Samahani; hiyo post uliyokwoti niliiandika kwenye iphone, na hao jamaa wa iphone huwa wana tabia ya kubadilisha maneno ninayoandika kwa kiswahili. Nimeshairekebisha.
Tukirudi kwenye mada, ukweli ni kuwa hakuna mtu anayejidai kuwa ni mwazilishi wa Mziki wa Rhumba huko Congo kwa sababu kadhaa, Muziki wa rhumba uliletwa eneo letu hili na Salim Abdallah Yazidu aliyekuwa na Bendi ya Morogoro Jazz baadaye akaanzisha ya kwake iliyoitwa Cuban Marimba. Hapo alivuta muziki wa Cuba na kuuweka katika marimba za kiafrika, na hiyo ilikuwa ni mwaka 1948. Muziki wa rhumba ya Salimu Abdallah ulimvutia sana Kabasele naye akaanzisha bendi yake ya African Jazz mwaka 1953, yaani miaka mitano baada ya Salim Abdallah kutangulia. Franco alianza muziki kama muajiliwa wa bendi ndogo ilyokuwa ikishandana na ile ya Kabasele; bendi hiyo ilikuwa inajulikana kama Bandidu. Mwaka 1956 ndipo alipoanzisha bendi iliyokuja kujulikana ka TP OK Jazz. Huyu Kabasele nadhani ndiye babawa Pepe Kalle, ila baadaye walishirikiana na Francko kwenye Muziki wao.
Kwa mtililiko huo, utagundua kuwa Franco alikuwa ni late comer sana kwenye muziki wa Rhumba. Isingekuwa kifo kumchukua Salimu Abdallah, labda Franco asingekuwa jina kubwa sana kama lilivyo leo.
View: https://www.youtube.com/watch?v=xAEDihQDV-I&list=RDxAEDihQDV-I&start_radio=1