beefinjector
JF-Expert Member
- Jul 23, 2009
- 2,762
- 2,736
Maji safi yaliyo chini ya ardhi kwa ajili ya matumizi ya binadamu huwa hayana mmiliki. Ukifaniukiwa kuchimba/kuchimbiwa au kuwa na kisima kikubwa unachomiliki kisheria kiasi cha kuweza kuwagawia wengine (e.g. DAWASCO), unaweza ukaamua kama utawagawia bure au watalipia, au hata usiwagawie kabisa utumie wewe mwenyewe tu, kama unaona matumizi yako ni makubwa au maji yako siyo mengi. Hata internet imefanana kiasi hivyo. Sema tu kuna mtu aliyegundua internet mwaka 1992 anaitwa Tim Berners Lee. Huyu ndiye aliyegundua internet ila sidhani kama ana hati miliki yake. Kwa mfano, ulishawahi kujiuliza kama kuna mtu ana hati milki ya masafa ya mawasiliano kv ya redio, simu nk? Nadhani sheria kama hiyo haipo duniani. Anyway ni mawazo yangu tu, naweza nisiwe sahihi kama ninavyodhani!
Correction Mkuu, Tim Berners Lee aligundua World Wide Web (www) na sio internet. Huu ni mojawapo tu ya mifumo ya matumizi ya internet ambayo inawezesha ku-access interlinked hypertext documents (samahani sijui tafsiri yake kwa kiswahili). Kwa lugha nyepesi ni kuwa WWW inawezesha ku-access wavuti (websites) mbalimbali ambazo zina maandishi, picha, video n.k kwa kutumia web browser (sijui tafsiri yake kwa kiswahili).