Namtafuta Baba yangu aitwaye Peter Matiko

Namtafuta Baba yangu aitwaye Peter Matiko

Status
Not open for further replies.
Mkuu kwanza nikupe pongezi kwa kukumbuka hilo.
Damu ni nzito kuliko maji.
Mimi nitakusaidia kutuma meseji yako kwenye magroup mbalimbali,nina rafiki zangu wakurya watasaidia kumtafuta.
Usijali penye nia pana njia
Shukran sana mkuu
 
Mkuu acha kabisa kuna watanzania ni mbumbumbu sana aisee.
Yaani wamekariri kwamba mtu akimtafuta ndugu yake labda lengo ni kwenda kuomba msaada tu kumbe wengine hufanya hivyo just kwa ajili ya upendo tu.
Mimi nina uzoefu wa kesi kama hizi jinsi gani watu waliolelewa na mzazi mmoja mateso wanayoyapata hasa ya kisaikolojia hata kama wanapata huduma zote.
Nilishawahi kuwa na rafiki yangu mmoja nilisoma naye alikuwa analelewa na mama yake tu na baba yake alikuwa hamjui.
Yule jamaa alikuwa anapewa kila kitu na mama yake yaani huduma zote muhimu alikuwa anazipata na alisomeshwa kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu.
Licha yule rafiki yangu kupata huduma zote muhimu lakini kuna kipindi alikuwa anakosa amani kwa kutomjua baba yake yaani ilikuwa inamkwaza,alitamani kumjua tu huyo baba yake yupoje na anafananaje hata kama hatopewa huduma yoyote.
Hii hali huwa inatokea kibinadamu.
Sasa huwa nashangaa mtu anapojitokeza kuomba msaada wa kumtafuta mzazi wake watu wanaanza kuuliza maswali ya kejeli na comments za ajabu ajabu.
Same case here broo, huyo ni mimi kabisa
 
Mambo Vipi Naitwa Noel Matiko, namtafuta baba yangu aitwaye Peter Matiko Nyamohanga walipotezana na mama yangu aitwaye Omega Macha maeneo ya Njiro Arusha miaka ya 1998

Nimeambiwa baba yake (babu yangu) alikua mwanajeshi moja ya kambi zilizopo jijini Dsm na ndio maana yeye naye alienda jeshini

Sikuwahi kumuona ningefurahi sana kupata taarifa zake, kama akipata ujumbe huu au kwa yeyote anayejua alipo anitafute kwa simu namba 0676238390

Natanguliza shukrani!
Umejaribu kumuuliza Esther Matiko?
 
Kama mama yako aliolewa na mwanaume mwingine akachukua jukumu la kukulea huyo ndie baba yako au mwanaume yoyote aliekulea mpaka kufika hapo huyo ndie baba yako wacha kupoteza nguvu zako kumtafuta biological father maana usitegemee kupata chochote Cha maana zaidi ya salamu hakuna namna unaweza fanya kwa Sasa ukapata ule upendo halisi wa baba na mtoto.

Endelea kumtafuta ila nakusihi usitarajie makubwa baada ya kuonana nae.
Huo ni ushauri au kumkatisha tamaa? Kwanza unaanza kwa kumhukumu baba yake. Wewe hujui ni nini kilichotokea. Huenda wote walikuwa watoto na kama watoto walipoteana hawakuonana tena.

Kama aliolewa wewe unajua labda asingeweza kumueleza mwanae amtafute baba yake wakati aliyemuoa alimkubali mtoto. Lakini wakati mwingine, ni muhimu kumfahamu baba yako mzazi (biological father). Kijana amefanya kitu kizuri kutaka kumjua baba yake.

Vivyo hivyo, kwa mtoto kumtafuta mama yake ambaye hamjui ni jambo la busara. Kama alivyosema mmoja wetu, kuwajua wazazi kunaweza kukakwepesha balaa la "incest" (dada na kaka kuoona). Acheni kasumba za kudhania kumtafuta baba au mama utapata au utawapa faida. Binadamu ukiishi bila kumfahamu mmojawapo wa wazazi wako unajisikia kupungukiwa!
 
"Akikua atanitafuta mwenyewe damu yetu haipotei" Kuna wazee fulani huwa wanaapiza haya maneno. Hasa unapotokea mtafaruku kwa pande mbili ili kuepusha shari ili maisha yasonge mbele. Bw. Mdogo hongera sana, wewe ni MWANAUME wa kweli. Suppa sana
 
Jaribu kupitia pitia nyuzu za humu JF.... wapo wazazi nao wanatafuta watoto baada ya kupoteana na mama zao kwa sababu hii au ile, huenda Mzee Peter naye alishaleta uzi humu.
 
Jaribu kupitia pitia nyuzu za humu JF....wapo wazazi nao wanatafta watoto baada ya kupoteana na mama zao kwa sababu hii au ile, huenda Mzee Peter naye alishaleta uzi humu.
Haahaa hao wazee wa jiwe moja hawana muda huo labda ajichokee sana halafu watu wamtonye dogo yuko njema
 
Nenda kambi yeyote ya jeshi wape taarifa zote watakusaidia kukupa taarifa zake kama kweli alikuwa mwanajeshi
 
Tatizo si kupata chochote....dogo ana haki ya kumjua baba ake
Hii ni moja kati ya dhana za kijinga ambayo imesababisha wanaume wengi wamekuwa washenzi, mtu anazaa anatelekeza mtoto haudumii kuanzia mimba wala kusomesha mtoto akitegemea mtoto akikukua lazima amtafute baba.

Wewe dogo kama chanzo cha kumtafuta baba yako ni ugumu wa maisha nakusihi pambana kivingine wababa wa aina ya baba yako kuwatafuta ni wendawazimu.
Sorry kama nimekukwaza lakini huo ndio ukweli.
 
Mtu hajakulea alitokomea halafu unamtafuta huyo haramia. Ningekuwa baba yako wa kambo ningekufukuzia mbali sana.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom