Naomba kujua kosa langu Wana jamvi

Naomba kujua kosa langu Wana jamvi

Ana tatizo la afya ya akili,au ameathirika kisaikologia, msaidie akapewe ushauri nasaha au tiba ya afya ya akili, asipokupa ushirikiano WACHANA NAE kabisa kabla hayajakukuta makubwa zaidi, mtiririko Wa maelezo yako unabainisha uwepo Wa psychological disorder.

Huu ni ushauri mkubwa sana kwenye hii thread , na mimi niongezee kuwa wote wanahitaji kupata matibabu ya akili.
Kwani wanaume huwa tumeumbwa na uvumilivu mkubwa sana sasa kwa huyo mwenzetu naona tofauti.
They have to see psychiatric doctor kabla hawajaruin maisha yao ya mahusiano.
 
Achana naye kabisa huyo atakusumbua sana kwenye maisha, utayaona machungu nakwambia. Yaani hapo mnakutana kwa mara ya kwanza hata hakufaham vizuri anabehave hivyo? Tuulize tulio kwenye mahusiano na wanawake wa aina hiyo. Alikusaidia sana kumwambia umshushe pale, si ajabu alikuwa anaenda kukutana na jamaa mwingine kwa hiyo wewe ulikuwa unamwekea kiwingu. Kwanza wewe ni mtu ambaye ni muwazi sana halafu yeye msiri kwa hiyo hamtawezana. Kimbia sana huyo ni ibilisi kwa sababu ana majaribu kuliko hata ibilisi mwenyewe. Achana nae kabisa.
 
miss chagga unamsingizia. Miss chagga hana swaga za kimakonde kama hivyo, I know her. She is very kind, jovial and charming, wala hutojuta kumfahamu ukishameet nae. Miss chagga ni shori mmoja ivi mstaarabu na anapenda friends & jokes.

Huyo demu wa mleta Uzi, ni just mgema minazi tu huko Chamazi mbagala. Alafu eti ni mwalimu, uwiiiii... majangest!

Ha ha ha ha kaveli nahis umekunywa kabla hujala maana unavyofyatua haya maneno, duh
 
Last edited by a moderator:
yani dada Nuru acha tu. kuna mademu wengine ni mambulula sana. nimesoma huo mkasa mpaka nikatamani ningekuwa mimi, ninge-return back nyodo ambazo ni 'advanced' hadi angejiona choo cha shimo. Huyo jamaa anaonekana ni innocent sana aisee. Mleta uzi bora angekutana na 'Panya Road' wa Kova, na sio huyo demu mwenye expiry date tayari.

Wewe ni noma,
 
Nashindwa kuelewa watu wanautoa wapi ujasiri.,, unaanza tu kukutana na mtu wa mtandaoni. Wengine majambaz/wabakaji wapo humu...

Ladies take care..

Nakuunga mkono kabisa...

Ndiyo maana huwa sielewi na sidhani kama itatokea niwaelewe wanaosema kuwa kazi kubwa ya PM ni kutongozana... Really??

Ila hata pale inapotokea, basi wahusika wachukue tahadhari kwa kujua kuwa kuna tofauti ya mtu halisi unayekutana naye mtaani, ukaongea naye na ku-enjoy body language, na mtu wa kwenye key boards ambaye unakula ugali kwa samaki (avatar)!..

cc: Mbu ...swahiba njoo haraka utoe msaada!
 
Mkuu pia pole sana , mtoa mada kwa kusoma seminari na kukuzwa maisha ya kiseminari, lengo kuu ulifanyiwa hivyo kulelewa maisha ya kitakatifu uje kuwa mtu bora kwenye jamii, but nilichokigundua kwako ww ni mtu mzuri wa vitendo na maneno ,ulivyo wewe unatakiwa utafute msichana aliyelelewa na kukuzwa kama ww ndio mtaendana let say ww umesoma seminari o leval na a level , na wakati upo primary ulikua unatumikia seminary , halafu huyo mwlm kasoma shule ya msingi mbagala, sekondari kata huko huko mbagala mkuu ww jpli unaenda church mwenzio kalala baada ya kukesha kwenye mnanda au kigodoro mkuu, mwenzio kaanza migegedano tangu darasa la pili ww , umeanza ulipokuwa chuo tena mwaka wa mwisho,!!ANGALIZO Mkuu mwanaume unatakiwe uwe na marafiki waliokulia kila maisha mfano waliokulia kishua na wauswazi, mm binafsi nashukuru kukulia ushuani na uswahilini so unakutana na changamoto hizo ukiwa bado 15's so ukubwani unakuwa na uwezo wakutambua kicheche na dem mkweli,
 
Ana tatizo la afya ya akili,au ameathirika kisaikologia, msaidie akapewe ushauri nasaha au tiba ya afya ya akili, asipokupa ushirikiano WACHANA NAE kabisa kabla hayajakukuta makubwa zaidi, mtiririko Wa maelezo yako unabainisha uwepo Wa psychological disorder.

Huyu jamaa ana lack of education shule ni darasa la 7
 
Tatizo umeshamuonyesha udhaifu wako,ila sisi wadada wakati mwengine tuna matatizo sasa hapo akikosa mume atasema ana gundu,wengine tunanyenyekea lakini wapii, Mtoa mada mimi sijaona kosa lako hapo hebu jaribu kupotezea uone kama hatokutafuta.

Umeona eee,wengine tunajishushaa wee lkn wapii?tumepata vichwa ngumu!!kweli upele humpata asiye na kucha!!
 
Back
Top Bottom