TheForgotten Genious
JF-Expert Member
- Jan 18, 2014
- 2,787
- 4,262
Mwaka 2023 kama sio 2024 niliweka uzi hapa unaohusu upweke na kujitenga sana kwa upande wange,basi kuna dada mmoja akanifuata pm,tukawa tunachati baadae tukawa tunawasilia kwa whatssap,yeye ni mwalimu ndio alikuwa ameripoti huko RUVUMA,ni mchaga na ana dada yake hapa dar,anawatoto 2 wote wa baba mmoja ila waliachana.
Basi likizo ya likizo ya mwezi wa 6 alikuja kuwaangalia watotot wake hapa Dar alifikia mbande ndiko aliko dada yake,mimi nashinda Chanika kijiweni kwangu,mbande na chanika ni rahisi kufika,akanitaka nimfuate,sasa mimi mtu kumfuata kwa mara ya kwanza ni mwiko nikamwambia aje mpaka chanika kweli akaja.
Alipofika tu nakumuona code ziligoma kabisa kuhusu afya yake haendani kabisa na ni mtu wa kukasirika haraka sana hata kwa mambo yasiyoeleweka,na mimi nilikuwa na upwiru kwelikweli almost a year,kadhalika na yeye(kwa madai yake).
Baada ya maongezi ya muda nikamwambia tupime HIV,akawa mzito,nikamuuliza baba wa wanao mliachana muda gani na umewahi kuwa na mahusiano baada ya hapo? akasema miaka 2(na ndio umri wa mtoto mdogo) na hakuwahi kuwa na mahusiano.
Akasema nimpime lakini nisimpe majibu nikamwambia kwa vyovyote iwavyo mimi nitajua namna yakukuhandle kwakuwa ni mtu wa afya, na hapa natoa huduma za afya.
Nikachukua kitendanishi nikamuandaa nakuchukua damu,nilipoweka buffer nikaficha asione,ilipo dissolve tu kikasoma positive,sikushituka sababu code zilinigoma tangia namuona nikamkabili kisaikolojia,nikamwambia hapa ni ofisini tuonane jmosi,basi akaondoka.
Alipofika kwake nikaanza kumuhoji ,katika kumuhoji akaonekana kama ni mtu anayejijua kwa muda mrefu ila alifikiri mimi nimwepesi angeweza niingiza mkenge,nilichojiuliza kama ni miaka 2 na hakuwa na mahusiano maana yake alipata huo ukimwi kwa mumewe au wakati wa kujifungua,maana nilimuhoji kuhusu kunyonya mtoto akasema aliacha akiwa na miezi 6 sababu yeye alipata kazi mbali na alimuachia mtoto mama yake,je kama alipata wakati wa kujifungua ama kwa mumewe aliwezaje kukaa miaka 2 bila kujigundua kama ameathirika? nikajua kalikuwa kananichota.
Sikutaka kumnyanyapaa,mwenyewe naona akanilima block fasta 😀
kuweni makini.
Basi likizo ya likizo ya mwezi wa 6 alikuja kuwaangalia watotot wake hapa Dar alifikia mbande ndiko aliko dada yake,mimi nashinda Chanika kijiweni kwangu,mbande na chanika ni rahisi kufika,akanitaka nimfuate,sasa mimi mtu kumfuata kwa mara ya kwanza ni mwiko nikamwambia aje mpaka chanika kweli akaja.
Alipofika tu nakumuona code ziligoma kabisa kuhusu afya yake haendani kabisa na ni mtu wa kukasirika haraka sana hata kwa mambo yasiyoeleweka,na mimi nilikuwa na upwiru kwelikweli almost a year,kadhalika na yeye(kwa madai yake).
Baada ya maongezi ya muda nikamwambia tupime HIV,akawa mzito,nikamuuliza baba wa wanao mliachana muda gani na umewahi kuwa na mahusiano baada ya hapo? akasema miaka 2(na ndio umri wa mtoto mdogo) na hakuwahi kuwa na mahusiano.
Akasema nimpime lakini nisimpe majibu nikamwambia kwa vyovyote iwavyo mimi nitajua namna yakukuhandle kwakuwa ni mtu wa afya, na hapa natoa huduma za afya.
Nikachukua kitendanishi nikamuandaa nakuchukua damu,nilipoweka buffer nikaficha asione,ilipo dissolve tu kikasoma positive,sikushituka sababu code zilinigoma tangia namuona nikamkabili kisaikolojia,nikamwambia hapa ni ofisini tuonane jmosi,basi akaondoka.
Alipofika kwake nikaanza kumuhoji ,katika kumuhoji akaonekana kama ni mtu anayejijua kwa muda mrefu ila alifikiri mimi nimwepesi angeweza niingiza mkenge,nilichojiuliza kama ni miaka 2 na hakuwa na mahusiano maana yake alipata huo ukimwi kwa mumewe au wakati wa kujifungua,maana nilimuhoji kuhusu kunyonya mtoto akasema aliacha akiwa na miezi 6 sababu yeye alipata kazi mbali na alimuachia mtoto mama yake,je kama alipata wakati wa kujifungua ama kwa mumewe aliwezaje kukaa miaka 2 bila kujigundua kama ameathirika? nikajua kalikuwa kananichota.
Sikutaka kumnyanyapaa,mwenyewe naona akanilima block fasta 😀
kuweni makini.