Logikos
JF-Expert Member
- Feb 26, 2014
- 17,572
- 27,395
chief-mkwawa, cable na wi-fi same applies as mobile provider kulingana na majibu yako. Mf. Anaeweka kwenye restaurant atanunua kwa local isp na local kwa intl isp mpaka kwa mwenyewe anaetengeneza bytes
mkuu bytes hazitengenezwi mfano kuna picha ya michael jackson imehifadhiwa marekani kwenye computer fulani wewe unapoclick kwenye ile address ili upate ile picha; picha itavunjwa vunjwa katika bits ili kurahisisha usafirishaji (pua; mdomo; kifungo; kifungo n.k.) baada ya kufunjwa vunjwa na modem ya kule kwenye picha ilipo kila bits zitatafuta njia nyepesi kuweza kufika kwenye modem yako huenda pua ikatumia satellite; mdomo ukatumia mkonga; sikio cable n.k na kama sikio likipotea njiani modem yako huku itagundua kuna kitu kinamiss itaomba tena. Sasa baada ya hizi bytes zote kufika kwenye destination zitakuja na information jinsi ya kuunganisha hizi bytes zote kumtengeneza michael jackson ili uweze kumuona kwenye pc yako ingawa huenda njia iliyotumia na pua na sikio ni tofauti.....
Kwahio hata wewe ukitaka unaweza kuwa internet service provider wa eneo lako ila itabidi uwe na njia bandwidth ya kuweza kuwapa wateja wako iwe cable au satellite yako (au kukodisha kutoka kwa isp mkubwa) mfano ttcl anaweza akakukodisha kiasi fulani ili messages information za wateja wako ziweze kufika kwenye gateway (yaani njia kuu kwa maneno mengine) kwahio wewe utakuwa unawalipa ttcl tu kwa hio service. Pia kumbuka google na kina facebook wanataka kuleta internet bure through satellites kwahio na wao watakuwa wanamiliki hizo satellites na hawatakuwa answerable kwa yeyote yule. Kumbuka internet ndio maana ikaitwa web yaani ni kama nyumba ya buibui ukikata njia moja unaweza ukapita pengine ili uweze kufika
Last edited by a moderator: