antanarivo
JF-Expert Member
- Jan 9, 2018
- 448
- 870
Naweka wazi kuwa Mimi ni mtu niliyetumia Kila mbinu kumtafuta Mungu wa kweli natoa maelezo mafupi kutokana na maoni yangu
Nimeanza kumuamini Mungu nikiwa naanza kidato Cha kwanza , hapo nilikuwa na Kasi ya 5G ya kumtafuta Mungu huku nikiwa ni mtu wa Toba Kila saa nilikuwa nikisoma biblia na kuifundisha haswa kwa wanafunzi wenzangu kwa kuwa shule ilikuwa ya kutwa basi nilijikuta njia nzima nikihubiri na kufundisha watu kuhusu biblia.
Baadae katika pitapita na kutafuta ukweli wa ipi dini ya kweli na yupi Mungu wa kweli , nikaja kupata kitabu Fulani hivi ambacho kilikuwa hakina anwani Wala jina la dhehebu lililoandaa hiko kitabu maana Ganda la kitabu hicho na karatasi zingine za mwanzo zilikuwa zisha chanika.
Ninavyoendelea kukasoma kale ka kitabu nikaona kina majibu ya maswali mengi niliyo kuwa najiuliza na kwa huo muda nilikuwa tayari nishabatizwa kanisa la babtist ambako speed nilivyokuwa nayo ya kutafuta kweli ya Mungu iliwashangaza wengi pale kanisani maana ilifika kipindi Hadi mchungaji akiwa kwenye mahubiri nanyoosha mkono nikitaka ufafanuzi wa kile alichohubiri.
Na ilifika kipindi usiku naenda kulala kanisani pekeangu nikiwa nasali na pia Kuna siku nilipewa fee ya mtihani wa form Four nikaenda kutoa 10000 kama sadaka yaani hapa ndo siku ambayo imani yangu juu ya hili kanisa la babtist ikaanza kupungua.
Kumbe kipindi tunatoa sadaka mchungaji anaangalia nani katoa sh ngapi , Sasa baada ya ibada kuisha mchungaji kanifuata eti Mimi mwanafunzi ile hela anirudishie nitoe hata 1000 daah Mimi nikasema nimeitoa kwa moyo wote so aondoe shaka.
Sasa katika pitapita za hapa na pale nikakutana na mwinjilist wa kisabato ambaye naye alijitanipa SoMo na baadae nikaja kugundua kumbe kile kitabu nilichokipataga hapo kabla kilikuwa Cha wasabato.
Baadae nikaingia rasmi usabatoni na nikabatizwa huko nikapewa na biblia maisha yakaendelea na Kijijini kwetu pamoja na kwenye ukoo wetu Mimi peke angu ndo msabato , vita home ikawa kubwa hawataki niwe msabato lakini Mimi nikadai naitafuta kweli na kweli ipo sabato.
Baadae nikaanza kufuatilia midahalo ya kina mazinge ,mwaipopo,Dr sule na wahadhiri wengine wa kiislamu dhidi ya wakristo nikaja kugundua Kuna uhalisia upo katika Imani ya kiislamu.
Nikaenda nikaslimu na kupewa jina la Salimu, nikapewa vijuzuu na vitabu fulani na zawadi za vibarakashia, nikaanzishiwa darsa la kujua kusoma na kuswali lakini mwishowe nikabaini niliyoyabaini.
Na kufupisha stori ni kuwa Muumbaji yupo bila kujali jina lake ni nani na ww katika kuishi kwako omba nafsi ikuongoze kulingana na Muumbaji wako anavyohitaji acha papara za ipi dini ya haki au ya uongo , Mungu alituumba automatically na tunamsifu na kumwabudu automatic bila sisi kujijua (nature) hakuna kitu kinachoitwa kufundisha namna ya kumwabudu Mungu epuka matapeli.
Kama vile ndege, wanyama, wadudu wamwabuduvyo Mungu ndivyo hata sisi tunamwabudu bila ya sisi kujijua.
Ova
Kuhusu kuwa ukiomba unajibiwa hio ni kazi ya ubongo
Soma kitabu Cha THE POWER OF SUBCONSCIOUS MIND BY JOSEPH MURPHY
Nimeanza kumuamini Mungu nikiwa naanza kidato Cha kwanza , hapo nilikuwa na Kasi ya 5G ya kumtafuta Mungu huku nikiwa ni mtu wa Toba Kila saa nilikuwa nikisoma biblia na kuifundisha haswa kwa wanafunzi wenzangu kwa kuwa shule ilikuwa ya kutwa basi nilijikuta njia nzima nikihubiri na kufundisha watu kuhusu biblia.
Baadae katika pitapita na kutafuta ukweli wa ipi dini ya kweli na yupi Mungu wa kweli , nikaja kupata kitabu Fulani hivi ambacho kilikuwa hakina anwani Wala jina la dhehebu lililoandaa hiko kitabu maana Ganda la kitabu hicho na karatasi zingine za mwanzo zilikuwa zisha chanika.
Ninavyoendelea kukasoma kale ka kitabu nikaona kina majibu ya maswali mengi niliyo kuwa najiuliza na kwa huo muda nilikuwa tayari nishabatizwa kanisa la babtist ambako speed nilivyokuwa nayo ya kutafuta kweli ya Mungu iliwashangaza wengi pale kanisani maana ilifika kipindi Hadi mchungaji akiwa kwenye mahubiri nanyoosha mkono nikitaka ufafanuzi wa kile alichohubiri.
Na ilifika kipindi usiku naenda kulala kanisani pekeangu nikiwa nasali na pia Kuna siku nilipewa fee ya mtihani wa form Four nikaenda kutoa 10000 kama sadaka yaani hapa ndo siku ambayo imani yangu juu ya hili kanisa la babtist ikaanza kupungua.
Kumbe kipindi tunatoa sadaka mchungaji anaangalia nani katoa sh ngapi , Sasa baada ya ibada kuisha mchungaji kanifuata eti Mimi mwanafunzi ile hela anirudishie nitoe hata 1000 daah Mimi nikasema nimeitoa kwa moyo wote so aondoe shaka.
Sasa katika pitapita za hapa na pale nikakutana na mwinjilist wa kisabato ambaye naye alijitanipa SoMo na baadae nikaja kugundua kumbe kile kitabu nilichokipataga hapo kabla kilikuwa Cha wasabato.
Baadae nikaingia rasmi usabatoni na nikabatizwa huko nikapewa na biblia maisha yakaendelea na Kijijini kwetu pamoja na kwenye ukoo wetu Mimi peke angu ndo msabato , vita home ikawa kubwa hawataki niwe msabato lakini Mimi nikadai naitafuta kweli na kweli ipo sabato.
Baadae nikaanza kufuatilia midahalo ya kina mazinge ,mwaipopo,Dr sule na wahadhiri wengine wa kiislamu dhidi ya wakristo nikaja kugundua Kuna uhalisia upo katika Imani ya kiislamu.
Nikaenda nikaslimu na kupewa jina la Salimu, nikapewa vijuzuu na vitabu fulani na zawadi za vibarakashia, nikaanzishiwa darsa la kujua kusoma na kuswali lakini mwishowe nikabaini niliyoyabaini.
Na kufupisha stori ni kuwa Muumbaji yupo bila kujali jina lake ni nani na ww katika kuishi kwako omba nafsi ikuongoze kulingana na Muumbaji wako anavyohitaji acha papara za ipi dini ya haki au ya uongo , Mungu alituumba automatically na tunamsifu na kumwabudu automatic bila sisi kujijua (nature) hakuna kitu kinachoitwa kufundisha namna ya kumwabudu Mungu epuka matapeli.
Kama vile ndege, wanyama, wadudu wamwabuduvyo Mungu ndivyo hata sisi tunamwabudu bila ya sisi kujijua.
Ova
Kuhusu kuwa ukiomba unajibiwa hio ni kazi ya ubongo
Soma kitabu Cha THE POWER OF SUBCONSCIOUS MIND BY JOSEPH MURPHY