Naombeni msaada kuhusu huu utata ulipo kwenye dini

Naombeni msaada kuhusu huu utata ulipo kwenye dini

Habarin wakuu

Kwanza kabisa mimi ni mkatoliki pure, nimekulia na kulelewa katika misingi ya imani..

Kama ujuavyo tena sisi wakatoliki sio watu wa kusoma biblia, mara nyingi tunaskiliza tu mahubiri na kusomewa neno halafu ndo inakua imetoka hiyo.

Kuna mwaka fulani nilibahatika kukaa na watu wanaopenda sana dini hivyo ikapelekea na mimi kuanza kuichimba biblia kisawasawa na nikafanikiwa kusoma vitabu vingi ambavyo viliniacha na maswali mengi sana

1.wana wa israel wamewahi kuibiwa sanduku la agano baada ya kuchezea kichapo kikali sana ila baadaye walifanikiwa kulirudisha, utata ndo unaanzia hapo kwenye kulirudisha, wakiwa njiani wamelibeba lile sanduku ilitokea ajali ndogo ambayo ilipelekea lile sanduku litake kudondoka hivyo bwana mmoja akaona ni vema akaliwahi ili lisidondoke ila cha kushangaza alikufa pale pale kwa sababu yeye haruhusiwi kulishika sanduku hilo

Swali langu likawa ni kwa hao walioliiba walikua wamelibebaje bila kuwa dhuru au ndo ilikua ni mipando ya mungu tu?


2.yesu akiwa mlimani alitokewa na watu wawili ambao ni musa na elia hali iliyopelekea simion kumwambia yesu wajenge vibanda vitatu, tukirudi nyuma tunaambiwa roho ya elia ilikuwa ndani ya yohana mbatizaji(swali litengeneze mwenyewe)

Maswali ni mengi mengine nitayaweka kwenye comment.


Ikabidi nizame kwa weslamu au mnyaazi.

Kiukweli kile kitabu ni kigumu sana kukisoma kutokana na mfumo wake wa uandi na ukitaka ukielewe inatakiwa usome kwanza kitabu cha mithali halafu ndo uanze kusoma quran

Ukizichambua hadithi hata hizo sahih utaona kabisa kuna fix nying zimewekwa
Maswali yako ya kitoto swali la pili yohana mbatizaji ndiyo elia na alikuwa amesha katwa kichwa na kuuliwa ...hivyo elia ameishi duniani mara 2 ya kwanza akuuliwa alitwaliwa walipo kuwa na elisha na mara ya pili alikuja kama Yohana mbatizaji.
 
Hiyo story ya sanduku kuibwa ndio naisikia. Ila kwa hao waliochukua kichapo kwa kuiwahi lisidondoke mie nitaona kwamba yeye alijua kabisa hapaswi kuligusa, ila hao "walioliiba" hawakujua halipaswi kuguswa. Sasa Mungu kama anahukumu kwa haki, kwa nini ampe kichapo mtu ambae hajawahi kuambiwa usiliguse katika mazingira yeyote?

Hsyo ya Elia sijui vibanda nadhani ni maono tu, sio jambo halisi. Musa na Eliya walishakufa sku nyingi!
Mbona walihukumiwa tumieni akili tatizo lenu ni kumpangia mungu mtindo wa hukumu wafilisti walikufa maelfu kwa tauni hadi wakaliachia sanduku lirudi nchi yake na lilipo rudi wana wa Israel wakalifungua na kulikagua ndani nao myngu akawaua makumi elfu hapo ni kabla ya icho kisa cha daudi cha kuyumba kwa sanduku ...SOMENI UPYA WAFILISTI WALIULIWA HADI WAKAMSUJ7DIA MUNGU WA ILO SANDUKU NA KULIRUDISHA KWA KUMTOLEA SADAKA MUNGU WA ISRAEL
 
Hiyo story ya sanduku kuibwa ndio naisikia. Ila kwa hao waliochukua kichapo kwa kuiwahi lisidondoke mie nitaona kwamba yeye alijua kabisa hapaswi kuligusa, ila hao "walioliiba" hawakujua halipaswi kuguswa. Sasa Mungu kama anahukumu kwa haki, kwa nini ampe kichapo mtu ambae hajawahi kuambiwa usiliguse katika mazingira yeyote?

Hsyo ya Elia sijui vibanda nadhani ni maono tu, sio jambo halisi. Musa na Eliya walishakufa sku nyingi!
Elia na yohana mbatizaji ni mtu mmoja ....elia alirudishwa duniani akazaliwa tena ili kuwa mtangulizi wa Yesu .

YOHANA MBATIZAJI NDIYO ELIA
 
Labda nikufafanulie kidogo ili twende sawa

Mwanadamu anaundwa na vitu viwili vikuu
1.roho(pumzi)
2.mwili

Roho ya mwanadamu haina uwezo wa kujigawa mara mbili.

Yohana alibeba roho ya elia(maana yake roho ya elia imewahi kukaa kwenye miili miwili ya kibinadamu)

Wakati musa na elia wamekuja bado yohana alikua yupo hai
Umekosea kidogo ...yohana alikuwa amesha uliwa ...ndiyo maana baadae wanafunzi wakimuuliza yesu " mbona watu wanasema elia atakuja kabla ya yesu na weee ndiye yesu inakuwaje ...yesu akawajibu kuwa Elia alishak7ja wasimtambue wakamtenda 7ovu kama walivyo taka (yaani wakamuua maana yohana aliuliwa kwa kukatwa kichwa ) ndipo wanafunzi wake wakatambua kuwa anaongea habari za yohana mbatizaji.
 
Wale walilivyolitwaa Kuna madhara waliyapata ndio wakuamua kulirudisha likiwa limekokotwa kwa ngombe.ndani ya Israel si Kila mtu aliruhusiwa kubeba Hilo sanduku,ni makuhani tuu ndio walihusika kwenye huo mchakato,ndio maana baada ya huyo mtu kufa katika harakati za kulizuia kwa mikono daudi aliwatafuta makuhani walibebe kulingana na vile torati ilivyokuwa inaagiza
 
Mkuu hongera sana kwa kuamua kuchukua hatua ya kuanza kujisomea biblia takatifu ili kupata elimu ya Mungu kwa kina.

Katika kitabu cha Mithali 1:7 Biblia inasema kumcha Bwana ni chanzo cha Maarifa.

Naomba nianze kukujibu maswali yako mazuri kama ifuatavyo:

1. Ilikuwaje walioliiba Sanduku la Agano Hawakudhurika?

Tukio linalozungumziwa ni pale Waisraeli walipopigwa na Wafilisti (1 Samweli 4), na Sanduku la Agano likaibiwa na Wafilisti. Kwenye Biblia, imeandikwa kwamba Wafilisti walilichukua Sanduku hilo na kulipeleka kwenye mji wao, lakini haikuishia vizuri kwao.

Kwa nini Wafilisti hawakufa pale pale kama ilivyomtokea yule Mwisraeli?

Kwanza, ni kweli kwamba kuna watu waliokufa au kuadhibiwa walipoligusa Sanduku bila ruhusa, mfano mzuri ni Uza (2 Samweli 6:6-7). Alikufa papo hapo kwa sababu aliligusa Sanduku “bila ruhusa” akiwa na nia njema.

Kwa upande wa Wafilisti, hawakuwa na elimu ya sheria za Mungu wa Israeli, hawakujua Sanduku linapaswa kushikwa na Walawi tu, na kwa utaratibu maalumu. Lakini licha ya kutokufa papo hapo, waliadhibiwa sana: magonjwa, majipu, na miji yao ikapata majanga (1 Samweli 5:6-12).

Kwa hiyo, hawakudhurika kwa njia ile ile, lakini waliadhibiwa vikali, mpaka wakaamua kurudisha Sanduku la Agano kwa Waisraeli. Mungu alikuwa na lengo la kuwaonyesha ukuu wake, siyo tu kwa Waisraeli bali pia kwa Wafilisti na mataifa mengine.

Kwa nini Uza alikufa papo hapo lakini Wafilisti hawakufa?

Uza alijua sheria, alikuwa Mwisraeli. Mungu alikuwa anatoa fundisho la uzito wa kutii maagizo yake kwa watu wake. Wafilisti, hawakuwa na ufunuo huo; wao waliadhibiwa lakini hawakufa papo hapo. Ilikuwa fundisho kwa Waisraeli na pia onyo kwa mataifa.

2. Yesu, Musa, na Elia Wakitokea Mlimani na Roho ya Elia Ndani ya Yohana Mbatizaji?

Petro, Yakobo, na Yohana waliwaona Musa na Elia wakiwa na Yesu, ndipo Petro akasema, “Tujenge vibanda vitatu…” (Mathayo 17, Marko 9, Luka 9).

Swali la msingi hapa ni:

Kama Elia alikuja tena kama Yohana Mbatizaji (yaani roho yake), mbona anaonekana bado kama Elia mlimani akiwa na Yesu? Je, kuna “roho mbili” au “Elia wawili”? Au Elia ni mmoja tu, na bado anaonekana mlimani na Yesu, wakati tayari “roho yake” ilikuwa ndani ya Yohana Mbatizaji?

Yesu alisema wazi kwamba Yohana Mbatizaji ndiye “Elia atakayekuja” (Mathayo 11:14, Luka 1:17), lakini sio kwamba Yohana ni Elia aliyerudi, bali alikuja katika “roho na nguvu za Elia” yaani tabia, kazi, na utume wa Elia.

Yohana Mbatizaji mwenyewe alikanusha kwamba yeye ni Elia aliyerudi mwilini (Yohana 1:21).

Elia aliyekuja mlimani na Yesu hakuwa Yohana Mbatizaji bali ni yule Elia wa agano la kale. Hili lilionyesha kwamba Yesu ndiye anaunganisha Agano la Kale (Elia na Musa) na Agano Jipya (Yeye mwenyewe).

Kwa hiyo, si kwamba kuna roho mbili za Elia, bali ni kwamba Yohana alipewa utume wa Elia, siyo roho au nafsi ya Elia.

Wale waliotokea mlimani ni Musa (mwakilishi wa sheria) na Elia (mwakilishi wa manabii), wakiongea na Yesu kama uthibitisho kwamba Yesu ndiye utimilifu wa Sheria na Manabii.

Kwa hiyo, Wafilisti hawakudhurika sawa na Waisraeli kwa sababu hawakuwa na ufunuo wa sheria, ila walipata adhabu zao kwa namna tofauti. Yohana Mbatizaji hakuwa Elia aliyerudi, bali alikuja katika roho na nguvu za Elia yaani tabia na utume, sio roho ileile ya Elia. Elia aliyekuwa na Yesu mlimani ni yule yule wa agano la kale, akitokea kimuujiza ili kudhihirisha mamlaka ya Yesu.
Hapo umepotosha yohana ndiye eliya 100% na kipindi yesu anatokewa na Musa na Eliya yohana alikuwa amesha katwa kichwa amekufa katika mwili
 
1.wana wa israel wamewahi kuibiwa sanduku la agano baada ya kuchezea kichapo kikali sana ila baadaye walifanikiwa kulirudisha, utata ndo unaanzia hapo kwenye kulirudisha, wakiwa njiani wamelibeba lile sanduku ilitokea ajali ndogo ambayo ilipelekea lile sanduku litake kudondoka hivyo bwana mmoja akaona ni vema akaliwahi ili lisidondoke ila cha kushangaza alikufa pale pale kwa sababu yeye haruhusiwi kulishika sanduku hilo

Swali langu likawa ni kwa hao walioliiba walikua wamelibebaje bila kuwa dhuru au ndo ilikua ni mipando ya mungu tu?
Hili ni swali zuri ambalo watu wengi wamewahi kujiuliza.


Wakati Wafilisti walipochukua Sanduku la Agano (1 Samweli 4–6), walilipeleka katika nchi yao na kuliweka kwenye hekalu la mungu wao Dagon. Biblia haisemi moja kwa moja kama Wafilisti waliligusa Sanduku kama Waisraeli walivyofanya, lakini inaeleza kwamba kila mahali walipoliweka, Wafilisti walipata mapigo, majipu na hofu kuu. Mungu aliwaadhibu kwa njia nyingine badala ya kuwaua papo hapo kwa kuligusa Sanduku.


Wafilisti walipoamua kulirudisha Sanduku, waliweka juu ya gari jipya lililovutwa na ng’ombe, bila kuligusa moja kwa moja kwa mikono yao. Pia, hawakuwa chini ya maagizo yale yale ya agano kama Waisraeli, hivyo Mungu aliwashughulikia kwa namna tofauti—kupitia mapigo na hofu, siyo adhabu ile maalum aliyoweka kwa Waisraeli.


Kwa upande wa Waisraeli, Mungu alikuwa ametoa maagizo makali kwamba ni Walawi tu (hasa wa ukoo wa Kohathi) waliokuwa na ruhusa ya kubeba Sanduku, na walipaswa kulitumia mipiko maalum (Hesabu 4:15, Kutoka 25:14–15). Uza alipoligusa Sanduku ili kulizuia lisidondoke (2 Samweli 6:6-7), alikiuka amri hii takatifu, na Mungu alimwadhibu papo hapo kama onyo kwa Waisraeli kuhusu uzito wa maagizo Yake.
 
Umechanganya matukio ....sanduku kutekwa ni kisa tofauti na hicho cha sanduku kutaka kudondoka likisindikizwa na daudi baada ya daudi kupata mamlaka
Umesoma biblia?
 
Umekosea kidogo ...yohana alikuwa amesha uliwa ...ndiyo maana baadae wanafunzi wakimuuliza yesu " mbona watu wanasema elia atakuja kabla ya yesu na weee ndiye yesu inakuwaje ...yesu akawajibu kuwa Elia alishak7ja wasimtambue wakamtenda 7ovu kama walivyo taka (yaani wakamuua maana yohana aliuliwa kwa kukatwa kichwa ) ndipo wanafunzi wake wakatambua kuwa anaongea habari za yohana mbatizaji.
Hilo tukio lilitokea kabla ya yohana kikatwa kichwa
 
Hilo tukio lilitokea kabla ya yohana kikatwa kichwa
Wacha ubishi wa kipumbavu soma ...yesu mwenyewe alipokuwa anashuka mlimani anasema..
👉Yesu akajibu, “Wako sahihi kusema ni lazima Eliya aje, na ni kweli kuwa Eliya ataweka mambo yote kama yanavyopaswa kuwa. 12 Lakini ninawaambia, Eliya amekwisha kuja. Watu hawakumjua yeye ni nani, na walimtendea vibaya, wakafanya kama walivyotaka. Ndivyo itakavyokuwa hata kwa Mwana wa Adamu. Watu hao punde tu watamletea mateso Mwana wa Adamu.” 13 Ndipo wafuasi wakaelewa kuwa Yesu aliposema kuhusu Eliya, alikuwa anazungumza juu ya Yohana Mbatizaji..

Mathayo 14 yohana anakatwa kichwa ...Mathayo 17 Elia na Musa wanamtokea Yesu.

WAKRISTO AKILI ZENU NI MBOVU NDIYO MAANA MNADANGANYWA MAKANISA MAMBO MENGI SANA ...HATA MNADANGANYA KUWA YESU ALIPOKUFA ALIENDA KUZIMU NA SIKU YA 3 ALITOKA KUZIMU KWA KUFUFUKA ...ukimsikia mtu anasema hivyo jua huyo ni mpumbavu.
 
Umesoma biblia?
Ukiniona mimi naongea kuwa makini ..tukio la sanduku kutekwa lilitokea kipindi samweli bado mtoto mdogo ..na tukio la sanduku kutaka kuanguka lilitokea Samweli akiwa ni marehemu ...kumbuka kuwa daudi alipakwa mafuta na mzee samweli hapo daudi alikuwa hata ajulikani samweli kafa kabla ya daudi kuwa mfalme...tukio la sanduku kuyumba daudi alikuwa mfalme tayari ....kwa nyongeza kuna jamaa alikujibu kwa kusema wana wa Israel walijua uzito wa sanduku ndiyo maana Mungu alimuua papo hapo kwa radi ila wafilisti awakujua ...siyo sahihi ilo jibu ...jibu sahihi ni kwamba usimpangie mungu aina ya hukumu ....hata Wafilisti waliuliwa kwa sababu ya sanduku na walipo lirudisha wana wa Israel walilishika na kulifungua kuangalia ndani kama kuna vitu ...maana ndani lilikuwa na mabaki ya mana na kopo na fimbo ya musa ...walipo lifungua na kuangalia ndani nao awakuuliwa papo hapo bali waliuliwa maefu kwa kosa la kulishika na kulifungua ndani ila waliuliwa kwa ugonjwa wa tauni ...hapo tunaona wana wa Israel wakipata mapigo tofauti kwa kosa lile lile ...moja kaligusa akapigwa radi na kufa papo hapo na wengine wameligusa na kulifungua kabisa ila awakuuliwa papo hapo bali waliuliwa kwa tauni sawa na Wafilisti walivyo uliwa.
 
Wacha ubishi wa kipumbavu soma ...yesu mwenyewe alipokuwa anashuka mlimani anasema..
👉Yesu akajibu, “Wako sahihi kusema ni lazima Eliya aje, na ni kweli kuwa Eliya ataweka mambo yote kama yanavyopaswa kuwa. 12 Lakini ninawaambia, Eliya amekwisha kuja. Watu hawakumjua yeye ni nani, na walimtendea vibaya, wakafanya kama walivyotaka. Ndivyo itakavyokuwa hata kwa Mwana wa Adamu. Watu hao punde tu watamletea mateso Mwana wa Adamu.” 13 Ndipo wafuasi wakaelewa kuwa Yesu aliposema kuhusu Eliya, alikuwa anazungumza juu ya Yohana Mbatizaji..

Mathayo 14 yohana anakatwa kichwa ...Mathayo 17 Elia na Musa wanamtokea Yesu.

WAKRISTO AKILI ZENU NI MBOVU NDIYO MAANA MNADANGANYWA MAKANISA MAMBO MENGI SANA ...HATA MNADANGANYA KUWA YESU ALIPOKUFA ALIENDA KUZIMU NA SIKU YA 3 ALITOKA KUZIMU KWA KUFUFUKA ...ukimsikia mtu anasema hivyo jua huyo ni mpumbavu.
Nataman kujenga hoja ila lugha unayoitumia sio rafiki kwangu
 
Una maneno yenye kuudhi watu hivyo najiepusha usije kuniharibia siku
Mbona mimi nimefundishwa kuongea maneno mazuri yenye kupendeza watu isipokuwa wapumbavu tu 🤔🤔
 
Mbona mimi nimefundishwa kuongea maneno mazuri yenye kupendeza watu isipokuwa wapumbavu tu 🤔🤔
Ok twende kazi

Biblia kuna vitu imevisema ambavyo kiuhalisia ni vigumu kuvichukua kama vilivyo.. tukihoji tunaambiwa mambo ya roho mtakatifu, kama ni hivyo kwanini iliandikwa kwa wanadam?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom