BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,118
Hashimu Ally anadai, Pauline Gekul alitoa bastola, akamueleza achague kukalia chupa mwenyewe au apigwe risasi na mwili wake wakautupe katika Ziwa Babati. Alipogoma, wakampiga sana, wakamuingizia chupa sehemu ya haja kubwa.
Hashimu Ally anasema alituhumiwa na bosi wake (Pauline Gekul) kutumwa kuweka sumu ili kumuua Pauline Gekul, tuhuma ambazo hazijathibitishwa popote hata na jeshi la polisi, akasulubiwa sana kisha kukabidhiwa polisi Babati na kumpiga kila siku asubuhi na jioni, kwa siku nne.
Hashimu Ally anasema alikana tuhuma zote hizo akiwa kituo cha polisi Babati Mjini na hata chini ya mikono ya mateso ya Pauline Gekul. Baada ya kupigwa kwa siku nne mfululizo akiwa polisi Babati, alidhaminiwa na baba yake mzazi lakini baadaye akaitwa ofisi za Manyara ili kutoa maelezo.
Hata hivyo, Mbunge Pauline kupitia Katibu wake alikanusha taarifa hiyo katika ujumbe uliowekwa kwenye mitandao ya kijamii ukimtuhumu Hashimu kufanya udanganyifu na kushirikiana na washindani wa Pauline wa kibiashara kumfanyia ushirikina na baadaye ujumbe huo kufutwa kwa maelezo kuwa suala hilo liko mikononi mwa Polisi.
Saa chache baada ya tuhuma hizi kusambaa na kupigiwa kelele na wadau mbalimbali ikiwemo wa JamiiForums, Rais Samia Suluhu, jioni ya tarehe 25 Novemba 2023, ametengua uteuzi wa Naibu Waziri huyo wa Wizara ya Katiba na Sheria.
====
Zaidi soma >>
Breaking News: - Rais Samia Suluhu atengua uteuzi wa Pauline Gekul saa chache baada ya kutuhumiwa kufanya unyanyasaji
Pauline Gekul ajibu tuhuma za kumdhuru na kumdhalilisha kijana
Pauline Gekul anastahili kuvuliwa uanachama na kufikishwa mahakamani haraka sana. Amekichafua na kukipaka matope chama
CCM Manyara yakutana kumjadili Pauline Gekul, kutoa tamko Novemba 27, 2023
Audio: Emmanuel Gekul akitoa vitisho vya kutaka kumdhuru anayedaiwa kusambaza Video ya kijana aliyefanyiwa ukatili na Pauline Gekul
Mbunge Pauline Gekul akamatwa na Jeshi la Polisi akijaribu kutoroka nchini kuelekea nchini Kenya
Mbunge Pauline Gekul ahojiwa Polisi na kupewa dhamana, karudi nyumbani kwake
Peter Madeleka kusikiliza kesi ya Gekul mahakama ya Wilaya kwa tuhuma alizonazo dhidi ya Hamis
Mbunge Pauline Gekul atakiwa kufika Mahakamani Disemba 27, 2023 kujibu tuhuma dhidi yake
Nani anamlinda Gekul? DPP asema hana mpango wa kuendelea na kesi
Ya Gekul hayajaisha, Wakili Madeleka kukata rufaa
DPP: Hakukuwa na nia ya kufungua kesi ya Jinai dhidi ya Pauline Gekul
Rufaa ya Pauline Gekul (Mbunge Babati Mjini) yapigwa kalenda
Shauri dhidi ya Mbunge Gekul lasikilizwa Mahakamani, Wakili Madeleka asema DPP hakuwa na Mamlaka ya kufuta kesi
Rufani dhini ya Mbunge Pauline Gekul yatupiliwa mbali, wapanga kufungua kesi ya madai kwa wote waliomchafua