Nani ndo GOAT wa rhumba?

Nani ndo GOAT wa rhumba?

Kwa mara ya kwanza tangu nikufahamu umeandika uzi kabambe.

Hata hivyo si rahisi kumtaja mtu mmoja kwenye swali lako, hii ni kwa sababu Rhumba ina vipengere kadhaa, hakuna msanii mmoja anaweza kufit mote.

Yuko pia Nyoka Longo, lakini kwenye kizazi kipya kuna Ferre Gola, kiukweli hili ni eneo pana mno!
we jamaa upo? usije ukawa umekata moto
 
Goat ni Fally Ipupa, yéyé ni mwendo wa hit tuu, kijana anajua sana tokoos
 
Goat ni Fally Ipupa, yéyé ni mwendo wa hit tuu, kijana anajua sana tokoos
Kuna goma lake mayday na mh so poa

Ukimskilza Fall ipupa uje uwasikilize na Hawa wasenge wababa pua bingofleva unajua hatuna vipaj
 
Kumbe kuna rhumba ya kimarekani na ya kiafrika
secretarybird
Nawakubali wote (Franco, papa Wemba, Tabu Let Rochereau, na pepe kale) lakini ngoja leo nimchague Tabu Let Rochereau muzee ya masauti muzuri.

Tabu Let nakumbuka miaka hiyo alifunga harusi angani kwenye ndege na msanii mwenzake M'bilia Bel bibi yake Monetary doctor kwa shamra shamra ya kufa mtu na hatimaye kuzaa binti mtamu Melody Tabu.

Baada ya kuachana, na Mbilia Bel kuolewa na mtoto wa Rais Gabon kwa kipindi kile bwana Tabu ley alitetereka sana kiafya kwa wivu wa kinyegere hali iliyosababisha kifo chake.

Kwa hakika upendo uliochanganyikana na wivu kama wa nyegere ni UKUMANYOKO!

Dr am 4 real PhD DR Mambo Jambo min -me
 
Franko Alikuwa kiongozi Mzuri lakini siyo mtunzi mzufri vile. Anapitwa mbali sana na Tabu Ley kwenye utunzi. TP OK Jazz ilitawala angala la muziki huo kwa vile Franko (kama Injinia Hersi) alikuwa anatengeza timu imara sana ya watunzi. Kwa mfano Simaro Massiya Lutumba, na Josky Kyambukuta waliibeba sana bendi ya TP Ok Jazz kwa tungo zao. Madilu System naye alileta mchango mkubwa sana. Nyimbo kumi bora za TP OK Jazzi hazikutungwa na Franck, bali zilitungwa na hao waimbaji niliowataja hapo.
 
Franko Alikuwa kiongozi Mzuri lakini siyo mtunzi mzufri vile. Anapitwa mbali sana na Tabu Ley kwenye utunzi. TP OK Jazz ilitawala angala la muziki huo kwa vile Franko (kama Injinia Hersi) alikuwa anatengeza timu imara sana ya watunzi. Kwa mfano Simaro Massiya Lutumba, na Josky Kyambukuta waliibeba sana bendi ya TP Ok Jazz kwa tungo zao. Madilu System naye alileta mchango mkubwa sana. Nyimbo kumi bora za TP OK Jazzi hazikutungwa na Franck, bali zilitungwa na hao waimbaji niliowataja hapo.
huo ni uongo, Franco alikua mtunzi na mwimbaji mzuri infact alikua exceptional mpaka kwenye guitaa! Pia alichaguliwa kua kiongozi mkubwa wa mziki congo, kwa kutumia mfano wa tanzania alichaguliwa kama kiongozi mkuu wa basata, pia anajulikana kwa solo zake nyingi tu mfano marioo, mamuu, zingine ameshirikiana na wasanii wengine hio ni nje ya bendi
 
huo ni uongo, Franco alikua mtunzi na mwimbaji mzuri infact alikua exceptional mpaka kwenye guitaa! Pia alichaguliwa kua kiongozi mkubwa wa mziki congo, kwa kutumia mfano wa tanzania alichaguliwa kama kiongozi mkuu wa basata, pia anajulikana kwa solo zake nyingi tu mfano marioo, mamuu, zingine ameshirikiana na wasanii wengine hio ni nje ya bendi
Pamoja na lugha yako mbovu kwenye mjadala umeshindwa kutoa ushahidi wa kuonyesha kuwa Franco alikuwa mtu za mzuri sana; ni kweli alikuwa mtu za na mingapi solo laki tungo zinazokumbukwa sana TP OK jazz siyo tundu zake. Anzia mbali sana miaka ya sitini. Nyinbo zilizokuwa zilikuwa ni za watu kama Youlou, Sam Mangwana, Kyamangwa Mateta, na hao wengine Nilikutana mwanzoni. Mwaka 1971 walipoondoka na kwema kuanzisha bendi zao wenyewe, Franco alipumulia mashine kabla Simaro Massiya, Josky Kyambukuta, Mayaula Mayoni na Madilu System hawajarudisha Uhai kwenye bendi. Ni kipindi hicho alipoanza kutumia wainbaji wa kike, Nana Akumu, Jolie detta Yondo sister na wengineo
 
Pamoja na lugha yako mbovu kwenye mjadala umeshindwa kutoa ushahidi wa kuonyesha kuwa Franco alikuwa mtu za mzuri sana; ni kweli alikuwa mtu za na mingapi solo laki tungo zinazokumbukwa sana TP OK jazz siyo tundu zake. Anzia mbali sana miaka ya sitini. Nyinbo zilizokuwa zilikuwa ni za watu kama Youlou, Sam Mangwana, Kyamangwa Mateta, na hao wengine Nilikutana mwanzoni. Mwaka 1971 walipoondoka na kwema kuanzisha bendi zao wenyewe, Franco alipumulia mashine kabla Simaro Massiya, Josky Kyambukuta, Mayaula Mayoni na Madilu System hawajarudisha Uhai kwenye bendi
🤣 🤣 unajua rhumba aliianzisha nan?
 
Swali liloo hapa ni Nani alitunga rumba Zuri. Zamani sana walikuwapo wanamuziki wengi sana wakipiga kwenye Kumbi za baa kwa mfano Dr Nico Kassanda kabla hata Franco hajapasua Ganda la yai lake
 
Swali kuliko hapa na Nani alitungs rumba Zuri. Zamani sana walikuwapo wanamuziki wengi sanawakipiga kwenye Kumbe za mbwa kwa mfano Dr Nico Kassanda kabla hat Franco hajapasua Ganda la yai lake
mziki wa rhumba ulianzishwa na kundi la OK JAZZ, wao ndo walimix vionjo flan vya cuba ukatoka mziki wa rhumba haukuepo kabla
 
mziki wa rhumba ulianzishwa na kundi la OK JAZZ, wao ndo walimix vionjo flan vya cuba ukatoka mziki wa rhumba haukuepo kabla
Samahani; hiyo post uliyokwoti niliiandika kwenye iphone, na hao jamaa wa iphone huwa wana tabia ya kubadilisha maneno ninayoandika kwa kiswahili. Nimeshairekebisha.

Tukirudi kwenye mada, ukweli ni kuwa hakuna mtu anayejidai kuwa ni mwazilishi wa Mziki wa Rhumba huko Congo kwa sababu kadhaa, Muziki wa rhumba uliletwa eneo letu hili na Salim Abdallah Yazidu aliyekuwa na Bendi ya Morogoro Jazz baadaye akaanzisha ya kwake iliyoitwa Cuban Marimba. Hapo alivuta muziki wa Cuba na kuuweka katika marimba za kiafrika, na hiyo ilikuwa ni mwaka 1948. Muziki wa rhumba ya Salimu Abdallah ulimvutia sana Kabasele naye akaanzisha bendi yake ya African Jazz mwaka 1953, yaani miaka mitano baada ya Salim Abdallah kutangulia. Franco alianza muziki kama muajiliwa wa bendi ndogo ilyokuwa ikishandana na ile ya Kabasele; bendi hiyo ilikuwa inajulikana kama Bandidu. Mwaka 1956 ndipo alipoanzisha bendi iliyokuja kujulikana ka TP OK Jazz. Huyu Kabasele nadhani ndiye babawa Pepe Kalle, ila baadaye walishirikiana na Francko kwenye Muziki wao.

Kwa mtililiko huo, utagundua kuwa Franco alikuwa ni late comer sana kwenye muziki wa Rhumba. Isingekuwa kifo kumchukua Salimu Abdallah, labda Franco asingekuwa jina kubwa sana kama lilivyo leo.


View: https://www.youtube.com/watch?v=xAEDihQDV-I&list=RDxAEDihQDV-I&start_radio=1
 
Back
Top Bottom