Namtafuta Baba yangu aitwaye Peter Matiko

Namtafuta Baba yangu aitwaye Peter Matiko

Status
Not open for further replies.
Kama mama yako aliolewa na mwanaume mwingine akachukua jukumu la kukulea huyo ndie baba yako au mwanaume yoyte aliekulea mpka kufika hapo huyo ndie baba yako wacha kupoteza nguvu zako kumtafuta biological father maana usitegemee kupata chochote Cha maana zaidi ya salamu hakuna namna unaweza fanya kwa Sasa ukapata ule upendo halisi wa baba na mtoto.

Endelea kumtafuta ila nakusihi usitarajie makubwa baada ya kuonana nae.

Yaani damu iliyo ndani ya huyu Dogo ndio ipo kwa Baba yake! Hata kama ni jambazi ana haki na ni vyema amtafute!

Baba ni Baba tu, na ana Baraka zake! Kwa hiyo usimkatishe tamaa Dogo, Mwache amtafute Baba yake!
 
Jina Matiko hilo ni la kabila ya WAKURYA HASA wilayani TARIME mkoani MARA. Jina Matiko ni maarufu sana na hupenda kutumika katika koo mbalimbali ni sawa na kusema MASANJA ambalo hutumika sana na Wasukuma. Nakushauri ujaribu kupeleleza walau kijiji alichozaliwa, itakuwa rahisi kumpata lakini Ukisema Matiko, hapa utasumbuka sana au itachukua muda kumpata ndugu yangu.
 
Kama mama yako aliolewa na mwanaume mwingine akachukua jukumu la kukulea huyo ndie baba yako au mwanaume yoyte aliekulea mpka kufika hapo huyo ndie baba yako wacha kupoteza nguvu zako kumtafuta biological father maana usitegemee kupata chochote Cha maana zaidi ya salamu hakuna namna unaweza fanya kwa Sasa ukapata ule upendo halisi wa baba na mtoto.

Endelea kumtafuta ila nakusihi usitarajie makubwa baada ya kuonana nae.
Wewe bhana ukimjua baba yako ni nusu ya pepo
 
Hakuna cha ushauri konki wala nini? Tatizo mmeset negative mind, mnajua kitu kilichofanya wapotezane na mama yake? Mnakijua? Labda mama ndio alitoroka na mtoto.....

Kwetu tunasema asemaye peke yake hana haki, mpaka usikie upande wa pili. Uzuri mleta mada hajasema kitu kilichofanya wapotezane. So hatuwezi jua ni ugomvi au msukumo wa ndugu.

Nakupa mfano, mtu umempa mimba mtoto wa watu na hukumuoa. Baba yake akakasirika na kukwambia marufuku kumjua mwanawe na kiumbe kitakachozaliwa-na hii hutokea sana kwa familia tajiri mtoto wao akipewa mimba na mtoto wa masikini. Mwisho wa siku binti na mwanawe wanapotea kusikojulikana na huwezi kuwatambua tena waliko.

Je, mtoto atakayezaliwa hana haki ya kumjua baba yake?
Think.
well said
 
Daah ila watu wana stress sana yaan mtu kumtafuta baba yake kuna mwingine anakereka mara usimtafute mara hutaongeza chochote

Mzazi ni mzazi tu na kuna ile hali ya kutaka kujua baba anafananaje , ndugu zangu wengine wakoje ni vitu vinatokea vyenyew tu

Mkuu nikupongeze na kukupa moyo endelea kumtafuta mzaz wako kama walitofautian au kuna sabab zilitokea hizo ni changamoto kama zilivyo changamoto nyingine usibebe vitu vya wazaz ukarith ww
sawa mzee, uchumi wa kati umeleta makasiriko sana miouoni mwa watu
 
Jina Matiko hilo ni la kabila ya WAKURYA HASA wilayani TARIME mkoani MARA. Jina Matiko ni maarufu sana na hupenda kutumika katika koo mbalimbali ni sawa na kusema MASANJA ambalo hutumika sana na Wasukuma. Nakushauri ujaribu kupeleleza walau kijiji alichozaliwa, itakuwa rahisi kumpata lakini Ukisema Matiko, hapa utasumbuka sana au itachukua muda kumpata ndugu yangu.
nitajitahidi
 
Ni vizuri kumtafuta mzazi wako, ila jiandae kisaikolojia unaweza usimpate, au ukimpata akaku reject, kama aliku shit ulivyokua mdogo anaweza kuku shit pia uko kubwa, sikukatishi tamaa ila jiandae...
 
Mambo Vipi Naitwa Noel Matiko, namtafuta baba yangu aitwaye Peter Matiko, walipotezana na mama yangu aitwaye Omega Macha maeneo ya njiro arusha miaka ya 1998

Sikuwahi kumuona ningefurahi sana kupata taarifa zake, kama akipata ujumbe huu au kwa yeyote anayejua alipo anitafute kwa simu namba 0676238390

Natanguliza shukrani!
Kumbe unaitwa Noel Matiko na namba zako ndio hizo oky ngoja tuendelee kutafuta
 
Watu mna dharau, unamuita mtu usiyemjua dogo , usikute huyo unayemuita hivyo anakuzaa we we mara saba ..
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 Mara 700 kabisaa
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom