Namtafuta Baba yangu aitwaye Peter Matiko

Namtafuta Baba yangu aitwaye Peter Matiko

Status
Not open for further replies.
Kama mama yako aliolewa na mwanaume mwingine akachukua jukumu la kukulea huyo ndie baba yako au mwanaume yoyte aliekulea mpka kufika hapo huyo ndie baba yako wacha kupoteza nguvu zako kumtafuta biological father maana usitegemee kupata chochote Cha maana zaidi ya salamu hakuna namna unaweza fanya kwa Sasa ukapata ule upendo halisi wa baba na mtoto.

Endelea kumtafuta ila nakusihi usitarajie makubwa baada ya kuonana nae.
Kwani unateseka?
 
Kwa nini usitoe details kama alikua anafanya issue gani hapo Arusha na alienda wapi baada ya hapo?
 
Mtu anatafuta baba yake kuna vijimwanamke vinashupaza shingo kumshauri asimtafute kwa kufikiri kila mwanamke mwanamme wanapotengana na kushindwa kulea mtoto pamoja basi baba nd'o mwenye makosa.

Sometimes inaweza kuwa kweli mkosefu ni baba, na mara nyingine akawa mama. Na inawezekana kusiwe na makosa kwa yeyote yule ila mazingira yamelazimisha iwe hivyo.

Mtoto ana haki ya kumtafuta na kumjua mzazi wake aliepotezana nae no matter what.

IMG_20201205_195031.jpg
 
Mtu anatafuta baba yake kuna vijimwanamke vinashupaza shingo kumshauri asimtafute kwa kufikiri kila mwanamke mwanamme wanapotengana na kushindwa kulea mtoto pamoja basi baba nd'o mwenye makosa.

Sometimes inaweza kuwa kweli mkosefu ni baba, na mara nyingine akawa mama. Na inawezekana kusiwe na makosa kwa yeyote yule ila mazingira yamelazimisha iwe hivyo.

Mtoto ana haki ya kumtafuta na kumjua mzazi wake aliepotezana nae no matter what.View attachment 1642464
Thank You So Much!
 
Ushauri konkiii
Hakuna cha ushauri konki wala nini? Tatizo mmeset negative mind, mnajua kitu kilichofanya wapotezane na mama yake? Mnakijua? Labda mama ndio alitoroka na mtoto.

Kwetu tunasema asemaye peke yake hana haki, mpaka usikie upande wa pili. Uzuri mleta mada hajasema kitu kilichofanya wapotezane. So hatuwezi jua ni ugomvi au msukumo wa ndugu.

Nakupa mfano, mtu umempa mimba mtoto wa watu na hukumuoa. Baba yake akakasirika na kukwambia marufuku kumjua mwanawe na kiumbe kitakachozaliwa-na hii hutokea sana kwa familia tajiri mtoto wao akipewa mimba na mtoto wa masikini. Mwisho wa siku binti na mwanawe wanapotea kusikojulikana na huwezi kuwatambua tena waliko.

Je, mtoto atakayezaliwa hana haki ya kumjua baba yake?
Think.
 
Daah ila watu wana stress sana yaan mtu kumtafuta baba yake kuna mwingine anakereka mara usimtafute mara hutaongeza chochote

Mzazi ni mzazi tu na kuna ile hali ya kutaka kujua baba anafananaje , ndugu zangu wengine wakoje ni vitu vinatokea vyenyewe tu

Mkuu nikupongeze na kukupa moyo endelea kumtafuta mzazi wako kama walitofautiana au kuna sabab zilitokea hizo ni changamoto kama zilivyo changamoto nyingine usibebe vitu vya wazazi ukarith wewe
 
Ndugu yangu wewe endelea kumtafuta mzee wako

Ila kwa hayo majina ya MATIKO, nenda kitunda hivi,kama ndio surname yako utakuta ndgu zako tele huko..
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom