stakehigh
JF-Expert Member
- Aug 9, 2019
- 19,480
- 15,333
- Thread starter
- #41
sasa hujachagua GOATMpaka umeona Mtu kwa Kuheshimika kwa Kazi yake kaitwa Mitre (Mwalimu) jua kuwa Luambo Luanzo Franco Makiadi a.k.a Mitre (Mwalimu) hana Mpinzani na kwa Taarifa yako tu ni kwamba Wasanii wengine wote wamejifunza na kupita njia zake. Ulichokosea ni kutomtaja Mtu ambaye kwa Sisi wenye Muziki wetu wa akina Bandeko Nangai (bana Congo DR) tunajua ndiyo alipikwa vyema na Marehemu Franco katika Miziki ya Rhumba na ndiyo alikuwa Mfalme baada ya Franco Kufariki ambaye ni Marehemu Madilu Multi System. Hakuna Rhumba ya Madilu System huwezi kutoicheza na huyu ndiyo alikuwa Mrithi sahihi wa Marehemu Franco na ndiyo maana alipendwa nae sana kama siyo mno tu.
Na mwisho kwa Kukusaidia tu ni kwamba kumuweka hapa katika List yako Marehemu Pepe Kalle umekosea sana kwani huyu ndiyo Baba wa Muziki aina ya Sebene na kwa msiojua Pepe Kalle ndiyo Mwanzilishi wa huu Mtindo wa Kughani (Watoto wa Mjini mnauita Kurapu) ila kwa kule Congo DR wanaita Atalaku katika Miziki na ndiyo pia alimfundisha Rapa / Mghani (Atalaku) wa Kwanza Bileku Mpasi (Jina lake halisi ni Djuna Mombafu) aliyefanya vyema katika Bendi yake ya Empire Bakuba hadi baadae kuja Kuigwa na Wengineo kama akina Alain Kounkou, Roberto Wunda Enkokota wa Wenge BCBG na wengineo wengi hadi akina GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE (Jina halisi ni Pitshou Lisimo) wa Wenge BCBG yake JB Mpiana ambaye kwa sasa hana Mpinzani katika Medani nzima ya Kughani / Kurapu (Atalaku) huko Congo DR japo kwa mbali anatishiwa na Rapa Kijana Hatari sana wa Extra Musica ya Roga Roga (zamani Extra Musica Zangul Zangul) aitwa Zaparo Degere.