Naenda Tanga Kuoa

Naenda Tanga Kuoa

Tanga hmmmm!!!! labda jaribu Njombe i.e Njombe mjini, Wanging'ombe, makete, Ludewa, Makambako n.k!! teh teh teh
 
Mbona hujazungumzia chura jamaa, btw shairi zurisana hongera
 
Joverest kadisco UDSM.
Msifanye mchezo na JF. Alikuwa anaacha kukomaa na chuo yupo na iphon yake anavizia thread mpya.
Siku nzima 24 hrs mnategemea nini?
Mkuu acha uongo, Joverest ndiye Dr Shika sasa hivi yuko busy anapiga deals mara tangazo, mara collabo na ney wa mitego mara video na madee, mara interview mara special appearance fiesta kwa hiyo hana muda wa kuwa jf
 
Tatizo la Watu wa Tanga walio wengi wametawaliwa na uchawi na ushirikina! Na ndo maana pamoja Kwamba iko karibu na Dar lakini maendeleo hakuna! Natamani ndugu zangu utokee uamsho utakao pelekea kuona uchawi na ushirikina hauna faida zaidi ya hasara!
Kila mtu na mawazo yake huwezi pingwa
 
TANGA

Bora nikaoe Tanga, tena bint wa Pangani,
Yule anovaa kanga, na mitandio kichwani,
Aongea kwa kuringa, na lafudhi ya kipwani,
Awe na kauli njema, kwangu na kwa ikhwani.

Pangani nikimkosa, natafuta wa Handeni,
Niweze peleka posa, nioe niweke ndani,
Naenda haraka hasa, nisichelewe njiani,
Nitampenda kwa dhati, upendo toka moyoni.

Au nishuke Muheza, nikamsake mwandani,
Apate kuniliwaza, na uchovu wa kazini,
Najua hatanikwaza, kuniumiza moyoni,
Niliwazwe hasahasa, ili niwe wa thamani.

Au awe wa Lushoto, tena kule milimani,
Alozoea msoto, kupanda kushuka chini,
Azijua changamoto, zilizopo maishani,
Siku nikisema sina, asiende kwa jirani.

Au niende Korogwe, nimpate wa ubani,
Mchuzi atie ngogwe, nyanya chungu za mjini,
Nisemwe au nirogwe, sisikii na sioni,
Nitalia kwa makeke, akimtwaa fulani.

Wa Kilindi simpiti, na yeye namthamini,
Aweze kunidhibiti, ili nisitoke ndani,
Masham matashtiti, kwa udi pia ubani,
Katu asinisaliti, nikiwa na hali duni.

Ndugu zangu wa Mkinga, naomba nipokeeni,
Nakuja kutia nanga, nimsake wa moyoni.
Asiwe wa kujivunga, aishike sana dini,
Sio kama nabagua, natafuta mke mwema.

Au nibakie Tanga, nioe pale mjini,
Walipojaa nyakanga, wafundao wari ndani,
Panauzwa hadi shanga, sijui za kazi gani,
Kama nyumba nitajenga, hata kule mikanjuni.

Hapa sasa naishia, mawazo tele kichwani,
Wapi nitajipatia, mke yule mwenye shani,
Nipate kufurahia, raha ya ndoa ndoani,
Ila atokee Tanga, mjini au wilayani.

Cc : Mshana Jr
Hivi Tanga huwa wanandoa hawaachani au kutengana? Maana si kwa sifa hizi kwamba mapenzi yamezaliwa huko
 
TANGA

Bora nikaoe Tanga, tena bint wa Pangani,
Yule anovaa kanga, na mitandio kichwani,
Aongea kwa kuringa, na lafudhi ya kipwani,
Awe na kauli njema, kwangu na kwa ikhwani.

Pangani nikimkosa, natafuta wa Handeni,
Niweze peleka posa, nioe niweke ndani,
Naenda haraka hasa, nisichelewe njiani,
Nitampenda kwa dhati, upendo toka moyoni.

Au nishuke Muheza, nikamsake mwandani,
Apate kuniliwaza, na uchovu wa kazini,
Najua hatanikwaza, kuniumiza moyoni,
Niliwazwe hasahasa, ili niwe wa thamani.

Au awe wa Lushoto, tena kule milimani,
Alozoea msoto, kupanda kushuka chini,
Azijua changamoto, zilizopo maishani,
Siku nikisema sina, asiende kwa jirani.

Au niende Korogwe, nimpate wa ubani,
Mchuzi atie ngogwe, nyanya chungu za mjini,
Nisemwe au nirogwe, sisikii na sioni,
Nitalia kwa makeke, akimtwaa fulani.

Wa Kilindi simpiti, na yeye namthamini,
Aweze kunidhibiti, ili nisitoke ndani,
Masham matashtiti, kwa udi pia ubani,
Katu asinisaliti, nikiwa na hali duni.

Ndugu zangu wa Mkinga, naomba nipokeeni,
Nakuja kutia nanga, nimsake wa moyoni.
Asiwe wa kujivunga, aishike sana dini,
Sio kama nabagua, natafuta mke mwema.

Au nibakie Tanga, nioe pale mjini,
Walipojaa nyakanga, wafundao wari ndani,
Panauzwa hadi shanga, sijui za kazi gani,
Kama nyumba nitajenga, hata kule mikanjuni.

Hapa sasa naishia, mawazo tele kichwani,
Wapi nitajipatia, mke yule mwenye shani,
Nipate kufurahia, raha ya ndoa ndoani,
Ila atokee Tanga, mjini au wilayani.

Cc : Mshana Jr


KAMA UNAAMINI KUWA MABILIONI YA #DOCTOR_SHIKA HAYAWEZI KULETWA BONGO-
DUFUA "LIKE" HAPA
ILI TWENDE SAWA!!!

 
Tatizo la Watu wa Tanga walio wengi wametawaliwa na uchawi na ushirikina! Na ndo maana pamoja Kwamba iko karibu na Dar lakini maendeleo hakuna! Natamani ndugu zangu utokee uamsho utakao pelekea kuona uchawi na ushirikina hauna faida zaidi ya hasara!
Pole mkuu, ila na wewe upunguze ushirikina ili upate maendeleo
 
Ambiele Kiviele ,
Mkuu, karibu sana Tanga, uoe hutakaa ujute.

Binafsi, Poise, sijawahi kujuta, hata nusu sekunde kwa kuoa mke kutoka Tanga.

Nashukuru sana Tanga, kuwa Tanzania!!

Cc: emmyta na wanawake wengine wa Tanga wote heko kwenu kwa kunipeni mke mwema mliyemfunda vyema.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom