilaya gani ndio ingekuwa sawa na si upendeleo!.

Jibu swali acha kurukaruka kama marage jikoni.
 
Nimekuuliza ulitaka hizo barabara zilizo jegwa huko chato unazosema ni upendeleo ulitaka zijengwe mkoa,ama wilaya gani ndio ingekuwa sawa na si upendeleo!.

Jibu swali acha kurukaruka kama marage jikoni.

Nani alikuwa akilipa alipokuwa akiyafanya kwenu?

Huyu naye ahakikishe Zenji ni Ulaya kabisa ili akili ziwakae sawa mamburula nyie.

Hamkujua umuhimu wa nchi kuzingatia katiba huko ila leo?

Sasa hivi linda kaburini jomba maana imeisha hiyo!
 
Si walisema mwenye kicheko bora si ni yule mwenye kucheka mwisho? Wala isiwe taabu tutakumbushana. Inshallah.
Hayo yalikuwa enzi hizo, now tuna AI, mambo mapya kabisa, ukileta usumbufu sana tunakushushia drone then maisha yanaendelea
 
Hayo yalikuwa enzi hizo, now tuna AI, mambo mapya kabisa, ukileta usumbufu sana tunakushushia drone then maisha yanaendelea

Drone mpate wapi si mseme tu kina Goodluck wamesokomeza watu kwenye viroba kwa niaba yenu?
 
Ndugu zangu wa JF

Nitoe maoni yangu kama Mtanzania Mzalendo kufuatia kauli ya Ndugai kubeza kitendo cha Rais Samia kuendelea na Sera ya kukopa Fedha nje ya Nchi kugharamia miradi ya Maendeleo

Kauli ya Mheshimiwa Ndugai sio tu inabeza na kudharau mamlaka ya Rais bali inalenga kuhujumu jitihada za makusudi za Rais Samia kukamilisha miradi mikubwa ya maendeleo inayohitaji Fedha nyingi sana kuikamilisha

Mheshimiwa Ndugai akiwa Kiongozi wa Bunge ameshindwa kuonyesha uwajibikaji wa pamoja wa kidola na ameamua kwa makusudi kutumia nafasi yake vibaya kwa maslahi binafsi

Ieleweke Rais Samia anakopa fedha kwa maslahi ya Nchi yetu na amekuwa muwazi kwenye suala hili

Ieleweke kuwa Fedha za Tozo haziwezi kugharamia miradi yote mikubwa ya kimkakati na haiwezi kuwa mbadala wa kukopa Fedha

Mheshimiwa Ndugai angeliweza kuomba kuonana na Rais Samia na kumshauri aonavyo badala ya njia aliyoitumia ya kuropoka HADHARANI!

Kwa maoni yangu kauli ya Mheshimiwa Ndugai likusudia kukwamisha juhudi za Rais wetu kukamilisha miradi mbalimbali ya Maendeleo kama ilivyoelekezwa kwenye Ilani ya CCM

Nashauri Mheshimiwa JOB NDUGAI ajiuzulu mara moja wadhifa wake wa Uspika na akishindwa kufanya hivyo mamlaka husika zimchukulie hatua za kumvua uanachama wa CCM kwani kwa sasa sio Mwenzetu tena

Tumpe ushirikiano Rais Samia

KaziIendelee
Ni kweli ajiuzulu tu

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Unaendelea kukariri nyimbo za umaskini wa afrika chanzo ni wazungu. Walishaondoka tangu mwanzo wa miaka ya sitini, mbona bado umaskini unatutesa mpaka leo?.

Switzerland kwa eneo ni ndogo sana lakini wanajitegemea. Tanzania kuna maeneo mpaka leo hayajaguswa lakini tunalia umaskini.

Tatizo ni nyie, wewe, na wenzako mnotawala hii nchi.

Lazima uwe CCM hata kama huna akili kutawala hii nchi kupata nafasi, kuongoza.

Watanzania wengi wana vipaji, hawana vyama, Wangepata nafasi za uongozi wangefanya vizuri sana.
 
Tatizo ni nyie, wewe, na wenzako mnotawala hii nchi.

Lazima uwe CCM hata kama huna akili kutawala hii nchi kupata nafasi, kuongoza.

Watanzania wengi wana vipaji, hawana vyama, Wangepata nafasi za uongozi wangefanya vizuri sana.
Kazi iendelee 2022
 
Back
Top Bottom