Naomba kujua kosa langu Wana jamvi

Naomba kujua kosa langu Wana jamvi

Superbrand

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2013
Posts
509
Reaction score
158
Habari wana jamvi

Naomba ushauri wa kutambua Kosa langu katika hili labda naweza jifunza na kuomba msamaha

Nilipendezewa kiukweli sana na binti mmoja mwana jamvi humu nikaanza kumtokea lakini alinieleza kuwa ana yupo likizo ktk mahusiano ya kimapenzi kwa sasa.

Niliendelea kumshawishi ili aweze kumaliza hiyo likizo na kumuahidi sita mpa majonzi ya kumfanya achukue likizo tena.

Hakukubali direct ila tuliendelea kuchati kwa muda mrefu tu na tulikuwa tukiwasiliana hadi muda wa kulala tunaagana ndo kila mtu ana lala,nilipenda kumuandikia sms nikiishia na neno Mpz lakini alisema mimi sio mpz wako bado.Mimi nilimwambia sawa japo halidhuru chochote basi nitakuwa nikiandika sms siliandiki na badala yake nikifika sehemu ya kuandika nitaja kimoyoni tu halafu naendelea.

Tuliwasiliana kwa muda lakini hakuwa Daresalaam alikuwa ameenda Mkoani bt siku moja alianza kucharuka na kusema mbona siku hizi nimebadilika na simuiti mpz tena hata simu sipigi.

Nilijitetea kuwa nilikupigia mbona Mara moja akasema mwanzo ulikuwa unapiga Mara tatu sasa umepunguza Mimi nikaona isiwe mada nikaomba radhi akakubali tukaendelea na mawasiliano.

Siku moja aliniambia ujue Mimi nina mtoto nikamuuliza baba yake yupo wapi akasema amenitelekeza nikamwambia pole but maisha yanawezekana pia bila huyo baba yake.akasema ni kweli hadi sasa mtoto ana miaka 3 ana mlea mwenyewe nikasema hongera kwa uvumilivu na kuamua.

Tuliendelea na mazungumzo ila siku moja tarehe kama 30/12/2014 tukiwa tunachati ghafla niliona kaniblock watsapp nikamwandikia sms kawaida nikamuuliza kulikoni hakujibu!!nilikuja kumpigia saa tano usiku akawa ana kata na baadae alituma sms na kusema hawezi pokea Simu amelala na mtoto ataamka nikakubali na kesho yake akaendelea kuwa kimya.

Aliniambia ana taraji kurudi tarehe 1/1/2015 kwa kuwa ni mwalimu wa shule moja hivi lakini kwa kuwa hakuwa anawasiliana nami tena niliamua kupotezea tu,Leo majira ya saa nne asb nikaona sms yake on my way!!nikamwambia umeanza safari ya kuja akasema ndio basi nikamwambia karibu sikutaka kukumbusha yale .


Tuliendelea kuwasiliana hadi alipofika nikaenda kumpokea baadae nilimuambia vipi ulisema unakuja na mwanao mbona hujaja nae akasema hana dada wa kazi ameamua kumuacha na mama yake baadae aliniuliza una mtoto nikamwambia ndio akasema hawezi olewa na mwanaume mwenye mtoto nilimuambia kwa nini aksema huwa mna kumbushia nikasema Jf Leo kulikuwa na Uzi wa hii mada na ulikuwa unachangia kuonesha inawezekana Leo vipi akasema hayo ni mamabo ya mtandaoni siwezi kuzungumzia

Tukaendelea na safari nikawa nimepigiwa Simu na dada yangu mmoja nikaongea nae na baadae niliongea na Mama wa mwanangu ambaye alinipigia Simu akaanza kuniuliza mwanao ana itwa nani? Nikamwambia akasema na huyo mama yake nikasema ndio akasema mbona mna active communication nikamwambia ni active communication na sio active mapenzi.

Akaanza kuwa mkali na kusema nimshushe njiani kwani hapendi kudanganywa nikamwambia hapo uongo upo wapi?akasema unawezaje kuwa na mpz na ukaongea na ex Wako nikamwambia inawezekana akasema Mimi nilikudanga sina mtoto nilitaka kukupima!!!!???

Najiuliza

1. lengo la kusema ana mtoto ndo kumpima mwanaume?
2. Mbona aliniomba nimtafutie dada wa kazi kwa ajili ya mwanae au alikuwa ana nipima back
3.Mbona nilipopiga simu usiku alisema amelala na mtoto au ndo alikuwa ana nipima?

Najiuliza maswali mengi zaidi ya hayo ?na baadae aliomba nimushushe njiani ila nilimtoa ubungo hadi Mbagala maji matitu kwa umbali huo na alikuwa naelekea chamazi akadai ana boreka na uongo wangu na pretending na ndo maana hawapendi wanaume akaomba kushuka na ikabidi nimshushe japo nilimwambia Leo Luna panya road umewaona nakuonea huruma just nikufikishe karibu na kwako alikataa na nikabidi nishushe na sijui amefika au LA


Nawasilisha naweza mtaja akiridhia na sheria za Jf kama zina ruhusu kwani nimeumia na kuwaza sana which kind of woman is this

Naomba radhi kwa kuwachosha japo lengo langu muelewe kwa kiasi pa kuanzia kunishauri


Regards,
Superbrand
 
Hahahaaha..kaazi kweli kweli.

Mtumie PM mwambie na wewe ulivyoanza nae maongezi ulikuwa unampima, vipimo vimekamilika huna uhitaji nae tena.

Akishangia hoja ya kutopendwa mwanamke analalamika sana na kuonekana wanawake ndo huwa wanaonewa sana ktk mahusiano
 
Hiyo ni defensive mechanism brother,hapo kuna sababu zimejificha nyuma ya pazia na wala tatizo siyo mtoto wako au mawasiliano na mama watoto wako. Nakushauri endelea kukaa kimya huu ujumbe umemfikia
 
mkuu, hakuna mwanamke hapo. piga chini gume-gume hilo lisilojitambua. na kama alikuwa anatikisa kiberiti ili aone umezimikaje kwake, basi maliza kabisa na funga ukurasa! Umeliheshimu na kuchoma mafuta yako all the way from Ubungo to Mbagala, limeona lishafika mbagala alafu ndo linajifanya kususa na kushuka??!! si ajabu halijasema ata 'AHSANTE' kwa lift.

Demu anakuwa mkali/mkorofi kiasi hicho just at the FIRST DATE??!! puuuuuuuuh. huyo ndo maana kaishia kuzalishwa na kutelekezwa tu. Mwanaume gani anaejitambua aoe jike lenye akili-mibange kama hilo?

mademu wenye kupretend 'mapozi-mbuzi' kama huyo ndo huwa na-DELETE fastaaaa kwenye memory yangu, tena na-format kabisa.

Mkuu, pole kwa mkosi huo ambao naamini umekuharibia jioni yako ya leo. Plus ungekutana na 'Panya Road' wa Kova, ndo kabisaaa ungezimia na roho yako. Endelea kutafuta mke, wewe ni 'SUPER BRAND' bhana, Mungu akujaalie upate mke ambae ni super-branded as well.

-Kaveli-
 
Happy new year venine....

Mapenzi huwa yako hivyo aisee... Ila kuna wengine wanazidisha usanii!!

Happy new year to you too babu DC. Hayo mapenzi yanaonekana kama bado mapya hivi. sasa badala ya kufurahiana, wao wanapigana mikwara. Hebu waambie wafurahiane kwanza, mambo mengine yatajipanga taratibu
 
mmmh pole ndo inavyokuwaga mwanaume mpole lazima akutane na mwanamke mwenye visa na mikasa and viceversa

Kwa nini usimshauri Miss neddy mbona unafahamu lakini visa vya nini
Wanasema "if you dont love him/her be a way from him/her"ni kwani nini hasa visa??
 
Sijaona tatizo hapo maana alisha kwambia alikuwa ana kupima!
Hii story ungeweza kuileza bila kusema muhusika ni mwana Jf!

Nilikuwa na lengo jema kusema Mwana Jf kwanza nikiweka kumbukumbu sawa kwa kuwa huko sijui kama kafika salama? Kwa purukushani za jana kwani inatokeaga mtu akipata matatizo makubwa wana Usalama wa raia huwa wanahusisha pia mawasiliano ya simu yake ya mwisho na ya mara kwa mara


Pili wengine wanaweza kupata somo kwa kuamini positive moja kwa moja kuwa Mtazamo wa mtu humu Jf may be ndo mtazamo wa maisha kama mimi.

Kusema kunipima kwake ameongea kwa kupanic na hasira sana kiasi kuwa si rahisi kuamini ni uhalisia aliokisudia?

Nahisi kama una mpima mtu kwa hayo aliodai hakuna sababu ya kupanic,kupata hasira na kuzira pia ikiwa ndo moja ya matokeo ktk upamaji wake.

Kwani mwl huwezi ukawa unatengeneza na ku mark mitihani kwa Jazba kwa wanafunzi kifel wakati ndo matokeo wa walichokielewa.
Asante.
 
Mkuu umeangukiwa na jumba bovu...

Kama miguu yako inaweza kuchanganya vizuri basi kaza mwendo ukimbie haraka mno...

Humu ndani kuna kila aina ya watu wengine wapo kibiashara, wengine ni vizabizabina wanatafuta tu habari, wengine ni mboga ya jana...nk
 
mkuu, hakuna mwanamke hapo. piga chini gume-gume hilo lisilojitambua. na kama alikuwa anatikisa kiberiti ili aone umezimikaje kwake, basi maliza kabisa na funga ukurasa! Umeliheshimu na kuchoma mafuta yako all the way from Ubungo to Mbagala, limeona lishafika mbagala alafu ndo linajifanya kususa na kushuka??!! si ajabu halijasema ata 'AHSANTE' kwa lift.

Demu anakuwa mkali/mkorofi kiasi hicho just at the FIRST DATE??!! puuuuuuuuh. huyo ndo maana kaishia kuzalishwa na kutelekezwa tu. Mwanaume gani anaejitambua aoe jike lenye akili-mibange kama hilo?

mademu wenye kupretend 'mapozi-mbuzi' kama huyo ndo huwa na-DELETE fastaaaa kwenye memory yangu, tena na-format kabisa.

Mkuu, pole kwa mkosi huo ambao naamini umekuharibia jioni yako ya leo. Plus ungekutana na 'Panya Road' wa Kova, ndo kabisaaa ungezimia na roho yako. Endelea kutafuta mke, wewe ni 'SUPER BRAND' bhana, Mungu akujaalie upate mke ambae ni super-branded as well.

-Kaveli-

Angesema asante Mkuu hata kwa lift ningefarika tu hata kwa hilo ningejua huyu mtu bado kuna walau chembe ya vitu anavitambua kwa uthamani wake
 
Huwezi Jua umuhimu wa kitu mpaka ukiwa haunacho tena.

Amesha kuona zoba huyo,Hata kama ndio she is playing hard to get that is too much.

Dhumuni la kupenda ni kupendwa na kupata amani moyoni,Sasa kama hakuna dalili ya kuvipata hivyo wewe nyoosha kisigino tu.
 
Back
Top Bottom