Nani ndo GOAT wa rhumba?

Nani ndo GOAT wa rhumba?

Mpaka umeona Mtu kwa Kuheshimika kwa Kazi yake kaitwa Mitre (Mwalimu) jua kuwa Luambo Luanzo Franco Makiadi a.k.a Mitre (Mwalimu) hana Mpinzani na kwa Taarifa yako tu ni kwamba Wasanii wengine wote wamejifunza na kupita njia zake. Ulichokosea ni kutomtaja Mtu ambaye kwa Sisi wenye Muziki wetu wa akina Bandeko Nangai (bana Congo DR) tunajua ndiyo alipikwa vyema na Marehemu Franco katika Miziki ya Rhumba na ndiyo alikuwa Mfalme baada ya Franco Kufariki ambaye ni Marehemu Madilu Multi System. Hakuna Rhumba ya Madilu System huwezi kutoicheza na huyu ndiyo alikuwa Mrithi sahihi wa Marehemu Franco na ndiyo maana alipendwa nae sana kama siyo mno tu.

Na mwisho kwa Kukusaidia tu ni kwamba kumuweka hapa katika List yako Marehemu Pepe Kalle umekosea sana kwani huyu ndiyo Baba wa Muziki aina ya Sebene na kwa msiojua Pepe Kalle ndiyo Mwanzilishi wa huu Mtindo wa Kughani (Watoto wa Mjini mnauita Kurapu) ila kwa kule Congo DR wanaita Atalaku katika Miziki na ndiyo pia alimfundisha Rapa / Mghani (Atalaku) wa Kwanza Bileku Mpasi (Jina lake halisi ni Djuna Mombafu) aliyefanya vyema katika Bendi yake ya Empire Bakuba hadi baadae kuja Kuigwa na Wengineo kama akina Alain Kounkou, Roberto Wunda Enkokota wa Wenge BCBG na wengineo wengi hadi akina GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE (Jina halisi ni Pitshou Lisimo) wa Wenge BCBG yake JB Mpiana ambaye kwa sasa hana Mpinzani katika Medani nzima ya Kughani / Kurapu (Atalaku) huko Congo DR japo kwa mbali anatishiwa na Rapa Kijana Hatari sana wa Extra Musica ya Roga Roga (zamani Extra Musica Zangul Zangul) aitwa Zaparo Degere.
sasa hujachagua GOAT
 
Hii kamba unamaanisha nimesema uongo?

Labda kukusaidia tu, tafuta kitabu kinachoutwa Rumba On the River kimeandikwa na Gary Stewart. Utapata full story ya muziki wa Congo zote mbili kuanzia karen ya 18 mpaka sasa.

Unatakiwa kuwajua watu kama Verckys, Joseph Kabesele a.k.a The Grand Kalle, Dr Nico, Trio Madjes, Bavon Marie Marie, Abeti Masikini.
 
Hii kamba unamaanisha nimesema uongo?

Labda kukusaidia tu, tafuta kitabu kinachoutwa Rumba On the River kimeandikwa na Gary Stewart. Utapata full story ya muziki wa Congo zote mbili kuanzia karen ya 18 mpaka sasa.

Unatakiwa kuwajua watu kama Verckys, Joseph Kabesele a.k.a The Grand Kalle, Dr Nico, Trio Madjes, Bavon Marie Marie, Abeti Masikini.
umemaliza kwa uongo kwamba yoyote anaetaka kwenda nje inabidi apewe ruhusa ya franco
 
Nimekasirika sana kutoona jina la Madilu System hapo 😠
uyo alikua mwanafunzi wa huyo wa kwanza apo juu, alikua anahudumu kwenye bendi yake ilikua inaitwa OK JAZZ ila baadae ilikuja kubadiishwa jina ikawa inaitwa TP OK JAZZ, baada ya franco kufa familia walikua wanapewa 30% ya mapato ya bendi mpaka pale walipoingiza tamaa bendi ikavunjika yote ndo wakatoka sasa wakina madilu kwenda kujitegemea, pia kuna nyimbo nyngi alikua anaimba kama bak vocal ziko youtube unaweza kuzicheki
 
umemaliza kwa uongo kwamba yoyote anaetaka kwenda nje inabidi apewe ruhusa ya franco
Ndivyo ilivyokuwa hivyo Kongo.
Serikali ya Mobutu ilianzisha kitu kinaitwa UMUZA ambayo ni kama BASATA ya Tanzania. Hii UMUZA ilikuwa na mamlaka ya kutoa vibali kwa wanamuziki kwenda nje. Ilisimamiwa na Franco. Serikali pia iliamrisha Studio kubwa ya Wazungu, MAZADIS akabidhiwe Franco katika Zaireanisation ya kupora mali za wakoloni kuwapa wenyeji.

Soma history ya wimbo wa Franco unaoitwa Cherie Bandowe, ambao ulipotoka ilibidi Mobutu atoe amri kuwa kila mwenye nakala ya wimbo huo aikabidhi serikali.
 
Ndivyo ilivyokuwa hivyo Kongo.
Serikali ya Mobutu ilianzisha kitu kinaitwa UMUZA ambayo ni kama BASATA ya Tanzania. Hii UMUZA ilikuwa na mamlaka ya kutoa vibali kwa wanamuziki kwenda nje. Ilisimamiwa na Franco. Serikali pia iliamrisha Studio kubwa ya Wazungu, MAZADIS akabidhiwe Franco katika Zaireanisation ya kupora mali za wakoloni kuwapa wenyeji.

Soma history ya wimbo wa Franco unaoitwa Cherie Bandowe, ambao ulipotoka ilibidi Mobutu atoe amri kuwa kila mwenye nakala ya wimbo huo aikabidhi serikali.
never knew this but your RIGHT
 
Chuma hiki ilikua hatarii "maidoda"
Screenshot_2025-07-19-00-27-43-149_com.spotify.music.jpg
 
kwahio wewe pepe kale ndo GOAT
Pepe Kalle (Kabasele Yampanya) ni mtoto mdogo na hawafikii wakongwe kwa umaarufu. Yeye mwenyewe Pepe Kalle alikiri kuwa aliyemvutia kuingia kwenye mziki ni Joseph Kabasele a.k.a Le Grand Kalle.
 
Pepe Kalle (Kabasele Yampanya) ni mtoto mdogo na hawafikii wakongwe kwa umaarufu. Yeye mwenyewe Pepe Kalle alikiri kuwa aliyemvutia kuingia kwenye mziki ni Joseph Kabasele a.k.a Le Grand Kalle.
nlikua namuuliza jamaa apo naona katuma screenshot
 
Pepe Kalle (Kabasele Yampanya) ni mtoto mdogo na hawafikii wakongwe kwa umaarufu. Yeye mwenyewe Pepe Kalle alikiri kuwa aliyemvutia kuingia kwenye mziki ni Joseph Kabasele a.k.a Le Grand Kalle.
Muziki kila mtu anaupokea kwa ladha yake , mimi binafsi nasikiliza nyimbo za Pepe kalle mpaka leo.
 
1. Franco luambo makiadi
View attachment 3410299

2. Tabu Ley Rochereau
View attachment 3410301

3. Papa wemba

View attachment 3410303

4. Pepe kale
View attachment 3410306

List hii ni ya OG wa rhumba, wakina fally wanaimba Rhumba ya kimarekan
Kwa mara ya kwanza tangu nikufahamu umeandika uzi kabambe.

Hata hivyo si rahisi kumtaja mtu mmoja kwenye swali lako, hii ni kwa sababu Rhumba ina vipengere kadhaa, hakuna msanii mmoja anaweza kufit mote.

Yuko pia Nyoka Longo, lakini kwenye kizazi kipya kuna Ferre Gola, kiukweli hili ni eneo pana mno!
 
Back
Top Bottom