JamiiForums
JF Official Account
- Nov 9, 2006
- 6,247
- 5,731
TAARIFA KWA UMMA
Mnamo Septemba 6, 2025, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ilisitisha Leseni ya Maudhui Mtandaoni ya JamiiForums na kuzuia upatikanaji wa jukwaa kwa siku 90, kwa madai ya ukiukwaji wa Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta. Pamoja na kutambua athari kwa haki ya wananchi kupata taarifa na kutoa maoni, tulitii agizo hilo hadi huduma ziliporejeshwa Desemba 06, 2025.
Tangu kurejeshwa, tumepokea taarifa kutoka kwa watumiaji wetu wa Tanzania kuwa kuanzia Desemba 7, 2025 hawawezi kufikia jukwaa bila kutumia mbinu au nyenzo za ziada.
Tunapenda kuufahamisha umma kuwa hatuhusiki na hali hii, na tunalaani vikali kitendo cha kuzuia upatikanaji wa jukwaa bila taarifa rasmi kwa umma, kwani ni kinyume na ukiukwaji mkubwa wa haki ya kutafuta, kupokea na kutoa taarifa.
Tunatoa wito kwa yeyote au mamlaka yoyote inayohusika kuondoa mara moja vizuizi hivi na kuruhusu wananchi kupata huduma bila vikwazo.
Tutaendelea kusimamia haki za kidijitali na uhuru wa watu kujumuika mtandaoni, kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo, na kuhimiza uwajibikaji katika jamii.
Desemba 12, 2025