Kabla Hujafunga Biashara Yako, Soma Hii Kwanza.

Kabla Hujafunga Biashara Yako, Soma Hii Kwanza.

kabweza

Member
Joined
Feb 3, 2017
Posts
11
Reaction score
23
Wakuu wa jukwaa,
Leo nataka niongee kitu ambacho naamini kinaweza kubadilisha namna tunavyoendesha biashara zetu za kila siku hasa sisi wafanyabiashara wadogo na wa kati.

Ukweli ni huu
Biashara nyingi Tanzania zinaendeshwa kwa mazoea. Tunatumia daftari, kumbukumbu za kichwani, au wakati mwingine hata WhatsApp kuhifadhi taarifa. Mwisho wa siku unakuta
  • Hujui faida yako halisi ni kiasi gani
  • Hujui bidhaa gani zinaenda sana
  • Hujui pesa imepotelea wapi
Hapo ndipo suluhisho kama Obiashara linaingia.

Obiashara ni nini?
Obiashara
ni app (mfumo wa simu) uliotengenezwa kusaidia wafanyabiashara kusimamia biashara zao kwa urahisi kabisa.

Kwa lugha rahisi:
Ni kama “msimamizi wa biashara yako ndani ya simu”.
Kupitia mfumo huu unaweza
  • Kusajili bidhaa zako zote bila kikomo
  • Kufuatilia stoki (bidhaa kuisha au kubaki)
  • Kurekodi mauzo na matumizi
  • Kufuatilia madeni ya wateja
  • Kupata ripoti za biashara yako
  • Kusimamia biashara zaidi ya moja kwa wakati mmoja
Na kitu kikubwa zaidi…
- Unafanya kazi hata bila mtandao wa internet.
Ingia hapa obiashara kupdata maelezo kina.

Kwanini mfumo kama huu ni muhimu sana?
Hebu tujiulize kidogo...
Ni wafanyabiashara wangapi
  • Wanaishia kufunga biashara bila kujua walikosea wapi?
  • Wanauza sana lakini hawana faida?
  • Wanakosa bidhaa bila kujua ziliishaje?
Tatizo si biashara…
Tatizo ni usimamizi wa biashara.
Kwa kutumia Obiashara
  • Unajua kila kitu kinachoingia na kutoka
  • Unafanya maamuzi kwa kutumia data, sio kubahatisha
  • Unapunguza hasara zisizoonekana
Kwa kifupi
Unaanza kuendesha biashara kama “mtaalamu”, sio kwa mazoea

Obiashara inatofautianaje na mifumo mingine?
Soko lina mifumo mingi ya biashara, lakini ukweli ni kwamba mingi ina mapungufu mengi.
Kwa mfano, mifumo mingine
  • Inahitaji internet muda wote
  • Ina features chache
  • Haijaendana sana na mazingira ya Tanzania
  • Haina uchambuzi wa kina
Lakini Obiashara imeboreshwa zaidi kwa mazingira yetu:

1. Inafanya kazi hata bila internet

Hili ni muhimu sana kwa mazingira yetu ambapo mtandao sio wa uwakika sana.

2. Inasimamia kila kitu sehemu moja

  • Mauzo
  • Stoki
  • Matumizi
  • Madeni
  • Ripoti

3. Rahisi kutumia (Kiswahili ndio lugha mama)

Imezingatia mtumiaji wa kawaida kabisa kwa kutumia lugha aliyoizoea, Pia anaweza kuchagua lugha ya kiingereza.

Mfano halisi
Fikiria una duka la jumla au rejareja
  • Mteja akinunua -> unaandika kwenye app
  • Bidhaa ikipungua -> unapewa alert
  • Mwisho wa siku -> unaona faida yako
  • Mwisho wa mwezi -> unaona biashara imekua au imeshuka
Hii yote bila stress.

Namna bora ya kuitumia Obiashara
Ili uone matokeo makubwa, fanya hivi
  1. Weka bidhaa zako zote kwenye mfumo
  2. Rekodi kila mauzo (hata madogo)
  3. Rekodi matumizi yote
  4. Angalia ripoti kila siku au kila wiki
  5. Tumia mapendekezo ya mfumo kuboresha biashara
Ukifanya hivi kwa mwezi mmoja tu, utaona tofauti kubwa sana.

Obiashara ni kwa nani?
Mfumo huu unafaa kwa
  • Wenye maduka (rejareja & jumla)
  • Wafanyabiashara wa mitandaoni
  • Wauzaji wa bidhaa mbalimbali
  • Wenye biashara zaidi ya moja
  • Hata wanaoanza biashara

Kwa kifupi
Kama unafanya biashara yoyote - unauhitaji huu mfumo

Leo hii dunia inabadilika.
Biashara zinaendeshwa kwa data, sio kubahatisha.
Kama bado unatumia daftari pekee, ukweli ni kwamba unajichelewesha mwenyewe.

Obiashara ni hatua ya kutoka
“biashara ya mazoea”
kwenda “biashara ya kisasa”

Anza leo
Pakua app hii sasa Hapa

Asanteni wanajamii forums naimani biashara yako utoifunga sasa!
 
hayo yote excel inaweza kuyafanya
Ni kweli kabisa Excel inafanya vizuri lakini ina mapungufu kadhaa kulingana na mazingira
1. Ni ngumu kwa mmiliki wa biashara kupata taarifa mpaka awepo kwenye biashara yake au atumie njia zingine ambazo ni Technical sana(Sio kila mtu anaweza).
Lakini mfumo huu kila kinachofanyika kwenye biashara mmiliki anaweza kupata notification kwenye simu yake pia na sms ya kawaida kila biashara inapofungwa.
2. Excel Ina hitaji ujuzi wa ziada ili kuweza kutumia kwa ufanisi(Sio rafiki kwa kila mtu kuielewa kwa urahisi)
Lakini mfumo wetu ni rahisi zaidi kuuelewa na kuweza kuutumia bila hata maelezo ya zaidi
3. Asilimia kubwa Excel inahitaji matumizi ya kompyuta inaleta ugumu pale kunapotokea matatzio ya umeme kukatika (Hasa haya mazingira yetu ya Tanzania)
Lakini mfumo huu unaweza kuutumia kwenye simu bila kuhofia swala la umeme kukatika au laah!
4. Ni rahisi kupoteza taarifa kwenye excel maana asilimia kubwa uhifadhi na kuziamini kompyuta zao, ambazo ki uhalisia muda sio salama sana maana taarifa zinaweza kupotea, kuharibika au hata kupoteza kutokana na majanga mbali mbali kama moto nk.

Mwisho nitoe ushauri kama wewe ni mtumiaji wa excel unaweza kujaribu mfumo huu pia ili uweze kuona utofauti wewe mwenye, kujua niliyo yasema ni sahihi au laah!
Pia Mr Smooth Criminal ushauri kama unatumia excel jaribu kutumia ya online ili kuhepuka matatizo au mapungufu niliyo orodhesha hapo juu.
 
Nitajipa muda kufatilia mfumo wenu, huenda ikawa na utofauti na app nyingine za usimamizi wa biashara kupitia simu janja ama Laptop
 
Back
Top Bottom