Uwesutanzania
JF-Expert Member
- Feb 9, 2019
- 859
- 1,012
Hii ni kwa waislamu,
Mlioruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja.
Yaani unayaanza maisha ukiwa hauna lolote vile unapambana na msichana wa watu (mkeo), vile anakupa njia wapi pa kuanzia wapi pa kumalizia, vile unaanguka anakusaidia kusimama tena. Mdada wa watu (mke mkubwa) mara achome vitumbua mara uende nae shamba.
Life linaanza kuwa sawa mara kwa genge mara ka pikipiki mara mashamba makubwa life hilooo mara nyumba mzuri, life limeongoza na kitambi juu.
DINI yako inakuja kukushawishi uongeze MKE wa pili.
Sawa ushapata mke wa pili.
Bado DINI YAKO inakushawishi eti ugawe haki sawa kwa sawa. Yaani huku nyama na kule nyama.
Kwa bi mdogo siku 2 na kule kwa ukikoanza naye maisha siku 2.
Ndugu yangu wacha nikushauri kitu.
Hiyo unayoifanya ni dhurma.
Haumtendei haki mdada wa watu.
Kumbuka maisha ya shida mlioyapitia, kumbuka ulivyokuwa unamshindisha na njaa mdada wa watu.
Kama wewe ni wakufata sana misingi ya dini si ungeongeza mke kipindi kile unavaa suruali imetoboka kati?
Si ungeongeza mke kipindi kile unakaanga samaki pale sokoni.
Si ungeongeza mke kipindi kile unacharanga kuni na kuuza kwa mzee Kimaro.
HIYO NI DHURMA.
Kumbuka ulipotoka.
Mlioruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja.
Yaani unayaanza maisha ukiwa hauna lolote vile unapambana na msichana wa watu (mkeo), vile anakupa njia wapi pa kuanzia wapi pa kumalizia, vile unaanguka anakusaidia kusimama tena. Mdada wa watu (mke mkubwa) mara achome vitumbua mara uende nae shamba.
Life linaanza kuwa sawa mara kwa genge mara ka pikipiki mara mashamba makubwa life hilooo mara nyumba mzuri, life limeongoza na kitambi juu.
DINI yako inakuja kukushawishi uongeze MKE wa pili.
Sawa ushapata mke wa pili.
Bado DINI YAKO inakushawishi eti ugawe haki sawa kwa sawa. Yaani huku nyama na kule nyama.
Kwa bi mdogo siku 2 na kule kwa ukikoanza naye maisha siku 2.
Ndugu yangu wacha nikushauri kitu.
Hiyo unayoifanya ni dhurma.
Haumtendei haki mdada wa watu.
Kumbuka maisha ya shida mlioyapitia, kumbuka ulivyokuwa unamshindisha na njaa mdada wa watu.
Kama wewe ni wakufata sana misingi ya dini si ungeongeza mke kipindi kile unavaa suruali imetoboka kati?
Si ungeongeza mke kipindi kile unakaanga samaki pale sokoni.
Si ungeongeza mke kipindi kile unacharanga kuni na kuuza kwa mzee Kimaro.
HIYO NI DHURMA.
Kumbuka ulipotoka.