Namna ya kumkamata mwanaume!!

...to be on the safe side ili usiwekwe kiti moto na kuanza kujihami ni bora tu pale ambapo mapenzi yameshamiri kuanika kila kitu unachoona mwenzako anastahili kukijua kwa wakati huo.

...ina maana kumwambia 'udhaifu' wako na wa kwenu...au sio?
 
...ina maana kumwambia 'udhaifu' wako na wa kwenu...au sio?

Mkuu Mbu nazungumzia mfano ambao King'asti ameutumia katika uzi huu.

BAK umeongea kitu muhimu sana. Sio ex tu ama watoto, kuna issue ya wanafamilia wakorofi pia. Hii tabia (hasa ya wadada) ya kujifanya unatokea familia takatifu is really disgusting. Hata kama babako mchawi muambie mwenzio, ajue u don't side with mambo yake. Ili hata huko mbele ya safari akikusakama nao umuambie the loss is his asiwacheke ndugu zako manake nao ni sehemu yenu.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Tatizo hatuelewani, hakuna mwanamke anaye omba kichapo kutoka kwa mme wake, na hakuna sheria inayo sema wakubali kupigwa sasa vipi wanyamaze? Hawana mdomo wa kulalamika kwa nini wana nyanyaswa.

FYI, Mwenyezi mungu anasema hapendi wajinga....Sheria za mungu ziko wazi, mwanamke anaye nyanyaswa asikae kwa mme wake sababu mme wake hathamini kuwepo kwake.

Kumshakia mke wako anafanya kitu kibaya ni kosa, vipi ukampige makofi na kumnyanyasa....

Hayo yanayo zabuliwa vibao na kupigwa ni majinga lolo tu, hata kama angekuwa bibi yangu :A S shade:

Sawa mkuu,

Labda ungejuvya kidogo ili nisijekuonena nabisha tu au naongea mambo ambayo ni enzi zetu za 1947,.....

Hivi mwenzetu umezaliwa, ukakulia na bado unaishi hapa kwetu Tanzania?

Babu DC!!
 
...Siyo kila GF Babu DC!!! bali yule ambaye unaona kabisa kwamba kuna kila dalili ya wote kufikia maamuzi ya kufunga pingu za maisha.

BAK,

Siyo rahisi kujua ni BF/GF yupo mtafikia hatua hiyo mkiwa bado kwenye hatua za awali. Kama ingekuwa hivyo, mauvumi ya mapenzi yasingekuwa yameenea kila kona.....Bado nasisitiza kuwa kuna umuhimu wa kwenda mdogo mdogo ili mtu asijeuza silaha za maangamizi kwa mwenzi wake pasipo sababu!!


...'bahati mbaya' na kwa makusudi kabisa, tunapokuwa tu wahitaji hasa kwenye mapenzi...tunajitahidi kwa kila liwezekanalo kutojionyesha tuna dosari yeyote....

Hivi ukionesha dosari zako mapema ni plus au ndo unajimaliza?

Nadhani katika hatua za awali ni vizuri kumwaga sera zinazokuuza badala ya kuweka vionjo ambavyo vinaweza kukuangamiza!

...Naam mara nyingi huwa hivyo. Watu hawafikirii kile ambacho wamejaribu kukuficha huweza kumfikia mwenzio kupitia source tofauti na hapo kupunguza imani ambayo alianza kuijenga kwako na hili linaweza kuharibu na hatimaye kuuvunja kabisa uhusiano mzuri wa kimapenzi uliokuwepo.

Nakubaliana na majibu ya Mbu hapo chini!!

....inategemeana na utavyojibu baada ya ukweli kubainika. Dont Panic...!
Sote tuna maskendeli na maskeletoni kabatini...mfano, unapohojiwa kwamba unatabia
mbaya ya uzinzi, upigaji, nk...jielezee vizuri tu Umejifunza na umebadilika ili kumjengea imani mpya
mpenzi wako...

Lakini ukijidai kupandisha hasira, Ooohh, "nani kakwambia....sio kweli!"...hapo unatengeneza mazingira
ya mwenza wako mpya ku doubt ukweli wako..Likewise, mapungufu mengineyo ya familia yenu, mfano
mawifi washari,....au 'wanga!'

Yapo mambo mengi ambayo tunauzwa kwenye mahusiano, iwe katika hatua za urafiki, uchumba au ndoa na ambayo tunatakiwa kutoa majibu yasiyo na kona kona ili kuwapa wenzi watu imani. Kwa hiyo tatizo siyo kuulizwa, ila kasheshe ni jinsi mtu anavyolipokea swali na kulijibu!


...to be on the safe side ili usiwekwe kiti moto na kuanza kujihami ni bora tu pale ambapo mapenzi yameshamiri kuanika kila kitu unachoona mwenzako anastahili kukijua kwa wakati huo.

Kiti moto katika mahusiano hakiepukiki. Ushauri wangu ni kama alivyosema Mbu hapo juu, na additional comments zangu!

Babu DC!!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
BAK,

Siyo rahisi kujua ni BF/GF yupo mtafikia hatua hiyo mkiwa bado kwenye hatua za awali. Kama ingekuwa hivyo, mauvumi ya mapenzi yasingekuwa yameenea kila kona.....Bado nasisitiza kuwa kuna umuhimu wa kwenda mdogo mdogo ili mtu asijeuza silaha za maangamizi kwa mwenzi wake pasipo sababu!!

Babu DC!!

...Hapo hatua za awali zinakuwa zimeshakamilishwa....Kila mmoja karidhika na mwenziye katika idara zote za mahusiano.
 
...ina maana kumwambia 'udhaifu' wako na wa kwenu...au sio?

Hata mie sielewi mkuu,

Uanze kusema kuwa, unajua sweetie, baba yangu ni mchawi, kaurithi uchawi kwa bibi yake mzaa mama. Na mama yangu ni mwizi namba moja pale mtaani....Halafu, dada yetu mkubwa ni changudoa.....

Huyo GF/BF naamini atakuona kama nati fulani za kichwa zimelegea!!

Mkuu Mbu nazungumzia mfano ambao King'asti ameutumia katika uzi huu.

BAK umeongea kitu muhimu sana. Sio ex tu ama watoto, kuna issue ya wanafamilia wakorofi pia. Hii tabia (hasa ya wadada) ya kujifanya unatokea familia takatifu is really disgusting. Hata kama babako mchawi muambie mwenzio, ajue u don't side with mambo yake. Ili hata huko mbele ya safari akikusakama nao umuambie the loss is his asiwacheke ndugu zako manake nao ni sehemu yenu.


BAK,

Haina tija kueleza negatives za familia yako, labda kama kuna sababu ya msingi au zitaingia katika equation ya maisha yenu huko mbele ya safari.

Na umri wangu huu, kuna mambo kibao ya familia yetu ambayo sijawahi kumweleza Bibi DC na wala sitamwambia. Naamini hata yeye akija kuyajua hataniuliza kwa sababu yajaadhiri ndoa yetu kwa namna yoyote ile.

Babu DC!!
 
asante kwa somo mamaa kubwa! ulipitia unyangoni kwa maana nikimpata huyo mume ntazifanyia kazi.
 
...Hapo hatua za awali zinakuwa zimeshakamilishwa....Kila mmoja karidhika na mwenziye katika idara zote za mahusiano.

Vyovyote vile, kuna umuhimu wa kuongea yale ambayo unaamini yataigusa ndoa yenu kwa namna fulani.

Mfano, uncle yetu mmoja alimsusa last born wake kwa kuwa alipoenda kumwana baada ya kuzaliwa huku akiwa amelewa, alihisi kuwa ni mwarabu. Kwa kuwa alikuwa na rafiki mwarabu ambaye alikuwa anakuja hapo nyumbani kwake kumtembelea mara kwa mara (wakipata wote pombe ya kienyeji), alihisi kuwa huyo mtoto ni wa huyo mwarabu. Mama alipotoka hospitali alienda kwao hadi wazee wakaingilia kati. Huyo mtoto ni kijana mkubwa sasa na hana hata nyembe ya weupe wowote acha kufanana na huyo baba mwarabu.

Sina hakika kama huyo kijana alishaambiwa na mtu yeyote. Je unadhani kama kijana analijua jambo hilo, kuna umuhimu kumweleza mchumba wake?

Babu DC!!
 
Hata mie sielewi mkuu,

Uanze kusema kuwa, unajua sweetie, baba yangu ni mchawi, kaurithi uchawi kwa bibi yake mzaa mama. Na mama yangu ni mwizi namba moja pale mtaani....Halafu, dada yetu mkubwa ni changudoa.....

Huyo GF/BF naamini atakuona kama nati fulani za kichwa zimelegea!!




BAK,

Haina tija kueleza negatives za familia yako, labda kama kuna sababu ya msingi au zitaingia katika equation ya maisha yenu huko mbele ya safari.

Na umri wangu huu, kuna mambo kibao ya familia yetu ambayo sijawahi kumweleza Bibi DC na wala sitamwambia. Naamini hata yeye akija kuyajua hataniuliza kwa sababu yajaadhiri ndoa yetu kwa namna yoyote ile.

Babu DC!!

...Babu DC hayo yalikuwa ni mwaka 47!!! Nawafahamu GF/BF ambao walipendana sana na kuamua kufunga pingu za maisha. Kwa mwanamke hawakuwa na tatizo na upande wa mwanaume lakini BF alivyoenda kutangaza nia kwao ya kutaka kuoa binti fulani basi wakaanza uchunguzi wa familia ya Binti fulani (kwa maoni yangu familia ya binti fulani haikuwa na tatizo lolote lile la kutisha la kusababisha kutengua nia ya kijana wao) bin fulani akawekwa kiti moto kwamba wazazi hawatapenda amuoe binti fulani kutokana na waliyoyasikia kuhusu familia yake. Bin fulani akajitahidi kutetea familia ya binti fulani ili aruhusiwe kufunga naye pingu za maisha lakini Wazazi wakagoma kata kata. Bin Fulani akawa hana jinsi ila kusitisha mahusiano na hivyo kuanza mchakato mpya wa kumtafuta mwenzie. Bin fulani ameshao lakini binti fulani hajapata mtu na amejawa na majonzi makubwa sana sasa hivi anatafuta hata mtu ampe ujauzito tu ili naye aweze kuitwa mama hata kama itakuwa ni nje ya ndoa.

Yaliyokuwa yanakubalika mwaka 47 ni tofauti kabisa na mwaka 2012....Na hapa ndio kwa maoni yangu hakukuwa na tatizo lolote katika familia ya mwanamke sasa fikiria kama kuna tatizo ambalo umeamua kulificha makusudi na mwezako akalisikia kwingine, tayari linaharibu/linapunguza imani ambayo aliyoianza kuijenga kwa mwenzie.

Sisemi kwamba uhusiano utavunjika lakini huwezi kujua reaction ya mtu na mtu. Mwingine anaweza kukwambia tu sikupenda kulisikia hili pembeni lakini hakuna neno tutaendelea kama wapenzi na mwingine akasema hili nilistahili kulisikia toka kwako sijui kwa nini uliamua kunificha. Sikuamini tena, sasa hapo uhusiano tayari unakuwa unaelekea pabaya.
 
Moskwito, unasahau kwenye uhondo wa ngoma haingii peke yake na wewe unamtangulia. Cha kupatia broken heart? Yaani na mie nimeshakolea ndo nasema ama jamaa anagundua anasepa? Yaani wakati tu marafiki tu mi nakuambia yoote ujue kama utasuka ama kunyoa. Sihitaji kukutega manake ndo utakuja kuninyanyasia penzi likichuja. Dingi anavuta mibhange, so ukija kunisema mi nakucheka ww! Lol
naomba nimsaidie mkuu DC kujibu, ....mfano kuna "ugonjwa wa wazimu kwenye familia"...
mwache akishaingia kwenye uhondo wa ngoma, aicheze.
 
Dark City, kuhusu kijana aliyedhaniwa muarabu, mbona mie mpenzi namchukulia kama rafiki? Mtu mnayeweza kupiga michapo, umbea na udaku na ukakaa mioyoni mwenu! Mi nikitaka kumsengenya hata mama yake mzazi nataka nimsengenye kwake ili yasirudi kwa mama nikasutwa. Kama ni mie ningemsimulia tena nikicheka amuone babangu anavyoweza kuwa katuni. Mwenza atakayenihukumu kwa sababu ya alichofanya babangu ama mamangu kwa kweli hanifai. Nimepitia vitu mbalimbali and I learned from them. Tena ningependa mwenza aniambie 'mupenzi, you are repeating your mom's mistake. Hukupenda alivyofanya a b c d, but haina tofauti na unachofanya sasa'. Mbona atakuwa kanisaidia sana na kunifungua macho? I love open relations kiukweli! Give me all ur dirties!

Kuhusu issue ya uchawi, I guess ningesema tu kiukweli! Ili aelewe kwa nini nakaa mbali na baba yangu. Kuna mtoto wa binamu yangu alikataliwa kumuoa binti fulani kwa sababu ya background ya familia yake. Mdingi akaiongelea siku moja about kuchagua familia bora. Aisee, sikumkopesha! Nilimuambia huku kwetu mbona kuna 1 2 3? Hata sie hatufai basi eeh! Ilibidi awe mpole. Yule mpwa wangu hakumuoa yule binti, na Mungu sio King'asti dada wa watu is happily married. Mpwa kaishia kutundika mimba mwanamke asiempenda, presha ya familia yetu 'takatifu' kaishia kumuoa. Kamtesaaa na sasa kamtelekeza kwa wazazi wake kaenda 'kupumzika' marekani. Na ana visa ya mwaka, sijui kama kuna kurudi tena hapo!
 
Last edited by a moderator:
Kumbe mpo wote humu eeee!! Hapo nimewakubali, hongereni na mzidi kusonga mbele na kutusaidia mauzoefu.

Tupo tumejaa tele.

Mama Ashrat ndio ubavu wangu
Yeye ndio mwenza wangu
Naombea watu wasituletee majungu
Maana Mwenye'ezi ndio kanitunuku

Kwake mimi taaban
Hata watu wachokoe vipi
Mimi sisikii wala sioni
 
namba 7,11,13,15,17,18 hizo nimekupa big up sana. nakubaliana na wewe asilimia 200 itabidi niiprint hii nimepelekee mtu flani:A S shade:
 
Mbu, Dark City , BAK , King'asti nimependa sana michango yenu, asanteni.

Binafsi naungana na BAK + Kung'asti kuwa kufunguka pale unapoamua kwamba huyu anaonekana ndie ili kujiweka wazi mwenzio apate kuchagua mwenyewe kama asuke au anyoe ni vizuri zaidi. Inawezekana kwamba mengine yasiwe na umuhimu kwenye mahusiano yenu ila usitoe nafasi kwa yale yatakayohusu yamshangaze kwa kusikia kwa wengine.

Mf. swala la kuwa na mchawi kwenye familia au hata kusingiziwa tu, unaweza kumdokeza ili watu watakapoanza kunong'ona akija omba uchumba kwenu asikimbie/kosa/punguza imani aliyokuwa nayo juu yako.
Kuna mengine mengi madogo madogo ambayo hayawezi kudhuru ukishea, ila yanaweza ukiyaficha. Mf. mzuri ni kuwa na mtu mbea/mwenye maneno sana kwenye familia, asipojua kwamba huyu ndio zake anaweza akaambiwa mambo hata yasiyokuwepo na yakaelekea kuharibu mahusiano yako kwa namna moja ama nyingine.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Tupo tumejaa tele.

Mama Ashrat ndio ubavu wangu
Yeye ndio mwenza wangu
Naombea watu wasituletee majungu
Maana Mwenye'ezi ndio kanitunuku

Kwake mimi taaban
Hata watu wachokoe vipi
Mimi sisikii wala sioni

Baba Ashrat

Asante baba!!

Kwangu wewe ndie mfalme,
Mwenye kila sifa ya kufaa kuitwa mume.
 
Last edited by a moderator:
Mama Ashrat

Ubarikiwe sana Shosti..naprint na mie nikamkamate wangu!

BAK, Soulmate na Babu DC mmesomeka katika hii thread. (Thread ya kwanza kuona BAK kaandika, na kuandiiiiika)

Wachangiaji wengine wote big up sana kwa michango yenu maridhawa...haya wadada shime tukakamate! lol
 
...Hapo hatua za awali zinakuwa zimeshakamilishwa....Kila mmoja karidhika na mwenziye katika idara zote za mahusiano.

....mnh, huyu kaka BAK wa leo ndiye kweli?
'Hatua za awali+"kila mmoja" karidhika+idara zote= kuambiana ukweli!

.....mjumuisho huo nautazama kwa jicho la kupendana "blindly" and irresponsibly.
Anyway, labda na tahadhari zangu sababu najua athari na faida nilizonipata thru past and present relationship.
 
Back
Top Bottom