Ila tu cha msingi kama ukifanikiwa kupata mawasiliano yake au alipo tafadhali nenda taratibu na kwa hekima kubwa kabisa maana yawezekana ana familia nyingine na hajaiambia chochote kuhusu uwepo wako hivyo itabidi utumie mbinu mbadala kama utakuta hali hiyo ili familia yake ibaki salama.
Lakini pia achana na hao wanaosema usimtafute kwa sababu wanafikiri upande mmoja pekee, wao wame base sana kwa wewe kupata msaada kutoka kwa huyo baba, wewe nenda na yote, maana kwa mfano: ni vipi kama baba yako huyo yupo katika hali ngumu sana sana ya maisha au kiafya kutokana na kuwa na kipato duni ilihali wewe una hali nzuri kifedha? Huoni kumtafuta kwako kutamuokoa?
Nina mfano hapa rafiki yangu naye alimtafuta sana baba yake kwa mda mrefu kumbe yule mzee alikuwa hoi anaumwa kalazwa pale BUGANDO na hana msaada kwani hali yake ngumu na bahati mbaya mke aliye oa hakujaliwa kupata nae mtoto lakini aliishi naye hivyo na yupo anamuuguza pale tatizo ni kukosa pesa laki 7 tu ya upasuaji
Sasa jamaa alipo enda kumtembelea mfanya kazi mwenzie aliye pata ajali ya gari ndio anasikia manesi wana elezana kwenye korido kwa kutaja jina la mgonjwa kwamba wanataka wamruhusu tu aende nyumban maana hata akibaki pale hakuna cha kufanya, ndio jamaa alipo sikia jina linatajwa ndio kuuliza kwa manesi akapewa maelezo alipo ruhusiwa kwenda kumuona huyo mzee na kumdadis maswali kumbe ni baba yake mzazi kabisa
Jamaa akalia sana na hasa akiangalia hali na hadhi yake halafu na hali aliyo nayo baba yake mazazi pale kitandani na hapo ndio ikawa pona ya mzee maana alimsafirisha akaja kutibiwa hapa muhimbili na yupo safi hadi sasa na anazidi kumpa baraka mtoto wake
Na jamaa kiumweli kabisa ananiambia mambo yake yameanza kumyookea na hasa baada ya kufanikiwa kumpata baba na kubwa zaid kumnusuru na kifo cha maradhi ya kukosa pesa
Huo ni mfano dhahir kabisa ulio mtokea rafiki yangu wa karibu kabisa
Lakini pia waweza tumia facebooj, tweeter au mitandao mingine ya kijamii we andika tu majina ya baba huyo kwenye search bar lazima yatakuja majina yanayo fanana anzia hapo